Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 9/15 kur. 19-23
  • “Basi Tusilale Usingizi Kama Wengine’’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Basi Tusilale Usingizi Kama Wengine’’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Usingizi wo Kiroho
  • Hatari kwa Wakristo wa Kweli
  • Ni Jambo la Maana Sana Kujichunguza Binafsi
  • Namna ya Kuepuka Kusinzia
  • Iga Mfano wa Yehova wa Kuwa Macho
  • Sababu ya Mwili Wako Kuhitaji Usingizi
    Amkeni!—1995
  • Usingizi Ni Starehe Tu au Ni Muhimu?
    Amkeni!—2003
  • Nifanye Nini Ili Nipate Usingizi wa Kutosha?
    Vijana Huuliza
  • Kupata Usingizi Unaohitaji
    Amkeni!—2004
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 9/15 kur. 19-23

“Basi Tusilale Usingizi Kama Wengine’’

“NI FURAHA kweli kweli kuwa hai!” Je! wewe umepata kujisikia hivyo baada ya kuamka katika usingizi mzuri wa usiku uliopita, ukiwa umeburudika, ukiwa na nguvu mpya, ukiwa tayari kutenda jambo jipya? Au, je! umepata kufanya usingizi uwe kimbilio lako la kukuwezesha kushinda huzuni fulani au hali ya kukatishwa tamaa? Naye ni nani, akiisha kukabili uamuzi mzito, hajapata kusema jambo kama ‘Acha tutaona tu, kwanza nitaenda kulala niflkirie la kufanya’? Uchunguzi mwingi wa kisayansi uliofanywa majuzi unaonyesha kwamba usingizi hata unaweza kusaidia mtu katika masomo yake na katika kukumbuka mambo. Kwa kweli, usingizi ni kipawa kutoka kwa Muumba wa mwanadamu, Yehova.

Kitabu The Encyclopcedia Britannica kinaueleza usingizi kuwa “hali yenye kutokea-tokea mara nyingi ya kukosa utendaji, upungufu wa fahamu na upungufu katika kuitikia mambo yanayotukia katika mazingira ya mtu.” Ni wazi kwamba si siku-zote ‘hali ya kukosa utendaji’ au ‘upungufu wa fahamu na wa kuitikia mambo’ inapokuwa nzuri. Huenda tukatumia kipawa cha usingizi, sawa na vipawa vile vingine vilivyotoka kwa Yehova Mungu, kwa njia yenye kutuumiza sisi wenyewe. Mithali 20:13 inaonya hivi: “Usipende usingizi usije ukawa maskini.”

Kwa hiyo inawapasa Wakristo wajitahidi kuwa na maoni yaliyosawazika juu ya usingizi. Bila shaka inafaa mtu apate pumziko la kutosha ili aweze kutimiza vizuri wajibu wake mbalimbali wa Kikristo. Kwa upande mwingine, haitupasi ‘kupenda usingizi’ kwa njia ya uvivu mpaka tuje kuachilia mambo yaliyo ya maana sana.

Yesu alitupa sisi mfano mwema wa kufuata. Yeye alikuwa na nia ya kupenda kujibidiisha katika kazi, kuponya wagonjwa na kufukuza mashetani hata “kulipokuwa jioni, na jua limekwisha kuchwa.” Lakini siku iliyofuata, “alfajiri na mapema sana,” alikuwa tayari amekwisha kuamka, na katika kisa hiki kusudi lilikuwa kupata hali ya faragha ili ampelekee Baba yake sala.​—Marko 1:32, 35.

Mtume Paulo, aliyekuwa mzee katika kundi la kwanza la Kikristo, ni mfano kwa wazee Wakristo leo. Akisema na wanaume wazee wa kundi katika Efeso, alinena hivi: “Mkikumbuka ya kwamba miaka mitatu, usiku na mchana, sikuacha kumwonya kila mtu kwa machozi.” (Matendo 20:31) Ndiyo, “usiku na mchana.” Pia, aliandika habari ya “nyakati za usiku za kukesha” zilizotokana na jitihada zake zenye kudhamiria kulisaidia kundi.​—2 Wakorintho 6:5; 11:27, NW.

Usingizi wo Kiroho

Walakini, kuna namna nyingine ya usingizi inayoitwa usingizi wa kiroho, na huo ndio Paulo aliokuwa akiutaja kwenye 1 Wathesalonike 5:6 aliposema: “Basi tusilale usingizi kama wengine.”

Kwa kusema “tu-,” ni wazi alikuwa akimaanisha Wakristo wa kweli, ambao kwa njia ya kidini ni wenye bidii, wenye kuitikia mwelekezo wa Yehova na kufahamu hatua-hatua za maendeleo ya makusudi ya Mungu. Ni lazima wao wawe macho kiroho! Wale “wengine” ni watu, labda hata kutia ndani wengine wanaojisema kuwa Wakristo, ambao wamelala usingizi wa kiroho na hivyo wanakosa kujali “kuwapo” kwa Yesu na “uharibifu wa ghafula” wa waovu unaokuja​—1 Wathesalonike 4:15; 5:1-3, NW.

Leo namna hiyo ya usingizi au ubaridi wa kiroho inahusu watu wengi zaidi ya vile ilivyohusu watu katika siku za Paulo. Hata wengine wa viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo wanahisi jambo hilo. Usingizi wa kiroho uliopo kwa wingi unaonyeshwa wazi na kusemwa-semwa nyakati zote juu ya “hatua mpya ya kidini ‘ya kuamsha watu.’ “Likitoa maelezo juu ya jambo hilo, katika Aprili 1978, gazeti The Detroit News lilisema kwamba “huenda ikawa ni mapema mno kutoa ripoti za kwamba hali ya kidini imeanza kufufuka katika United States, na labda hata kusema hivyo ni kutia chumvi kabisa, . . Nalo lilitaja maneno ya kiongozi mkubwa wa seminari (chuo) ya Kiprotestanti katika Oklahoma kuwa alisema hivi: “Kulingana na uamuzi wangu, mimi naona kanisa limeingia katika nyakati za magumu kwa sababu ni wazi kwamba pole kwa pole limekosa maarifa ya kuijua imani.” Namna gani katika nchi zile nyingine? Jarida la kidini la Austria linaloitwa das gesprach (maongezi) lilisema hivi: “Kardinali Konig [wa Austria] alionyesha wazi pia ni nani anayepaswa kulaumiwa kwa sababu ya hali ya ulimwengu yenye kusikitisha sana. . . . ‘Lawama linayakalia kwa kiasi kikubwa yale yanayoitwa “mataifa ya Kikristo” ati, ambayo zamani zilizopita yaliufanya karibu ulimwengu wote ukawa koloni layo halafu ndipo baada ya hapo yakaanza “kuufanya uwe wa Kikristo” ati. Lakini kwa kweli hayakuleta roho ya Kristo, ni jina lenyewe tu. Yameshindwa kuishi kupatana na yasemwayo na gospeli’ “(injili).​—Septemba 1976, uku. 2

Hatari kwa Wakristo wa Kweli

Paulo alitoa onyo la upole akasema “basi tusilale usingizi,” kuonyesha kwamba ni lazima hata Wakristo wa kweli wawe waangalifu kuepuka kuingizwa katika usingizi. Kumbuka kwamba katika usiku ule wa mwisho ambao Yesu alikuwa na wanafunzi, wao walilala usingizi, ijapokuwa alikuwa amewahimiza mara nyingi wakae macho. Ingawa usingizi wao ulikuwa wa kimwili, ulionyesha maelekeo ya kusinzia kiroho. Yesu alisema: “Wakati kama huu ninyi mnalala!” (Mathayo 26:40-45, NW; Marko 14:37-41) Ebu fikiria mambo yote yaliyohusika wakati huo: Ukweli wa Neno la Mungu, uaminifu wa Mwanaye, tokeo la mwisho kwa jamaa yote ya kibinadamu. Kwa sababu ya kufahamu kabisa mambo yote yaliyohusika, Yesu alikuwa macho kiroho, akawa akimwomba Baba yake nguvu alizohitaji. Ingalifaa kama wanafunzi wake wangaliiga mfano wake.

“Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni,” Yesu akawaambia. (Mathayo 26:41) Ni onyo la wakati wake lenye kufaa kama nini! Muda mfupi baada ya hapo, wakati wa kusalitiwa kwake, ‘wanafunzi wote walimwacha, wakakimbia,’ na Petro hata akafikia hatua ya kumkana mara tatu. (Mathayo 26:56, 69-75) Kusinzia kiroho ni hatari.

Jambo hilo linaweza kufahamiwa kwa sababu hata usingizi wa kimwili wa wakati usiofaa unaweza kuleta msiba. Tunamkumbuka Mwamuzi Samsoni aliyesalitiwa na Delila kisha “akaamka katika usingizi wake” na kumbe ‘Yehova ndiye aliyekuwa amemwacha.’​—Waamuzi 16:19-2L

Ikiwa usingizi wa kimwili wa nyakati zisizofaa unaweza kuleta msiba, ni zaidi sana usingizi wa kiroho. Sikuzote huo haufai. Ufunuo 16:15 unasema hivi juu ya usingizi wa namna hiyo: “Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake.” Ndiyo, usingizi wa kiroho unaweza kutufanya tupoteze mavazi yetu ya utambulishi wa Kikristo.​—Linganisha Mithali 23:21.

Ni Jambo la Maana Sana Kujichunguza Binafsi

Lakini wewe unafikiri ni kwa njia gani Wakristo wa kweli wanaweza kuendelea kukesha? Kutusaidia kujua, acheni tuangalie mambo fulani yanayolingana kati ya usingizi wa kimwili na wa kiroho. Hiyo itatusaidia pia tujichunguze binafsi ili tukizuie hata kielekeo kilicho kidogo zaidi cha kusinzia kiroho.

Tumejifunza kwamba usingizi ni ‘hali ya kukosa utendaji.’ Basi, ni kwa kadiri gani sisi tunakuwa wenye bidii katika mambo ya Kikristo, kama vile kuzitangaza “habari njema” za kwamba Yesu sasa yuko katika mamlaka ya Ufalme na karibuni ataleta “mwisho wa ghafula” juu ya waovu? Si kwamba tunataka kulinganisha kiasi cha utendaji wetu na kile cha wengine, kwa maana kufanya hivyo kungekuwa jambo lisilo la hekima, na hata la kukosa upendo. (Wagalatia 6:4, 5) Lakini, kwa kufikiria hali zetu za kibinafsi, afya yetu, madaraka yetu ya kijamaa, uwezo wetu wa kufanya mambo mbalimbali, na vilevile hali zetu za kupungukiwa, kila mmoja wetu anaweza kujiamulia mwenyewe kiasi anachopaswa kukesha katika jambo hilo. Kuhusu utendaji wetu mbali-mbali wa kiroho katika wakati huu wa mavuno, tunaweza kufaidika kwa kuyathamini maneno ya Mithali 10:5: “Akusanyaye wakati wa hari ni mwana mwenye hekima; bali asinziaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.”

Usingizi unazidi kuelezwa kuwa ni “upungufu wa fahamu.” Kwa hiyo, je! sisi tungali na fahamu za kuyajua mahitaji yetu ya kiroho, kama iwafaavyo Wakristo wanaoamini kikweli kwamba tuko karibu na mwisho wa mfumo huu wa mambo? Je! tunaonyesha tunayajua kwa kujifunza kwa ukawaida na kuhudhuria mikutano? Je! sisi tuna hamu nyingi ya kusoma vitabu vya karibuni zaidi vilivyochapishwa kutusaidia tuielewe Biblia? Ni vizuri zaidi kutumia wakati wetu katika mambo ya namna hiyo badala ya kuuharibu katika karamu zenye makelele mengi au kwa kutafuta anasa daima. Hilo ni jambo linalofanywa na wale waliolala usingizi wa kiroho.​—1 Wathesalonike 5:7.

Usingizi unaonyesha “upungufu katika kuitikia mambo.” Tunaweza kuuliza, ‘Je! mimi ninaitikiaje ninapotiwa moyo niwe katika utendaji fulani wa pekee wa Kikristo? Je! mimi naitikia moja kwa moja kwa njia yenye shauku? Je! naitikia kutumia mambo mapya niliyojifunza kama nilivyokuwa nikiitikia nilipofahamu kweli ya Neno la Mungu hapo kwanza?’

Acheni tuchukue mfano wa usingizi halisi kwa kiasi kidogo tena: Usingizi unapokuja joto la mwili linashuka na mpigo wa moyo unapungua. Je! sisi tunahisi tukiwa na hali ya kupoa katika juhudi yetu na upendo wetu kwa wengine? Au tungali ‘tumepashwa moto kwa roho,’ huku tukieleza wengine kwa juhudi ujumbe wa Kikristo? Je! sisi, kama Yeremia, tunaweza kusema kwamba ile kweli ni “kama moto uwakao” ndani yetu hata tunashindwa kuivumilia ibaki tu ndani yetu?​—Warumi 12:11, NW; Yeremia 20:9.

Sehemu nyingine ya usingizi ni kuota ndoto. Ndoto hazimpi mtu furaha yenye kudumu, na kwa kweli zinaweza hata kumkatisha tamaa akiisha kugutuka kwa kuyakabili mambo yaliyo tofauti na matazamio yake. Isaya 29:8 inaeleza hali hiyo kwa njia hii: “Tena itakuwa kama mtu mwenye njaa aotapo; kumbe, anakula; lakini aamkapo, nafsi yake haina kitu.”

Je! inaweza kuwa kwamba sisi tunaishi katika ‘ndoto,’ kwamba tumelala usingizi wa kutokuona tamasha ya ulimwengu ikibadilika, labda tukitumia wakati mwingi na pesa nyingi mno katika kufuatia faida za kimwili? Kama vile mwota-ndoto asivyofahamu wakati, je! sisi pia tumepoteza hisi ya kufahamu uharaka wa nyakati hizi tunamoishi? Kumbuka kwamba Paulo aliwaonya Wakristo Wathesalonike kwamba mwisho wa mfumo huu ungewafikilia watu wengi kama mwivi wakati wa usiku. (1 Wathesalonike 5:4; Mathayo 24:43, 33) Je! inaweza kuwa kwamba sisi tunafanya tafrija kupita kiasi, labda hata kukosa mikutano ya Kikristo ili tuzifuatie? Au tunaendeleza maoni ya kwamba nyakati za mikutano zibadilishwe ili zifaane vizuri zaidi na mipango yetu ya kibinafsi, badala ya kuwa na kusudi la kufikiria faida zilizo bora zaidi kwa kundi na kwa wale tunaowafundisha? Ni vizuri zaidi kuwa macho tuyaone mambo yaliyo ya kweli kabisa maishani: Ufalme wa Mungu uliosimamishwa unatawala kwa matendo; mfumo huu mbovu wa mambo unakabili uharibifu wa haraka na wa daima; tokeo letu binafsi la huko mwisho limo hatarini.​—1 Timotheo 4:16.

Namna ya Kuepuka Kusinzia

Tunahitaji kufahamu ni kitu gani kinacholeta usingizi. Usingizi wa kimwili hauletwi na kani (misukumo) za nje hasa. Ni kweli kwamba mambo kama vile kuwa katika chumba chenye joto, kukosa hewa safi, au kunywa maziwa yenye joto yanaweza kuleta usingizi. Lakini kwa uhalisi usingizi unachochewa na utendaji fulani ulio ndani ya mwili ambao mpaka sasa haujafahamiwa kwa ukamili. Vivyo hivyo, kani za nje zinaweza kufanya mtu asinzie kiroho. Kwa mfano, tunaweza kusinzia kiroho kwa sababu watu tunaowahubiri wana ubaridi. Au, kama Yesu alivyoonya kuacha mioyo yetu ‘ilemewe na kula kupita kiasi na kunywa kupita kiasi na masumbufu ya maisha’ kungeelekea pia kutuletea usingizi. (Luka 21:34, NW) Ni lazima hatari hizo ziepukwe. Lakini labda utu wetu wa ndani, wala si mazingira yetu ya nje, ndio baadaye utakaokuja ama kutufanya tuendelee kuwa macho kiroho ama kutufanya tupatwe na usingizi. Kwa hiyo ni lazima tulinde umbo letu la ndani, kuendelea kuuamsha moyo wetu uwe na upendo uliokuwa nao hapo kwanza. Ni lazima tuangalie sana mawazo yetu, makusudi yetu ya kufanya mambo, tamaa zetu, tuangalie kwa makini utu wetu wa ndani. (Waefeso 3:16-19) Shauri hili la mtume ni zuri sana: “Dumuni sana katika kuomba, mkikesha katika kuomba huku na shukrani”!—Wakolosai 4:2; 1 Wathesalonike 5:8, 11, 16-22.

Iga Mfano wa Yehova wa Kuwa Macho

Katika ‘kutolala kama wengine,’ Wakristo wa kweli wanaweza kufuata mfano mwema wa Yehova wa kuwa macho. Kwa hao “wengine” huenda ikaonekana kwamba Yehova ni mtu wa polepole katika kuleta mwisho wa mfumo wa sasa pamoja na ufisadi wake wote na udhalimu. (2 Petro 3:9) Basi inaelekea kwamba wao watakuwa bado ‘wamelala’ wakati ile “dhiki kubwa” itakapowafikilia kwa ghafula, (1 Wathesalonike 5:3) Lakini Yehova atajithibitisha kuwa macho kweli kweli. Wakati huo mwendo wake utalinganika na maelezo yaliyo katika Zaburi 78:65, 66: “Ndipo [Yehova] alipoamka kama aliyelala usingizi, kama shujaa apigaye kelele sababu ya mvinyo; akawapiga watesi wake akawarudisha nyuma, akawatia aibu ya milele.”​—Linganisha Yeremia 1:12.

Huu ndio wakati wetu wa kupata furaha ya Kikristo kwa kuwa wenye bidii katika utumishi wa Yehova, kuwa na fahamu za kutambua mahitaji yetu ya kiroho na wakati wenye hatari tunamoishi na kuitikia mwelekezo Wake. Huu ndio wakati wa kuwa macho kiroho sawa na vile Paulo alivyosema mahali penginepo pote: “Saa ya kuamka katika usingizi imekwisha kuwadia; kwa maana sasa wokovu wetu u karibu nasi kuliko tulipoanza kuamini. Usiku umeendelea sana, mchana umekaribia.”​—Warumi 13:11, 12.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki