Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 9/1 kur. 10-15
  • Twende Kwa Nani Isipokuwa Kwa Yesu Kristo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Twende Kwa Nani Isipokuwa Kwa Yesu Kristo?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “NGUZO NA MSINGI WA KWELl”
  • KUMTHAMINI YEHOVA
  • “Sl SEHEMU YA ULIMWENGU”
  • KUANGALIA MBELE
  • MWENDO WA HEKIMA
  • ‘Wanaendelea Kumfuata Mwana-kondoo’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • “Mtumwa” Ambaye Ni Mwaminifu na Mwenye Busara
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • “Ni Nani kwa Kweli Mtumwa Mwaminifu na Mwenye Busara?”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Mtumwa Mwaminifu na Mwenye Busara Ni Nani?
    Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 9/1 kur. 10-15

Twende Kwa Nani Isipokuwa Kwa Yesu Kristo?

“Bwana! Twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele. Nasi tumesadiki, tena tumejua, ya kuwa wewe ndiwe Mtakatifu wa Mungu.”​—⁠Yohana 6:68, 69.

1, 2. (a) Kwa sababu ya yale yaliyosemwa na Yesu Kristo, sababu gani Wakristo hawana shaka juu ya yeye wanayepaswa kwenda kwake? (b) Mapema Yesu alikuwa amesema nini juu ya kupata uzima, kwa jamii gani mbili?

KATIKA kipindi hiki cha uamuzi cha historia ya rnwanadamu, hakuna shaka lo lote akilini mwetu kwamba tutaenda kwa nani. Njia imekwisha onyeshwa wazi kabisa kwetu. Akizungumza na wale walioendelea kukaa pamoja naye katika majaribu yake, Yesu alisema hivi: “Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.” (Yohana 14:6) Kwenye kipindi icho hicho, aliendejea kusema: “Mimi ndimi mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima. . . . Akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo ‘huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote.”​​—⁠Yohana 15:1, 5.

2 Namna maneno hayo ya Yesu yalivyothibitika kuwa kweli katika maisha ya mitume na wanafunzi wengine wa zamani! Vilevile, yalithibitika kuwa ya kweli katika siku yetu ya leo. Ingawa yalielekezwa kwa wale waliokuwa kwenye mstari wa kupata nafasi katika ufalme wa Mungu, yanasema kweli ambazo wanafunzi wote wa Kristo leo wanaweza kufaidika nazo. Mapema mwanzoni mwa huduma yake Yesu alikuwa ametangaza: “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.” (Yohana 3:16) Maneno haya yanatumika vilevile juu ya kondoo wote ambao Yesu alisema habari yao katika Yohana 10:16: “Na kondoo wengine ninao, ambao si wa zizi hili; na hao nao imenipasa kuwaleta; na sauti yangu wataisikia; kisha kutakuwako kundi moja na mchungaji mmoja.”

3. (a) Njia moja ambayo katika hiyo Yesu amekuwa pamoja na wafuasi wake ni njia gani? (b) Ni katika njia gani nyingine ambayo vilevile yeye amekuwa pamoja nao?

3 Kupitia kwa Yesu Kristo, Yehova Mungu amekwisha fanya mipango mingi ya kutuongoza katika nuru ya kweli yenye kuendelea rnbele, na matumaini ya uzima wa milele. Wakati mfupi tu kabla ya Yesu kupaa mbinguni, wanafunzi 500 hivi waliokusanyika Galilaya, walitiwa nguvu imani yao kwa maneno haya ya Yesu: “Na, tazama! mimi nipo pamoja na ninyi siku zote mpaka mwisho wa taratibu ya mambo.” (Mt. 28:20, NW; 1 Kor. 15:6) Yeye amekuwa pamoja nao namna gani? Kwa njia ya roho yake takatifu; lakini kwa njia nyingine pia. Alipokuwa akiwaambia juu ya kuwapo kwake na mwisho wa taratibu ya mambo, Yesu alihakikishia wanafunzi wake kwamba angemweka “mtumwa mwaminifu mwenye akili” ambaye angeangalia faida zake na kuwalisha wafuasi wake chakula kwa wakati unaofaa katika utaratibu wote wa Kikristo. Kwa kujihakikisha kuwa jaminifu, jamii ya “mtumwa” huyo ingewekwa na Yesu juu ya vitu vyake vyote wakati wa kuja kwake kwa mara ya pili. Ndiyo, kupitia kwa huyu “mtumwa mwaminifu mwenye akili,” Yesu amekuwa pamoja na wafuasi wake pia.​​—⁠Mt. 24:45-47.

“NGUZO NA MSINGI WA KWELl”

4. (a) Kwa kuwa Yesu ametimiza ahadi yake, ni jambo gani linaloweza kusemwa juu ya kundi lake? (b) Ni unabii gani wenye kutia moyo unaotimizwa katika wafuasi wa kweli wa Yesu leo?

4 Kwa kuwa Yesu Kristo amekuwa pamoja na wafuasi wake waliotiwa mafuta, kundi la Kikristo limekuwa kabisa kama vile mtume Paulo alilitamka kuwa, “nguzo na msingi wa kweli.” (1 Tim. 3:15) Limejidhihirisha kuwa na roho ya Mungu, kwa kuzaa matunda yake. (Gal. 5:22, 23) Katika hizi na katika njia nyingine nyingi zaidi, sisi mashahidi Wakristo wa Yehova tunasimama tukiwa tofauti kabisa na madhehebu yote mengine ya Jumuiya ya Wakristo, ambayo ni Israeli wa kiroho kwa jina tu. Kwa kuwa Yesu Kristo yu pamoja nasi, rnaneno yenye kutia moyo yanayopatikana katika Isaya 65:13, 14 yanapata utimizo juu yetu: “Tazama, watumishi wangu watakula, bali ninyi mtaona njaa; tazama, watumishi wangu watakunywa, bali ninyi mtaona kiu; tazama, watumishi wangu watafurahi, bali ninyi mtatahayarika; tazama, watumishi wangu wataimba kwa furaha ya moyo, bali ninyi mtalia kwa huzuni ya moyo; mtapiga kelele kwa sababu ya uchungu wa roho zenu.”

5, 6. (a) Pale mwanzoni-mwanzoni jamii ya “mtumwa” ilionyesha imani yake juu ya kweli gani mbili kuu? (b) Sababu gani wale wa Babeli Mkuu hawawezi kulithamini fundisho la ukombozi? (c) Fundisho la Wanafunzi wa Biblia juu ya kuja kwa Yesu kwa mara ya pili lilikuwa la pekee sana katika njia gani?

5 Kwa hakika, tofauti hii ilianza kuonekana wazi tangu mwanzomwanzo wa historia yetu ya kisasa. Wajumbe hawa wa “mtumwa mwaminifu mwenye akili” chini ya uongozi wa Yesu Kristo, walionyesha imani yao yenye nguvu katika Biblia kutia na habari ya Mwanzo ya uumbaji kuwa ni Neno la Yehova Mungu lililoongozwa naye, kama alivyofanya Yesu Kristo. (Mt. 4:4-10; 19:4-6) Fundisho la msingi lilikuwa juu ya kweli inayohusu ukombozi uliotolewa na kifo cha dhabihu cha Yesu Kristo, Mwana wa Mungu. (1 Tim. 2:5, 6) Hakuna ye yote katika Babeli Mkuu anayeweza kuthamini fundisho hili kwa sababu ya kuamini mafundisho yasiyo ya kimaandiko kama vile Utatu, kutokufa kwa Yesu aliishi akiwa Logos kabla ya kuwa nafsi, au kwa sababu ya kukana kwamba mwanadamu na kwamba alizaliwa na bikira.​​—⁠Mt. 1:23; Yohana 1:1.

6 Unaokamatana na kuthamini waziwazi fundisho la ukombozi ni ufahamu wa kusudi na namna ya kuja kwa mara ya pili na “kuwapo” kwa Kristo. Wale “Wanafunzi wa Biblia,” wenye bidii kama vile walivyojulikana Mashahidi wakati huo, ndio peke yao waliofahamu waziwazi tofauti kati ya mwanadamu Yesu Kristo aliyetoa bei ya ukombozi na mtu wa kiroho mwenye utukufu aliyefufuliwa, anayekuja tena kutawala bila kuonekana kwa macho ya kibinadamu akiwa Mfalme katika ufalme wa Mungu.​​—⁠Mt. 24:3, NW; 1 Pet. 3:18.

7. Ni maandiko gani na sababu gani huonyesha kwamba kuna makao ya namna mbili kwa wale wanaofaidika kutokana na ukombozi wa Kristo?

7 Vilevile, pale pale mwanzoni mwa historia yao ya kisasa, wanafunzi hawa wa Biblia waliona kwamba kunayo makao mara mbili kwa wale wanaofaidika kutokana na ukombozi wa Kristo, makao ya kimbinguni na ya kidunia. Chini ya uongozi wa Yesu Kristo waliweza kupatanisha maandiko yanayoeleza thawabu ya kimbinguni na yale yanayoeleza juu ya baraka za paradiso ya kidunia. Hakuna kikundi kingine cho chote kinachojidai kuwa cha Kikristo ambacho kimekwisha pata ufahamu wa mambo haya kwa wazi, lakini, lo! namna yamekuwa wazi kwa wale waliofundishwa na “mtumwa mwaminifu mwenye akili” kwa muda huo umepita wa miaka 100 moja! Biblia inaeleza waziwazi kwamba uzao wa Ibrahimu ungebariki​—⁠nani? Si wao wenyewe bali jamii zote za kibinadamu. (Mwa. 22:17, 18; Gal. 3:16, 29) Wale 144,000 watata-wala pamoja na Kristo kama wafalme na makuhani juu ya nani? Si juu yao wenyewe, bali juu ya wengine wa wanadamu watakaokuwa wakiishi katika paradiso ya kidunia.​​—⁠Ufu. 14:1, 3; 20:4, 6; 21:4.

KUMTHAMINI YEHOVA

8. Wanafunzi wa Biblia wa mwanzoni-mwanzoni walijifunza kuthamini jambo gani juu ya jina la Yehova na sifa zake kuu?

8 Kwa kuwa Yesu Kristo alikuwa akitumia jamii ya “mtumwa,” ufahamu wao wa Neno la Mungu uliendelea kuwa wazi zaidi na kuwa sahihi zaidi. Walikuja kuthamini kwamba “Yehova” ndilo jina la maana la Mungu wa kweli, na kwamba lilitumika kwa Muumba peke yake, Aliye Juu Zaidi. (Zab. 83:18; 100:3) Ye yote anayeshikilia fundisho la Utatu la. Imani ya Athanasio hawezi hata kidogo kuthamini kweli hiyo. Vilevile, walipata kuthamini sana sifa kuu za Yehova Mungu: hekima, uweza, haki ya hukumu, na upendo. Imani za Jumuiya ya Wakristo zinazofundisha juu ya matohara, mateso ya moto wa milele na kwamba Mungu anajaribu kuuongoa (kuugeuza) ulimwengu wa wanadamu, zinatoweka kwa kukubali Mungu aliye na sifa kuu kama hizo.​​—⁠Rum. 11:33; Mwa. 18:14; Kum. 32:4; 1 Yohana 4:8.

9. Ni jambo gani limepata kujulikana juu ya sababu ya Mungu kuruhusu uovu? (Ayubu, sura 1 na 2; Eze. 23:49)

9 Nuru ya Neno la Mungu ilipong’aa zaidi na zaidi, kulingana na kanuni inayoonyeshwa katika Mithali 4:18, watu wa Yehova walipata kuona kwa wazi zaidi sababu ya Yehova Mungu kuruhusu kila namna ya uovu na taabu. Hakuna wengine wo wote wanaojidai kuwa Wakristo wameweza kueleza hili. Yehova ameruhusu hali hizi kwa sababu gani? Kwa sababu ya suala (ulizo) juu ya haki, na kufaa kwa enzi kuu ya Yehova ya ulimwengu wote iliyotiliwa mashaka na Shetani Ibilisi; vilevile suala linalohusiana na hilo juu ya uwezekano wa wanadamu kushika ukamilifu wao Ibilisi ajapofanya yote awezayo.

“Sl SEHEMU YA ULIMWENGU”

10, 11. (a) Yohana 17:16 limetimizwaje juu ya watu wa Mungu? (b) Msimamo wao wa kutokuwamo umefanya maneno gani ya Yesu yatumike juu yao kwa njia ya pekee sana?

10 Ushuhuda zaidi kuonyesha kwamba Yesu Kristo amekuwa pamoja na jamii ya “mtumwa mwaminifu mwenye akili” wake kwa muda wote unaonekana kwa vile wamefahamu tofauti kati ya tengene-zo la Yehova na tengenezo la Shetani Ibilisi. Watu wa Yehova hawawezi kushiriki katika matendo ya kuchanganya imani! Hakuna kushirikiana na dini ya uongo, wala sehemu nyingine yo yote ya ulimwengu wa Shetani. (2 Kor. 4:4; 6:14-16) Maneno ya Yesu yanayopatikana katika Yohana 17:16, NW yanawahusu wao peke yao: “Wao si sehemu ya ulimwengu, kama vile mimi nisivyo sehemu ya ulimwengu.” Kwa hiyo, kutokuwamo kwao katika vita vya ulimwengu pamoja na siasa zake kumewatambulisha Mashahidi wa Yehova kuwa watu wa pekee kweli kweli. Sana sana hii ilikuwa kweli ilipoanza Vita ya Ulimwengu ya Pili. Ijapokuwa msimamo wao umefanya na unaendelea kuwafanya wengi wao wapate mateso makali, kutiwa gerezani na hata kuuawa, hata hivyo, mara nyingi umewafanyia mema, ukafanya maisha ya wengine yaokolewe, kama vile huko Ireland ya Kaskazini, Lebanoni, Rhodesia pamoja na nchi nyingine zenye vita.

11 Msimamo wao wa kutokuwamo hata umewatambulisha Mashahidi kuwa Wakristo wa kweli. Namna gani? Kwa kuwa ni kati yao peke yao maneno haya ya Yesu yaliyoandikwa katika Yohana 13:34, 35 yanatimizwa: “Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo. Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi.” Kwa kuwa na upendo kama huo wanapinga madai yote ya kuwafanya wajiingize katika magombano ya kikabila, kitaifa, mbari za watu au vyama vya kisiasa.

12. Ni kanuni gani anabayo imewawezesha Wakristo wapatanishe maandiko yanayoelekea kupingana juu ya kumtii Kaisari?

12 Kwa kutokuwa sehemu ya ulimwengu, Mashahidi wa Yehova wanakubali kabisa kanuni waliyotangaziwa watawala Wayahudi na mitume: “Imetupasa kumtii Mungu [kama mtawala] kuliko wanadamu.” (Matendo 5:29) Wakati uo huo wanatii shauri linalopatikana katika Warumi sura ya 13 juu ya kutii mamlaka iliyo kuu. Wameweza kupatanishaje matakwa haya yanayoelekea kupingana? Kwa kufuata kanuni ya kuwa na utii wa kadiri. Ndiyo, Wakristo hawa wanawatii wenye mamlaka, wawe ni wazazi, kwa habari ya watoto; waume, kwa habari ya wake; wenye kuajiri au wakuu wa serikali, maadamu kuwatii hakuvunji amri yo yote ya Mungu. Na kwa sababu wanatii, si kwa sababu ya woga tu lakini kwa sababu ya dhamiri zao, kama wanavyoamriwa wafanye katika Warumi 13:5, wamepata kuheshimiwa ulimwenguni pote na kuonwa kuwa raia wenye amani, wenye kutii sheria, na kama walipa-kodi wanyofu. Kwa kweli, jitihada nyingi na zenye kuendelea hufanywa katika pande zote ili kukazia kanuni za adili jema katika akili na mioyo ya wale wanaoshirikiana na Wakristo hawa. Jitihada hizo zinazofanywa na Mashahidi wa Yehova waaminifu ni za pekee sana kati ya vikundi vinavyodai kuwa vya Kikristo. Linaloonwa kuwa la maana ni hali yao bora, wala si wingi wao.

13. Ni msimamo gani wa Kimaandiko ambao umechukuliwa na wale walio pamoja na jamii ya “mtumwa” juu ya matumizi ya damu?

13 Jambo jingine linalowatambulisha Wakristo hawa kuwa si sehemu ya ulimwengu ni msimamo wao juu ya matumizi ya damu. Leo watu hawa peke yao wanaochukua jina la Yehova ndio wanaofahamu sawasawa na kutii amri ya Kimaandiko ya “kuendelea kushika mwiko wa . . . damu,” ambayo inahusu utakatifu wa uhai. Kwao hali yao njema ya kiroho ndiyo wanayotanguliza. (Mwa. 9:4-6; Matendo 15:28, 29) Msimamo wao juu ya damu umefanya wachukiwe na wengi, kwa kuwa wanashikamana nao hata uhai wao wa sasa unapokuwa hatarini. Walakini, mara nyingi msimamo wao umewaepusha na matokeo mabaya ambayo mara nyingi hutokana na kutiwa damu mishipani. Jinsi Neno la Mungu linavyoeleza jambo hili waziwazi na kulirudia mara nyingi, hata hivyo, isipokuwa watu wa Yehova, ni nani wengine wanaolitii kwa moyo wote? Hakuna!

KUANGALIA MBELE

14. “Mtumwa mwaminifu mwenye akili” amekuwa akiangalia mbele kwenye taraja gani?

14 Kama mlinzi mshikamanifu, jamii ya “mtumwa mwaminifu mwenye akili” imekuwa ikiangalia nayo inaendelea kuangalia mbele ione ni mambo gani ambayo Yehova ameweka mbele. Wakiwa katika mahali pao pafaapo wamefahamu ushuhuda unaoongezeka wa kukaribia kwa dhiki kubwa ambayo itaonyesha mwisho wa taratibu hii ya mambo katika utimizo wa unabii wa Yesu unaopatikana katika Mathayo sura ya 24 na 25, Marko 13 na Luka 21. Twaweza kuwa na hakika kwamba taratibu mpya itakayofuata baada ya dhiki hiyo baraka za ajabu zinawangoja wanadamu. Paradiso halisi ya kidunia, ikikaliwa na wanadamu waliokombolewa na Yesu Kristo! Lo! ni taraja la ajabu wee! Hakika wote wapendao kweli na haki wanatazamia kwa shauku nyingi utawala wa ufalme wa Mungu usiozuiliwa na unaokaribia nao wanaendelea kuuombea hata kama vile alivyotufundisha Yesu kuomba.​​—⁠Mt. 6:10; Ufu. 20:6; 21:4.

15. (a) Uhakika wa kwamba jamii ya “mtumwa” haijapata kamwe kuwa bila makosa imewahitaji wafanye nini? (b) Hili limewataka wale wanaoshirikiana na ”‏mtumwa” huyu wafanye nini?

15 Kwa sababu ya tumaini hili, “mtumwa mwaminifu mwenye akili” amewafahamisha watu wote wa Mungu ishara ya nyakati inayoonyesha kukaribia kwa utawala wa Ufalme wa Mungu. Walakini, kwa habari hii, lazima ikubaliwe kwamba huyu “mtumwa mwaminifu mwenye akili” hajapata hata kidogo kuwa nabii, wala kuwa bila makosa. Yale maandishi yaliyoandikwa na washiriki fulani wa jamii ya “mtumwa” huyu yaliyopata kuwa sehemu ya Kikristo ya Neno la Mungu yaliongozwa na roho ya Mungu na hayakuwa na makosa, walakini haikuwa hivyo kwa habari ya maandishi mengine tangu wakati huo. Mambo yaliyochapwa hayakuwa bila makosa katika siku za Charles Taze Russell, msimamizi wa kwanza wa Sosaiti; wala hayakuwa bila makosa katika siku za J. F. Rutherford, msimamizi aliyefuata. Mwangaza unaoongezeka wa Neno la Mungu pamoja na mambo ya hakika ya historia mara nyingi yamehitaji kuwe na marekebisho ya namna moja ama nyingine hata mpaka wakati wetu. Walakini hatupaswi kusahau kwamba makusudi ya huyu “mtumwa” sikuzote yamekuwa safi, yasiyo ya choyo; nyakati zote yamekuwa na kusudi jema. Zaidi ya hayo, maneno yanayopatikana katika Warumi 8:28 (NW) yanafaa hapa vilevile: “Mungu hufanya kazi zake zote zishirikiane kwa faida ya wale wampendao Mungu, wale walioitwa kulingana na kusudi lake.” Kwa kweli, marekebisho yo yote ambayo yamefanywa juu ya ufahamu yametoa nafasi kwa wale wanaotumikiwa na “mtumwa” huyu waonyeshe ushikamanifu na upendo, namna ya upendo ambayo Yesu alisema kwamba ingewatambulisha wafuasi wake. (Yohana 13:34, 35; linganisha 1 Petro 4:8.) Wale wanaoipenda sheria ya Mungu kweli kweli hakuna la kuwakwaza.​​—⁠Zab. 119:165.

MWENDO WA HEKIMA

16. Kwa sababu ya hayo yaliyotangulia kutajwa, tunafikia uamuzi gani usioepukika?

16 Kurudia kujikumbusha hivyo historia ya “mtumwa mwaminifu mwenye akili” wa Yehova, kama vile inavyotofautiana na historia ya Jumuiya ya Wakristo, kunatufikisha kwenye uamuzi gani? Huu, kwamba Yesu Kristo ametimiza ahadi yake. Yeye amekuwa pamoja na kundi lake la Kikristo kama vile lilivyowakilishwa na “mtumwa” huyo tangu alipopaa mbinguni mpaka siku ya leo. “Mtumwa” huyu pamoja na wale wanaoshirikiana naye wamekuwa na roho ya Yehova kwa wingi sana, wanapoendelea kuzitii amri za kuhubiri habari njema za Ufalme na kufanya wanafunzi. (Mt. 10:7; 24:14; 28:19, 20) Kukaa na Yesu Kristo kunamaanisha kukaa pamoja na wale anaopendezwa kuwatumia. Nje ya kundi la Kikristo la kweli, kuna tengenezo gani jingine? Ni tengenezo la Shetani tu la “mnyama” wa kisiasa na milki yake ya ulimwengu ya dini ya uongo ya Kibabeli.​​—⁠Ufu. 13:1, 14, 15; 17:3-6.

17, 18. (a) Sababu gani ulikuwa ujinga wengine kumwacha Yesu kwa sababu ya yale aliyosema juu ya kula mwili na kunywa damu yake? (b) Hivyo, basi, ni mwendo gani ulio wa hekima kwetu sisi leo?

17 Yesu alipowaambia wanafunzi wake kwamba wasipokula mwili wake na kunywa damu yake hawawezi kuwa na uzima ndani yao, bila shaka wote walishangaa. Wengi wao walichukizwa wasianda-mane naye tena. Kwa sababu ya usemi mmoja tu uliokuwa mgumu kufahamika aliousema Yesu, walichukizwa sana hata wakamwacha. Looo! ujinga huo! Kwa kufuata mwendo huo, walitupilia mbali kweli zote za ajabu ambazo Yesu alikuwa amewafundisha kufikia wakati huo, kama zile za Mahubiri ya Mlimani. Namna gani juu ya miujiza yote ambayo Yesu alikuwa amefanya, kuthibitisha kwamba yeye ndiye Masihi aliyeahidiwa, Mwana wa Mungu?​​—⁠Linganisha Luka 7:20-23.

18 Yesu alikuwa na sababu nzuri ya kuwauliza mitume wake: “Je! ninyi nanyi mwataka kuondoka?” Lakini Petro alikuwa na jibu lenye kufaa: “Bwana! Twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele. Nasi tumesadiki, tena tumejua, ya kuwa wewe ndiwe Mtakatifu wa Mungu.” (Yohana 6:67-69) Ndivyo na leo; kulingana na hayo yote ambayo yametangulia kutajwa, mwendo wa hekima ni kuendelea kushirikiana na “mtumwa mwaminifu mwenye akili.” Kwa upande mmoja, “mtumwa” huyu, hutusaidia kufahamu “maneno ya uzima wa milele,” na kwa upande mwingine hutusaidia kutumia “maneno” hayo maishani mwetu kwa hali njema yetu ya wakati huu na wa milele. Je! haitupasi tumshukuru Yehova Mungu pamoja na Yesu Kristo kwa kutupa “mtumwa” huyo miongoni mwetu?

19. Ni katika njia gani mbalimbali twaweza kuonyesha kwamba tunamshukuru Yehova Mungu kwa sababu ya utumishi wa “mtumwa mwaminifu mwenye akili”?

19 Twaweza kuonyeshaje shukrani zetu? Katika njia nyingi. Twaweza kuzionyesha kwa kushirikiana na ‘mtumwa huyu mwaminifu’ katika kuhubiri na kufanya wanafunzi. Twaweza kuonyesha shukrani zetu vilevile kwa kutumia kwa shauku chakula cha kiroho kinachotolewa na huyu “mtumwa” kwa njia ya vitabu na magazeti, na kwa kuhudhuria mikutano ya kundi. Wala tusisahau pendeleo letu la kuomba kwamba roho ya Yehova iongoze na kuitia nguvu jamii ya “mtumwa” huyu kwa ajili ya kazi ambayo Yeye anaitaka ifanye. Na kulingana na uwezo wetu tuna pendeleo la kutoa michango yetu ya mambo ya kimwili ili kusaidia kulipia gharama za matumizi ya “mtumwa” huyu katika utendaji wake wa ulimwenguni pote. Ndiyo, katika njia hizo zote tunaweza kuonyesha kwamba tunathamini sana njia ambayo katika hiyo Yehova Mungu anamtumia na kumbariki “mtumwa mwaminifu mwenye akili,” na kwa njia hiyo tuonyeshe kwamba tunayo imani iliyo hai, inayojionyesha kwa matendo.​​—⁠Yak. 2:17, 26.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki