“Kati ya Bonde la Uvuli wa Mauti”
Mtunga zaburi Daudi alisema: “Nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, sitaogopa mabaya.” (Zab. 23:4) Daudi alikuwa amefahamu sana hatari wanazopata kondoo kwa maana alikuwa mvulana mchungaji. Huenda wanyama-mwitu wakaotea katika bonde lenye giza. Au huenda wanyang’anyi wakawa wanaotea. Huenda pia yakawako mashimo kadha yenye vina virefu. Kwa hiyo, kondoo angekuwa katika hatari kubwa asipotunzwa na mchungaji. Vivyo hivyo, Daudi aliingia katika hali zenye hatari. Lakini kwa sababu alimtumaini Yehova, Mchungaji Mkuu, Daudi alijisikia akiwa salama.