Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 12/15 kur. 13-19
  • Kuhubiri Katika Ulimwengu Wenye Uasi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuhubiri Katika Ulimwengu Wenye Uasi
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUFUATA KIOLEZO CHA KARNE YA KWANZA
  • JESHI LA “NZIGE” LASONGA MBELE
  • KUSHINDA MATESO
  • “NYUMBA KWA NYUMBA” ULIMWENGUNI POTE
  • Kwa Nini Huduma ya Nyumba kwa Nyumba Ni ya Maana Sasa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Siku ya Yehova Iko Karibu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Karibisha Akilini Siku ya Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Fundisha Peupe Na Kutoka Nyumba Kwa Nyumba
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 12/15 kur. 13-19

Kuhubiri Katika Ulimwengu Wenye Uasi

“Kwa sababu ya kuongezeka kwa kutokutii sheria upendo wa wengi utapoa. Walakini atakayevumilia mpaka mwisho ndiye atakayeokolewa. Na habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa na watu kwa ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakapokuja.”​—Mt. 24:12-14, NW.

1. Uasi umeenea kwa kiasi gani ulimwenguni leo? (2 Tim. 3:1-5)

JE! UNAONA uasi ukiongezeka leo? Katika sehemu nyingi za dunia kutokuheshimu sheria na utengemano kunaongezeka kwa wingi sana. Uvunjaji wa sheria ni mwingi sana katika mingi ya miji mikubwa. Si salama tena kutembea barabarani. Katika miaka ya karibuni, serikali nyingi zimepinduliwa na maasi, na nyingine zinalundika silaha nyingi ili kupinga maasi ya ndani na vitisho vya kutoka nje. Hata ulimwengu wa Kikomunisti unapata matatizo, kadiri utukuzo wa taifa unavyotangulizwa mbele ya “umoja” wa kijamii.

2. Je! leo uasi umepenya mengi ya madhehebu ya Jumuiya ya Wakristo?

2 Namna gani Jumuiya ya Wakristo? Kama alivyotabiri Yesu juu ya siku zetu, “kuongezeka kwa kutokutii sheria” kumekuwa na matokeo yenye kuharibu juu ya mengi ya madhehebu yake. Biblia, ambayo inatangaza kutii kunakofaa kwa sheria na utengemano, sasa inaonwa na wengi kuwa ya ‘kizamani.’ Makanisa mengi yamekubaliana na jamii yenye kuruhusu ufisadi ya siku hizi, yakijifanya kama kwamba hayaoni uasherati, ngono za wanaume kwa wanaume na za wanawake kwa wanawake na upotovu​—hivyo wakitokeza matunda ya Wakristo wa kujifanya, wa namna ambayo ‘haitaurithi ufalme wa Mungu.’​—Mt. 24:12; 1 Kor. 6:9, 10.

3. Je! waasi wamejaribu kupenyaje katika kundi la Kikristo, naye Yesu anasemaje kuhusu watu hao?

3 Watu wenye kuasi hata wamejaribu kupenya katika kundi la kweli la Kikristo, wakibisha kwamba ‘kuwapo kulikoahidiwa’ kwa Bwana wetu si katika siku hizi. Wao wanawadhihaki wazee na wanabisha kuwekwa kwa “mtumwa mwaminifu mwenye akili” na Bwana ili aangalie faida za Ufalme wake duniani. (2 Pet. 3:3, 4; Mt. 24:45-47) Watu wa namna hii wanatiwa ndani ya onyo la Yesu lililoandikwa katika Mathayo 7:15-23: “Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali. . . . [Siku hiyo] nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.”

4. Tunatiwa moyo tusitawishe sifa gani, na twaweza kuionyeshaje?

4 Hata hivyo, Yesu alisema hivi kuhusu watu walio ‘mfano wa kondoo’ kweli kweli: “Atakayevumilia mpaka mwisho ndiye atakayeokolewa.” Twaweza kuonyeshaje kwamba tuna sifa hii ya uvumilivu? Ala! kwa kushiriki katika kutimiza maneno yaliyofuata ya Yesu: “Na habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa na watu kwa ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakapokuja.” (Mt. 24:13, 14, NW) Kwa uvumilivu wetu katika kutangaza “habari njema hizi za ufalme” tutaweza kupata wokovu.

5. (a) Kwa sababu gani inaweza kusemwa kwamba hatuko peke yetu katika kazi yetu? (b) Ni kuhukumu gani kunakofanywa sasa, na kunafanywa na nani?

5 Sisi hatuko peke yetu katika kufanya kazi hii, kwa kuwa unabii wa Yesu juu ya “mwisho wa taratibu ya mambo” unaendelea kutuambia kwamba “atakapokuja Mwana wa Adamu katika utukufu wake, na malaika watakatifu pamoja naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu wake.” Kutoka mbingu zisizoonekana anaongoza kazi ya kuhukumu, ambayo katika hiyo anawabagua watu wa mataifa “kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi.” Kazi hii ya kubagua inafikia upeo wake katika “dhiki kuu,” wakati ambapo “mbuzi” wasiotii watakapoenda ‘kukatiliwa mbali milele,’ hali “kondoo” wenye kutii wanaalikwa kuurithi ufalme ambao Baba amewatayarishia tangu ‘kuwekwa kwa msingi wa ulimwengu.’​—Mt. 24:3, NW, 21; 25:31-46.

6. (a) “Kondoo” na “mbuzi” waliwezeshwaje kujionyesha? (b) Uongozi wa kimalaika wa utumishi wetu wa nyumba kwa nyumba umeonyeshwaje mara nyingi?

6 “Kondoo” na “mbuzi” wanajionyeshaje kuwa hivyo? Haya ni matokeo ya kutoa ushuhuda yanayofanywa duniani na “ndugu” waliotiwa mafuta wa mfalme na wenzi wao, kazi ambayo inafika ‘hata mpaka sehemu za mwisho za dunia.’ (Matendo 1:8) Kwa ujumla, hii imekuwa kazi ya duniani pote ya kuhubiri nyumba kwa nyumba. Utendaji huo unatokeza kuitikia kwa kuthamini mambo ya kiroho kunakoonyeshwa na maneno ya Mfalme kuelekea jamii ya “kondoo”: “Nalikuwa mgeni, mkanikaribisha,” (Mt. 25:35) Anahesabu kupokelewa kwa “ndugu” zake kuwa jambo analofanyiwa yeye. Kunatofautiana na ukaribishaji unaotolewa na watu wakaidi wasioyajali mambo ya kiroho. Hakika kazi hii ya kubagua imeendelezwa chini ya uongozi wa kimalaika. (Mt. 25:35) Na kuhusiana na hili kumekuwako msaada wa kimalaika katika kutangaza hizi “habari njema,” kwani ni mara nyingi namna gani imetukia kwamba mtu mwenye unyofu wa moyoni amemwomba Mungu msaada, kisha kumwona mmoja wa Mashahidi wa Yehova amesimama mlangoni pake! Na ni mara nyingi namna gani Shahidi ameongozwa na hali isiyo ya kawaida kutembelea nyumba fulani wakati ambapo msaada wa kiroho unahitajiwa kuliko wakati mwingine wote! Kwa kuona tegemezo la maelfu ya malaika wa kimbinguni, na tusiache kamwe kutafuta watu wanaostahili kwa kuhubiri nyumba kwa nyumba kwa juhudi.

KUFUATA KIOLEZO CHA KARNE YA KWANZA

7. (a) Ni nini kinachoonyesha kwamba Wakristo wa kwanza walishughulika sana katika kutoa ushuhuda ‘waziwazi na nyumba kwa nyumba’? (b) Ni ufanani gani mwingine unaoweza kufanywa kati ya Wakristo wa karne ya kwanza na wa kisasa?

7 Kati ya Wakristo wa karne ya kwanza hakukuwa na tofauti kati ya viongozi wa dini na watu wa kawaida. Wale waamini katika Bwana Yesu Kristo hawakuwa wenye kukaa kitako vitini tu. Walikuwa wanaume na wanawake wenye kutenda, wenye kushughulika sana sana katika kutoa ushuhuda “waziwazi, na nyumba kwa nyumba.” (Matendo 20:20) Kwa halisi ‘waliujaza Yerusalemu kwa mafundisho yao’ na wakahubiri habari njema “katika kuumba kote kuliko chini ya mbingu.” (Matendo 5:28; Kol. 1:23, NW) Wao walifaulu kwa sababu, kama mwana-historia E. Arnold anavyotaja katika kitabu chake The Early Christians: “Hata na washiriki wa chini zaidi wa ujamii wao walikuwa wajumbe, wakieneza kweli waliyopewa.” Ni lazima iwe vivyo hivyo leo, kwa kuwa maneno haya ya Paulo yanahusu Wakristo wote wenye kuamini: “Kwa maana kwa moyo mtu [hutumia imani kwa] haki, [lakini] kwa kinywa [mtu hufanya tangazo la waziwazi la] wokovu.” Na mara nyingine matokeo ni kwamba wengi wanazisikia “habari njema,” kwa kuwa, “sauti yao imeenea duniani mwote, Na maneno yao hata miisho ya ulimwengu.”​—Rum. 10:10, 18.

8. Ni tofauti gani kubwa inayoonekana kati ya dini za Jumuiya ya Wakristo na Ukristo wa kweli?

8 Lo! namna ujumbe wa kiunabii wa Wakristo wa kweli unavyotofautiana na sherehe za kidesturi za Jumuiya ya Wakristo! Mwana-historia H. G. Wells alitaja tofauti hii katika kitabu chake Outline of History, kama ifuatavyo:

“Inatupasa kumkumbusha msomaji tofauti kubwa sana kati ya Ukristo buu uliositawi kabisa wa Nicæa [wa 325 W.K.] na mafundisho ya Yesu wa Nazareti. . . . Linaloelekea kuwa wazi ni kwamba mafundisho ya Yesu wa Nazareti yalikuwa mafundisho ya kiunabii ya namna mpya iliyoanza na manabii Waebrania. . . . Tengenezo lake la pekee lilikuwa tengenezo la wahubiri, na kazi yalo kubwa ilikuwa mahubiri. Walakini Ukristo uliositawi kabisa wa karne ya nne . . . kwa sehemu kubwa ulikuwa dini ya kikuhani ya namna ambayo ulimwengu ulifahamiana nayo kwa maelfu ya miaka. . . . ulikuwa na tengenezo lenye kusitawi kwa haraka la mashemasi, makasisi, na maaskofu.”

Kwa mafundisho yao ya kiunabii leo, Wakristo wa kweli wanazo habari njema zenye thamani za ufalme uliosimamishwa, ambazo lazima ‘kwanza zihubiriwe katika mataifa yote’ kabla ya mwisho kuja.​​—Marko 13:10.

9. Ni utumishi gani wa nyumba kwa nyumba ulioanzishwa katika mwaka 1919 unaoendelea kwa kufaulu mpaka siku hii?

9 Kuhubiri huku kwa kisasa kwa “habari njema” kulipata kichocheo zaidi baada ya kutangazwa kwa gazeti mpya lililokusudiwa The Golden Age katika kusanyiko la Septemba 5, 1919, Cedar Point, Ohio, U.S.A. Sasa gazeti hilo linaitwa kwa kichwa cha Kimaandiko “Amkeni!” (Rum. 13:11) Likawa chombo cha kazi ya pekee iliyotangazwa na Sosaiti kwenye kusanyiko hilo:

“Kazi ya THE GOLDEN AGE ni ukaguzi wa nyumba kwa nyumba kwa ujumbe wa ufalme, likitangaza siku ya kisasi ya Mungu wetu na kufariji wale wanaoomboleza.”

Mpaka siku hii, kazi ya nyumba kwa nyumba kwa kutumia Amkeni!, na vilevile kwa gazeti la Mnara wa Mlinzi, inaendelea kuwa mojawapo wa njia bora zaidi za kufikia watu kwa ukawaida na “habari njema.”

10. Ni mwito gani wenye kuchochea uliotolewa katika mwaka 1922, na ulihusianaje na utendaji wa nyumba kwa nyumba?

10 Utumishi wa nyumba kwa nyumba wa Mashahidi wa Yehova ulipata nguvu zaidi kutoka kwa kusanyiko la pili la Cedar Point katika mwaka 1922, ambapo mwito huu wa kukumbukwa ulitangazwa:

“Songeni mbele katika vita mpaka kila baki la Babeli limefanywa kuwa ukiwa. Utangazeni ujumbe karibu na mbali. Ni lazima ulimwengu ufahamu kwamba Yehova ni Mungu na kwamba Yesu Kristo ni Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana. Siku hii ndiyo siku kubwa kupita zote. Tazama, Mfalme huyu atawala! Nyie ni mawakili wake wa kumtangaza. Kwa hiyo mtangazeni, mtangazeni, mtangazeni, Mfalme na ufalme wake.”

Siku moja ya kusanyiko hilo iliwekwa kando kwa ajili ya kutoa ushuhuda nyumba kwa nyumba vikundi vikundi, na iliripotiwa kwamba vitabu 10,000 viligawa na wahubiri hao wa Ufalme. Mpaka siku hii, programu za pekee za kuhubiri nyumba kwa nyumba kwenye makusanyiko zinaongeza furaha ya wale wanaokusanyika.

JESHI LA “NZIGE” LASONGA MBELE

11. (a) Jeshi la Mashahidi lilifananishwa Kimaandiko na nini katika kazi yao ya kuhubiri nyumba kwa nyumba? (b) Utendaji huu wa “nzige” umekuwaje na matokeo juu ya (i) viongozi wa dini, (ii) watu wenye mioyo minyofu?

11 Wakati wa miaka ya kuanzia na 1920 na ya kuanzia na 1930 huku kutoa ushuhuda kwa bidii nyumba kwa nyumba kulikuwa kama shambulio la nzige lenye kupitia katikati ya Jumuiya ya Wakristo. Kama vile Ufunuo 9:7-10 unavyolitaja jambo hili, “na maumbo ya hao nzige yalikuwa kama farasi waliowekwa tayari kwa vita . . . Na sauti ya mabawa yao ilikuwa kama sauti ya magari, ya farasi wengi waendao vitani. Nao wana mikia kama ya nge.” Jeshi ‘lenye nguvu’ la Mashahidi wenye juhudi lilijazana katika miji na vijiji vya Jumuiya ya Wakristo likifunua wazi mafundisho yasiyo sahihi na mazoea ya kidini ya unafiki. Mara nyingi hili liliwauma viongozi wa kidini na kuwafanya walete upinzani kwa bidii. Jeshi hili la “nzige” lilitoa onyo kuhusu siku inayokaribia ya kisasi ya Yehova juu ya wote wanaosuta jina lake, na waliwafariji watu wenye mioyo minyofu kwa habari njema za dunia iliyo paradiso itakayorudishwa chini ya enzi kuu ya Mungu.​—Isa. 61:2.

12. (a) Sababu gani “siku za mwisho” hizi siyo wakati wa kustarehe? (b) Maneno ya Yoeli kuhusu “nzige” yanaweza kutumiwaje kuhusiana na utendaji wa Mashahidi wa Yehova?

12 “Siku za mwisho” hizi siyo wakati wa kustarehe. (2 Tim. 3:1) Kama vile nabii wa Mungu Yoeli anavyotangaza: “Siku ya [Yehova] inakuja. Kwa sababu inakaribia.” (Yoeli 2:1) Ijapokuwa hii itakuwa siku ya huzuni na maumivu kwa wenye dini za uongo, wale ambao wanampenda Mungu wanaweza kufurahia sasa katika kuelimishwa kwa kiroho ambako ni kama “mapambazuko yakitandazwa juu ya milima.” (Yoeli 2:2a) Kama jeshi la “nzige,” walipeleka ujumbe wa Ufalme nyumba kwa nyumba. Nabii wa Mungu anaeleza tendo lao lenye juhudi katika maneno haya yenye kutokeza:

“[Kuna watu walio wengi] tena wenye nguvu, mfano wao haukuwako kamwe, wala hautakuwako baada ya hao, hata katika miaka ya vizazi vingi. Moto unakula mbele yao; na nyuma yao miali ya moto inateketeza; hiyo nchi inafanana na bustani ya Adeni mbele yao, na nyuma yao imekuwa jangwa tupu; naam, hakuna [kilicho]okoka [ki]sipatikane nao.” (Yoeli 2:2b, 3)

Ni kweli, hakujapata kuwako jeshi la kiroho kama vile mashahidi hawa waliotiwa mafuta wa Yehova! Wameizunguka dunia yote, wakifunua wazi makosa ya dini za Kibabeli, wakiacha ukiwa milki yao yote ya utendaji yenye kufanana na Adeni, walakini wakileta faraja kwa nyumba zile zinazopokea “habari njema” hizo. Kupitia kwa Yoeli, Yehova Mungu anasema hivi juu ya jeshi hili la Mashahidi:

“Hupiga mbio kama mashujaa; huupanda ukuta kama watu wa vita. . . . naye [Yehova] anatoa sauti yake mbele ya jeshi lake; maana matuo yake ni makubwa sana; kwa maana yeye ni hodari atekelezaye neno lake; kwa kuwa siku ya [Yehova] ni kuu yenye kitisho sana; naye ni nani awezaye kuistahimili? (Yoeli 2:7-11)

Wakiwa wanalindwa na maelfu ya malaika wa kimbinguni, “nzige” hawa wa kiroho wameendeleza ziara zao nyumba kwa nyumba. Watu wa kawaida wamewasikiza kwa furaha, kadiri ‘siku ya Yehova yenye kutisha’ inavyokaribia.​—Tazama Religion, sura 6 na 7 (1940 W.K.); pia The Watchtower, makala ya Juni 15 mpaka Julai 15, 1939, chini ya “Maangamizi ya Dini.”

13. Ni “farasi” gani wametumiwa leo kama vyombo vya jeshi la “nzige,” na ni ushuhuda gani mkubwa wa nyumba kwa nyumba umetokezwa?

13 Nabii Yoeli aliona kwa njozi jeshi hili la “nzige” kama kwamba likikimbia kama vile “farasi” walio tayari kwa vita, wakitoa sauti kama ile ya magari ya vita. (Yoeli 2:4-6) Hakika watangazaji hawa wa Ufalme ulimwenguni pote ni jeshi kubwa, wanapofanya vita vya kiroho, wakihubiri ‘nyumba kwa nyumba’! Na njozi ya Yohana inaendelea kusimulia farasi waliopandwa wanaofanyiza “majeshi ya wapanda farasi” kuwa wanafikia hesabu ya “elfu ishirini mara elfu kumi”​—200,000,000! (Ufu. 9:16-19) “Farasi” hawa wamekuwa vyombo vyenye nguvu kusaidia utangazaji wa hukumu za Yehova! Namna wanavyofananika vema na mamilioni ya mamilioni ya Biblia, vitabu na magazeti ambayo jeshi hili la “nzige” limegawa wakati wa miaka hii katika utendaji wao wa nyumba kwa nyumba! (Tazama “Then Is Finished the Mystery of God,” sura 17.) Katika mwaka 1978 peke yake, wao, wakiandamana na “mkutano mkubwa” wa Ufunuo 7:9-17, waligawa kwenye nyumba nakala 216,709,937 za magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Bila shaka kuhubiri kwa nyumba kwa nyumba kwa jeshi la “nzige” kunatokeza ushuhuda mkubwa.

KUSHINDA MATESO

14. Yoeli 2:7 inaweza kutumiwaje kuhusiana na utendaji wa Mashahidi wa Yehova ulio chini ya marufuku?

14 Adui za kweli wamejaribu kusimamisha utendaji huu wa kuhubiri. Katika nchi nyingi, watawala wenye kutukuza taifa wametangaza marufuku juu ya kazi hii ya “nzige.” Wamejaribu kusimamisha “ukuta” juu ya utendaji huu wa kuhubiri Ufalme. Walakini jeshi hili la “nzige” linapanda kuta hizo “kama watu wa vita.” Katika miji mingine ambako kazi imepigwa marufuku, watu wa sehemu hizo wamejiunga na Mashahidi, wakiwaongoza kwenye nyumba zile ambazo wanafahamu kuwa watu ni wenye urafiki. Nyakati nyingine wanatoa ushuhuda nyumba moja au mbili katika jengo moja na kisha wanasonga mbele ili kufanya vivyo hivyo katika jengo jingine la nyumba. Mara nyingi wanatoa ushuhuda kwa kutumia Biblia peke yake. Katika nchi nyingine wanafanya kazi yenye matokeo kwa ushuhuda wa vivi hivi, huku wakiitarajia kwa tamaa nyingi siku ambayo pengine pingu zenye kuzuia zitavunjwa, ili kwamba waweze tena kwenda nyumba kwa nyumba kwa uhuru.

15. Mahakma Kuu ya United States ilijitokezaje katika kuunga mkono kuhubiri kwetu kwa nyumba kwa nyumba?

15 Wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu, viongozi wa kidini katika United States walifanya wawezavyo ili kuhakikisha utendaji wa nyumba kwa nyumba wa Mashahidi wa Yehova umepigwa marufuku. Hata hivyo, pindi nyingi, Mahakma Kuu ya United States ilikubali kwamba kuhubiri huku kwa nyumba kwa nyumba kulikuwa kunaungwa mkono na mahakikisho ya katiba ya kufuata dini na uhuru wa kusema na wa magazeti. Ikiweka fikira juu ya msingi wa Maandiko wa utendaji wa Mashahidi wa Yehova, hiyo Mahakma Kuu ilisema hivi, katika maoni ya walio wengi katika kesi ya Murdock v. Commonwealth of Pennsylvania, katika Mei 1943:

“Wao wanadai kufuata mfano wa Paulo, wakifundisha ‘waziwazi, na ‘nyumba kwa nyumba.’ Matendo 20:20. Wanaichukua kwa halisi amri hii ya Maandiko, ‘Enendeni kwenye ulimwengu wote, na mhubiri injili kwa kila kiumbe.’ Marko 16:15. . . . Namna hii ya kiinjilisti inatumiwa leo kwa kadiri kubwa na madhehebu ya kidini ambayo watembeza vitabu wao hupeleka Injili kwa maelfu ya nyumba na kwa ziara za kibinafsi wanajaribu kupata wafuasi wa imani yao. Ni zaidi ya kuhubiri; ni zaidi ya kugawa vitabu vya kidini. Ni mwungano wa yote.”

Kweli kweli, jeshi la “nzige” na wenzi wao wamepata kufaulu katika kupanda kuta za kisheria ambazo adui wamejaribu kuweka ili kuzuia kazi yao ya nyumba kwa nyumba.

“NYUMBA KWA NYUMBA” ULIMWENGUNI POTE

16. (a) Ni utendaji gani wa kimalaika unaoendelea katika shamba la ulimwengu? (b) Sababu gani njia za “kuhubiri” za Jumuiya ya Wakristo zimeshindwa kufaulu?

16 Katika kueleza mojawapo wa mifano yake, Yesu alisema hivi: ‘Lile shamba ni ulimwengu . . . Mavuno ni mwisho wa taratibu ya mambo, na wavunaji ni malaika.’ (Mt. 13:38, 39, W) Vilevile mtume Yohana aliona katika njozi utendaji wa malaika katika ‘wakati huu wa mwisho,’ na kwa hiyo aliandika hivi:

“Nikaona malaika mwingine, akiruka katikati ya mbingu, mwenye Injili ya milele, awahubiri hao wakaao juu ya nchi, na kila taifa na kabila na lugha na jamaa, akasema kwa sauti kuu, Mcheni Mungu, na kumtukuza; kwa maana saa ya hukumu yake imekuja. Msujudieni yeye aliyezifanya mbingu na nchi na bahari na chemchemi za maji. Kisha mwingine, malaika wa pili, akafuata, akisema, Umeanguka, umeanguka Babeli, mji ule ulio mkubwa, maana ndio uliowanywesha mataifa yote mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake.” (Ufu. 14:6-8)

Watu wa jamii yote ya kibinadamu wangeelezwaje juu ya utawala wa Mungu wa Ufalme, na kuanguka kunakokaribia kwa milki ya ulimwengu ya dini ya uongo na kuharibiwa kwake? Je! ingekuwa kwa njia ya Jumuiya ya Wakristo ya kwenda nchi zinazoitwa za “kipagani”, kujenga shule, hospitali na sehemu za kusaidia wenye uhitaji na kuwahubiria vivi hivi Wakristo waliowajia? Sivyo, kwa kuwa njia hizo hazijaweza kufaulu hata wakati mmoja. Wao hawajapata kufaulu, na dini za Jumuiya ya Wakristo, ambazo zimekuwa zikishirikiana katika kufyatua risasi na vita vya kikoloni kwa karne nyingi, zinaheshimiwa kidogo sana katika nchi zote zisizo za Kikristo duniani.

17. Ni njia zipi zimetumiwa na wamisionari wa Mashahidi wa Yehova, na zikiwa na matokeo gani?

17 Malaika wa mbinguni wameongoza utumishi wa umisionari unaotofautiana na huo kabisa katika miaka ya karibuni. Kuanzia na mwaka 1943, Mashahidi wa Yehova wamekuwa wakiongoza Shule ya Biblia ya Gileadi ya Sosaiti (kwanza ilikuwa Kusini mwa Lansing, New York, U.S.A.) kwa kusudi lenye uharaka la kuzoeza wamisionari kwa ajili ya shamba la ulimwengu. Na wamisionari hawa wametumwa, ili kuhubiri ‘waziwazi na nyumba kwa nyumba,’ kuongoza funzo la Biblia la nyumbani na kukusanya watu wenye kupendezwa kwenye makundi mapya. Je! kuhubiri huku kwa ‘nyumba kwa nyumba’ kumepata kufaulu? Bila shaka ndiyo. Katika mwaka 1943, Mashahidi wa Yehova katika nchi 54 na maeneo ya dunia walikuwa wakitumikia katika makundi 6,310. Katika mwaka 1978, miaka 35 baadaye, kulikuwa na Mashahidi wenye kutenda 2,182,341, katika nchi 205, katika makundi 42,255.

18. (a) Je! kutoa ushuhuda nyumba kwa nyumba kuna maana leo, na sababu gani unajibu hivi? (b) Mashahidi wa Yehova wanapaswa kuionaje sehemu yao kuhusiana na kazi ya kuhukumu? (c) Twapaswa kufanya nini ili tuhakikishiwe kupata furaha mwishowe?

18 Kadiri “saa ya hukumu” ya Mungu inavyokaribia kwa haraka, nao utendaji huu wa nyumba kwa nyumba wa nyie mlio wamisionari kwenu na wamisionari wa ugenini unapaswa kuharakishwa kufikia mwisho wake. (Ufu. 14:7) Ingawa huenda watu wengi leo wakaonyesha maelekeo ya ‘namna ya mbuzi,’ kungali na “kondoo” wanaongojea katika maeneo yenu. Mnapoendeleza utendaji wenu wa nyumba kwa nyumba kwa ujasiri, malaika wa kimbinguni watahakikisha kwamba mnaongozwa kwa “kondoo” hawa. Mfalme aliyetawazwa, Kristo Yesu, ndiye Hakimu. Sisi tu watumishi wa chini tuliopewa pendeleo la kuwa na sehemu kuhusiana na kazi yake ya kuhukumu, na twaweza kufanya hivyo kwa ‘kutoa ushuhuda kikamilifu na kufundisha waziwazi’ na “nyumba kwa nyumba.” (Matendo 20:20, 21) Karibuni sana miji yenye kuasi ya Jumuiya ya Wakristo na ya dunia nzima ‘itaanguka iwe ukiwa, isiwe na wakaaji.’ Ndipo, wenye furaha watakuwa wale walioitikia mwito wa utumishi wa Yehova, wakisema: “Mimi hapa, nitume mimi.”​—Isa. 6:8-11.

—Kutoka The Watchtower July 15, 1979.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki