Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w80 1/15 kur. 16-19
  • Ezra Akazia Haki ya Hukumu na Rehema

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ezra Akazia Haki ya Hukumu na Rehema
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • HEKALU LAJENGWA UPYA KWA AJILI YA KUJA BAADAYE KWA MASIHI
  • MUNGU ATOA REHEMA NA MSAADA
  • REHEMA YA MUNGU, SI WEMA WA WAYAHUDI, YATIMIZA KUSUDI LAKE
  • Kitabu Cha Biblia Namba 15—Ezra
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Ezra
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Yehova Atimiza Ahadi Zake!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Dumisha Uhakika Katika Yehova Unapokabili Changamoto Zisizotarajiwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2023
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
w80 1/15 kur. 16-19

Ezra Akazia Haki ya Hukumu na Rehema

NI MUUMBA peke yake, mwenye hekima yote na maarifa kamili ya kila sehemu ya uumbaji wake, pamoja na uweza wote, ndiye angeweza kufanya sifa zake mwenyewe za haki ya hukumu na rehema zifanye kazi kwa usawa kamili kwamba kusudi lake litekelezwe kikamilifu. Matokeo ya sifa hizi juu ya watu wenye kumtumikia zinawaongoza hata kwamba aliyoazimia kimbele yanafanywa hasa, yakiwafaidi wote wenye kuhusika.

Kitabu cha Biblia cha Ezra kinakazia ushirikiano huu mzuri wa kazi za Yehova, ambazo wakati wote hufanywa kwa kupatana na utu wake mtakatifu, bila kuachana wakati wo wote na makusudi yake mazuri na sifa zake zisizobadilika. Mtume Paulo, ambaye alizifahamu njia za Mungu, atuhakikishia hivi: “Mungu hufanya kazi zake zote zishirikiane kwa faida ya wale wampendao Mungu.”​—Rum. 8:28, NW.

Ezra alikuwa mzao wa Haruni, Eleazari na Finehasi, na kwa hiyo alikuwa kuhani, ingawa si wa nasaba ya kuhani mkuu, cheo ambacho wakati wote kilichukuliwa na mwana mzaliwa wa kwanza katika kila kizazi. (Ezra 7:1-6) Babu wa mwisho wa Ezra kuchukua cheo cha kuhani mkuu alikuwa Seraia (inaelekea baba ya babu yake), aliyeuawa na Nebukadreza wakati wa kutekwa kwa Yerusalemu. Ezra alirudi Yerusalemu katika mwaka 468 K.W;K., miaka 69 baada ya kurudi kwa Wayahudi 49,000, kutia na watumwa, toka Babeli chini ya uongozi wa Zerubabeli (aliyeitwa Sheshbaza) wa kabila la Yuda. (Neh. 7:66, 67) Hata hivyo, masimulizi ya Ezra, kwanza yanaripoti sehemu fulani za kurudi huku kwa mapema zaidi chini ya Zerubabeli kabla ya kutoa kwa urefu habari za mambo ya hakika ya ziara yake mwenyewe ya baadaye.

HEKALU LAJENGWA UPYA KWA AJILI YA KUJA BAADAYE KWA MASIHI

Hata ingawa Mungu alikuwa ameruhusu Babeli iwachukue watu wake kwenye uhamisho kwa sababu ya dhambi na uasi wao, iliharibu hekalu na kuufanya ukiwa mji wa Yerusalemu, yeye alikusudia hekalu na mji vijengwe upya. Sababu gani? Kusudi ahifadhi ibada ya kweli duniani. Lililo la maana zaidi, Masihi alikuwa bado yuaja. Ili kutimiza kusudi la Mungu kwa habari ya kufika kwake ilihitaji kwamba Yerusalemu uwepo, mji wenye kukaliwa na watu, ukiwa na hekalu la Yehova katikati yake (ingawa mahali pake palikuwa pamechukuliwa na jengo la tatu wakati huo, lililojengwa na Herode.) Pamoja na hayo, lilikuwa jambo la lazima kwamba sheria ya Mungu iwe nguvu yenye kuongoza nchini wakati wa kuja kwa Masihi, Huku kuja kwa Masihi kwenye mji uliojengwa upya wa Sayuni (Yerusalemu) kulitabiriwa na manabii.​—Dan. 9:25.

Mungu alifahamu mbeleni kwamba kungalikuwako watu wachache katika hali ya uhamisho katika Babeli ambao wangekuwa wangali wanampenda na ambao wangetaka kufanya wawezayo ili kurudisha ibada safi. Yeye angewatumia kwa ajili ya kusudi lake. Ingawa, kabla ya kuhamishwa huko, dhambi nyingi za watu hao zilifanya iwe lazima kwa Mungu mwenye haki ya hukumu awaondoe kutoka nchi hiyo, rehema zake zingeonyeshwa kwa hawa wachache. Ufahamu huu wa Mungu wa kimbele ulifunuliwa miaka 200 kabla wakati Isaya aliye nabii alipozungumza juu ya kuja kwa mfalme fulani, mkombozi, ambaye angeitwa Koreshi.​—Isa. 44:28; 45:1.

Koreshi Mwajemi alijifunza kumfahamu Yehova bila shaka. Danieli aliyekuwa nabii alikuwa na cheo cha juu chenye heshima wakati wa mwanzo-mwanzo wa utawala wa Koreshi. (Dan. 6:28) Bila shaka Danieli alimwonyesha kutajwa kwa kiunabii kwa jina lake katika unabii wa Isaya. Mwanafunzi mmoja wa Biblia anaeleza hivi:

“Andiko Takatifu linaonyesha kilichomvutia Koreshi, kwa kusimulia sehemu aliyotimiza Danieli wakati wa kupinduliwa kwa ufalme wa Babeli, [Dan. 5:28, 30]. Sababu gani ishangaze kwamba mtimizaji wa unabii huu alijiona moyoni kuvutwa kwa nabii aliyeutamka, na kwa kupenda angerudisha vyombo ambavyo usiku ule Belshaza alikuwa amefanya dhambi ya kuvichafua?”a

MUNGU ATOA REHEMA NA MSAADA

Akitambua kuwapo kwa miungu wengine, Koreshi asingekuwa na shida kumwona Yehova kuwa Mungu, aliye Mungu wa kweli, Mungu aliye mkuu, na Ambaye, kama alivyosema, alimpa “falme zote za dunia.”​—Ezra 1:2.

Rehema zilizo kuu za Mungu, uwezo wake na uhakika wa kusudi lake yanafunuliwa katika kubariki kwake hesabu ndogo sana ya watu waaminifu. Wengi wa Wayahudi katika Babeli walikuwa wamekuwa sehemu ya maisha ya kibiashara ya Babeli nao hawakupendezwa au walipendezwa kidogo sana na kurudisha ibada ya kweli. Hata hivyo, rehema za Mungu zilifanya kazi kwa waaminifu hao wachache. Wakiwa na nia ya kuendeleza ibada safi, hawa waliondoka Babeli wakafika Yerusalemu baada ya kufurahia ulinzi wa Mungu katika safari yenye hatari kupitia jangwa kavu. (Isa. 35:2-10) Wakiwa wamezungukwa na jirani wenye uadui, walimjengea Yehova madhabahu na kuanza kuweka msingi kwa ajili ya hekalu. Wasamaria walijitoa wajiunge nao katika kazi hiyo, wakijisingizia urafiki. Walakini kwa kuwa walikuwa wanajizoeza namna ya ibada iliyochafuliwa kujitoa kwao kulikataliwa na Zerubabeli.​—Ezra 4:1-4; 2 Fal. 17:29.

Mungu alikubaliana na msimamo huu uliochukuliwa na Waisraeli waliorudishwa, kwa kuwa, kushirikiana na watu hawa ingekuwa kujifunga “nira pamoja na wasioamini” katika ibada ya kweli, kujaribu kuleta mapatano kati ya hekalu la Mungu na sanamu. (2 Kor. 6:14-16) Hata hivyo, roho nzuri ya mabaki hawa waliorudishwa ilianza kusita-sita wakati rafiki hawa wa kujidai walipoanza kuleta matata kupitia kwa uvutano wao juu ya serikali ya Uajemi, wakawadhoofisha Wayahudi hao kufikia kiasi cha kuacha kujenga hekalu mwishowe.​—Ezra 4:8-24.

Katika wakati huu, kuhangaikia nyumba zao na mambo yao wenyewe kuliwafanya Wayahudi waiache nyumba ya Mungu ikae ukiwa. Walakini kusudi la Mungu lisingeshindwa. (Hag. 1:8, 9) Aliwatuma manabii Hagai na Zekaria ili warudishe akili zao kwenye kusudi ambalo kwa ajili yake walikuwa wamerudi Yerusalemu. Waliitikia na kujengwa kwa hekalu upya kukaendelea, hata kukiwapo upinzani. (Ezra 5:1, 2) Yehova alibariki kutii kwao kusiko na woga. Walipokata rufani kwa Mfalme Dario Mwajemi, maliwali wa majimbo yaliyokuwa kandokando waliamriwa waache kuwazuia Wayahudi na wawasaidie kutoka kwa hazina ya watu wote kwa msaada wo wote wa fedha wenye kuhitajika. Kwa toleo hili la fedha kutoka kwa Dario kazi ilimalizwa na hekalu likazinduliwa kwa furaha kuu.​—Ezra 6:6-12, 16-22.

REHEMA YA MUNGU, SI WEMA WA WAYAHUDI, YATIMIZA KUSUDI LAKE

Hata hivyo, kufaulu huku katika kurudisha ibada safi hakukutimizwa na wema wa Wayahudi waliorudishwa, walakini, mahali pake, kulifanyika kwa rehema ya Mungu katika kutimiza kusudi lake. Namna gani hivyo? Kwa sababu ilimlazimu amtume mtumishi wake Ezra. Ujapokuwa ufunuo ulio wazi wa rehema na ulinzi wa Mungu, Wayahudi waliorudishwa walikuwa wamevunja kanuni ile ambayo hapo mbeleni walikuwa wameishikilia imara, yaani, kujitenga na waabudu wa kipagani. Sasa walikuwa wameenda sana hata kuingia kwenye uhusiano wa karibu sana—ndoa—pamoja na wanawake wasioamini, wenye kuabudu sanamu. Hata makuhani, Walawi na wana wa wafalme waliangukia kwenye kutokutii huku kwenye dhambi kwa amri ya Mungu.​—Ezra 9:1, 2.

Kwa msomaji asiye wa kawaida, mambo ambayo Wayahudi hawa walifanya huenda yasionekane kuwa mabaya sana. Walakini fikiria: Iwapo hesabu hiyo ndogo ya Wayahudi waliorudi Yuda wangekuwa sehemu ya mataifa yenye kuwazunguka, ambayo kwa kweli yalimpinga Mungu wao na ibada yake yenye kuendeshwa hasa kwenye hekalu hilo, matokeo yangekuwa nini? Ibada safi ingetoweka kutoka duniani. Kwani, miaka michache tu baadaye, katika wakati wa Nehemia, watoto waliotokana na ndoa hizo hawakuweza kuzungumza Kiebrania!—Neh. 13:24.

Ezra aliweza kuona maana yenye kuogopesha sana ya kutokutii huku. Yeye aliketi ameduwaa kwa muda fulani. Kisha, mbele ya Wayahudi waliorudishwa wenye kukusanyika, alitoa sala ya hadharani, akiweka wazi uzito wa kufanya kwao dhambi na kukosa shukrani kwa matendo yao. Yeye aliomba hivi, katika sehemu moja:

“Kwa sababu ya maovu yetu sisi, na wafalme wetu, na makuhani wetu, tumetiwa katika mikono ya wafalme wa nchi hizi, tumepigwa kwa upanga, tumechukuliwa mateka, tumenyang’anywa mali zetu, tumetiwa haya nyuso zetu, kama hivi leo. Na sasa kwa muda kidogo tumenemeeshwa na [Yehova], Mungu wetu, hata akatuachia mabaki yaokoke, akatupa msumari katika mahali pake patakatifu. Mungu wetu atutie nuru machoni mwetu, . . . Na sasa, Ee Mungu wetu, tuseme nini baada ya hayo? maana tumeziacha amri zako, . . . baada ya hayo yote yaliyotupata kwa sababu ya matendo yetu mabaya, na kwa sababu ya hatia yetu iliyo kuu, . . . je! tuzivunje tena amri zako?”​—Ezra 9:7-14.

Kwa hiyo Ezra aliungama mbele za Mungu na watu wote kule kukosa shukrani na uovu wa wale ambao alikuwa ameonyesha rehema zisizo za kawaida. Yeye hakuomba msamaha wa dhambi, kwa sababu watu wenyewe walipaswa kutubu na kunyosha mambo kabla ya kutazamia hasira ya Mungu iwaondokee. Kwa kuona hali yao mbaya, watu hao waliitikia kwa mioyo yenye majuto. Waliwafukuza wake zao wa kigeni. Ndipo Mungu angeweza kuwasamehe na kuwahifadhi katika nchi hiyo.​—Ezra 10:44.

Kwa hiyo rehema za Mungu hazikuwekwa mahali pabaya. Vilevile, kujali kulikoonyeshwa kwa kuwatuma manabii wake Hagai na Zekaria, pamoja na uongozi aliotoa kupitia kwa Ezra, vilihifadhi ibada safi kwa wakati huo. Leo, kama vile katika wakati uliopita, watu wanaotafuta kumjua Mungu na kuja kwenye uhusiano wa karibu naye wanaweza kutumikia kwa ajili ya kusudi lake na kupata rehema na ulinzi wake.

[Maelezo ya Chini]

a Kitabu Biblical Commentary on the Old Testament, kilichoandikwa na Keil na Delitzsch, juu ya Ezra, Nehemia na Esta, uku. 24.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki