Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 11/15 kur. 23-24
  • Wakati Usio wa Kujihurumia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wakati Usio wa Kujihurumia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Habari Zinazolingana
  • Maana ya Kumpenda Jirani Yetu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Kuishi Si Kwa Ajili Yetu Wenyewe Tena
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Ujihadhari na Mawazo ya Uadui
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • “Mpende Jirani Yako Kama Wewe Mwenyewe”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 11/15 kur. 23-24

Wakati Usio wa Kujihurumia

NANI asiyejaribu kujihurumia? Na ni nani asiyeshukuru kwa ajili ya huruma anazoonyeshwa na wengine? Hakuna mtu anayeuchukia mwili wake, bali huulisha na kuutunza. Hata hivyo, je! kunaweza kuwako jambo kama la kujihurumia isivyofaa? Ndiyo, hilo linaweza kuwa ikiwa mtu angechukua maoni yasiyo ya busara juu ya mambo kuliko kuwa na maoni ya busara.

Kwa mfano, chukua mwanamke wa kilo nyingi sana mwenye ugonjwa wa sukari. Lingekuwa jambo la ujinga kwake kutosheleza tamaa yake ya peremende. Kwa kujihurumia kwa muda tu, mwishowe, ataharibu mambo. Na ndivyo alivyo mlevi. Anapojihurumia pasipo busara, anaendelea kunywa na hivyo anaiharakisha siku ya kufa.

Mtu ambaye hakujiachilia achukuliwe na mwendo wa kujihurumia bila busara alikuwa Yesu Kristo. Wakati mmoja aliwaambia wanafunzi wake yaliyokuwa yanamngojea mbele, akionyesha kwamba “ni lazima aende Yerusalemu akapate mateso mengi kutoka kwa wanaume wazee, makuhani wakuu na waandishi, kisha auawe, na siku ya tatu ainuliwe.” Kwa kusikia hayo, mtume Petro “alimchukua kando akaanza kumkemea, akisema: ‘Jihurumie, Bwana; msiba kama huo hautakupata kamwe.’ Lakini, akigeuka, alimwambia Petro hivi: ‘Nenda nyuma yangu, Shetani! Wewe ni kwazo kwangu, kwa sababu unawaza, si mawazo ya Mungu, bali yale ya wanadamu.’”​—Mt. 16:21-23, NW.

Kwa wazi, Yesu aliliona jambo hilo kwa uzito sana. Ama sivyo hangalionyesha maoni hayo yenye mkazo na kutumia maneno hayo mazito. Bila shaka alifahamu kwamba Petro alikuwa akimshawishi hapa afuate mwendo wa kuchukua mambo kwa urahisi, bila kujitahidi, namna ile ile Ibilisi mwenyewe alivyojaribu kumshawishi Yesu katika mwanzo wa huduma ya Yesu.​—Mt. 4:1-10.

Ndiyo, dhamiri iliyoelimishwa yaweza kukuambia ule kiasi kwenye meza ya chakula na vinywaji. Au baada ya majaribu mengi na makosa, unaweza kufikia uamuzi wa kujiadibisha juu ya starehe na tafrija ili upate mapumziko ya kutosha na usingizi. Ikiwa ni hivyo, basi utataka kushikilia yale unayojua kuwa bora kwako bila kuacha rafiki zako wanaokuhurumia wakuondoe kwenye njia nyembamba ya hekima na uamuzi mzuri. Walimwengu wanasema “Usijishughulishe sana.” Lakini rafiki wa kweli wa wanadamu na aliye Mwalimu Mkuu ambaye alipata kuishi duniani alisema kinyume cha hayo. Katika kuwashauri wafuasi wake, aliwaambia: “Jitahidini kwa nguvu.”​—Luka 13:24, NW.

Kwa kweli maisha ni ya bure na hayana maana, yakiwa bila lengo lenye thamani. Na hakuna thamani inayopatikana bila uelekevu wa jitihada za kujiadibu. Mwanafunzi wa muziki anayejiwekea lengo la kupiga muziki katika jamii ya waimbaji hawezi kujihurumia anapojizoeza. Ni lazima atumie saa nyingi akijizoeza, kutulia, kujiadibu na kujinyima starehe nyingi ili atimizie lengo lake. Ni hali moja, kwa kiasi kikubwa au kidogo, na lengo la utaalamu wo wote ambao mtu anaweza kujiwekea. Jitihada za kujiadibu lazima zitumiwe ikiwa ujuzi na utalaamu huo utapatikana.

Sana-sana, ni lazima Mkristo aliyejiweka wakf aangalie asije akajihurumia mno anapostahili kujiadibu. Ni rahisi kama nini kuacha hali ya hewa isiyopendeza iwe sababu ya kutokwenda kwenye mikutano ya Kikristo ya kundi au kutoshiriki kwa bidii katika kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi! Kipindi cha televisheni kinaweza kumfanya mtu adharau wajibu wa huduma ya Kikristo. Magazeti ya kilimwengu yenye kuchapwa pindi kwa pindi na yenye kupendwa na wengi au vitabu vya hadithi vinaweza kuwa vyenye kuvuta sana hata kumfanya mtu apuze mahitaji yake ya kiroho. Mambo hayo yote ya kujihurumia kwa wakati huu tu, yanaweza kuwa na matokeo yenye madhara ya kudumu. Shairi hili la Kiingereza ni la kweli, “Kazi ikigongana na starehe, starehe na ziondolewe.” Ungojee wakati ambao kazi na starehe hazigongani.

Je! unaweza kukosa kujihurumia kwa njia isiyothawabisha? Ndiyo, ikiwa unakusudia kuwa tajiri, kupenda fedha kunaweza kukusukuma ufanye kazi, utoe jasho, utumie nguvu na hila. Kunaweza kukufanya uvunje sheria au kuharibu akili. Utafutaji wa utajiri kama huo ni kutojihurumia. Neno la Mungu laonyesha wazi kwa kusema: “Hao watakao kuwa na mali huanguka katika majaribu na tanzi, na tamaa nyingi zisizo na maana, zenye kudhuru, ziwatosazo wanadamu katika upotevu na uharibifu. Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi.”​—1 Tim. 6:9, 10.

Sheria ya pili na iliyo kuu ambayo Yesu Kristo alitoa—“mpende jirani yako kama nafsi yako”​—inahusu hasa hili. Lazima tujipende wenyewe, lazima tujihurumie lakini si kufanya hivyo kichoyo na bila akili. Kujipenda wenyewe kunathibitishwa na amri ya kwanza ambayo inatuhitaji tumpende Mungu kwa moyo, nafsi, akili na nguvu. Kutii amri hiyo kutamaanisha kwa mara nyingi “kutojihurumia.” Na kujipenda wenyewe kunathibitishwa na amri ya pili, kuwapenda jirani zetu kama sisi wenyewe. (Marko 12:29-31) Tukiuweka maanani wajibu wetu kwa Mungu wetu na kwa jirani zetu, tutaweza kuamua kati ya wakati unaotupasa na usiotupasa kujihurumia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki