Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 3/15 kur. 20-21
  • “Mtumikieni Yehova kwa Furaha”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Mtumikieni Yehova kwa Furaha”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Habari Zinazolingana
  • Tumikia Yehova kwa Shangwe ya Moyo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Waliotengwa Wawe Wasifaji Wenye Shangwe Ulimwenguni Pote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Ingia Katika Nyua za Hekalu la Yehova!
    Mwimbieni Yehova Sifa
  • Ni Nani Atakayemsifu Mfalme?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 3/15 kur. 20-21

Zaburi

“Mtumikieni Yehova kwa Furaha”

YEHOVA, Mfanyi wetu, ni “Mungu mwenye furaha” na anataka watumishi wake wafurahie kutimiza amri zake kwa uaminifu. (1 Timotheo 1:11, NW; Yakobo 1:25; Ufunuo 1:3) Msingi wa amri hizo ni upendo, kwa maana “pendo halimfanyii jirani neno baya.” (Warumi 13:8-10) Ndiyo sababu kumtii Muumba kunasaidia kuwapa wenzetu furaha na pia kunatuhakikishia kupata maisha yenye furaha na yenye uradhi.

Basi, je! haiwapasi watu wa mataifa yote washangilie wakimfurahia Yehova? Hivyo ndivyo mtunga zaburi mwenye kuongozwa na Mungu alivyotutia moyo, akisema: “Mfanyieni [Yehova] shangwe, dunia yote; mtumikieni [Yehova] kwa furaha; njoni mbele zake kwa kuimba.” (Zaburi 100:1, 2) Kwa kukubaliana na hili onyo la upole, sifa tunazotoa hazipasi kuwa za ulegevu bali za, nguvu na mkazo, ziweze kulinganishwa na ‘shangwe ya ushindi’ ya jeshi ambalo limejipatia ushindi ulio kamili kabisa. Haiwapasi watumishi wa Mungu wawe kama watumwa walio waoga-waoga, wenye kujikunja sana kwa hofu. Utumishi anaopewa Mungu si mzigo wala hauna uonezi. Haufanyi mtu awe asiyetaka mchezo hata kidogo wala haumfanyi awe na sura ya huzuni-huzuni, bila ya kuchangamka wakati wo wote. (1 Yohana 5:3) Utumishi anaopewa yeye unaburudisha, unampa mtu nguvu mpya, na kwa haki unafaa uambatane na furaha. Ndiyo sababu mtunga zaburi alihimiza watu waje mbele za Mungu “kwa kuimba.”

Jambo kubwa linalofanya mtu atake kutoa utumishi mtakatifu ni kwamba Yehova ndiye Mungu na ndiye Mfanyi wa wanadamu. Mtunga zaburi alitangaza hivi: “Jueni [tambueni, kubalini] kwamba [Yehova] ndiye Mungu; ndiye aliyetuumba [wala si sisi wenyewe] na sisi tu watu wake; tu watu wake, na kondoo wa malisho yake.” (Zaburi 100: 3) Kwa sababu yeye ndiye Muumba, sisi tu mali yake, kama vile kondoo walivyo mali ya mchungaji. Zaidi ya Uungu na Uumbi wa Yehova, utu wake ni kichocheo chenye nguvu cha kufanya watu wa mataifa yote waziingie nyua za patakatifu pake, wamtolee shukrani na sifa wakiwa hapo. Tena, inatupasa tulihimidi jina lake, yaani, tuseme mema juu ya Aliye Juu Zaidi, Yule anayesimamiwa na jina hilo. Mtunga zaburi anawahimiza watu kwa kuwaambia: “Ingieni malangoni mwake kwa kushukuru; nyuani mwake kwa kusifu; mshukuruni, lihimidini jina lake; kwa kuwa [Yehova] ndiye mwema; rehema zake ni za milele; na uaminifu wake vizazi na vizazi.”​—Zaburi 100:4, 5.

Hakika sifa za Yehova zinapasa kuongoza mtu amsifu yeye. Yeye ni mwema kabisa kabisa, wala hana kidoa cho chote cha ubaya, hata kilicho kidogo namna gani. Fadhili za upendo wake au huruma yake kwa watumishi wake zinaweza kutegemewa nyakati zote; zinaendelea kuwapo kwa wakati usiojulikana. “Vizazi na vizazi” Yehova ni mwaminifu, wala hana ugeu-geu katika kuwapenda wale wanaotaka kufanya mapenzi yake. (Warumi 8:38, 39) Basi, je! sisi hatuna sababu nzuri ya ‘kumtumikia Yehova kwa furaha’?

[Picha katika ukurasa wa 21]

“Sisi tu watu wake na kondoo wa malisho yake.”​—Zaburi 100:3

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki