Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w80 8/15 kur. 20-22
  • Ngono Bila Ndoa—Sababu Inaumiza

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ngono Bila Ndoa—Sababu Inaumiza
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • TAMAA YA UPENDO WA NDOA
  • YAFIKIRIE MASHAKA YA MAISHA
  • NI JAMBO LA KUMPENDEZA MUNGU
  • KUEPUKA MATATIZO YENYE KULETA UCHUNGU
  • JE! UNAHITAJI MSAADA
  • Je, Kweli Unathamini Zawadi ya Mungu ya Ndoa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Vijana, Je! Mwenendo Safi Unaosemwa na Biblia Ndiyo Njia Bora?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Maoni Yako Juu ya Ngono—Yanafanyiza Tofauti Gani?
    Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?
  • Acheni Yehova Aimarishe na Kulinda Ndoa Yenu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
w80 8/15 kur. 20-22

Ngono Bila Ndoa—Sababu Inaumiza

UVUTANO wa ngono unaweza kuwa wenye nguvu sana. Kwa wazi Muumba aliuweka katika wanadamu ili kufanya ndoa iwe kifungo kinachofungamanisha chenye kuleta furaha.

Watu wengine wanaweza kuchekelea kwa dhihaka wazo la kwamba inaumiza kushiriki katika ngono kwa watu wasiooana. Wanaweza kuuliza ni umizo gani linalopata miili yao wanapotenda kulingana na tamaa hizo nje ya ndoa. Lakini je! wao wanasahau wakoje ndani ya miili yao? Je! hawana utu, akili yenye kufikiria na moyo wenye kutamani upendo wa kweli na usalama? Uchungu wa ndani unaotokana na kuachwa na mpenzi wa muda unaweza kuumiza kwa miaka mingi. Vilevile, kuharibika kwa akili kwaweza kutokea, nako huko hakuwezi kuendeleza afya na furaha. Watu wanazidi kufahamu kwamba kutumia viungo vya uzazi nje ya ndoa hakuleti uradhi na furaha yenye kudumu.

TAMAA YA UPENDO WA NDOA

Wakati wa kufanya ngono mara ya kwanza, mke hubadilika mwilini na utu wake hubadilika pia. Inawezekana kwamba wakati alipokuwa bikira, alitamani rafiki-mvulana, mtu wa kusema naye na “wa kutegemea.”‏ Walakini, baada ya kufanya ngono, mwanamke huanza “kutamani mwanamume,” kwa maana nyingine ya neno hilo. Yehova Mungu, akiwa Muumba aliliita jambo hilo ‘kutamani mume wake.’​—Mwa. 3:16.

Msichana ambaye anatazamia sana kuolewa yumo hatarini ya kumpa rafikiye mvulana uhuru mwingi sana juu yake. Akiwa anaogopa kumpoteza rafiki huyo, anaweza kujaribu kumfunganisha naye kwa uchumba usiofaa. Lakini, nyie wasichana, tafadhalini jiulizeni hivi: ‘Je! namfunga na nini?’ Fikiria. Je! yeye anapendezwa kikweli na utu wako na sifa zako za akili na maono yako ya ndani yanayofaa? Au, mahali pake, yeye angekuacha iwapo huendelei kushiriki pamoja naye ngono? Wanawake wanaoshindwa na tamaa za uasherati wanaweza kuwavutia wenzi wao kwa muda mrefu kadiri gani? Muda ule ule kama mwanamke asiye na adili asivyoweza kuvuta fikira na kuamsha nyege za “rafiki” zake wasiojali. Kisha ni nani anayeachwa akiwa ameumizwa sana? Katika njia iyo hiyo, je! kijana mwanamume anayemfanyia rafikiye msichana mambo ya uasherati anaweza kutazamia kuheshimiwa naye katika maisha ya baadaye?

Maandiko yanaonyesha kwamba “waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu” mbaya. (Ebr. 13:4) Ni jambo gani linaloweza kuumiza zaidi ya hilo? Vilevile, kumbuka kwamba tendo moja la uasherati laweza kuharibu njia yote ya maisha ya mtu ambaye wakati mmoja alikuwa mtumishi wa Mungu mwenye furaha. Nalo jambo hilo haliwezi kurekebishwa na ndoa ya haraka-haraka. Kama vile mikwaruzo juu ya sahani ya santuri inavyoharibu muziki usifurahiwe kabisa, vivyo hivyo ndivyo amani na furaha kamili ya ndoa yenyewe inavyoweza kuharibiwa na ngono za wakati uliopita.

YAFIKIRIE MASHAKA YA MAISHA

Huenda wengine wakasema hivi: ‘Kuna ubaya gani tunapojiruhusu kufanya mambo fulani ya ngono nje ya ndoa? Tuna hakika kwamba tutaoana nasi twaamini kwamba sisi si wagonjwa kwa habari ya kuwa na magonjwa ya kisonono na kaswende.’

Walakini fikiria kwa dakika moja. Je! sisi tukiwa hatujakamilika na tukiwa wenye kufa, twaweza kusema wakati wo wote, ‘Tuna hakika kwamba tutaoana’? Je! sheria hii iliyoamriwa haitupasi sote, “Wakati na tukio lisilotazamiwa huwapata wote”? (Mhu. 9:11, NW) Wenzi wawili wanawezaje kuwa na hakika kwamba wataoana? Jambo kubwa wawezalo ni kutumainia kuweza kufanya hivyo. Ndugu mzazi mmoja na Yesu alionya kwa upole hivi: “Haya basi, ninyi msemao, Leo au kesho tutaingia mji fulani na kukaa humo mwaka mzima, na kufanya biashara na kupata faida; walakini hamjui yatakayokuwako kesho. . . . Badala [yake semeni], [Yehova] akipenda, tutakuwa hai na kufanya hivi au hivi.”—Yak. 4:13-15.

NI JAMBO LA KUMPENDEZA MUNGU

Vilevile, je! lingekuwa jambo la akili kuomba baraka ya Yehova juu ya jitihada zetu za kuwa na ndoa yenye furaha na wakati ule ule kuingia katika mwenendo ambao ‘Msikiaji wa sala’ analaumu? (Zab. 65:2, NW) Bila shaka, twapaswa kuamini kabisa kwamba matendo fulani yanalaumiwa na Mungu. Basi, bila shaka akitaja vitendo vichafu vya kufanya ngono, Yesu alitaja “ufisadi” kuwa kati ya mambo “maovu” mbalimbali. (Marko 7:22, 23) Mtume Paulo alisema kwamba wale wanaofanya “matendo ya mwili,” kama vile “uasherati, uchafu, ufisadi,” kwa hakika “hawataurithi ufalme wa Mungu.”‏ (Gal. 5:19-21) Bila shaka semi hizo haziachi shaka lo lote juu ya mawazo ya Yehova juu ya jambo hilo, sivyo?

Vitendo vya kufanya ngono nje ya ndoa humchafua mwanamume na mwanamke. Bila shaka, hayo ndiyo maoni ya Yehova Mungu. Kama sivyo, asingekataza watu ambao hawajaoana wasifanye ngono. (Linganisha 1 Wakorintho 7:1, 2.) Pamoja na hayo, Mwenye Enzi Kuu ya Ulimwengu Wote hawakubali watu wenye pupa na wasio na utaratibu. (1 Kor. 6:9, 10; 14:33) Kwa kuwa yeye ameweka sheria za adili zilizo za lazima katika maisha ya wanadamu, sheria hizo zinapaswa kufuatwa iwapo tutampendeza Muumba wetu na kufurahia kikweli. Mwendo mwingine wo wote utatuumiza.

Kutoa ahadi ya kuoana, au kujitayarisha kuoana, ni jambo tofauti na ndoa iliyofanywa tayari, ama sivyo? Basi fikiria: Ungemwonaje mtu ambaye hajawekwa kama mwangalizi katika kundi la Kikristo lakini anayejaribu kujichukulia cheo cha mzee? Yeye angekuwa mtu mwenye kiburi. Na ni mambo gani yaliyowapata watu fulani wa nyakati za zamani ambao kwa kiburi walikimbia mbele ya Yehova wala hawakumngojea? Je! waliumizwa? Ndiyo, pindi nyingine hata kufikia kufa, wakati huo au baadaye. (1 Sam. 15:22, 23; 2 Sam. 6:6, 7; 2 Nya. 26:16-21) Hakika, hakuna mtu ye yote mwenye kumcha Mungu ambaye angependa kutenda kwa kiburi kwa kuwa na uhusiano wa kimwili unaokatazwa na Yehova, au kwa kushiriki katika vitendo vya urafiki vinavyoshirikishwa na ndoa kabla ya kuoana.​—Efe. 5:3.

KUEPUKA MATATIZO YENYE KULETA UCHUNGU

Heshima, kuheshimiana sana ndiyo mojawapo ya nguzo kubwa za ndoa yenye furaha. (Efe. 5:33; 1 Pet. 3:7) Walakini wenzi wawili waliochumbiana wanaweza kusitawishaje kuheshimiana kikweli ikiwa wote wanaona na kufahamu kwamba wamekuwa na mwenendo wenye pupa na wa uasherati? Je! jambo hilo linatokeza uhakika? Sivyo, kwa kuwa wivu mwingi katika ndoa unaletwa na mambo mabaya kati ya mtu na mwenzake kabla ya kufunga ndoa. Je! mke aliyeshuka moyo hawezi kusema miaka mingi baadaye: “Ulikuwa unataka mwanamke tu, si mimi”? Naye mume anaweza kuthibitishaje kwamba si ndivyo ilivyo? Hawezi. Basi, mwanamume anaweza kuthibitishaje anampenda kweli kweli mwanamke fulani kabla ya ndoa? Kwa kuheshimu usafi wake. Kwa njia hiyo anaonyesha upendo wake usio na choyo kwa mke wake wa wakati ujao. Vilevile anaonyesha kwamba anatimiza ahadi zake. Pengine alikuwa ameahidi baba ya msichana huyo kwamba asingemgusa kwa njia mbaya. Lingekuwa jambo la aibu kama nini ikiwa angelazimika kukiri kwamba amemtia mimba binti ya mtu huyo! Je! hicho kingekuwa chanzo kizuri cha ndoa?

Matatizo yenye kuleta uchungu yanaweza kuepukwa na wazazi, hata na wenzi waliochumbiana, kwa kulifikiria jambo hilo kwa njia ya sala. Jambo hilo ni la maana sana katika ulimwengu huu uliopo ulioshuka sana adili. Kanuni za adili kama zilivyowekwa na Mungu hazijapata kuelekeana na mashambulio mengi sana kama yale ya siku zetu. Hakika Biblia yapaswa kuwa uongozi wa kila siku kwa habari ya rafiki, uchumba na ndoa. Sababu gani? Maandiko yanajibu hivi: “Tangu sasa msienende kama Mataifa waenendavyo, katika ubatili wa nia zao; ambao akili zao zimetiwa giza, nao [wametenganishwa] na uzima wa Mungu.”‏ Watu wengi ‘wamekwisha kufa ganzi,’ nao wanajitia “katika mambo ya ufisadi wapate kufanyiza kila namna ya uchafu kwa kutamani.”‏ Walakini mtume Paulo aliwasihi waamini wenzake ‘wavue utu wa kale unaofanana na namna ya mwenendo wenu wa zamani,”‏ na “kuvaa utu mpya ulioumbwa kulingana na mapenzi ya Mungu katika haki ya kweli na uaminifu.”‏ (Efe. 4:17-24) Ndiyo, fanya jambo hilo nawe waweza kuepuka uchungu na msiba ambao hauna budi kuwapata wale wanaoendelea kupuza kanuni za haki za Mungu.

JE! UNAHITAJI MSAADA

Iwapo ye yote ana tatizo kwa habari ya jambo hilo, lingekuwa jambo zuri kuzungumza na mmoja wa wazee waliowekwa katika kundi la Kikristo. Yeye yu katika hali ya kukusaidia kwa kufahamu. Mtu wa namna hiyo ni mzee au mwangalizi kwa sababu ya kuwa na sifa za kiroho, na bila shaka yeye ni mpigaji vita mwenye ujuzi juu ya tamaa zake mwenyewe za mwili, kama vile alivyokuwa mtume Paulo.​—1 Kor. 9:26, 27.

Vilevile, wenzi waliochumbiana wanaweza kuzungumza waziwazi wao kwa wao. Jambo hilo linaweza kutia nguvu nyote wawili katika uamuzi wenu imara wa kumpendeza Yehova. Kwa kusaidiana ili kujipatanisha na mapenzi ya kimungu, hakika hamtaumizwa. Mahali pake, nyote wawili mtafahamu furaha ya kweli inayofurahiwa na watumishi washikaminfu wa Mungu. Je! hilo si ndilo jambo unalotaka maishani?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki