Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 7/1 uku. 16
  • Sherehe Isiyo na Mfano Wake

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sherehe Isiyo na Mfano Wake
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Habari Zinazolingana
  • Sifuni Yah kwa Hukumu Zake!
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
  • “Msifuni Yah, Enyi Watu!”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Jitihada za Kupinga Jina la Mungu
    Amkeni!—2004
  • Kitabu cha Ufunuo Kinamaanisha Nini kwa Wakati Wako Ujao?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 7/1 uku. 16

Sherehe Isiyo na Mfano Wake

‘‘VITA ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi” kwenye Har—Magedoni itakuwa ndiyo vita kubwa zaidi katika historia ya dunia yetu, nayo ndiyo itakayokuwa ya mwisho. (Ufu. 16:14, 16) Kama vile nabii wa Mungu alivyotangaza, kwa faraja ya wale wanaompenda: “Yehova ni mwema, ngome katika siku ya taabu. . . . Yeye anaangamiza kabisa. Taabu haitatokea kwa mara ya pili.”​—Nah. 1:7-9, NW.

Ni nini kitakachofuata? Mtume Yohana hutuambia kwamba asikia “sauti [kuu] kama sauti ya makutano mengi, sauti kubwa mbinguni.” Katika wimbo wa kuitikia, kundi hili kubwa la kimalaika linaimba hivi: “Haleluya; Wokovu na utukufu na nguvu zina [Yehova] Mungu wetu; kwa kuwa hukumu zake ni za kweli na za haki; maana amemhukumu yule kahaba mkuu aliyeiharibu nchi kwa uasherati wake, na kuipatiliza damu ya watumwa wake mkononi mwake.” (Ufu. 19:1, 2) Ni furaha kama nini! Kwa sababu, kwa umilele wote, uonevu, ukafiri na njia zenye kuleta kifo za milki ya ulimwengu ya dini za uongo, “Babeli Mkuu,” zimefagiliwa mbali na kuondolewa juu ya uso wa dunia ya Mungu.

Mtume huyo anasikia nini zaidi? “Wakasema mara ya pili, Haleluya”‏! Kisha “Haleluya”! ya tatu yasikika, na kwa kufaa, Yohana ambaye mahali pengine anaitwa ‘mwana wa ngurumo,’ anaongeza maneno haya yenye kuonyesha upeo: “Nikasikia sauti kama sauti ya makutano mengi, na kama sauti ya maji mengi, na kama sauti ya radi [ngurumo] yenye nguvu, ikisema, Haleluya; kwa kuwa [Yehova] Mungu wetu, Mwenyezi, amemiliki.”​—Ufu. 19:3-6; Marko 3:17.

Kuimba kwa sauti hizo za kimbinguni ni kuzuri zaidi kuliko wimbo wo wote wa “Haleluya” uliopata kusikiwa hapa duniani. Maelfu hayo ya malaika wanajua maana ya wimbo huo. Kwa hiyo wanauimba wakiwa na furaha: “Haleluya!”​—maana yake “Msifuni Yah, enyi watu!” Watu wa Mungu duniani wanatoka kwenye “dhiki ile iliyo kuu” washiriki katika kuimba wimbo huo, wakimsifu Yah, Yehova, Bwana Mwenye Enzi Kuu wa ulimwengu wote, kwa ushindi wake mkuu juu ya majeshi yote yenye uovu.

Matukio mengine yenye utukufu yafuata. Watu wa Yehova wanaalikwa ‘wafurahi, na kushangilia,’ kwa sababu sasa ndoa yafanyika mbinguni. Mwana-Kondoo aunganishwa na “mke” wake—hesabu kamili ya wale “watakatifu” 144,000 waliofufuliwa, wanaotambulishwa na “matendo ya haki” waliyotenda walipokuwa wanadamu duniani. (Ufu. 19:6-8; 14:1-5) Ule mpango wa kiserikali wa “mbingu mpya na dunia mpya” sasa wakamilika. Tayari, kabla ya ile ‘dhiki kuu,’ Mwana-Kondoo amekuwa akichunga “mkutano mkubwa” wa waabuda wanadamu. (Ufu. 7:9, 14) Walakini sasa ile ahadi ya kwamba Mungu “atafuta kila chozi katika macho yao” itatimiziwa wanadamu wote, kutia na wafu waliofufuliwa, wakati jamii ya “dunia mpya” ianzapo kutenda miongoni mwa wanadamu.​—Ufu. 21:1, 4; 2 Pet. 3:13, NW.

Washikamanifu wa Mungu mbinguni na duniani wataungana katika kuimba Haleluya hiyo yenye kurudiwa-rudiwa iliyo nzuri sana na yenye maana sana. Kwa kuwa Yah, Yehova atakuwa amejipatia ushindi!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki