Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w78 5/1 kur. 22-23
  • Maswali Kutoka Kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka Kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Heshimu “Kile Ambacho Mungu Ameunganisha”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
w78 5/1 kur. 22-23

Maswali Kutoka Kwa Wasomaji

● Mume wangu asiyeamini alikubali kwamba ana mwanamke mwingine. Je! kukubali kwake hivyo ni msingi unaotosha wa talaka kulingana na Maandiko?

Nyakati nyingine mwenzi asiyeamini wa Mkristo akikubali kwamba amefanya uasherati, huo ungekuwa msingi wa talaka unaolingana na Maandiko, na hapo Mkristo asiye na hatia angekuwa na uhuru wa kuoa au kuolewa tena.

Sheria ambayo Yehova Mungu alilipa taifa la kale la Israeli iliruhusu kuwe na talaka kwa sababu mbalimbali. (Kum. 24:1, 2) Sababu zilizofanya ndoa imalizwe ni uzinzi, hali ya mwanamume kulala mwenzake au mwanamke kulala mwenzake, vilevile kulalana na mnyama; mwenye hatia alipaswa kuuawa. (Kum. 22:22-24; Law. 18:22, 23) Lakini, Torati iliweka takwa hili la maana: “Huyo atakayeuawa na auawe kwa midomo ya mashahidi watatu; asiuawe kwa mdomo wa shahidi mmoja.” (Kum. 17:6; 19:15; Hes. 35:30) Kwa kuwa Yehova “huzipenda haki na hukumu,” alitaka mambo hayo yaamuliwe kwa kuhakikishwa na mashahidi, si kwa kuwa na shuku tu. (Zab. 33:5) Bila shaka, maneno hayo yalitajwa kuhusiana na adhabu ya kifo, si kuhusiana na talaka.

Hali nyingine iliyoshughulikiwa katika Torati pia inaonyesha ubora wa kutoa uhakikisho. Mwanamume alipaswa kufanya nini akishuku kwamba mkewe alikuwa amefanya uzinzi lakini akaukana na mashahidi wakawa hawapatikani? Sheria ya Mungu ilionyesha hatua iliyopasa kuchukuliwa, lakini ilikuwa hatua kubwa ambayo ingemletea mke matokeo ya daima akionekana kuwa mwenye hatia na mume vivyo hivyo mkewe akionekana hana hatia. Mke huyo angeweza kuletwa mbele ya kuhani na kuagizwa afuate mpango uliowekwa wa kunywa maji fulani ya pekee. Ikiwa alikuwa mwenye hatia, angepata adhabu ya kimungu ya ‘kupooza paja,’ na inaelekea maana ya maneno hayo ni kwamba uke wake ungepooza apoteze uwezo wake wa kuzaa. (Hes. 5:12-31) Ingawa mke huyo mzinzi alipata adhabu hiyo kubwa sana kutoka kwa Mungu, hakuuawa kwa sababu alikana kwamba hakuwa na hatia tena hawakupatikana wale mashahidi wawili waliotakiwa.

Mambo yakoje leo katika kundi la Kikristo? Je! inawezekana kupata ushuhuda wa kutosha uwe msingi wa talaka inayolingana na Maandiko?

Yesu mwenyewe alisema kwamba msingi wa pekee wa talaka kwa wafuasi wake, ambao ungempa mtu uhuru wa kuoa au kuolewa tena, ni kama mwenzi wake alifanya porneia, uasherati mbaya sana unaohusu viungo vya uzazi. (Mt. 19:9) Je! kungekuwa na msingi wa kutosha wa talaka mke Mkristo akishuku tu kwamba mumewe ana hatia ya uzinzi? Hapana, kwa maana Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo yanaitaja pia ile kanuni ya kuhakikishwa kwa jambo na mashahidi wawili au watatu, kama itakiwavyo katika hukumu iliyosawazika. (Yohana 8:17, 18; 1 Tim. 5:19; Ebr. 10:28) Kwa hiyo, mke akimshuku mumewe kwamba amefanya uzinzi, lakini mume akane na wasipatikane mashahidi wo wote kuhakikisha jambo hilo, asingekuwa na msingi wa kutosha kuhakikishia kundi la Kikristo kwamba ana haki ya kumtaliki mumewe na kuwa huru aolewe tena.

Lakini, nyakati nyingine mwenzi asiyeamini anakubali kwamba ni mwasherati. Kwa mfano, huenda mume hata akajivuna kwamba amefanya uasherati ili amtese mkewe. Mke akitaka anaweza kuuachilia upotovu wake. Lakini namna gani akiona kwamba hawezi au hapaswi kuuachilia? Je! kukubali kwa mume ni uhakikisho unaotosha?

Katika hali hiyo mume haonekani kama anasema yeye ni safi au kama anakana kabisa kwamba hana hatia ya uzinzi. Bali, anakubali na kumwambia mkewe kwamba ameufanya, lakini hawezi kukubali jambo hilo mahakmani au mbele ya watu wengine asije akajiharibia sifa. Mke anaweza kufanya nini hapo?

Kwa kuwa yeye ni sehemu ya kundi la Kikristo lililo safi, inampasa ajue kwamba ni jambo la maana kushughulikia jambo hilo inavyofaa ili kusiwe na mashaka juu ya kama yeye anaweka ‘malazi yake yawe safi’ akiolewa tena baada ya kumtaliki mumewe. (Ebr. 13:4) Kwa kusudi hilo anaweza kuwapa wazee wanaoliwakilisha kundi barua yenye kueleza hali yake, yenye kutaja kwamba mumewe asiyeamini amemwambia kwamba alifanya uasherati. Tena anaweza kutaja kwamba kulingana na Mathayo 19:9 anataka kumwondolea mbali, apate talaka kisheria na hivyo aimalize ndoa kulingana na Maandiko na sheria.

Wazee watafikiria kama kuna sababu yo yote ya kuonyesha kwamba mwenzi asiyeamini hakufanya uasherati. Isipokuwako, wanaweza kuikubali taarifa iliyotiwa sahihi na mke.

‘Lakini,’ huenda mtu akasema, ‘je! hakuna uwezekano wa kutoa taarifa ya udanganyifu, isiyo ya kweli, yenye kusema kwamba mumewe alimwambia amefanya uasherati na kumbe hakusema hivyo?’ Mtu ye yote angekuwa amefanya udanganyifu mbaya sana akijaribu kufanya hivyo. Wakati mmoja Daudi alisali hivi: “Umenichunguza moyo wangu, umefanya ukaguzi wakati wa usiku, umenitakasa; utagundua kwamba mimi sikufanya mpango wa hila.” (Zab. 17:3, NW) Kwa upande mwingine, Yehova anajua sana wakati mtu anapofanya hila, Naye atahakikisha kwamba mtu huyo hafaulu milele. Kwa hiyo, mwanamke Mkristo akiandika taarifa yenye kusema kwamba mumewe amekubali kwamba alifanya uasherati, Yehova anajua ukweli wa jambo hilo. Ni kama vile Biblia isemavyo: “Hakuna kiumbe kisichokuwa wazi mbele zake, lakini vitu vyote vi utupu na kufunuliwa machoni pake yeye aliye na mambo yetu.”​—Ebr. 4:13; Mit. 5:21; Yer. 16:17.

Kwa hiyo ikiwa hakuna sababu ya kuona mashaka juu ya taarifa ya mke, wazee wa kundi wanaweza kuliacha jambo hilo kati yake na Yehova. Hapo itamlazimu achukue daraka mbele za Mungu juu ya kama kweli mumewe amefanya uasherati, ambao ndio msingi unaolingana na Maandiko wa kumaliza ndoa hata ikiwa talaka imepatikana kisheria kwa msingi mwingine.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki