Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 1/1 uku. 9
  • Hali Inayokubalika Mbele za Yehova

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Hali Inayokubalika Mbele za Yehova
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Habari Zinazolingana
  • Kifo cha Taifa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Je, Kutahiriwa Ni Ishara ya Kuwa Mtu Mzima?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Kitabu Cha Biblia Namba 30—Amosi
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 1/1 uku. 9

Hali Inayokubalika Mbele za Yehova

Uhakika wa kwamba huenda wakati mmoja mtu akawa alikuwa mpokeaji wa kibali ya kimungu hauthibitishi wenyewe kwamba ataendelea kuwa mtumishi wa Yehova mwenye kukubalika. Kwa mfano, Waisraeli, walikombolewa na utumwa katika Misri wakaingizwa kwenye nchi ya Kanaani. Hata hivyo, kule kuwa watu wa Mungu walioteuliwa hakukuwapatia uhusiano usioweza kubadilika pamoja na Aliye Juu Zaidi. Wakati walipogeukia ibada ya sanamu na kupuza sheria za Yehova katika njia nyinginezo, kule kuchaguliwa kwao na Yehova kwa sababu ya babu zao waliokuwa waaminifu kulipoteza maana. Kupitia kwa nabii wake Amosi, Mwenye Nguvu Zote alitangaza hivi: “Je! ninyi si kama wana wa Wakushi kwangu mimi, enyi wana wa Israeli, asema [Yehova]? Je! mimi sikuwapandisha Israeli toka nchi ya Misri, na Wafilisti toka Kaftori, na Washami toka Kiri?”​—Amosi 9:7.

Huenda Waisraeli wakawa walijisifu wenyewe kwa kuwa walikuwa wamechaguliwa na Mungu. Lakini kwa sababu ya kutokuaminika kwao, wao hawakuwa na hali bora zaidi pamoja na Yehova kuliko vile walivyokuwa Wakushi. Kwa kweli tohara yao haikuwa na maana yo yote. Karne nyingi baadaye, mtume Paulo alikazia jambo ilo hilo, akisema hivi: “Kwa maana kutahiriwa kwafaa kama ukiwa mtendaji wa sheria, lakini ukiwa mvunjaji wa sheria kutahiriwa kwako kumekuwa kutokutahiriwa.”​—Rum. 2:15.

Vivyo, hivyo, kule kutolewa Misri kwa Waisraeli kwenyewe hakukuwahakikishia kwamba wangeendelea kuwa na hali bora yenye kukubalika mbele za Yehova Mungu. Waisraeli wasioaminika hawakupata uhakikisho wa kuendelea kuwa na kibali ya kimungu ati kwa sababu babu zao walikombolewa Misri. Wala Wafilisti na Washami ati kwa sababu walikuwa wakiishi sehemu tofauti na zile walizoishi wakati wa mapema.

Jambo hilo linakazia kwa nguvu sana kwamba kuwa na hali yenye kukubalika mbele za Yehova Mungu hakutegemei taifa, kabila au jamaa ya mtu. Kule kudai tu kuwa mtumishi wa Aliye Juu Zaidi hakuna maana yo yote. Mtu huyo lazima awe ni yule anayefanya mapenzi ya Yehova Mungu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki