Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • tr sura 17 kur. 151-156
  • Jinsi ya Kusali na Kusikiwa na Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi ya Kusali na Kusikiwa na Mungu
  • Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • NJIA YA KUMKARIBIA MUNGU KATIKA SALA
  • SALA ZINAZOPENDEZA KWA MUNGU
  • JINSI IFAAYO YA KUSALI
  • KUTHAMINI PENDELEO LA SALA
  • Mkaribie Mungu Katika Sala
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Namna ya Kupata Msaada kwa Sala
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Je! Mungu Anasikiliza Sala Zako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Sala Ambazo Zinajibiwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
Pata Habari Zaidi
Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
tr sura 17 kur. 151-156

Sura ya 17

Jinsi ya Kusali na Kusikiwa na Mungu

1. Zaburi 65:2 inasema nini juu ya Mungu, na ni nani awezaye kuja kwake na tumaini la kusikiwa?

BIBLIA husema kwa habari ya Yehova Mungu: “Wewe usikiaye kuomba, wote wenye mwili watakujia.” (Zaburi 65:2) Naam, Mungu huzisikia sala. Na watu waliomo katika dunia yote ambao huipenda kweli, watamanio sana kufanya mapenzi yake, na ambao humkaribia yeye katika njia ambayo yeye huikubali, wanaweza kujifurahisha pendeleo hili la thamani. (Matendo 10:34, 35) Kweli, ni pendeleo la ajabu namna gani kuweza kuzungumza kwa Mtawala mwenye utukufu wa ulimwengu wote mzima na kujua kwamba yeye hukusikia wewe!—Zaburi 8:1, 3, 4; Isaya 45:22.

2. (a) Kwa habari ye sala, ni ahadi gani ambayo Biblia hutoa katika Wafilipi 4:6, 7? (b) Kwa nini wengine huona shaka juu ya sala?

2 Kwa kutia moyo, Neno lake lililoandikwa huahidi: “Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu. Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.” (Wafilipi 4:6, 7) Walakini, huenda wengine wakaona shaka juu ya shauri la sala kwa sababu nyingi za sala zao huonekana kuwa zimetolewa bila kujibiwa. Kwa nini iko hivi? Ni jambo la muhimu kwetu kujua. Katika Neno lake, Mungu husema wazi ni nini mapenzi yake kwa habari ya sala.

NJIA YA KUMKARIBIA MUNGU KATIKA SALA

3. Sala zetu zote zimepaswa kuelekezwa kwa nani, na kwa nini?

3 Biblia inatuambia kwamba “yeye ambaye humkaribia Mungu lazima asadiki kwamba yeye yuko na kwamba yeye huwa mthawabishaji wa wale wanaomtafuta yeye kwa moyo.” (Waebrania 11:6, NW) Angalia kwamba andiko hili lasema inatubidi ‘kumkaribia Mungu.’ Kama Mungu wa kweli na aliye hai, Yehova hutaka sisi tusali kwake, si kwa mtu fulani mwingineo. Sala ni sehemu ya ibada yetu na kwa sababu hii imepasa ielekezwe kwa Muumba, Yehova peke yake. (Mathayo 4:10) Yesu Kristo aliwafundisha wafuasi wake kusali kwa ‘Baba yake aliye mbinguni.’ (Mathayo 6:9) Yesu hakuwafundisha kusali kwake mwenyewe, wala kwa mamaye wa kibinadamu Maria-mu, wala kwa mtu ye yote mwingine. Yehova ni mwenye nguvu zote, mwenye hekima yote, mkamilifu katika haki na katika upendo. Basi, kwa nini tumwendee mtu ye yote aliye mdogo zaidi? Tena, mtume Paulo aliyeongozwa na roho ya Mungu hutuhakikishia kwamba Mungu “hawi mbali na kila mmoja wetu,” ikiwa tunamtafuta katika njia ya kweli.—Matendo 17:27.

4. Kwa sala zetu kukubalika kwa Mungu, ni katika jina la nani zimepaswa kutolewa? Kwa nini?

4 Labda utasema, “Sisi kama viumbe visivyokamilika wenye dhambi iliyorithiwa, twawezaje kusali kwa Mungu ambaye ni mkamilifu na mwenye haki?” Kwa upendo Yehova ameangalia jambo hili na akatayarisha “Mwombezi” kusema kwa ajili yetu mbinguni. Mwombezi huyo ni “Yesu Kristo mwenye haki.” (1 Yohana 2:1, 2) Yeye alitoa uhai wake kama ukombozi kwa wanadamu. Tena, Yehova amemweka yeye kuwa kama Kuhani Mkuu. Yehova hutaka sisi tutambue cheo cha Mwanawe katika kusudi Lake na kutoa sala zetu zote katika jina lake. Ndiyo sababu kwa nini Yesu aliwaambia wafuasi wake hivi: “Mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.” (Yohana 14:6) Pia Yesu alisema: “Mkimwomba Baba neno lo lote atawapa kwa jina langu.” (Yohana 16:23) Ili sala zetu ziwe zenye kukubalika kwa Mungu, basi, lazima tusali kwa Yehova Mungu kupitia kwa Mwanawe, yaani, katika jina la Yesu.

SALA ZINAZOPENDEZA KWA MUNGU

5. (a) Kwa sababu ya yale ambayo 1 Petro 3:12 husema, jinsi gani imetupasa kwa unyofu wa moyo kujaribu kuishi maisha zetu ikiwa sala zetu zitasikiwa na Mungu? (b) Ni nani ambaye hangepaswa kumtarajia Mungu kusikia sala zake kwa msaada?

5 Katika 1 Petro 3:12 tunasoma hivi: “Macho ya [Yehova] huwaelekea wenye haki, na masikio yake husikiliza maombi yao.” Hivyo, ikiwa sala zetu zitampendeza Mungu, lazima tuwe na unyofu wa moyo katika kujaribu kuishi maisha zetu katika kupatana na kanuni za haki za Neno la Mungu. Ikiwa mtu anakataa Neno la Mungu na mapenzi yake hangepaswa kumtarajia Mungu kujibu sala zake kwa msaada katika wakati wa taabu. (Mithali 15:29; 28:9) Kwa mfano, kwa wale wasioheshimu utakatifu wa uhai, Mungu husema: “Mwombapo maombi mengi, sitasikia; mikono yenu imejaa damu.” (Isaya 1:15) Katika huu “wakati wa mwisho” wakati jeuri, ufisadi, udanganyifu, ibada ya uongo na mwenendo mwingine mbaya vinapoenea zaidi na zaidi, bila shaka lazima sisi tuangalie kwa uzito njia ambayo tunaishi maisha zetu za kila siku ikiwa tunataka sala zetu zisikiwe na Mungu.—1 Yohana 3:21, 22

6. (a) Kupatana na maagizo ya Yesu, ni mambo gani lazima yawe ndiyo ya kwanza kufikiria katika sala zetu (b) Jinsi gani Yesu alionyesha kwamba sala zetu hazipaswi kuwa kwa ajili yetu wenyewe tu? Basi, imetupasa tuombee nani?

6 Jambo ambalo tunaombea pia lina mengi ya kushughulika na kuamua kama Mungu atazijibu sala zetu. Yesu aliwapa wanafunzi wake sala ya kielelezo kuwaongoza kwa aina ya sala ambayo Mungu hukubali. (Mathayo 6:9-13) Sala hii huonyesha kwamba jina na makusudi ya Mungu lazima yawe ndiyo mambo ya kwanza kwetu kufikiria. Pili, twaweza kuombea mahitaji yetu ya kimwili, msamaha na kuokolewa na vishawishi na yule mwovu. Angalia, pia, kwamba Yesu hutufundisha sisi kusali kwa “Baba yetu” “utupe [sisi] leo riziki zetu” na “utusamehe [sisi].” Jambo hili laonyesha kwamba, wakati wa kusali, haimpasi mtu kufikiria yake mwenyewe tu, au juu ya matatizo yake na mahitaji yake mwenyewe. Badala yake imempasa bila choyo apanue sala zake huwatia na wengine. Haitupasi kutia jamaa na watu wa ukoo wetu wenyewe tu, bali na wengine wanaotafuta kumpendeza Mungu, na hasa wale wanaokabili majaribu na shida katika utumishi wao kwa Mungu.—Yakobo 5:16; Waefeso 6:18-20.

7. (a) Ni jambo gani la kwanza kwa nini sala nyingi hutolewa bila kujibiwa? (b) Ili kutoa sala zinazokubalika, imetupasa kufanya nini kwanza?

7 Mtume Yohana huandika: “Huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia.” (1 Yohana 5:14) Naam, kila sehemu ya maisha ya Mkristo ni jambo linalofaa kwa sala. Lakini jambo la muhimu ni la kwamba jambo ambalo yeye anaomba lipatane na mapenzi ya Mungu. Hii ndiyo sababu ya kwanza kwa nini sala nyingi hutolewa bila kujibiwa. Kwanza mtu hakujaribu kujua mapenzi ya Mungu ni nini. (Mithali 3:5-7) Hivyo, badala ya kuamua ni jambo gani ambalo sisi tunataka kufanya au kuwa nalo, na kusali kwa Mungu juu ya jambo hilo, je! si afadhali kujua kwanza Mungu anataka nini kwetu, ni nini mapenzi yake kwetu, ndipo tutunge sala zetu kupatana nayo?—Yakobo 4:3, 13-15.

8. (a) Jinsi gani twaweza kuelewa mapenzi ya Mungu? (b) Je! kweli Mungu atatupa sisi hekima kuongoza mwendo wetu katika maisha?

8 Kwa funzo letu la Neno la Mungu na kwa mambo tuyaonayo katika kumtumikia yeye katika ushirika na Wakristo wengine wa kweli twaweza kufahamu mapenzi yake. (Warumi 12:2) Mtunga zaburi alisali hivi: “Unifahamishe nami nitaishika sheria yako, naam, nitaitii kwa moyo wangu wote. Uniendeshe katika mapito ya maagizo yako, kwa maana nimependezwa nayo. Unielekeze moyo wangu na shuhuda zako, wala usiielekee tamaa.” (Zaburi 119:34-36) Ikiwa tunasali kwa Mungu katika imani, yeye kwa ukarimu atatupa sisi hekima tunayohitaji katika kushindana kwa kufaulu na matatizo ya maisha. (Yakobo 1:5-8) Yeye atatusaidia sisi kujua na kufanya jambo litakaloleta heshima kwa jina lake mwenyewe lililo kuu, na jambo hili pia litatokea katika furaha yetu wenyewe.—Zaburi 84:11, 12.

JINSI IFAAYO YA KUSALI

9. (a) Wakati tunaposali, je! kunatakiwa kikao fulani cho chote? (b) Yesu alionyesha nini juu ya sala ya peke yako? (c) Ni kusali kwa aina gani ambako Yesu alilaumu?

9 Je! Mungu anataka sisi tujitwalie kikao fulani wakati wa kusali au kwamba twende kwenye jengo fulani kusali? Neno lake linasema kwamba yeye hataki. (Nehemia 8:6; Danieli 6:10; Marko 11:25; Yohana 11:41) Yesu alionyesha kwamba inafaa kuwa na faragha katika sala ya peke yako, mtu akiingia katika chumba chake mwenyewe kwa kusali. (Mathayo 6:6) Na ijapokuwa Yesu mwenyewe nyakati fulani alisali katika mahali pa hadhara, yeye alilaumu kwa nguvu kusali mbele ya wengine kwa kusudi tu la kutazamwa na wao na mtu kujionyesha “utakatifu” wake. Alionyesha pia kwamba Mungu hakubali kutumia maneno yale yale kwa kuyarudiarudia katika sala. (Mathayo 6:5, 7, 8) Kwa nini iko hivi?

10. (a) Eleza sababu kwa nini haipasi sala zetu zisomwe kutoka katika kitabu cha sala? (b) Ni msemo wa aina gani ambao imetupasa kuutumia wakati tunaposali?

10 Ni kwa sababu jambo ambalo ni la muhimu kwa Mungu ni lile lililomo katika moyo wetu. “Maana macho ya [Yehova] hukimbia-kimbia duniani mwote, ili ajionyeshe mwenye nguvu kwa ajili ya hao, waliokamilika moyo kuelekea kwake.” (2 Mambo ya Nyakati 16:9) Jinsi gani sala yetu ingeweza kuonyesha jambo lililomo katika moyo wetu ikiwa inasomwa tu katika kitabu cha sala? Basi, wakati tusalipo, imetupasa kufanya hivyo kutoka katika moyo, kwa unyenyekevu. “Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu.” (Yakobo 4:6) Katika sala zetu hamna thamani katika kutumia msemo usio wa kawaida au msemo wenye majivuno. Badala yake, ime-tupasa tuzungumze kwa Mungu kama vile tungefanya kwa rafiki yetu wa karibu na mwenye kuaminiwa na kama mtoto kwa babaye. Sala yetu yaweza ikawa hata ya kimya, moyoni mwetu wenyewe. (1 Samweli 1:12, 13) Huenda nyakati fulani tusipate maneno yaliyo sahihi ya kusema mawazo yetu kwa Mungu. Lakini tunaweza kuwa watumainifu kwamba Mungu yuazijua haja zetu naye ataelewa sala yetu iliyo rahisi.

KUTHAMINI PENDELEO LA SALA

11. (a) Je! imetupasa tungojee mpaka wakati tunapohitaji msaada wa pekee kabla ya kusali kwa Mungu? (b) Kwa nini sala inafaa katika nyakati za chakula?

11 Sisi sote huwa tunazifikia nyakati katika maisha zetu wakati hapana msaada wa kibinadamu unaopatikana au wakati msaada ambao wanadamu hutoa hautoshi kwa mahitaji yetu. Ndipo inatupasa kugeukia kwa Mungu peke yake. Walakini, ikiwa twampenda Yehova na tunathamini pendeleo la sala bila shaka hatutangojea nyakati za namna hiyo ndipo tuseme kwake. Badala yake, tutamkaribia yeye kwa kawaida, mara kwa mara, na maonyesho ya kutoa shukrani na sifa, na pia na maombi na dua zetu. (Waefeso 6:18; 1 Wathesalonike 5:17, 18) Jamaa hufaidika sana na sala, hata usemi ulio rahisi wa shukrani kwa Mungu katika nyakati za chakula, kwa kufuata mfano wa Yesu.—Mathayo 14:19.

12. Eleza baadhi ya faida za ajabu za sala?

12 Kweli, sala ya faragha, sala ya jamaa na sala ya kundi zote huleta faida za ajabu. Sala huonyesha utambuzi wa wazi wa tegemeo letu kamili juu ya Mungu kwa kila kitu. Inatuvuta karibu na waabudu wenzetu. Inaleta juu yetu amani ya Muumba mwenye upendo. Inakuza mtiririko wa roho takatifu ya Mungu katika maisha zetu. Inatusaidia kuwa watumainifu juu ya wakati ujao. Ni karama kutoka kwa Mungu ambayo imetupasa kuthamini na kuitumia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki