Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w91 9/15 kur. 4-6
  • Ni Sala za Nani Hujibiwa?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Sala za Nani Hujibiwa?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Uthibitisho wa Kwamba Mungu Hujibu Sala
  • Kwa Nini Sala Fulani Hazijibiwi
  • Yesu ‘Alisikiwa kwa Upendelevu’
  • Jinsi Yehova Hujibu Sala Leo
  • Sala Zao Hujibiwa
  • Sala Ambazo Zinajibiwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Mkaribie Mungu Katika Sala
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Jinsi Yehova Anavyojibu Sala Zetu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2023
  • Utangulizi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2021
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
w91 9/15 kur. 4-6

Ni Sala za Nani Hujibiwa?

YEHOVA ndiye Mungu ajibuye sala. Kwa kweli, Neno lake, Biblia, humwita “Msikiaji wa sala.” (Zaburi 65:2, NW) Yeye ana nia ya kujibu sala. Lakini ni sala za nani ambazo yeye hujibu kwa kweli?

Mungu hujibu sala za watu mmoja mmoja wanaompendeza. Wao wana mtazamo wenye kicho wa mtunga zaburi aliyesema: “Kama ayala aioneavyo shauku mito ya maji. Vivyo hivyo nafsi yangu inakuonea shauku, Ee Mungu. Nafsi yangu inamwonea kiu MUNGU, Mungu aliye hai.” (Zaburi 42:1, 2) Hata hivyo, kuna ushuhuda gani wa kuthibitisha kwamba Yehova hujibu sala za waabudu wake wa kweli?

Uthibitisho wa Kwamba Mungu Hujibu Sala

Biblia ina kumbukumbu refu la kuthibitisha kwamba Yehova hujibu sala za watumishi wake waaminifu. Kwa kielelezo, Mfalme Yehoshafati wa Yuda aliposali kuomba ukombozi, Mungu alijibu sala yake na kumpa ushindi kwa kusababisha adui zake wapigane madharuba. (2 Nyakati 20:1-26) Mfalme Hezekia alipokabiliwa vivyo hivyo na jeshi lenye kuogopesha sana, alisali kwa Mungu kwa unyenyekevu kuomba msaada. Hezekia aliona wokovu wa Yehova wakati malaika alipowapiga chini Waashuri 185,000 katika usiku mmoja.—Isaya 37:14-20, 36-38.

Kwa nini Mungu alijibu sala hizo? Katika visa vyote viwili, wafalme hao walisihi kwamba kushindwa katika pigano kungeleta sifa mbaya juu ya jina la Yehova. (2 Nyakati 20:6-9; Isaya 37:17-20) Walihangaikia sifa yake. “Lengo kuu la sala,” yasema The International Standard Bible Encyclopedia, “si kutimiza faida ya mwombi tu bali heshima ya jina la Mungu.” Kwa hiyo, watumishi waaminifu wa Yehova waweza kuwa na uhakika kwamba yeye atawasaidia “kwa ajili ya jina lake.” Kumbukumbu linalothibitisha kwamba sala hizo zimejibiwa huwapa watu wa Mungu uhakika wa kwamba yeye husikia sala zao.—Zaburi 91:14, 15; 106:8; Mithali 18:10.

Lakini, hata ikiwa hali fulani inahusisha jina la Mungu, Mungu huamua kama atajibu sala fulani au sivyo. Huenda akawa na sababu halali za kutojibu sala fulani. Tukihisi kwamba sala zetu hazisikiwi, ni vema kufikiria sababu huenda ikawa nini.

Kwa Nini Sala Fulani Hazijibiwi

“Mwombapo maombi mengi, sitasikia,” Yehova akawaambia Waisraeli wakati mmoja. Akionyesha wazi sababu, aliendelea hivi: “Mikono yenu imejaa damu.” (Isaya 1:15) Mtu angewezaje kupuuza sheria ya Yehova na bado apate fursa ya kusikiwa naye? Mithali moja ya Biblia yatoa jibu la wazi, ikisema: “Yeye aligeuzaye sikio lake asiisikie sheria, hata sala yake ni chukizo.”—Mithali 28:9.

Biblia hutoa sababu nyingine kwa nini sala fulani hazisikiwi, isemapo: “Mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu.” (Yakobo 4:3) Yehova hatajibu sala za kutosheleza tamaa mbaya, hapana. Ni lazima pia tukumbuke kwamba Mungu haamrishwi-amrishwi na wanadamu. Ni Yeye aamuaye jinsi atakavyojibu sala zetu.

Zilizo na uhakika wa kujibiwa ni sala ambazo humwendea Mungu kwa moyo safi, kwa kusudio lifaalo, na katika njia yake iliyowekwa—kupitia Yesu Kristo. (Yohana 14:6, 14) Lakini hata wale ambao sala zao hutimiza matakwa hayo wamehisi nyakati fulani kwamba hawasikiwi. Kwa nini Mungu hangetaka kujibu sala fulani za watumishi wake mara ile ile?

Yehova ajua wakati bora kabisa wa kujibu sala. Ingawa mvulana aomba baiskeli, huenda baba yake asimpatie moja mpaka mtoto huyo atoshelee umri wa kuiendesha salama. Huenda ikawa hivyo kwa sala fulani za wale wampendao Mungu. Kwa kujua lililo bora kabisa kwao, yeye huwapa kile ambacho chahitajiwa kwenye wakati ufaao zaidi.

Hata hivyo, watumishi wa Yehova hawapati kila kitu ambacho huenda wakasali kwa ajili yacho. Kwa kuwa ni wasiokamilika, huenda wakatamani vitu fulani ambavyo havingekuwa kwa faida yao. Baba yao wa kimbingu mwenye upendo hangewapa chochote chenye madhara, kwa maana yeye ndiye Mpaji wa “kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili.” (Yakobo 1:17) Vivyo hivyo, huenda Mungu asitoe kitu kisicho cha lazima kutokana na maoni yake. (Linganisha 2 Wakorintho 12:7-10.) Yeye hujibu sala zipatanazo na mapenzi na kusudi lake kwa ajili ya watu wake.—1 Yohana 5:14, 15.

Yesu ‘Alisikiwa kwa Upendelevu’

Yesu Kristo alikuwa mwanamume wa sala. (Mathayo 6:9-13; Yohana 17:1-26) Alikuwa na uhakika kamili kwamba Baba yake wa kimbingu angesikia na kujibu sala zake. Wakati mmoja Yesu alisema: “Baba, . . . nalijua ya kuwa wewe wanisikia sikuzote.” (Yohana 11:41, 42) Lakini je! Yesu hakukatishwa tamaa kwenye mwisho wenyewe wa mwendo wake wa kidunia? Je! wakati huo yeye hakupaaza kilio hiki: “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”—Mathayo 27:46.

Yesu aliposema maneno hayo, kwa wazi alikuwa akitimiza unabii fulani kuhusu kifo chake. (Zaburi 22:1) Kwa umaana mdogo, Yesu angeweza pia kuwa alimaanisha kwamba Yehova alikuwa ameondoa ulinzi Wake na kuacha Mwana wake afe kifo chenye maumivu na aibu ili kutahini uaminifu wake wa kimaadili hadi upeo. Uchunguzi wa matukio katika siku hiyo ya mwisho ya maisha ya kidunia ya Yesu waonyesha kwamba Mungu alisikia sala zake.

Katika usiku wa kukamatwa kwake, Yesu alisali katika bustani ya Gethsemane. Mara tatu alisihi hivi: “Baba yangu, kama inawezekana, kikombe hiki cha mateso kinipite.” (Mathayo 26:39, 42, 44, Habari Njema kwa Watu Wote) Yesu hakukosa nia ya kutoa uhai wake uwe ukombozi kwa ajili ya ainabinadamu. Sivyo, bali ni wazi alihangaishwa kwa kina kirefu na uwezekano wa kumvunjia heshima Baba yake mpenzi sana kwa kufa juu ya mti wa mateso akiwa mkufuru aliyelaaniwa. Je! Yehova alisikia sala ya Yesu?

Miaka baadaye, mtume Paulo aliandika hivi: “Siku hizo za mwili wake, alimtolea yule, awezaye kumwokoa na kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, akasikilizwa [kwa upendelevu, NW] kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu.” (Waebrania 5:7; Luka 22:42, 44) Ndiyo, katika ule usiku wenye kuumiza vikali uliotangulia kifo chake, Yesu ‘alisikiwa kwa upendelevu.’ Lakini jinsi gani?

Yehova alituma malaika ambaye ‘alimtokea Yesu akamtia nguvu.’ (Luka 22:43) Akiwa ametiwa nguvu hivyo, Yesu aliweza kukabili kifo juu ya mti wa mateso. Kwa wazi, ndipo Yehova alipompa uhakikisho wa kwamba kifo chake juu ya mti wa mateso hakingeleta suto juu ya jina la kimungu bali ndicho kitu kile kile ambacho hatimaye kingetumiwa kulitakasa. Kwa kweli, kifo cha Yesu juu ya mti wa mateso kiliwafungulia njia Wayahudi, ambao ama sivyo walikuwa wamelaaniwa chini ya ile Sheria, waje waokolewe kutoka laana kali ya kifo.—Wagalatia 3:11-13.

Siku tatu baadaye, Yehova alimfufua Yesu na akamwondolea shtaka lolote liwezekanalo la kukufuru kwa kumkweza kwenye cheo cha kimbingu kilicho juu zaidi. (Wafilipi 2:7-11) Ni njia nzuri kama nini ya kujibu sala ya Yesu kuhusu “kikombe hiki”! Sala hiyo ilijibiwa katika njia ya Yehova. Na Yesu alipata mibaraka mizuri ajabu kwa sababu alikuwa amemwambia Baba yake wa kimbingu hivi: “Walakini si mapenzi yangu, bali yako yatendeke.”—Luka 22:42.

Jinsi Yehova Hujibu Sala Leo

Kama Yesu, wale wanaotafuta kumfurahisha Yehova leo wapaswa sikuzote kuomba kwamba mapenzi ya Mungu yatimie. Wao wahitaji kuwa na imani kwamba Yehova atajibu sala zao katika njia itakayowanufaisha kwa kadiri kubwa zaidi. Kwa kweli, yeye ‘atafanya mambo ya ajabu mno kuliko yote wayaombayo au wayawazayo.’—Waefeso 3:20.

Mwanamke Mkristo kijana aliyeishi pamoja na wazazi wake wasioamini aliona ukweli wa andiko hilo. Katika barua moja kutoka Watch Tower Society, yeye aliombwa afikirie kwa sala uwezekano wa kukubali mgawo maalumu wa kimisionari. Ingawa tamaa yake yenye kuhisiwa moyoni ilikuwa kukaa nyumbani kusaidia wazazi wake ili wawe Wakristo, alimwomba Mungu hivi katika sala: “Mapenzi yako ni nini? Je! ni kukubali mwaliko huu bila kujali upinzani wa wazazi wangu, au ni kusaidia wazazi wangu kwa kuendelea kuishi pamoja nao?” Kila wakati aliposali, dhamiri yake ilimwambia akubali mwaliko huo. Aliamua kwamba hili lilikuwa ndilo jibu kutoka kwa Yehova.

Mungu alimtia nguvu mwanamke huyo ashikamane na uamuzi wake. Alipoombwa ahamie Kisiwa Awaji, Japani, wazazi wake walishtuka na wakazidisha upinzani wao. Hata hivyo, kwa kutoweza kumsadikisha abadili nia yake, mama yake aliamua kujifunza Biblia ili aone tu kwa nini binti yake alifanya uamuzi wa jinsi hiyo. Miezi mitatu baadaye wazazi wake walimzuru. Walipoona jinsi alivyotunzwa vema na Mashahidi wengine wa Yehova, baba yake alivutiwa sana akatoa machozi kulipokuwa hakuna mtu mwingine karibu. Muda si muda yeye pia alianza kujifunza Biblia. Mwishowe wazazi wote wawili wa mwanamke huyo kijana walibatizwa wakaanza kumtumikia Yehova kwa uaminifu. Je! Yehova Mungu hakumbariki mwanamke huyo Mkristo kwa kadiri ya ajabu mno?

Sala Zao Hujibiwa

Je! wewe wakumbuka maneno ya mwanamke aliyetajwa mwanzoni mwa makala iliyotangulia? Yeye hakuwa kamwe amehisi ule msisimuko wa kujibiwa sala zake. Hata hivyo, baadaye alitambua kwamba Mungu alikuwa akijibu sala zake. Mwanamke huyo alikuwa ameweka kumbukumbu la mawazo makuu ya sala zake. Siku moja alikipitia kitabu cha maandishi yake na kung’amua kwamba Yehova alikuwa amesikia kadiri kubwa ya sala zake, hata zile ambazo yeye mwenyewe alikuwa amezisahau! Hivyo yeye alijua kwamba Mungu alikuwa akimtunza na kujibu sala zake kwa njia nyororo iliyomnufaisha kwa kadiri kubwa zaidi.

Ukihisi kwamba sala zako hazijibiwi, jiulize hivi: ‘Je! mimi nina uhusiano wa kibinafsi pamoja na Yehova, “Msikiaji wa sala”? Ikiwa sivyo, je! mimi ninachukua hatua za kujifunza juu yake na kuwa mmoja wa watumishi wake waliojiweka wakfu?’ Yeye hujibu sala za wale wampendao na kufanya mapenzi yake. Wao ‘hudumu katika kusali’ na husikiwa kwa upendelevu, kama Yesu alivyosikiwa. (Warumi 12:12) Hivyo basi, ‘funua [mwaga, NW] moyo wako’ kwa Yehova na ufanye mapenzi yake. (Zaburi 62:8) Ndipo sala zako zitakaposikiwa.

Leo, mamilioni ya watu wanasali kuomba kitu fulani maalumu. Ndiyo, na sala zao zinasikiwa. Acheni tuone kwa nini sisi twaweza kuwa na uhakika kwamba sala hizo zitajibiwa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki