Elimu ya Uzima
MWALIMU katika Ecuador ameongoza funzo la Biblia kwa wanafunzi zaidi ya 200 kwa ukawaida katika shule yake. Kabla ya kuanza kipindi cha shule, aliwaeleza wazazi wote jambo alilofikiria kufanya akawauliza kama kuna ye yote anayepinga. Hakukuwa hata mmoja aliyepinga—kwa kweli, wengine walisema kwamba walifurahia kuona watoto wao wakifundishwa mwenendo na mazoea mema. Shule hiyo ina madarasa kuanzia la pili mpaka la sita, kwa hiyo wanafunzi wa madarasa kuanzia la pili mpaka la nne walipewa kitabu “Kumsikiliza Mwalimu Mkuu,” lakini darasa la tano na sita walipata kitabu chenye mafundisho magumu zaidi “Your Youth—Getting the Best out of It.” Mafunzo yanaongozwa vikundi vikundi, kama vile masomo ya kawaida darasani, lakini mafunzo yanaanzwa na kufungwa kwa sala, kama katika funzo la Biblia la nyumbani.