Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w78 2/15 kur. 18-19
  • Kwa Sababu Gani Tutumaini Watu Wengine?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Sababu Gani Tutumaini Watu Wengine?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Habari Zinazolingana
  • Tumaini Laweza Kupatikana Tena!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Unaweza Kugeukia Wapi Ukiwa na Matumaini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Ongeza Uhakika Sasa Juu ya Wakati Ujao
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Kuliimarisha Tumaini Letu Katika Uadilifu wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
w78 2/15 kur. 18-19

Kwa Sababu Gani Tutumaini Watu Wengine?

TUKITUMAINI watu tunawaonyesha upendo. Biblia inatuambia kwamba upendo “huamini yote.” (1 Kor. 13:7) Hiyo si kusema kwamba upendo unadanganyika vyepesi, bali kupenda ndugu zetu Wakristo kutatuzuia tusiwe tukiwaonea mashaka isivyofaa, tusiwafikirie mabaya. Naam, kusipokuwa na uhakikisho ulio wazi wa kutilia watu mashaka, upendo unatuongoza tuwatumaini. Hata waamini wenzetu watukatishapo tamaa kwa njia fulani, hatutafanya haraka kusema kwamba walikuwa na makusudi mabaya.

Lakini je! hata Mungu nyakati nyingine hakosi kutumaini watumishi wake? Tunaona kwamba Elifazi Mtemani alisema kwamba Muumba hatumaini watu: “Tazama, yeye hawategemei watumishi wake; na malaika zake huwahesabia upuzi.” (Ayubu 4:18) Elifazi alikubali kwamba mwenye kumfanya aseme hivyo alikuwa “pepo.” (Ayubu 4:15) Kwa kuwa baadaye Yehova Mungu alimkaripia Elifazi na wenzi wake kwa sababu ya kusema uongo, inahakikisha kwamba “pepo” huyo alikuwa mwovu, wa kishetani. Kwa hiyo Elifazi alikuwa akirudia tu kusema uongo ulioongozwa na shetani fulani.​—Ayubu 42:7.

Kwa kweli, Yehova, ambaye ni Mungu mwenye upendo, ndiye mfano mzuri zaidi wa kutumaini viumbe vyake vyenye akili. (1 Yohana 4:8) Ni wazi kwamba anawapa wanawe wa kiroho uhuru mwingi wanapotimiza wajibu wao. Nyakati nyingine anawaruhusu watoe maoni yao juu ya mgawo fulani, kisha anawapa ruhusa ya kuutimiza. Mfano mmoja ni masimulizi yaliyo katika 1 Wafalme 22:20-22, tunaposoma hivi: “[Yehova] akasema, Ni nani atakayemdanganya Ahabu, ili akwee RamothGileadi akaanguke? Basi huyu akasema hivi; na huyu hivi. Akatoka pepo, akasimama rnbele za [ Yehova], akasema, Mimi nitamdanganya. [Yehova] akamwambia, Jinsi gani? Akasema, Nitaondoka, na kuwa pepo wa uongo kinywani mwa manabii wake wote. Akasema, Utamdanganya, na kudiriki pia; ondoka ukafanye hivyo.” Ndipo pepo au malaika huyo alipotumia uwezo wake juu ya manabii wa Ahabu hata wakasema mambo yaliyokuwa mioyoni mwao, lakini walisema uongo maana Ahabu alitaka kuwasikia wakimwambia mambo ya kumpendeza.

Hasa Yehova anamtumaini Mwanawe mzaliwa pekee kwa njia ya ajabu. Yeye alimpa huyo mzaliwa wake wa kwanza pendeleo la kushirikiana naye kuumba vitu vya kiroho na vinavyoonekana. Yehova Mungu hakuwa na woga akidhani kwamba cheo chake cha kuwa Muumba kingepungukiwa heshima akishirikiana naye. Yeye alifunulia wanadamu kwa furaha daraka ambalo Mwanawe alikuwa nalo, kwa hiyo Mwanawe akaheshimiwa sana. (Kol. 1:15-17) Wakati Mwanawe alipohakikisha uaminifu wake mpaka kufa akiwa mwanadamu Yesu Kristo, Baba alimfufua na kumpa cheo kikubwa kuliko kile alichokuwa nacho kabla hajaja duniani. Biblia inasema, “Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina; ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe . . . na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa Mungu Baba.” (Flp. 2:9-11) Kwa sababu Yehova Mungu anamtumaini Mwanawe kabisa, anajua kwamba Yesu Kristo hatatumia vibaya kamwe cheo hicho kikubwa.

Vilevile, Yehova Mungu ametumaini sana wanadamu wasio wakamilifu. Miaka mia kumi na tisa iliyopita amekuwa akichagua wanaume na wanawake 144,000 watawale pamoja na Mwanawe. Akiisha wafufua wakaishi mbinguni, anawapa hali ya kutokufa na kutoharibika. (1 Kor. 15:42-54; Ufu. 5:9, 10; 14:1-4; 20:6) Ingawa Yehova anawatukuza wapate cheo kikubwa kuliko cha malaika, yeye ana hakika kwamba watawala hao hawatatumia vibaya kamwe cheo chao.​—1 Kor. 6:3.

Kwa kuwa Yehova Mungu anatumaini watumishi wake hivyo, je! haitupasi tuige mfano wake? Ikiwa wewe unataka kumwiga, utawaona waamini wenzako kama watu wanaotaka kumtumikia Yehova Mungu kikweli. Ni kweli kwamba huenda nyakati fulani wengine wao wakakukatisha tamaa. Lakini wale waliojitoa kweli kweli wamtumikie Yehova Mungu hawataki kuumiza mtu ye yote. Wao wanasikitika sana wakati udhaifu na kutokamilika kwao kunapotokeza matatizo.

Hasa inawapasa wazee katika kundi la Kikristo wajiangalie sana waendelee kuwa na maoni yanayofaa juu ya waamini wenzao. Wakati wazee wanapokumbuka kwamba ndugu zao wanataka kikweli kufanya yaliyo haki, hawatafanya haraka haraka ya kuwalaumu kwa sababu ya vijambo vidogo walivyosahau kufanya. Wataepuka pia kuwapa maoni ya kwamba kazi haiwezi kufanywa vizuri bila ya wao kuchunguza sana kila mtu. Hakika, watu wanapokuwa waaminifu kuhusu kazi yao, wanapaswa kutumainiwa.

Zaidi ya hilo, inawapasa wazee waombe mashauri ya wale walio na ujuzi, majaliwa au busara nyingi kuliko wao wenyewe. (Mit. 15:22) Hakika mtu hapati utukufu wo wote kwa kuanzisha mpango unaoonekana kuwa ovyo baadaye. Bali, mwenye hekima ni mtu anayejaribu kufaidika kutokana na ujuzi, maarifa na majaliwa ya wengine. Unyenyekevu wake utaleta masikilizano na kuwezesha watu wengi zaidi wafurahie pamoja kazi ambayo wameifanya vizuri.

Vivyo hivyo, ndoa inaweza sana kuendelea kuwa yenye furaha mume akimtumaini mkewe. Mke asiyepewa uhuru mwingi wa kutumia akili yake mwenyewe anapotimiza madaraka yake ataacha kufurahia kazi yake baada ya muda mfupi. Atajisikia amesongwa-songwa asiweze kutumia maarifa, ujuzi na majaliwa yake, halafu atavurugika moyoni. Kwa upande mwingine, mumewe akimwacha ajiamulie mambo fulani ya maana, mke atafurahi kufanya mambo kwa njia itakayompendeza mumewe.

Wakati wazazi wanaposhughulika na watoto wao, inafaa wawahakikishie kwamba wanawatumaini. Njia moja ya kufanya hivyo ni kuwasaidia watoto wafahamu kwamba wamepewa mapendeleo na madaraka waliyo nayo kwa sababu ya kutumainiwa. Watoto wakijua hivyo, watataka zaidi kuonyesha wazazi wao kwamba hawawatumaini bure.

Kweli kunaweza kuwa na matokeo mazuri mtu akitumaini wenzake. Basi inafaa tuige mfano wa Yehova Mungu. Tena, inatupasa tujitahidi tusije tukakatisha tamaa wale wanaotutumaini. Tukitumaini watu na kuhakikisha kwamba hata sisi tunastahili kutumainiwa nao, tutasaidia sana kuendeleza uhusiano mwema na wanadamu wenzetu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki