“Mpayukaji”
WANAFILOSOFIA fulani Wagiriki walimwita mtume Paulo “mpayukaji.” (Matendo 17:18, NW) Neno la Kigiriki walilotumia laweza kumaanisha ‘kunguru ambaye huokota-okota mbegu.’ Katika maana ya mfano, usemi huu ulitumiwa juu ya mtu anayeokota-okota vipande vipande kwa kuombaomba au kwa kuiba. Kwa kutumia usemi huo juu ya Paulo, wanafilosofia hao walikuwa wakimaanisha kwamba alikuwa mtu ambaye hurudia-rudia vipande vipande vya maneno ya wengine, hivyo, mpayukaji maneno asiyefaa kitu.