Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 4/1 kur. 23-24
  • Ufahamu Katika Habari

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ufahamu Katika Habari
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “Jina Jipya Lahitajiwa”
  • Musumbiji​—Ufahamu wa Mtawa wa Kike
  • Uangalizi wa Wazazi ni wa Muhimu Sana
  • “Testamenti ya Kale” au “Maandiko ya Kiebrania”—Jipi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Mashahidi wa Yehova na Yale Maangamizi Makubwa ya Wayahudi—Biblia Inasema Nini?
    Habari Zaidi
  • Kwa Nini Wayahudi Wengi Waliuawa? Kwa Nini Mungu Hakuzuia?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Mamilioni Waliuawa—Je, Itatokea Tena?
    Amkeni!—2001
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 4/1 kur. 23-24

Ufahamu Katika Habari

“Jina Jipya Lahitajiwa”

● Kwa karne nyingi dini za Kikatoliki na za Kiprotestanti zimetumia majina “Agano la Kale” na “Agano Jipya” kumaanisha sehemu za Biblia za lugha ya Kiebrania na ya Kigiriki. Juu ya hili; gazeti “National Catholic Reporter” lilisema karibuni hivi: “Jina ‘Agano la Kale’ hutokeza wazo la hali ya chini na ya ukale,” kwa hiyo “jina mpya lahitajiwa.”‏

Hiyo ni kweli, kwa kuwa Neno la Mungu lasema: “Kila andiko [ni] lenye pumzi ya Mungu, [na] lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza.” (2 Tim. 3:16) Kwa hiyo Biblia ni kitabu kimoja kikamilifu. Ujumbe wake unapatana kutoka mwanzo mpaka mwisho. Maandiko ya Kiebrania ndio msingi wa Maandiko ya Kigiriki. Yote mawili yana unabii unaotimizwa katika siku zetu, au ambao utatimizwa katika wakati ujao. Hakuna sehemu iliyo ya kikale, au iliyo “kuukuu.”

Gazeti hilo la Kikatoliki linapendekeza hivi: “‘Maandiko ya Kiebrania’ . . . linafaa zaidi sana kuliko ‘Agano la Kale.’” Vilevile linapendekeza jina “Maandiko ya Kikristo” kwa sehemu ya Kigiriki.

Mashahidi wa Yehova wamekuwa na maoni hayo kwa muda mrefu. Ndiyo sababu katika tafsiri yao “New World Translation of the Holy Scriptures,” na katika vitabu vyao vyote na magazeti, wamekuwa wakitumia majina “Maandiko ya Kiebrania” na “Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo” kwa sehemu hizo za Biblia.

Musumbiji​—Ufahamu wa Mtawa wa Kike

● Kushikilia kanuni bila kugeuka-geuka kunaweza kuvutia hata watu walio na maoni tofauti. Mtawa wa kike wa Rumi Katoliki aliandika katika gazeti “Andare alle genti” la Ukatoliki wa Kireno juu ya aliyoona kwa Mashahidi wa Yehova katika Musumbiji. Mtawa huyu wa kike, Dalmazia Colombo, alisema kwamba Mashahidi “wanapelekwa hata katika uhamisho wa watu wengi kwa sababu ya kukataa kujiingiza katika matengenezo fulani ya kisiasa.”‏ Anaendelea [kusema] hivi:

Kwa kweli, katika [mwaka] 1972 nilipokuwa Mecanhela (katika jimbo la askofu la Lichinga) niliona elfu kumi yao waliokuwa wamefukuzwa kutoka Malawi na walikuwa wakitafuta njia ya kukaa Musumbiji. Mimi ningali naweza kukumbuka vizuri sana namna wao walivyofika wakiwa vikundi-vikundi, wakiwa wamechoka na wakiwa wamevikwa kimaskini, watoto wao wakiwa pamoja nao, wamebeba vyombo vya nyumbani vichache tu na Biblia zao. Mimi ningali naweza kuwaona wamekaa chini ya miti kwa muda wa siku nyingi, wakiwa na uvumilivu, utulivu . . . wakingojea wenye mamlaka wawaruhusu kupata kisehemu cha ardhi ili waanze maisha tena.”

“Miaka kadha imepita tangu wakati huo na kwa mara nyingine nyakati zimekuwa zenye magumu kwa Mashahidi wa Yehova. Sasa hivi, katika ‘Gulag’ [kambi za mateso] hizi mpya za kuelimishia [watu] tenu zilizoanzishwa katika [Musumbiji], Mashahidi wa Yehova 25,000 kutoka Malawi na Musumbiji wamefungiwa pamoja [humo].’

“Kuna ukweli katika mengi ya mambo wasemayo na wanastahili sifa yetu . . . Lo! namna ulimwengu ungalikuwa tofauti ikiwa sote tungeamka asubuhi moja tukiwa tumeamua kabisa kutochukua silaha tena, bila kujali hasara au sababu gani, kama vile Mashahidi wa Yehova! . . . Ingekuwaje ikiwa kwa sababu ya imani yao wote wanaomwamini Mungu wangekuwa na nia ya kukusanya mali zao zote za kilimwengu katika mfuko mmoja tu na kungojea pamoja wakiwa na wake na watoto wao kandokando ya barabara mpaka gari la Gulag lije na kuwachukua (hii imetukia hapa mimi nikiona kwa macho yangu); kungalikuwa na sababu yo yote ya mateso zaidi ya kidini? Bila shaka ulimwengu haungegeuzwa uwe kambi ya mateso bali, tofauti yake, [ungekuwa] makao ya kufundishia yaliyo wazi kwa wenye kujitolea kwa ajili ya shule ya Kristo mwenyewe wasiotumia jeuri.”

Uangalizi wa Wazazi ni wa Muhimu Sana

● Katika mkutano wa wataalama wa utunzaji wa watoto katika Canada, Dakt. John Bowlby, akitoa hotuba ya utangulizi, alisema hivi: “Watoto wengi wanaachiliwa sana na wazazi wao ambao wanawapa uhuru mwingi kupita kiasi na hali ya kujitegemea.”‏ Alisema kwamba mambo kama vile kambi za watoto, vituo vya kutunzia watoto mchana pamoja na mayaya yaliongeza tu ule mtengano wa watoto na wazazi. Yote hayo, akasema Bowlby, yalileta “hali zisizofaa kwa maisha ya jamaa,” nayo yamekuwa na matokeo yenye msiba kwa watoto wengi.

Uchunguzi uliofanywa huko Chicago wa vijana matineja (umri wa miaka kati ya 13-19) na wazazi wao vilevile ulionyesha namna uangalizi wa wazazi ulivyo jambo la muhimu sana katika ukuzi wa watoto. Katika uchunguzi huo matineja waliangaliwa kwa muda wa miaka mitano, tangu umri wa miaka 12 mpaka miaka 17. Mwishowe, ushuhuda ulikuwa “wenye nguvu sana” kwamba wale wa miaka 17 waliokuwa wenye urafiki, wenye usawa zaidi, wenye matokeo, na waliothaminiwa sana na wengine walikuwa wale ambao wazazi wao walikuwa wametumia muda mwingi sana pamoja nao.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki