“Sinagogi la Mahuru”
■ Kati ya watu waliobishana na Stefano, wengine walikuwa wa “lililoitwa sinagogi la Mahuru.” (Matendo 6:9) Hao walikuwa watu gani? Mtu huru alikuwa mtumwa aliyekombolewa. Kwa hiyo, huenda ikawa kwamba walioshirikiana na “sinagogi la Mahuru” walikuwa watumwa waliowekwa huru, waliokuwa wamekuwa waongofu Wayahudi au Wayahudi waliotekwa na Warumi na baadaye wakaachiliwa.