Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 3/15 kur. 3-4
  • Je! Yakupasa Uiamini Biblia?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Yakupasa Uiamini Biblia?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUWA NA MASHAKA YASIYOFAA AU KUFANYA UCHUNGUZI UNAOFAA
  • BIBLIA​—MSINGI WA IMANI
  • IMANI​—NI SIFA YENYE KUTAMANIKA LEO
  • IJARIBU BIBLIA
  • Wenye Uhakika katika Ulimwengu Unaozungukwa na Mashaka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Usiruhusu Imani Yako Iharibiwe na Shaka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Je, Umeifanya Kweli Iwe Mali Yako Mwenyewe?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Je, Kweli Una Imani Katika Habari Njema?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 3/15 kur. 3-4

Je! Yakupasa Uiamini Biblia?

IMANI au mashaka? Yenye kutegemeka au isiyotegemeka? Mambo hayo yamekuwa sehemu ya maisha ya kila siku ya watu. Mambo mengi sana tunayosoma na kusikia hayategemeki. Kuhusu hekima ya kibinadamu mwandikaji Aldous Huxley aliandika hivi wakati mmoja: “Kutafuta sababu mbaya kwa ajili ya yale anayoamini mtu kwa ajili ya sababu mbaya nyinginezo—hiyo ndiyo filosofia.”

Kwa habari ya sayansi, rafu za vitabu katika maktaba zote kubwa za taifa lote zimejazwa vitabu vya wataalamu wa sayansi ambavyo vimekuwa vya kizamani baada ya miaka 50 iliyopita. Basi haishangazi kwamba watu wamekuwa wenye kutilia mashaka wanayosoma.

KUWA NA MASHAKA YASIYOFAA AU KUFANYA UCHUNGUZI UNAOFAA

Katika ulimwengu ambao kutilia mashaka kunakuwa ngao ya lazima kujilinda na kudanganywa na hila, mtu anaweza kwa urahisi kuwa na zoea la kuwa na mashaka juu ya kila kitu na kila mtu. “Akiumwa mara moja, mara ya pili anaogopa,” ni msemo unaotumiwa sana (Kiingereza), nalo hilo lafahamika. Walakini je! kweli kweli inaridhisha kuishi katika ulimwengu wa mashaka? Je! mtu anaweza kuwa na masadikisho thabiti iwapo hana chanzo cha habari chenye kutegemeka?

Mashaka yasiyofaa hayatakufaidi kwa vyo vyote. Kuuliza maulizo kwa unyofu na uchunguzi unaofaa, kwa upande mwingine, vyote hivyo vyaweza kuwa vyombo vyenye kufaa kwa mwenye kutafuta kweli. Hivyo ndivyo ilivyo kwa habari ya sayansi. Katika kitabu chake kilichoandikwa kwa ufundi Introduction a l’etude de la medecine experimentale (Utangulizi wa Masomo ya Utibabu wa Kujaribia), mwanasayansi Mfaransa Claude Bernard aliandika hivi: “Takwa la kwanza linalopaswa kutimizwa na mwanasayansi mwenye kuchunguza matukio ya asili ni kuendelea kujitegemea kabisa katika kufikiri. . . . Yeye atiliaye mashaka ni mwanasyansi wa kweli, akiwa na mashaka juu yake mwenyewe na juu ya ufasiri wake mwenyewe wa mambo, lakini akiweka imani katika sayansi.”

Kwa hiyo kulingana na mtaalamu huyo mwenye kujulikana sana wa elimu ya viumbe hai, uchunguzi wa kisayansi unataka mashaka na imani. Mwanasayansi mwenye kufanya uchunguzi anatilia mashaka kama kila kitu kimekwisha jifunzwa katika masomo fulani, walakini akifanya majaribio yake analazimika kuwa na imani katika yale yanayofikiriwa kuwa kweli ya kisayansi katika masomo mengineyo. Kwa maneno mengine, hatilii mashaka sayansi kwa ujumla. Mashaka yake katika masomo fulani yanafaa, mradi anatumaini kuendeleza faida za sayansi kwa kuvumbua jambo jipya.

Hiyo yaweza kuwa kweli kwa habari ya dini. Pasipo kutilia mashaka kuwapo kwa Mungu, mtu anaweza kutilia mashaka kwa haki baadhi ya mafundisho yanayofundishwa na makanisa yanayodai kuwa ya Kikristo. Uchunguzi wa unoyfu unaweza kutokeza kukataa makosa ya kidini; vilevile unaweza kuongoza kwenye kuvumbua ibada ya kweli. Lakini uchunguzi huo unaweza kufanywa juu ya msingi gani?

BIBLIA​—MSINGI WA IMANI

Msingi unaokubaliwa ulimwenguni pote wa kuchunguza dini ya Kikristo ni Biblia Takatifu. Kwa kupendeza, Biblia yenyewe haitaki wasomaji wake wawe na imani isiyoona mambo. Ikionya juu ya kuamini pasipo sababu, inasema hivi: “Mjinga huamini kila neno; bali mwenye busara huangalia sana aendavyo.” (Mit. 14:15) Na tena: “Hakikisha mambo yote; shika sana yaliyo mema.” (1 The. 5:21, NW) Hiyo inaonyesha uchunguzi wa uangalifu, kuchagua, kutumia ‘uwezo wako wa kufikiri’ na kisha kushikamana na yale yanayoonekana kuwa ya kweli.​—Rum. 12:1, 2, NW.

Kufikiri kwa njia hiyo, na kujithibitishia, kunamwezesha mtu apate masadikisho. Nayo masadikisho hayo yanasitawisha imani. Kama inavyoelezwa katika Biblia, “Imani ni taraja lililohakikishwa la mambo yanayotumainiwa, wonyesho dhahiri wa mambo ya hakika ijapokuwa hayaonwi.” (Ebr. 11:1, NW) Imani ya Biblia inahitaji “wonyesho,” uthibitisho. Inahitaji maarifa ili kuwa na namna ya imani inayopendekezwa katika Biblia. Mtu hazaliwi akiwa na imani hiyo. Ni jambo linalokua pamoja na maarifa na ujuzi. Biblia inaendelea kusema hivi: “Imani inatokana na kuusikiliza ujumbe, na huo ujumbe unatokana na neno la Kristo.” (Rum. 10:17, .HNWW) Na mahali pa pekee pa kupata ‘neno juu ya Kristo’ lililo la kweli ni katika Biblia.

IMANI​—NI SIFA YENYE KUTAMANIKA LEO

Ili kuisitawisha imani yako, unahitaji maarifa na uwezo wa kuyatumia. Uwezo huo ndio ambao Biblia huita “hekima.” Kwamba unaweza kufanya jambo fulani juu ya kupata hekima hiyo inaonyeshwa na shauri lifuatalo la Biblia: “Ikiwa ye yote kati yenu anapungukiwa na hekima, acheni yeye aendelee kumwomba Mungu, kwa kuwa yeye huwapa wote kwa ukarimu na bila kuwalaumu; naye atapewa hiyo. Lakini acheni yeye aendelee kuomba kwa imani, bila kushuku hata kidogo, kwa kuwa yeye ashukuye anafanana na wimbi la baharini lipeperushwalo na upepo huku na huku. . . . yeye ni mtu anayesita, asiyeimarika katika njia zake zote.”​—Yak. 1:5-8, NW.

Katika ulimwengu unaozungukwa na mashaka na usio na hakika juu ya yatakayoupata, ulimwengu ambao umekataa ubora wa adili ambazo zimeonyeshwa ni zenye kufaa kwa kadiri wakati ulivyopita, je! si ni wazi kwamba wanahitaji dira ya kiroho ya kujiongoza nayo? Mwenye kutilia mashaka kabisa “anafanana na wimbi la baharini lipeperushwalo na upepo huku na huku,” anatupwa-tupwa na filosofia zenye kubadilika za wanadamu wasio imara. Mtu wa namna hiyo hana hakika ya jambo lo lote. Hana masadikisho. Hakuna hoja yo yote, hata iwe ni ya akili namna gani, inayoweza kumsadikisha. Hawezi kuamini kwa sababu hataki kuamini.

IJARIBU BIBLIA

Watu hao wenye mashaka wanatilia mashaka kwamba maisha hayana maana yo yote. Wanatosheka kuishi muda wao wote wa maisha (ambao ni mfupi kuliko ule wa wanyama fulani) kisha wafe, bila tumaini lo lote la kuishi milele. Twatumaini kwamba wewe, Ee msomaji mpendwa, u kati ya wale wanaoona kuwa si jambo la akili kukubali kwamba wanadamu waishi miaka 70 au 80 peke yake kisha wafe, wakiwa na maarifa na ujuzi wote waliokusanya na kuupoteza milele. Inatumainiwa kuwa u kati ya wale wenye kutafuta uzima, ambao pia ndio wanaotafuta kweli. Kuhusu watu hao waliokuwa wakiishi katika karne ya kwanza, Biblia inasema hivi: “Wote waliokuwa na maelekeo yanayofaa ya uzima wa milele wakawa waamini.”​—Matendo 13:48, NW.

Ili kukusaidia uamini kwamba Biblia inaweza kutoa maarifa yenye kutoa uhai twakukaribisha ufikirie uthibitisho ufuatao wa ubukuzi wa mambo ya kale kuwa Biblia inategemeka.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki