Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w78 7/1 uku. 18
  • Adabu Nzuri ya Kike

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Adabu Nzuri ya Kike
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Mtindo Wako wa Mavazi Unamtukuza Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Kuvaa na Kujipamba kwa Kiasi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Kiasi cha Kikristo Ni Uthibitisho wa Hekima
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Kwa Nini Mavazi na Mwonekano Wetu Ni Muhimu?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
w78 7/1 uku. 18

Adabu Nzuri ya Kike

● Je! “adabu nzuri” ni sifa inayopatika sana katika mitindo ya kisasa ya mavazi ya wanawake katika sehemu za kwenu? Duniani pote wanaume na wanawake wanaweza kujibu kwa sauti kubwa wakisema “Sivyo!” Hata wakati kunapokuwa na mtindo wa kuvaa mavazi marefu, mara nyingi mavazi yanayovaliwa yanakuwa yasiyositiri yasiyo ya adabu nzuri. Labda wewe mwenyewe umeona hivyo.

Hivyo, basi, je! wanawake Wakristo wanapaswa kujitahidi kununua au kushona mavazi yanayopatana na sifa ya adabu nzuri? Elfu nyingi za wanawake mashahidi Wakristo wa Yehova katika mataifa mbalimbali wanajua kwamba huo ndio mwenendo unaopendekezwa. Ingawa wanajitahidi kuwa malidadi na wenye kuvutia katika kujipamba kwao, wanaacha kufikiri kwao kuongozwe na kanuni iliyoongozwa na Mungu inayosema kwamba wanawake Wakristo wanapaswa “wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi.”​—1 Tim. 2:9.

Afisi ya tawi ya Watch Tower Society katika Puerto Rico ilipokea barua yenye kupendeza kuhusu jambo hili kutoka kwa Shahidi kijana. Ilisema hivi:

Juzi tuliona jambo lililotufurahisha kweli kweli, na ninataka kuwasimulia. Mimi pamoja na dada wengine wawili vijana tulikuwa tukitembea barabarani ya mji tukielekea katika kazi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba wakati mwanamume mmoja alipotusimamisha. Mwanzoni hatukutaka kusimama kwa sababu hatukujua kusudi lake, lakini kwa sababu alisisitiza, tulisimama ili tujue alikuwa akitaka nini. Alisema: ‘Nataka kumpongeza kwa sababu ya namna mnavyovalia.’ Tulimweleza kwamba sisi tu Mashahidi wa Yehova wa Kikristo na kwamba Biblia inasema kwamba tunapaswa kuvalia katika adabu nzuri, kwa hiyo sisi tunafanya hivyo. ‘Ni kwa sababu hiyo ninataka kumpongeza,’ akasema yule mwanamume, ‘kwa sababu dini yangu ni Evangelist, lakini mimi ninaona kwamba ninyi ndio watu peke yao wanaovalia vizuri kulingana na Biblia.’ Kwa hiyo tunataka kuwaambia namna tulivyo na furaha na tunavyoshukuru kwa sababu ya shauri zuri la Biblia juu ya vile tunavyopaswa kuvalia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki