Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 1/1 kur. 22-23
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Habari Zinazolingana
  • Ni Mambo Gani Yanayochafua Mtu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Ni Mambo Gani Yanayochafua Mtu?
    Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Ni Nini Hasa Kinachomchafua Mtu?
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Marko ‘Mwenye Faida kwa Ajili ya Huduma’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 1/1 kur. 22-23

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

● Ni jambo gani linalomaanishwa katika Marko 7:19 tusomapo: “Kwa kusema hivi [Yesu] alivitakasa vyakula vyote.”?

Kwa msingi, jambo linalomaanishwa ni kwamba mtu hachafuliwi kiroho na vitu anavyokula, kama vile kula chakula pasipo kunawa mikono kulingana na kawaida za kidini.

Kama maneno yanayozunguka Marko 7:19 yanavyoonyesha, Mafarisayo na waandishi walikuwa wamemlaumu Yesu kwa sababu wanafunzi wake walikuwa “wakila chakula kwa mikono najisi, yaani, isiyonawiwa,” hali viongozi wa kidini ‘hawakula chakula wasiponawa mikono mpaka kiwiko.’ (Marko 7:l-3) Yesu aliwalaumu kwa kushikilia mapokeo ya wanadamu huku wakidharau kanuni nzito zaidi za Mungu, kama vile kuwaangalia wazazi wao. Aliendelea kusema hivi: “Hakuna kitu kilicho nje ya mtu ambacho kikimwingia chaweza kumtia unajisi, bali vile vimtokavyo, ndivyo vimtiavyo unajisi yule mtu.”​—Marko 7:5-15.

Ndipo wanafunzi wa Kristo walipomwuliza alivyokuwa akimaanisha. Habari ya Marko inaendelea kusema: “[Yesu] akawaambia, , . . Hamfahamu ya kwamba kila kitu kilicho nje ya mtu, kikimwingia, hakiwezi kumtia unajisi; kwa sababu hakimwingii moyoni, ila tumboni tu; kisha chatoka kwenda chooni? Kwa kusema hivi alivitakasa vyakula vyote.”​—Marko 7:18, 19.

Katika sehemu ya mwisho ya mstari wa 19 sarufi zimepangwa katika njia isiyo ya kawaida katika Kigiriki cha asili, walakini watafsiri wengi wamefahamu kwamba hayo yalikuwa maneno ya maelezo yaliyoongezwa na mwandikaji Marko. Lakini kwa sababu gani Marko aongeze: “Kwa kusema hivi alivitakasa vyakula vyote”?

Maelezo ya Marko yangekuwa kwa sababu ya hali iliyokuwako wakati Yesu alipokuwa akisema yale aliyoyasema. Wakati huo torati ya Musa ilikuwa bado inafuatwa, hivi kwamba chakula fulani, kama ‘vile nyama ya nguruwe, vilikuwa “najisi” kwa watumishi wa Mungu. Hali iliendelea kuwa hivyo mpaka wakati kifo cha Yesu kilipokomesha Torati pamoja na vizuizi vyake juu ya chakula najisi na kisicho najisi. Linganisha Mambo ya Walawi sura ya 11; Wakolosai 2:13, 14; Matendo 10:9-16.

Kwa hiyo, bila shaka Marko alikuwa akiongea juu ya chakula kilichokuwa “safi” kulingana na torati ya Musa’ iliyokuwa ikitumika wakati huo. Viongozi hao wa kidini walioshikilia sana mapokeo waliona kwamba kula hata chakula kama hicho wangetiwa unajisi ikiwa hawakufuata kwanza kawaida nyingi za kujitakasa. Nao walijaribu kutwika waamini wote kawaida hizi ambazo hazikuwa sehemu ya sheria ya Mungu bali yalikuwa mapokeo tu ya wanadamu. Kwa hiyo, Yesu alipoonyesha makosa ya kufikiri huku kwa viongozi wa kidini, Marko angeweza kwa kufaa kuongeza maelezo kuhusu maana ya yale yaliyosemwa na Yesu. Ndiyo, chakula kilichoruhusiwa na torati ya Musa hakingemnajisi mwenye kukila ati kwa sababu tu alikuwa hajanawa mikono kulingana na kawaida za kidini.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki