Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 3/15 kur. 4-7
  • Sala Ambazo Zinajibiwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sala Ambazo Zinajibiwa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Habari Zinazolingana
  • Mkaribie Mungu Katika Sala
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Ni Sala za Nani Hujibiwa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Je! Mungu Anasikiliza Sala Zako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Ni Sala za Nani Hujibiwa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 3/15 kur. 4-7

Sala Ambazo Zinajibiwa

ILE tamaa ya kuwasiliana na nguvu fulani ya juu zaidi ni ya rika moja na mwanadamu mwenyewe. Mathalani, maandishi fulani ya kutiwa nakshi ya Kimisri yana sala kadhaa. Baadhi ya hayo yaliomba himaya kutoka kwa mungu fulani, hali mengine yalikuwa taarifa za sifa au za uhakika katika kiabudiwa kilichokuwa kikisemeshwa. Miongoni mwa Wagiriki wa karne ya nane K.W.K., tenzi za kidini na pia sala za kishairi na kisherehe zilikuwa kawaida. Katika sala za Kiroma, uangalifu ulihitajiwa katika kusemesha mungu fulani hususa, kwa kuwa wakati huo ni waungu wengi walioabudiwa.

Mpaka leo hii, sala ni sehemu ya kawaida ya dini zile kubwa-kubwa za ulimwengu. Wanaojulikana sana kwa kutumia-tumia sala ni wafuasi wa Buddha, Wahindu, Wayahudi, Waislamu, na wale wanaojidai kuwa wanafuata Ukristo. Ingawa sala imeenea sana katika dini ya karne ya 20, zile namna nyingi sana za njia na mitindo ya kutoa sala zinatatanisha wengi wanaotafuta kujibiwa sala zao.

Je! Sala Yo Yote Tu Itafaa?

Kwa kuwa sala ni ya namna nyingi, je! sala yo yote tu itakuwa na matokeo mazuri? Watu fulani wanahisi kwamba maadamu mtu mwenye kusali ana weupe wa moyo na “anaitikadi,” si kitu sana hata akitumia sala ya namna gani. Wewe unaonaje? Kwa sababu ya kupitana-pitana kwa maoni juu ya jambo hilo, inahitajiwa kabisa kuchukua hatua inayoyazidi maoni ya wanadamu na kutafuta habari zilizofunuliwa kutokana na chanzo cha juu zaidi.

Majibu yaliyo katika kurasa zinazofuata yametolewa katika chanzo hicho, Biblia Takatifu. Hiyo inaonyesha kwamba ikiwa mtu anatazamia kusikiwa na kujibiwa, si sala yo yote tu itakayofaa.

Biblia Inaeleza:

Ni nani ambaye sala zinapasa kuelekezwa kwake

Sababu gani sala fulani-fulani hazijibiwi

Ni mambo gani yanayoweza kuombwa katika sala

Ni sehemu gani ambayo mtu mwenye kutoa sala anashiriki?

Takwa moja kubwa ni imani, si weupe wa moyo tu kwamba Mungu yuko na anaweza kuzisikia sala. (Waebrania 11:6) Imani hiyo inaonyeshwa katika kujitahidi kuishi kwa kupatana na kanuni za uadilifu za Mungu zilizoonyeshwa wazi katika Biblia. Katika Mahubiri ya Mlimani yake, Yesu Kristo alikazia jambo hili: “Si kila mmoja ambaye anaita mimi ‘Bwana, Bwana’ ataingia katika Ufalme wa mbinguni, bali ni wale tu ambao wanatenda kile ambacho Baba yangu katika mbingu anataka wao watende.”​—⁠Mathayo7:​21, Today’s English Version.

Kama kielelezo cha wale ambao sala zao hazingesikiwa, Isaya nabii Mwebrania aliandika hivi: “Hata ingawa ninyi mfanye sala nyingi, mimi [Yehova Mungu] siwi ninasikiliza; mikono yenu yenyewe imekuwa yenye kujazwa umwagaji-damu.” (Isaya 1:​15, NW ) Kwa hiyo watu wo wote ambao hawastahi utakato wa uhai hawawezi kutazamia sala zao zisikiwe, hata kama wao wanasali mara ngapi na kwa juhudi ya namna gani.

Kwa sababu gani mara nyingi “waitikadi” fulani hawapati majibu kwa sala zao?

Itikadi tu haitoshi kupendeza Mungu na kumfanya ajibu sala zetu. Hata mtu mwenye kukubali-kubali mambo bila msingi mzuri anaweza kudai kuwa mwenye itikadi. Ili itikadi iwe na uzito unaostahili, ni lazima itegemezwe juu ya msingi wa maarifa sahihi, ambayo yanaweza kupatwa kwa funzo la Biblia tu. Kwa kuongezea, ni lazima itikadi na imani zithibitishwe na kazi ambazo hizo zinatokeza. “Kama vile mwili pasipo roho umekufa, hivyo pia imani pasipo kazi imekufa.”​—⁠Yakobo 2: 26, NW.

Mwitikadi wa kweli angehitaji kufikiria Mungu kila siku, si kukimbilia sala wakati tu anapoelekeana na dharura. Yeye angetenda pia vitendo vya imani, kazi zinazofaa ambazo ni kutia ndani kuambia wengine itikadi na imani yake katika Mungu.

Sala inapasa kuwa ya namna gani?

Sala haipasi kuwa desturi ya kidini tu, wala haipasi kusomwa kutokana na kitabu fulani. Wala sala haipasi kuwa na vifungu vya maneno ya kurudiwa-rudiwa kama kwamba mrudio-rudio unaipa matokeo yenye nguvu zaidi. Na sala haipasi ‘kufanywa kitamasha’ ili kuonyesha au kuvutia wengine. Yesu alitoa shauri hili jema juu ya namna ambayo sala zetu zinapasa kuwa nayo na mambo ambayo inatupasa kuepuka: “Wakati ninyi mnaposali, lazima ninyi msiwe kama wanafiki; kwa sababu wao wanapenda kusali wamesimama katika masinagogi na pembe za zile njia pana ili waonekane kwa wanadamu. . . . Wakati mnaposali, msiseme mambo yale yale tena na tena, sawa na vile watu wa mataifa wanavyofanya, kwa maana wao wanawazia watapata usikizi kwa kutumia kwao maneno mengi.”​—⁠Mathayo 6:​5-7, NW.

Hakuna kikao fulani cha kimwili ambacho kimeandikiwa sala ili ziweze kusikiwa. Hata hivyo, mwenye kusali angehitaji kuwa mnyenyekevu na mwenye staha katika kikao na katika maneno pia yanayotumiwa katika sala yake.

Sala zinapasa kuelekezwa kwa nani?

Kitabu cha Biblia cha Waebrania kinasema juu ya mtu ambaye ‘anafikia Mungu.’ (Waebrania 11:​6, NW ) Ni nani Mungu huyo? Kuna Mungu Mweza Yote mmoja tu, ingawa kuna miungu mingi bandia ya kutengenezwa na wanadamu. (1 Wakorintho 8:​5-6) Yule Mungu Mweza Yote wa Biblia anaitwa jina lake Yehova. (Zaburi 83:18) Yeye ndiye Muumba wa vitu vyote, na kwa hiyo sala inapasa kuelekezwa kwake tu. Kwa uwazi Yesu Kristo alifundisha wafuasi wake kusali hivi: “Baba yetu uliye katika mbingu.” (Mathayo 6:​9, NW ) Yesu hakufundisha wanafunzi wake kusali kuelekea yeye, kuelekea Mariamu mama yake, wala kuelekea mtu mwingineye yote. Lakini Mungu sasa anatoa takwa la kwamba sisi tutambue cheo cha Mwana wake na kutoa sala zetu zote katika jina la Yesu. Hiyo ndiyo sababu Kristo aliambia wafuasi wake hivi: “Hakuna mmoja ambaye anakuja kwa Baba isipokuwa kupitia mimi.”​—⁠Yohana 14:​6, NW.

Basi, ili sala zikubalike kwa Mungu ni lazima zielekezwe kwa Yehova Mungu kupitia Mwana wake, Yesu Kristo. Yaani, ni lazima zisemwe kuelekea Mungu katika jina la Yesu.

Ni mambo gani yanayoweza kuombwa katika sala?

“Hata kiwe ni kitu gani ambacho tunaomba kulingana na mapenzi yake, yeye [Mungu] anatusikia.” Huo uhakikisho kamili unaoonekana kama kwamba haustahili kuaminiwa umeandikwa kwenye 1 Yohana 5:​14, NW. Lakini je! wewe umeona sharti linalohusika​—⁠“kulingana na mapenzi yake”? Ndiyo, sababu moja kubwa sana inayofanya sala nyingi zisijibiwe ni kwamba mwenye kusali hajajaribu kwanza kutafuta ajue mapenzi ya Mungu ni nini.​—⁠Mithali 3:​5-7.

Yesu aliwapa wanafunzi wake sala ambayo leo inajulikana kote kuwa “Sala ya Bwana,” ili iwe mwongozo au kiolezo chenye msaada. (Mathayo 6:​9-13) Ingawa hata hiyo haipasi kusemwa kama desturi ya kidini tu, inaonyesha waziwazi mambo yanayofaa kutangulizwa. Kwanza linakuja jina na kusudi la Mungu. Halafu yanaorodheshwa mahitaji ya kimwili, msamaha, na kukombolewa kutoka ushawishi wa yule mwovu. Yale maneno “Baba yetu”yanaweza kusaidia mwenye kusali apanue sala zake na kufikiri kwake ili awatie ndani, si washiriki wa jamaa na watu wa ukoo tu, bali pia wengine wanaotafuta kupendeza Mfanyi wao.​—⁠Matendo 17:​26, 27.

Sala zinapasa kuwa na urefu gani?

Biblia haionyeshi waziwazi urefu wo wote ambao sala zinapasa kuwa nao. Hizo zinaweza kuwa fupi au zinaweza hata kutolewa kwa kimya. (Nehemia 2:4; 1 Samweli 1:​12, 13) Kwa upande ule mwingine, sala zinaweza kuwa ndefu sana. Ilikuwako pindi moja ambapo Yesu “aliendelea usiku mzima katika sala kwa Mungu.” Inaonekana alifanya hivyo kuomba usaidizi wa kimungu katika kuchagua mitume wake 12. (Luka 6:​12, NW ) Kwa hiyo urefu wa sala zenye kukubalika unatofautiana kulingana na mahitaji.

Ni Wazi Kabisa Kwamba Sala Zinajibiwa

Biblia ina masimulizi tele ya sala ambazo zilijibiwa na yule “Msikiaji wa sala” aliye mkuu, Yehova Mungu. (Zaburi 65:​2, NW ) Kielelezo cha kutokeza ni ule “mtihani wa sala” katika siku za Eliya nabii, ambao umeandikwa katika kumbukumbu katika 1 Wafalme sura 18. Katika karne ya kwanza, wanafunzi wa Yesu walipata jibu hili la mara hiyo kwa sala: “Wao walipokuwa wamefanya dua, mahali ambapo wao walikuwa wamekusanyika pamoja palitikiswa; na mmoja kwa wote wakajazwa kwa roho takatifu na wakawa wakisema neno la Mungu kwa ujasiri.”​—⁠Matendo 4 23-31, NW.

Miongoni mwa mambo mengi yaliyoonwa ambayo yamepokewa na wachapishaji wa jarida hili ni yale ya wanaume na wanawake wa umri wote ambao walihisi wamefikia hatua hatari maishani. Kwa sababu ya tokeo la kufanya hivyo, wao wanasadiki kwamba sala zao zimesikiwa na kujibiwa.

Kielezi ni hiki: Kijana mwanamume mmoja mwenye kuishi katika bonde la mlima wa Switzerland karibu na mpaka wa Italia anasema: “Mimi nilikuwa hoi kabisa katika kupata utatuzi [kwa matatizo ya maisha] hata nikaona ni laiti ningekufa. . . .

Nilifanya jambo lile moja tu lililokuja akilini mwangu. Nilisali hivi: ‘O Mungu usiyejulikana, bila shaka wewe uko, na bila shaka wewe ni Mungu wa upendo. Nisaidie mimi! Mimi siwezi kusonga mbele ya hapo​—⁠nisaidie mimi kupata ukweli.’ “Siku chache baadaye, vijana wawili waliofunga ndoa, ambao walikuwa Mashahidi wa Yehova, walizuru mwanamume huyo. Funzo la Biblia lilianzwa, na sasa yeye ni shahidi aliyebatizwa wa Yehova.

Mwanamke mmoja aliye muuguzi-msajiliwa ambaye alikuwa na maisha yasiyo na furaha kwa sababu ya mume wake kutembea ovyo-ovyo na wanawake, halafu mwishowe wakatengana, alikuwa mwanadini kwa kina kirefu. Siku moja yeye alisali sana, akijitetea kwamba Mungu amjulishe kama yeye [Mungu] alikuwa na kusudi lenye mafaa. Alasiri hiyo hiyo, Mashahidi wa Yehova walikuja mlangoni kwake wakiwa katika kazi yao ya nyumba kwa nyumba. Yeye aliwaalika ndani ya nyumba yake, akauliza maswali mengi, na kufurahia kupokea majibu ya Kimaandiko. Baada ya muda, muuguzi mwenyewe akawa mtangazaji wa zile “habari njema” na akawa akiongoza funzo la Biblia.​—⁠Mathayo 24:14.

Mmoja wa Mashahidi wa Yehova alikuwa akisoma Mnara wa Mlinzi katika gari lake wakati mtu fulani alipomshika shingoni kwa ghafula. Yeye alimpelekea sala Yehova Mungu kwa juhudi. Mshambulizi yule akazubaa pale pale, na kulegeza fumbato lake. Shahidi alichoma gari moto, akamwaga mwanamume huyo, na kumwacha amesimama kama kinyago katikati ya barabara.

Katika ulimwengu wa makisio-kisio na mashaka yanayoongezeka, wapenda Mungu na ukweli wanaweza kujipa moyo kutokana na uhakikisho chanya kwamba sala zinazotolewa kuelekea Yehova Mungu, kupitia ule mfereji unaofaa, katika ile njia inayofaa, na kwa ule mwelekeo unaofaa wa akili na moyo, zinasikiwa. Si kwamba Mungu Mweza Yote atasikia tu sala hizo bali yeye atazijibu pia pasipo kushindwa, kulingana na mapenzi yake ya kimungu na kwenye wakati wa chaguo lake.

[Box on page 4]

Namna za Sala

Uchunguzi mfupi wa namna mbalimbali za sala zinazotumiwa leo utatoa mwanga wenye kuelimisha.

Inayotumiwa mara nyingi katika dini ya Kihindu ni sala moja ya msingi ambayo inampa heshima za ibada mungu au mungu-mke fulani aliyechaguliwa, na inafikiriwa miungu hao ni 330,000,000 katika mahekalu yapatayo 10,000. Ingawa hivyo, mara nyingi zaidi Wahindu wanatumia namna ya sala yenye madoido ambayo inaweza kuwa ya namna mbili​—⁠ama utafakari (dhyana) ama sifa (stotra). Umaana mwingi unawekwa juu ya kusema sala kwa sauti kubwa.

Katika makao ya Kichina ya watawa walio wafuasi wa Buddha na Watao, sala zinasemwa kwa ukawaida mara tatu kwa siku (mapema asubuhi, adhuhuri, na usiku). Sala hizo zinaandamanwa na mlio wa kengele ndogo. Ili kuwasaidia kusali, watawa walio wafuasi wa Buddha wanachukua uzi wenye shanga 108. Wanadini fulani wasio na cheo wanatumia njia hiyo ya kuwa na tasbihi ili kuhesabu mara ambazo sala zinasemwa.

Kwa habari ya Waislamu wenye kujitoa sana, sehemu iliyo ya maana zaidi ya ibada yao ni ile sala ya kila siku (salat). Hiyo inapasa kurudiwa mara tano kwa siku, huku wakielekeza nyuso Meka katika Saudi Arabia.

Sala za Kiyahudi zinatia ndani zile ambazo zimetolewa moja kwa moja katika Bibila, kama zile zaburi. Sala nyingine zinatia ndani zile ambazo marabi mbalimbali wameongeza.

Miongoni mwa wenye kujidai kuwa Wakristo, kuna mpangilio mkubwa wa sala na njia mbalimbali za kusali. Hizo ni kuanzia sala ambazo zinarudiwa-rudiwa huku tasbihi ikiwa mkononi hadi sala zilizopigwa chapa, na pia zile za maneno machache yanayosemwa bila kufanyiwa mazoezi.

[Picture on page 7]

Sala za Yesu zilijibiwa. Zako zinaweza kujibiwa pia

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki