Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w80 11/15 kur. 14-19
  • ‘Tumia Kila Namna ya Sala na Kusihi’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Tumia Kila Namna ya Sala na Kusihi’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUMSIFU MUNGU KATIKA SALA
  • KUMPA YEHOVA SHUKRANI
  • KUMTOLEA YEHOVA MAOMBI
  • KWA KUSIHI
  • TWAPASWA KUTENDA KULINGANA NA HAYO
  • JE! TWAWEZA KUFANYA SALA ZETU ZIWE BORA ZAIDI?
  • ZAWADI ZA MOJA KWA MOJA NA ZISIZOKUWA ZA MOJA KWA MOJA
  • “Maombi Yenu na Yajulishwe Mungu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Mkaribie Mungu Katika Sala
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Sala Zako Zinafunua Nini Kukuhusu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Jinsi ya Kusali na Kusikiwa na Mungu
    Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
w80 11/15 kur. 14-19

‘Tumia Kila Namna ya Sala na Kusihi’

“Kwa kila namna ya sala na kusihi . . . endeleeni kuomba katika kila pindi katika roho. Na kwa kusudi hilo endeleeni kukesha wakati wote na kusihi kwa ajili ya watakatifu.”​—Efe. 6:18, NW

1. (a) Twapaswa kumfikiria Yehova Mungu katika njia gani tunapomjia katika sala? (b) Kuna namna gani nne za sala?

MUUMBA, Yehova Mungu, si Mwanzilishi tu asiye na hali ya utu bali yeye ni mtu mwenye maono ya kindani. Yeye aweza kuona na kusikia. Sikuzote twapaswa kumfikiria kwa njia hiyo tunapomfikia katika sala. Neno la Mungu linatushauri tufanye hivyo “kwa kila namna ya sala na kusihi.” (Efe. 6:18, NW) Jambo hilo linatia nini ndani? Kuna namna nne za sala​—kusifu, kutoa shukrani, maombi na kusihi.

KUMSIFU MUNGU KATIKA SALA

2, 3. Ni namna gani moja ya sala iliyo bora sana na ya heshima, na ni sababu gani chache kati ya nyingi kuonyesha kwamba Yehova anastahili kutolewa sala?

2 Bila shaka kusifu ni namna ya sala iliyo bora sana na ya heshima. Muumba anaistahili kwa sababu ya sifa zake na mambo aliyofanya. Akiwa “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova,” mamlaka yake hailinganiki na ya mwingine. (2 Sam. 7:28, NW) Akiwa hana mwanzo wala mwisho, Yehova Mungu ndiye “Mfalme wa milele” aliye mzee zaidi. (1 Tim. 1:17) Yeye ni mtu mwenye utukufu mwingi mno hata kwamba hakuna mwanadamu anayeweza kumwona akaishi. (Kut. 33:20) Aliye Juu Zaidi halinganiki, mwenye uwezo na hekima isiyo na kikomo, mwenye haki kabisa na mwenye kuonyesha upendo usio na choyo. (Kum. 32:4; Ayubu 37:23; Rum. 11:33; 1 Yohana 4:8) Yeye alifanya vitu vyote na kwa hiyo ulimwengu wote ni mali yake. (Mwa. 1:1, 31; Zab. 50:10) Halinganiki katika jina wala katika kujulikana. Yeye peke yake ndiye aliye na jina Yehova, ambalo maana yake yafahamika kuwa “yeye hufanya iwe.” (Kut. 3:14, NW; 6:3) Yeye peke yake ndiye awezaye kutangaza hivi: “Mtanifananisha na nani, na kunisawazisha naye, na kunilinganisha naye, ili tuwe sawasawa?” “Mimi ni Mungu, wala hapana mwingine; mimi ni Mungu, wala hapana aliye kama mimi.”​—Isa. 46:5, 9.

3 Akiwa juu ya wengine wote, Mungu huyo asiyelinganika, asiye na kifani, mzee zaidi, ambaye hapana mwingine kama yeye, anastahili sifa yetu. Kwa kufaa, mara nyingi sana, tangu kutoka 15:11 hadi Ufunuo 19:6, tunatiwa moyo tumsifu Yehova. Kwa kupatana na hilo, tuendelee kumsifu Aliye Juu Zaidi katika sala zetu, vilevile, mazungumzo yetu ya kila siku yavute fikira kwake bali si kwetu. Hatuna kitu cho chote ambacho hatukupewa na, kama si yeye, kwa kweli hatungeweza kutimiza jambo lo lote.​—Zab. 127:1; 1 Kor. 4:7.

KUMPA YEHOVA SHUKRANI

4, 5. Waandikaji mbalimbali wa Biblia wanasema nini juu ya sisi kumtolea Yehova shukrani, na ni sababu gani chache kati ya nyingi zinazotufanya tumshukuru?

4 Jambo linalohusiana sana na kumsifu Yehova ni kumtolea shukrani. Inafaa kwamba tuonyeshe kuthamini yote yale ambayo Yehova amefanya, anayofanya na atakayofanya kwa ajili yetu. Waandikaji wa zaburi wanaonekana kuwa walitambua kwamba inafaa kumtolea Yehova shukrani zetu. Mara nyingi twasoma semi kama “[Watu] na wamshukuru [Yehova] kwa fadhili zake, na maajabu yake kwa wanadamu.” (Zab. 107:8, 15, 21, 31) Vivyo hivyo, Paulo anatushauri tutoe ‘sala za kusihi pamoja na shukrani.’ Ndiyo, twapaswa tuwe ‘tukimshukuru Mungu Baba sikuzote kwa mambo yote.’​—Flp. 4:6, NW; Efe. 5:20.

5 Ni mambo mengi sana tunayopaswa kumshukuru Baba yetu wa kimbinguni kila siku kwa ajili yake! Twapaswa tumshukuru kwa ajili ya mambo yote ya kimwili na mali tunayopata na ambayo yanafanya maisha yawezekane na vilevile yafurahishe. (Yak. 1:17) Je! twathamini baraka zote za kiroho ambazo Yehova humimina juu ya watumishi wake​—faida za dhabihu ya Kristo, Neno la Mungu na roho yake, kundi la Kikristo na zawadi ya sala? Je! twathamini baraka ya kushirikiana pamoja na waamini wenzetu, pendeleo la kuhudumia mahitaji ya wengine, na tumaini bora sana la Ufalme? Ikiwa ndivyo, ebu tutoe shukrani katika sala zetu. Ni kweli kwamba huenda sikuzote tusikumbuke au kutaja yote ambayo Mungu ametufanyia. Walakini twapaswa kuona kama vile mtunga zaburi: “Mbariki Yehova, Ee nafsi yangu, nawe usisahau matendo yake yote.”​—Zab. 103:2, NW.

KUMTOLEA YEHOVA MAOMBI

6. Maombi yetu yanahusu sehemu zipi tatu kubwa, na kwanza kabisa, Yesu alituagiza tuombe kuhusu nini?

6 Kweli kweli ni faraja kubwa kwamba twaweza kumjia Yehova kwa ‘uhuru wa kusema’ tunapotoa maombi yetu. (Ebr. 4:16, NW; 1 Yohana 3:21) Kama alivyoonyesha Yesu katika Sala ya Kiolezo, maombi yetu yanahusu sehemu zilizo kubwa​—ushindi wa haki, mahitaji yetu ya kiroho na mahitaji yetu ya kimwili. Kwa kufaa, Yesu alituambia tuombe, kwanza kabisa, jina la Yehova litukuzwe, ufalme wake uje na mapenzi yake yafanywe duniani. Yesu mwenyewe aliomba hivi: “Baba, ulitukuze jina lako.” (Mt. 6:9, 10; Yohana 12:28) Mambo ambayo yanatiwa katika maombi hayo ni kwamba Yehova afanikishe kazi ya watumishi wake duniani na kwamba awategemeze wale wanaopatwa na magumu na majaribu kwa ajili ya jina lake. (Zab. 118:25) Wala hatupaswi kupuza onyo la upole la Paulo juu ya kuwaombea wote wale walio na vyeo vya kiserikali ili “tuishi maisha ya utulivu na amani, katika utauwa wote na ustahivu.”​—1 Tim. 2:2.

7, 8. Kisha twapaswa kumwomba Yehova juu ya mambo ya kibinafsi ya namna gani?

7 Vilevile sala zetu zinapaswa zionyeshe kuhangaikia sana hali yetu ya kiroho. Jambo hilo latia ndani kuomba Baba yetu wa mbinguni atusamehe dhambi zetu. “Na kama mtu akitenda dhambi tunaye Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye haki.” (1 Yohana 1:8–2:1) Vilevile twapaswa kuomba roho ya Mungu zaidi na kwamba tusiihuzunishe. (Luka 11:13; Efe. 4:30) Wakati wa kupambana na hali zenye kujaribu, twatiwa moyo na Maandiko tuombe tupewe hekima. (Yak. 1:5-8) Zaidi ya hayo, twaweza na twapaswa kuomba baraka ya Yehova juu ya utumishi wetu mtakatifu, kutia ndani kuhubiri na kufundisha kwetu shambani. Sala hizo zinakubali kanuni ya kwamba, ingawa twapanda na kutia maji, ni Mungu anayefanya vitu vikue, anayesitawisha vitu.​—1 Kor. 3:7.

8 Zaidi ya hayo, katika kumwomba Mungu kwa bidii, tusipuze kukosana ko kote ambako huenda tukawa na ndugu yetu Mkristo, na mwenzi wetu wa ndoa au mshiriki mwingine ye yote wa jamaa yetu. Nyakati hizo yaweza kuwako maelekeo ya kuacha kupashana habari​—⁠mwendo rahisi kuchukua lakini wa upumbavu. Mahali pake, twapaswa kuomba uongozi na nguvu za kutatua tatizo hilo tulilo nalo. Vilevile na tuombe msaada wa kusamehe na kusahau manung’uniko, ili tusiwe na uchungu moyoni na kuweka kinyongo.​—Mt. 6:12.

9, 10. Tuna msingi gani wa Kimaandiko wa kumwomba Yehova kuhusiana na mambo ya kimwili?

9 Licha ya mambo ya kiroho, Yesu alionyesha kwamba inafaa tukimwomba Yehova Mungu kwa bidii atupe riziki yetu ya kila siku, mahitaji yetu ya kimwili. (Mt. 6:11) Ndiyo, twaweza kumwomba Yehova Mungu juu ya mahitaji yo yote na yote pia, kwa kila siku mojayapo. Hiyo ni kwa kupatana na aliyoendelea Yesu kusema katika Mahubiri yake ya Mlimani. “Msiwe na wasiwasi juu ya kesho; kesho itajiangalia. Kila siku ina taabu zake za kutosha.”​—Mt. 6:34, The New English Bible.

10 Je! tumekosa kupata kazi, hatujaajiriwa (hatujaandikwa)? Basi twaweza kumwomba Yehova Mungu abariki na kuongoza jitihada zetu za kupata kazi. Je! tu wagonjwa? Twaweza kuomba hekima, nguvu na uvumilivu na kupambana na ugonjwa wetu kwa njia bora zaidi iwezekanayo. Hakika ni jambo lenye kufariji kwamba twaweza kumweleza Yehova mahangaiko yetu yote, kama vile tusomavyo: “Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.” (Flp. 4:6) Bila shaka, kwa habari ya mambo yote hayo twaomba kwamba mradi​—‘Yakiwa ni mapenzi ya Mungu,’ kama vile tu Yesu alivyoomba katika bustani ya Gethsemane.​—Mt. 26:39; 1 Kor. 4:19; Yak. 4:15.

KWA KUSIHI

11-13. (a) Maana yake nini kumsihi Yehova, nalo jambo hilo lafaa sana kwa habari ya mambo gani? (b) Jambo lililoonwa na mvulana mmoja laonyeshaje hilo?

11 Tunaambiwa tuombe kwa “kila namna ya sala na kusihi.” (Efe. 6:18, NW) Sababu gani kuongeza kusihi katika maombi yetu? Kwa sababu kusihi ni zaidi ya maombi. Sana sana ni sala nzito, ya bidii, kuomba sana kutoka moyoni. Kusihi kunafasiriwa kuwa “kuomba kwa bidii sana na kwa unyenyekevu.” Katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, neno la lugha ya awali linatumiwa sikuzote kwa habari ya Mungu. Kwa hiyo linakazia uhakika wa kwamba, pamoja na kuendelea katika sala, kuna uhitaji wa kuchukua mambo kwa uzito kweli kweli. Inafahamika kwamba maombi yetu yote si kusihi. Lakini sala zetu zinapaswa kutia ndani hayo. Hata twasoma kwamba Yesu Kristo alitoa ‘sala za kusihi . . . kwa kulia sana na machozi, naye akasikiwa ifaavyo kwa ajili ya hofu yake ya kimungu.’ (Ebr. 5:​7, NW) Vivyo hivyo, tunaposikia juu ya ndugu zetu wakiteswa vikali sana, si kumwomba Mungu tu kwa ajili yao bali pia kumwomba Yehova kwa kusihi awape nguvu za kuvumilia na kushinda kusudi la mateso.​—Linganisha 2 Wakorintho 1:8-11.

12 Tunapomsihi Yehova atupe msaada katika jitihada za kupiga-piga miili yetu, kwa kufaa twaja mbele zake kama waombaji. (Rum. 7:15-24; 1 Kor. 9:27) Je! kuna tatizo la kuzuia mawazo au hasira? Basi, zaidi ya kufanya marekebisho kwa sababu labda mtu amemwudhi mwenzake, anapaswa kumsihi Yehova Mungu kwa unyenyekevu ampe msaada. Namna gani ikiwa tatizo linahusu kula au kunywa? Kwa mara nyingine, ingefaa kumsihi Yehova akupe msaada na vilevile kuomba msaada wa washiriki wa jamaa na/au wazee wa kundi.

13 Wanapokuwa wamefundishwa vizuri, hata watoto wanaweza kumsihi Yehova wasikiwe. Kwa mfano, mvulana mmoja mwenye umri wa miaka 10 aliandikia Sosaiti yafuatayo: “Katika Novemba 20 saa 9 alasiri wavulana wawili walinijia katika uwanja wa shule, naye mmoja wao akaweka kisu kooni mwangu wakitaka kuniua. Nikamwomba Yehova, na mara tu motokaa ya polisi ikapitia hapo wavulana hao wakakimbia.”

TWAPASWA KUTENDA KULINGANA NA HAYO

14, 15. Wale wanaoomba wanapaswa kupatana na nini, nayo ni mifano gani ya Kimaandiko inayoionyesha kanuni hiyo?

14 Bila shaka, tunapomwomba Yehova Mungu, twapaswa pia kuwa na nia ya kufanya sehemu yetu. Si Kwamba Mfalme Daudi alimsihi Mungu tu wakati wa taabu kubwa bali pia alichukua hatua zilizofaa. (2 Sam. 15:31–17:14) Watumishi wengineo waaminifu kwa Yehova, kama vile Yakobo, walifanya vivyo hivyo. (Mwa. 32:9-21) Ndiyo, matendo yetu yanapaswa kupatana na maombi yetu.

15 Je! twaiomba riziki yetu ya kila siku? Basi twapaswa kuwa na nia ya kufanya kazi, kwa kuwa “ikiwa mtu hataki kufanya kazi, basi, asile chakula.” (Mt. 6:11; 2 The. 3:10) Je! twaomba kwamba tusitiwe majaribuni? Basi twapaswa kuepuka kujitia makusudi katika hali zenye kuleta kukana imani. (Mt. 6:12) Je! twaomba amani iwe kati yetu? Basi twapaswa kuwa wafanya amani. (Zab. 122:​6-9; 1 Pet. 3:11) Maana yake hiyo ni kwamba twapaswa kuwa waangalifu tusikasirishe wengine bila sababu wala kufanya ugomvi usio wa lazima. Twapaswa kuepuka kuwa wenye kukasirika haraka-haraka isivyofaa. Je! sisi huomba kwamba kazi ya Mungu iongezeke? Basi twapaswa kuwa na “mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana.” (1 Kor. 15:58, NW) Je! twaomba tupate hekima? Basi vilevile twapaswa kutumia njia zote ambazo Mungu ametoa za kupata hekima.​—Yak. 1:5-8; Zab. 119:105; 2 Tim. 3:16; Ebr. 10:23-25.

JE! TWAWEZA KUFANYA SALA ZETU ZIWE BORA ZAIDI?

16, 17. Twawezaje kufanya sala zetu ziwe bora zaidi tukizifanya ziwe zenye shauku zaidi na zenye maana?

16 Sala zetu hufunua namna tunavyoyafikiria mambo ya kiroho kweli kweli. Je! twaweza kufanya sala zetu ziwe bora zaidi na, ikiwa ndivyo, namna gani hivyo? Kwanza kabisa, twapaswa kuchukua sala zetu kwa uzito na kusema yaliyo moyoni. Kwa kutafakari (kufikiri) zaidi juu ya wema wa Mungu na fadhili za upendo zake, kwa kumfikiria yeye kuwa Baba mwenye upendo ambaye vilevile ni imara kwa yaliyo haki, twaweza kufanya sala zetu ziwe zenye shauku zaidi na za kutoka moyoni. Ni kweli twataka kuzungumza na Mungu kutoka moyoni, kwa unyenyekevu. Kwa hiyo, twapaswa kujiangalia tusifanye haraka-haraka katika sala zetu. Ingawa mambo mengine yanaweza kupuzwa, sala zetu zisipuzwe kamwe.

17 Vilevile twaweza kufanya sala zetu ziwe bora zaidi kwa kujitahidi tusitumie maneno na semi zile zile tena na tena. (Mt. 6:7) Kurudia-rudia huko kwaweza kufanya zikose maono ya moyoni kabisa na kukosa maana ya kweli. Maneno ya kukariri, inaelekea zaidi yanatoka katika akili wala si katika moyo. Sana sana Wakristo wanaoongoza katika sala za jamaa kila siku wanapaswa kuwa waangalifu katika habari hiyo. Kutumia maneno yale yale siku baada ya siku kwaweza kufanya akili za wale wanaosikiliza zitange-tange. Kutafakari kila siku mawazo ya Kimaandiko na kusitawisha kuthamini kwingi zaidi fadhili za Yehova zisizostahilika tunazoonyeshwa kwaweza kutusaidia kufanya sala zetu ziendelee kuwa na shauku na zenye maana.

ZAWADI ZA MOJA KWA MOJA NA ZISIZOKUWA ZA MOJA KWA MOJA

18. Sababu gani wengine ambao hawatimizi matakwa ya Mungu juu ya sala zinazokubalika hukata shauri kwamba maombi yao yamejibiwa?

18 Sala ni namna ya ibada inayofanywa ulimwenguni pote. Watu wengi huamini kwamba Mungu hujibu sala zao, hata ingawa maombi yao hayatimizi matakwa ya kimungu ya sala. Jambo hilo linaloelekea kupingana laweza kuelezwaje? Jambo moja, inaweza kuwa ni namna tu mambo yanavyotukia. Kwa mfano, husemekana kwamba askari wote wanaokuwa katika mahandaki huomba. Kwa kuwa wakati mwingi wengi wao huokoka, wanaookoka huenda wakakata shauri kwamba Mungu alijibu sala zao. Au, labda hilo ni tukio lililotokea kwa wakati ule ule likalingana na tukio jingine. Halafu tena, huenda sababu ikawa ni kawaida ya kutendeana kwa akili na mwili, yaani, matokeo ya akili juu ya mwili.

19. Kuna ushuhuda gani kwamba Yehova Mungu hujibu sala za wale walio watu wake kweli kweli na ambao wanatimiza matakwa ya sala?

19 Hata hivyo, wale wanaotimiza matakwa ya kimungu ya sala wana ushuhuda usiokanushika kwamba Yehova Mungu hujibu sala zao kweli kweli. Wameona baraka ya Yehova juu ya jitihada zao za umoja na za kibinafsi. Kama matokeo, ‘mdogo amekuwa elfu, na mnyonge akawa taifa hodari.’ (Isa. 60:22) Katika kujibu sala zao, Yehova ameongoza mambo hata kwamba ‘kila silaha iliyofanywa juu yao haikufanikiwa.’​—Isa. 54:17.

20. Yehova hujibu maombi yenye unyofu wa moyoni anayoombwa kupitia kwa njia gani mbalimbali?

20 Yehova hutumia watumishi wake wa kimbinguni na wa kidunia pia katika kujibu mambo ya unyofu wa moyo yanayotolewa kwake. Nyakati nyingine, malaika ndiye anayeongoza mambo ili kwamba mtu anayemtafuta Mungu kwa njia ya sala atembelewe nyumbani mwake na mmojawapo wa watumishi wa Yehova. (Linganisha Matendo 10:​30-33; 17:26, 27.) Kisha tena, Yehova hujibu sala nyingi kupitia kwa vyombo vyake vya kidunia. Anaweza kuweka katika akili ya mmojawapo wa watu wake aonyeshe upendo au afanye tendo la fadhili kwa mtu anayestahili ambaye ana uhitaji kweli kweli. Au, jibu la sala ya mtu laweza kuja kupitia kwa funzo la Neno la Mungu, kwa kusoma kwa uangalifu kitabu ambacho msingi wake ni Biblia, au mambo ambayo yanavutwa katika fikira zake na wazee katika kundi. Hiyo inakuwa hivyo kwa sababu sala za watumishi wa Yehova mara nyingi zinakuwa za kuelimisha au kuomba hekima katika kukabiliana na hali fulani.

21. Ni faida gani za sala zisizokuwa za moja kwa moja?

21 Pamoja na hayo, twaweza kupata faida zisizokuwa za moja kwa moja kwa kusali. Uhakika wa kwamba tumejikabidhi kwa Yehova bila mzigo, Baba yetu wa kimbinguni, hutufanya tujione kuwa tuko karibu sana naye. Kwa kumwonyesha kuthamini katika kusifu na kushukuru, twasaidiwa kuridhika (kutosheka) zaidi na fungu letu. Kwa kumsihi sana Yehova kwa sala, twasaidiwa tuwe wanyenyekevu na kumtegemea yeye mahali pa kutegemea ufahamu na nguvu yetu. (Mit. 3:​5, 6; Flp. 4:13) Na, Bila shaka, tunapoomba, akili zetu zinafikiria mambo yenye kujenga. (Flp. 4:4-8) Kwa mfano, unaposhindwa kulala usiku, hakika ingefaa zaidi kuomba juu ya faida za Ufalme na mambo ya kiroho kuliko kuwa na wasiwasi au kuhangaika, kufikiria huzuni, kufikiria mambo yasiyowezekana au kuacha akili zetu zirudie mambo ya mwili. Ndiyo, twataka ‘kumtupia Yehova mahangaiko yetu yote, kwa sababu anatujali.’ Tusipomficha cho chote Baba yetu wa kimbinguni, hilo litatusaidia tujichunguze wenyewe na kutuwezesha tumkaribie zaidi na kuhusiana naye zaidi.​—1 Pet. 5:7; 2 Kor. 13:5.

22. Maana yake nini kuchukua sala zetu kwa uzito, ikitokeza uhakika gani?

22 Kweli kweli, sala, kutia ndani kusifu, shukrani na kusihi, ni pendeleo lenye thamani, nasi tutafaidika sana tukichukua sala zetu kwa uzito. Huonyesha kwamba tuna imani kweli kweli. Hakika, twataka kutenda kulingana na sala zetu, tusiziseme haraka-haraka kamwe, wakati wote tujaribu kuzifanya ziwe bora zaidi, na tusiziachilie ziwe jambo la kawaida la kurudia maneno. Kufanya hivyo, kutatufaidi kwa njia isiyokuwa ya moja kwa moja, nasi twaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova Mungu atatuthawibisha kwa kujibu sala zetu zinazopatana na mapenzi yake.

​—Kutoka The Watchtower June 1, 1980.

[Picha katika ukurasa wa 15]

Twapaswa kumshukuru Mungu kwa ajili ya Neno lake, vitu vya lazima maishani, kundi la Kikristo na mapendeleo ya sala na utumishi.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki