Hata Ndege ‘Wanajua Wakati Wao’
KULIKUWAKO hali yenye kusikitisha sana kati ya Waisraeli katika wakati wa Yeremia. Mwendo wao ulitofautiana na ule wa ndege wenye kuhama. Tunasoma hivi: “[Hata] koikoi angani ajua nyakati zake zilizoamriwa; na hua na mbayuwayu na korongo huangalia wakati wa kuja kwao; bali watu wangu hawazijui amri za [Yehova].”—Yer. 8:7.
Ijapokuwa ndege wenye kuhama kama vile koikoi, hua, mbayuwayu na korongo wanajua wakati wa kuja kwao na wakati wa kuondoka, Waisraeli hawakujali hukumu za Yehova. Kwa habari ya ndege hao wenye kuhama, kuja na kuondoka kwao ni jambo la lazima ili waendelee kuwa hai. Vivyo hivyo, hali njema pamoja na ufanisi wa Waisraeli ulitegemea juu ya kujipatanisha kwao na hukumu za Yehova. Walakini Waisraeli walishindwa katika jambo hilo, na kwa hiyo, hawakuweza kuonyesha hata busara inayoonyeshwa na ndege wasio na akili ambao hujua wakati wao wa kuhama.