Sababu Matumaini Yetu Mema Yatatimizwa Bila Shaka
“Mungu hufanya kazi zake zote zishirikiane pamoja kwa faida ya wale wampendao Mungu.”—Rum. 8:28, “NW”
1. Katika karne yetu ya 20 hesabu yenye kuongezeka ya washiriki wa viumbe vya kibinadamu wanaougua wamepata kuelezwa juu ya nini, nayo hali ya tumaini lao ikoje baada ya makumi yote hayo ya miaka yaliyopita, na sababu gani?
KATIKA karne yetu ya 20 hesabu yenye kuongezeka ya washiriki wa viumbe vya kibinadamu wamepata kuelezwa juu ya “kufunuliwa kwa wana wa Mungu” kunakokaribia, na sasa wanafahamu wanayopaswa kutazamia karibuni. Kujapokuwa ‘kuugua na kuwa katika maumivu’ ambako viumbe vya kibinadamu vimetiishwa mpaka sasa, watu hao wenye kupashwa habari, wanaotazamia, wanafurahi katika tumaini. Yajapokuwa makumi ya miaka ambayo yamepita tangu “mkutano mkubwa” ulipoanza kufanywa, tumaini lao vilevile ni lenye uzima. Kama vile “mti wa uzima,” linaishi ndani ya mioyo yao, kwa sababu msingi wake ni ahadi ya Mungu iliyoandikwa katika kurasa za Biblia.—Mit. 13:12; Ufu. 7:9; 21:5; Rum. 8:19-22, NW.
2. (a) “Mkutano mkubwa” huomba Yehova Mungu atetewe akiwa katika cheo gani kilicho haki yake? (b) Wanapoomba “Jina lako litukuzwe,” wanaomba tendo gani lifanyike, nayo yatatimizwa wakati gani?
2 Zaidi ya yote, wanatazamia kutetewa mapema kwa enzi kuu ya ulimwengu wote ya Yehova aliye Muumba. Wanathamini kwamba yeye ni mwenye haki katika kuitumia enzi yake juu ya ulimwengu wote wa kuumba kwake. Hivyo, wao wanampinga bila kugeuka-geuka “nyoka wa zamani,” Shetani Ibilisi, ambaye anaikosea na kuisingizia enzi kuu ya Yehova na ambaye amegeuza sehemu kubwa ya kuumba kwa kibinadamu kuipinge. Wao humwomba Yehova Sala ya Bwana na kusema: “Jina lako litukuzwe.” (Mt. 6:9, 10) Kwa hiyo wao humwomba Yehova mwenyewe atukuze jina lake. Yeye atajibu sala hiyo wakati wa “dhiki kubwa” inayokaribia, ambayo itafikia upeo wake katika “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi” katika Har–Magedoni na ambayo itafuatwa na kufungwa na kutupwa shimoni kwa “nyoka wa zamani” na wale wa “uzao” wake.—Eze. 36:23; 38:16, 23; 39:27; Ufu. 16:14, 16; 20:1, 2.
3. Kwa kulingana na Ufunuo 7:9, 10, “mkutano mkubwa’ wa watu wenye tumaini wataokoka wapate kushuhudia matukio gani?
3 “Mkutano mkubwa” wa watu wenye tumaini utaokoka upate kushuhudia kutetewa kwa enzi kuu ya ulimwenguni pote ya Yehova na kutakaswa kwa jina lake. Kisha, kwa kufaa kabisa, Ufunuo 7:9, 10 unawafananisha kwa njia ya unabii kama wakisimama baadaye mbele ya kiti cha enzi ya Mungu aliyetukuzwa na mbele ya Mwanawe mwenye kujinyima, Yesu Kristo, na wakisema hivi kwa shukrani: “Wokovu una Mungu wetu aketiye katika kiti cha enzi, na Mwana-Kondoo.”
4. Kwa sababu “mkutano mkubwa” haushiriki woga wa watu wa ulimwengu, ni jambo gani wanalofanya kwa upole na kwa heshima nyingi mbele ya mamlaka ya kilimwengu?
4 Katika hali iliyopo leo kabla ya kufyatuka kwa “dhiki kubwa,” wakati ulimwengu unapolemazwa na woga, “mkutano mkubwa” hawaogopi yale ambayo watu wa kilimwengu wanaogopa. Kwa ujasiri wanatii yale aliyoandika mtume Petro: “Mtakaseni Kristo Bwana mioyoni mwenu. Mwe tayari sikuzote kumjibu kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo ndani yenu; lakini kwa upole na kwa hofu.”—1 Pet. 3:14, 15.
5. Wanashirikije katika utimizo wa unabii wa Yesu katika Mathayo 24:14, nao wanaionaje amri ya Yesu katika Mathayo 28:19, 20?
5 Bila choyo wanalishiriki tumaini hilo lenye utukufu pamoja na kila mtu anayefikika. Hivyo wanashiriki katika utimizo wa unabii wa Yesu: “Habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa na watu kuwa ushuhuda kwa mataifa yote.” Sasa ni jambo lenye uharaka zaidi kuliko wakati mwingine wo wote kutii amri ya Yesu: “Kwa hiyo nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, kuwabatiza, . . . kuwafundisha.”—Mt. 24:14, NW; 28:19, 20, NW.
6. Sababu gani sisi tutakuwa wenye kupendelewa zaidi kuliko Wakristo wa kwanza ambao walikuwa na tumaini ilo hilo karne nyingi zilizopita?
6 Hakuna wengine walio na tumaini lenye msingi wake katika Biblia kama lile letu. Ndilo jambo zuri zaidi tunaloweza kushiriki na wengine. Tumaini letu ni hazina ya kufurahia. Twaambiwa, “furahieni tumaini.” (Rum. 12:12, NW) Twaweza kutazamia kwa hakika kutimizwa kwalo hivi karibuni. Kungojea kwetu kwa uvumilivu lipate kutimizwa hakutakuwa kazi bure. Wakristo wa kwanza walitazamia tu yale ambayo sisi tumekaribia kuona yakitimizwa. Tutakuwa tumependelewa sana kuona utimizo wake mkubwa kwa njia ya halisi.
BILA SHAKA KAZI ZA MUNGU ZITASHIRIKIANA KWA FAIDA
7, 8. (a) Sababu gani hatutazamii mengi sana yatimizwe? (b) Kuhusiana na hilo, kama vile mtume Paulo, sisi twafahamu nini, kama inavyoelezwa katika Warumi 8:28-30?
7 Hatutazamii mengi sana yatimizwe, iwapo yameandikwa katika Neno la Mungu. Hakuna jambo lo lote lililoandikwa litakalokuwa haliwezekani kwake! Yeye hawezi kushindwa kutimiza ahadi yake yenye utukufu, kwa kuwa yeye ni Mungu Mwenye Nguvu Zote. Iwapo twampenda na kuthibitisha jambo hilo kwa utii wetu, hatakosa kutimiza kwa utukufu ahadi zake zote zilizo nzuri. Pamoja na mtume Paulo wa karne ya kwanza W.K., twafahamu jambo hilo. Katika kitabu cha Warumi 8:28-30 NW, kilichoandikwa wapata mwaka 56 W.K., Paulo alikubali hivi:
8 “Sasa twafahamu kwamba Mungu hufanya kazi zake zote zishirikiane pamoja kwa faida ya wale wampendao Mungu,a wale ambao ndio wameitwa kulingana na kusudi lake; kwa sababu wale aliowatambua mara ya kwanza ndio ambao pia alitangulia kuweka wafuatishwe kwa mfano wa Mwanawe, ili kwamba awe mzaliwa wa kwanza kati ya ndugu wengi. Zaidi ya hayo, wale ambao alitangulia kuweka ndio ambao pia aliita; na wale alioita ndio aliowatangaza kuwa wenye haki. Mwishowe wale aliotangaza kuwa wenye haki ndio ambao alitukuza pia.”
9. Tafsiri ya King James Version na tafsiri fulani za Biblia za kisasa zinatafsirije Warumi. 8:28, walakini tafsiri nyinginezo za kisasa zasemaje kama vile New World Translation?
9 Katika tafsiri ya Biblia ya King James Version, Warumi 8:28 lasema hivi: “Nasi twajua kwamba vitu vyote hufanya kazi pamoja kwa faida ya wale wanaompenda Mungu, kwa wale ambao wameitwa kulingana na kusudi lake.” Tafsiri nyingi za kisasa za Biblia zasomeka hivyo katika mstari huo. Hata hivyo The Bible in Living English ya Byington yasema hivi: “Nasi twajua kwamba wale wanaompenda Mungu, Mungu huwapa ushirikiano wote kwa faida ya wale ambao, kama inavyolifaa kusudi lake, wameitwa.” The Emphasised Bible ya Rotherham yasema hivi: “Twajua zaidi kwamba kwa wale wanaompenda Mungu, Mungu hufanya vitu vyote vifanye kazi pamoja kwa faida.” The New Testament ya Lattey yasema hivi: “Nasi twajua kwamba kwa wale wanaompenda Mungu yeye hufanya vitu vyote pamoja kwa faida.”—Tazama pia The Authentic New Testament ya Schonfield, uku. 338, fungu 2.
10, 11. (a) Ni kazi zipi anazofanya Mungu zishirikiane pamoja kwa faida ya aliyeitwa? (b) Ni matendo gani ya kibinafsi yasiyopaswa kutiwa ndani kati ya “mambo yote” yanayotajwa katika Warumi 8:28?
10 Vitu vyote vinavyotajwa katika Warumi 8:28-30, NW ni vya Mungu, si vya wanadamu. Kulingana na maandishi, ni kazi za Mungu anazofanya zishirikiane pamoja kwa faida ya wale walioitwa wanaompenda, kwa sababu yeye anataka waupate Ufalme ambao amewaitia. Walakini ye yote anayedai kuwa Mkristo aliyebatizwa aliye na taraja la ufalme wa kimbinguni akitenda kinyume cha taraja lake la kimbinguni, hatuwezi kutazamia Mungu afanye tendo hilo limfaidi mkosaji, au hata kwamba tendo lake lenyewe limfaidi. Kwa mfano, iwapo Mkristo anayedai kuwa na taraja la kimbinguni anashiriki sana katika michezo wakati wa kujipatia tafrija kisha avunje mguu au kifundo cha mguu wake, je! Mungu anafanya jeraha hilo limfaidi mchezaji huyo? Au iwapo, wakati wa udhaifu na maelekeo mabaya, mtu anayeitwa Mkristo anapitia katika eneo lenye sifa mbaya kwa ajili ya utafiti (kutaka kujua) au kuona wanaume wengine wakishawishwa kufanya uasherati na malaya naye mwenyewe atongozwe na malaya na kufanya uasherati, je! Mungu aweza kutazamiwa afanye jambo hilo limfaidi mkosaji huyo? Je! kumjaribu Mungu hivyo kunafaidi?
11 Matokeo ya jeraha hilo la kimwili au la kiadili yanategemea kabisa namna mtu huyo anayehusika anavyotenda kwa kupatana na yanayompata kwa ajili ya mwendo wake wa upumbavu. Huenda akapata somo kutokana na jambo zito hilo lililompata. Walakini je! kujifunza somo kunafanya jambo lote hilo kuwa mojayapo ya kazi za Mungu, sana sana kwa sababu huenda Yeye akamrehemu? Bila shaka sivyo! Jambo hilo halipaswi kuwekwa kati ya “mambo yote” yanayotajwa na Paulo katika Warumi 8:28 NW.
12. Kazi zote za Mungu zinazotajwa katika Warumi 8:29, 30 ni kazi za namna gani, naye Paulo anazisimulia zikifuatana namna gani?
12 Tunapoendelea kusoma mistari 29, 30 na kuona kazi za Mungu zinazotajwa humo, twafahamu kwamba, wakati wote, kazi zote za Mungu ni njema kwao waliotangulia kuchaguliwa, wanaoitwa Wakristo. Vilevile, zinafanya kazi pamoja kwa faida ya mrithi wa Ufalme katika kila hatua ambayo Mungu anaendesha mambo. Akitaja hatua hizo kutoka upande ule mwingine, Paulo anaandika hivi: “Maana wale aliowajua tangu asili, aliwachagua tangu asili wafananishwe na mfano wa Mwana wake, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi. Na wale aliowachagua tangu asili, hao akawaita; na wale aliowaita, hao akawahesabia haki; na wale aliowahesabia haki, hao akawatukuza.”
13. (a) Mungu anawatukuza wakati gani wale waliotangazwa kuwa wenye haki? (b) Kutangazwa kwa mtu kuwa mwenye haki kunafanywa juu ya msingi gani?
13 Mungu anatoa utukuzo wakati gani? Wakati anapowapa wale wenye kibali fahari ya maarifa ya Mwanawe mzaliwa wa kwanza ambaye sasa amekwezwa kwenye mkono Wake wa kuume. Kwa njia hiyo Mungu anawaweka kwenye njia inayoongoza kwenye utukuzo wa kimbinguni. Baada ya kazi hiyo ya kwanza ya Mungu, sasa aweza kuwatangaza kuwa wenye haki, walakini ni hapo tu wakimwamini Kristo aliyetukuzwa hata kufikia hatua ya kujitoa au kujiweka wakf kabisa kwa Mungu.
14. (a) Mtu anapataje kuwa kati ya wale ‘walioitwa’ na Mungu? (b) Inakuwaje kwamba mtu anatiwa kati ya wale ‘waliotangulia kuchaguliwa’ na Mungu?
14 Sasa, Mungu anamwitaje mwanafunzi aliyejiweka wakf na kubatizwa wa Mwanawe aliyetukuzwa, ili apate ‘kuhamishwa na kuingizwa katika ufalme wa Mwana wa pendo lake’? (Kol. 1:13) Mungu hufanya jambo hilo kwa kumzaa kwa roho Yake apate kuwa mwana wa Mungu aliyezaliwa kwa roho. Ndipo Mungu anapoweza kumwita au kumwalika mwana huyo wa kiroho awe sehemu ya ufalme wa kimbinguni, jambo linaloweza kufurahiwa na wale tu ambao mwishowe wanafufuliwa kuingia kwenye uzima wa roho mbinguni. (1 Kor. 15:43-50) Mungu alitangulia kuchagua kwamba jamii ya ndugu wenye asili ile ile ya kimungu na wenye kufanywa kwa kulingana na mfano wa Mwanawe mzaliwa wa kwanza, Yesu Kristo, washirikiane na Mwanawe. Kwa hiyo, baada ya kuitwa, mwana wa Mungu aliyezaliwa kwa roho anapata kuwa mshiriki wa jamii iliyotangulia kuchaguliwa, ambayo katika hiyo anapaswa kuendelea kuwa mwaminifu mpaka kifo chake cha kidunia. Mungu alitangulia kuchagua jamii hiyo, hakuna mtu ye yote anayeingia katika jamii hiyo kwa kuitwa kwa jina. Mungu alitangulia kuamuru kwamba hesabu ya ndugu za kimbinguni wa Kristo iwe 144,000, pasipo ye yote wao kutajwa kwa jina kuhusiana na habari hiyo.—Ufu. 14:1-3, NW.
15. Mungu “aliwatambua mara ya kwanza” wale waliotangulia kuchaguliwa wakati gani na namna gani?
15 Katika Warumi 8:29, 30 NW mtume Paulo anataja kwamba ile jamii ya Wakristo ambao Mungu hutukuza au kuheshimu na kukuza, kuwatangaza wenye haki, kuwaita na kutangulia kuwachagua, ‘aliwatambua mara ya kwanza.’ Hivyo ndivyo Mungu alivyofanya huko nyuma katika bustani ya Edeni wakati alipotoa unabii wake juu ya “uzao” wa “mwanamke” wake mwenyewe na tendo hodari la “uzao” huo. (Mwa 3:15) Kwa hiyo, maelfu mengi ya miaka kabla ya “uzao” huo kutokea, Mungu ndiye aliyekuwa wa kwanza kuuona uhitaji wake na mgawo wake wa pekee katika orodha ya mambo ya Mungu. Hivyo, jambo lile ambalo Mungu aliona lilistahili ‘kutambuliwa mara ya kwanza aliliweka akilini na moyoni muda wote mpaka wakati wa kutokeza “uzao” huo ukiwa Mwanawe Yesu Kristo na wanafunzi waaminifu waliozaliwa kwa roho wa Mwanawe. Muda wote mpaka wakati wa kutokea kwa “uzao” huo Mungu alitangulia kuujua naye aliukubali kwa kuupendelea kipekee.
16. (a) Kila mojayapo ya “kazi zake zote” zinazosimuliwa katika Warumi 8:28-30 inatimizaje sehemu yake? (b) Kwa hiyo ni jambo gani lililo hakika kwa wote wale ambao “wameitwa kulingana na kusudi lake”?
16 Kwa hiyo, tangu mwanzo mpaka mwisho, ni “kazi” za nani tunazoelezwa kwa urefu katika Warumi 8:28-30? Ni “kazi” za Mungu. Na kwa kuwa yeye ni Mungu asiyebadilika anayejipatanisha kabisa katika matendo yake yote, yeye “hufanya kazi zake zote zishirikiane pamoja kwa faida ya wale wampendao Mungu.” Hata mojayapo ya “kazi zake zote” haikosi kupatana, kulingana, na kazi nyingine zake zote zenye kusudi. Kazi hizo hutokea kwa utaratibu, kazi moja ikielekeza kwenye ile nyingine na kuitayarishia mambo. Kusudi la Mungu ni zuri sana, naye anafahamu kabisa namna ya kulitimiza kwa kufaulu. Kwa hiyo “wale ambao wameitwa kulingana na kusudi lake” wanaweza kuwa na hakika kwamba wakati wo wote hatashindwa kamwe. Iwapo wataendelea kuwa waaminifu na kushirikiana naye kwa upendo, wana hakika ya kuwa na sehemu katika utimizo wa kusudi lake kwa kushiriki kutenda kazi katika ufalme wake wa kimbinguni pamoja na Yesu Kristo.
JAMII NYINGINE YATANGULIA KUJULIKANA
17. Ni kusudi gani la upendo alilokuwa nalo Mungu kwa habari ya wale walioitwa, waliotangulia kuchaguliwa, na kuanzia wakati gani?
17 Kupitia kwa wale ‘walioitwa’ ambao Mungu ‘alitambua mara ya kwanza,’ yeye ana kusudi la upendo la kutimizwa. Jambo hilo lilifahamishwa waziwazi miaka 2,083 baada ya kuumbwa kwa Adamu, yaani, katika mwaka 1,943 K.W.K. Wakati huo Mungu alimwambia hivi Abrahamu mzee wa ukoo mwaminifu: “Katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa.” Kwa hiyo baraka hiyo ilitia ndani ulimwengu wote nayo ingepatikana kupitia kwa “uzao” wa Abrahamu. (Mwa. 12:1-3; 22:17, 18) “Uzao” huo uliotangulia kuchaguliwa ungetia ndani Yesu Kristo na wanafunzi wake 144,000 ‘walioitwa.’ (Ufu. 7:1-8; 14:1-3; Gal. 3:16, 29) Ahadi hiyo isiyo na mambo mengi ambayo Mungu alimpa Abrahamu ilionyesha maarifa Yake ya kimbele juu ya “uzao” ulio jamii bila ya yeye kutaja hesabu yao halisi. Kitabu cha mwisho cha Biblia peke yake ndicho kinachotupa hesabu hiyo.
18. Katika nyakati za kale zilizotangulia Kristo, Mungu alitumia watu mmoja mmoja na vikundi vya watu kufananisha kiunabii akina nani?
18 Katika nyakati za kale zilizotangulia Kristo, kulikuwa watu mmoja mmoja na vikundi vya watu waliofanya urafiki na wazao wa asili wa Abrahamu. Mungu aliwatumia hao kama vielelezo au mifano ya kiunabii ya watu wa nyakati zetu za kisasa ambao wanafanya urafiki na kushirikiana na baki dogo la wale ‘walioitwa’ ambao wangali duniani.
19. Ufunuo 7:9-14 unawafananishaje wale washiriki wenye kutenda kazi wa mabaki ya wale wanafunzi wa Kristo ‘walioitwa,’ nalo ni pendeleo gani litakalokuwa lao katika wakati ujao ulio karibu?
19 Kitabu cha mwisho kabisa cha Biblia, kilichoandikwa na mtume Mkristo Yohana wapata mwaka 96 W.K., kilitabiri na kuwafananisha washiriki hao wenye kutenda kazi wa mabaki ya wale ‘walioitwa’ kama “mkutano mkubwa” usio na hesabu. Washiriki wa huu “mkutano mkubwa” watahifadhiwa (watalindwa) hai waipite ile “dhiki kubwa,” ndiyo, kuipita “vita ya siku ile kuu ya Mungu mwenyezi” katika Har–Magedoni nao wataingia katika taratibu mpya katika dunia iliyosafishwa chini ya utawala wa miaka elfu wa Yesu Kristo na wale ‘walioitwa’ 144,000. Mfano huo wa kiunabii wa huu “mkutano mkubwa” kama ulivyoandikwa katika Ufunuo 7:9-14 ulisimuliwa kwa maneno na kwa kuandikwa katika mwaka 1935.—Ufu. 16:14, 16.
20. Kuanzia mwaka 1935, ni hesabu gani ya vielelezo na unabii unaofananisha mkutano mkubwa ulioelezwa wazi katika vitabu vyetu, na sababu gani tumaini lao ni la pekee hata hivyo litatimizwa hakika?
20 Katika miaka 45 tangu wakati huo, vielelezo au mifano ya kiunabii isiyopungua 42 ya huo “mkutano mkubwa” wa waokokaji wa Har–Magedoni imeelezwa katika vitabu ya Sosaiti. (Tazama You May Survive Armageddon into God’s New World, kilichochapwa katika mwaka 1955, na kurasa 367, 368.) Vielelezo na unabii wote huo unaonyesha kwamba Mungu alikuwa ameukusudia mema peke yake huo “mkutano mkubwa” uliotangulia kujulikana kimbele. Ni kwa sababu nao pia wanampenda. Wengi wao wamekuwa na nia ya kuthibitisha upendo wao kwake usiovunjika hata kufikia kifo cha kufia imani. Hakika, tumaini lililowekwa mbele ya huo “mkutano mkubwa” ni tumaini ambalo wengi wa kuumba kwa kibinadamu hawajapewa. Ingawa tumaini lao ni la pekee na zuri sana, kwa uhakika wanatazamia utimizo wake wa mapema. Hilo tumaini lao lenye uzima halitakatishwa tamaa kamwe, kwa kuwa Mungu yule anayetoa tumaini ni mwaminifu. Ahadi aliyowapa ni yenye kutegemeka na hakika: “Na yeye aketiye katika kiti cha enzi atatanda hema yake juu yao. Hawataona njaa wala hawataona kiu tena, wala jua halitawapiga, wala hari iliyo yote. Kwa maana huyo Mwana-Kondoo, aliye katikati ya kiti cha enzi, atawachunga, naye atawaongoza kwenye chemchemi za maji yenye uhai, na Mungu atayafuta machozi yote katika macho yao.”—Ufu. 7:15-17.
—Kutoka The Watchtower Apr. 1, 1980.
[Maelezo ya Chini]
a Maandishi hayo ni kulingana na Hati ya Vatican Na. 1209, Hati ya Alexandria, na Hati ya Mafunjo Na. 46. Tazama The Syriac New Testament kilichoandikwa na Dakt. James Murdock.