Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 9/1 kur. 8-9
  • Je! Watu Wote Wema Wanakwenda Mbinguni? . . .

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Watu Wote Wema Wanakwenda Mbinguni? . . .
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Habari Zinazolingana
  • Ni Nani Wanaoenda Mbinguni, na kwa Sababu Gani?
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Maisha Mapya kwa Wazazi Wetu wa Kale Waliokufa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Je, Watu Wote Wazuri Wanaenda Mbinguni?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Ukweli Kuhusu Mbingu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 9/1 kur. 8-9

Neno la Mungu Li Hai

Je! Watu Wote Wema Wanakwenda Mbinguni? . . .

. . . AU WENGI WAO WATAISHI KATIKA DUNIA YA PARADISO?

PENGINE watu wengi wanaamini hivyo. Lakini je! hivyo ndivyo Biblia inafundisha?

Baada ya Yesu Kristo kufufuliwa kutoka kwa wafu, mtume Petro aliuambia mkutano wa Wayahudi hivi: “Baba yetu mkuu, Daudi, . . . alifariki akazikwa, na kaburi lake liko kwetu hata leo. . . . Daudi hakupanda mbinguni.”​—Matendo 2:29, 34.

Je! Ayubu, yule mtu alikwenda mbinguni alipokufa? Alipokuwa akiteseka, Ayubu alimwomba Mungu hivi: “Laiti ungenificha [kaburini], ukanilinda kwa siri, hata ghadhabu zako zitakapopita, na kuniandikia muda ulioamriwa, na kunikumbuka!”​—Ayubu 14:13.

Wakati ambapo angekufa, Ayubu alitazamia kukaa kaburini bila fahamu. Walakini alikuwa na tumaini, kama vile alivyoeleza: “Mtu akifa, je! atakuwa hai tena? Mimi ningengoja siku zote za vita vyangu, hata kufunguliwa kwangu kunifikilie. Wewe ungeita, nami ningekujibu.”​—Ayubu 14:14, 15.

Yohana Mbatizaji alikuwa mtu mwema kweli kweli. Hata hivyo, Yesu alisema hivi: “Aliye mdogo katika ufalme wa mbinguni ni mkubwa kuliko yeye.” (Mt. 11:11) Iko hivyo kwa kuwa Yohana Mbatizaji hataenda mbinguni. Yeye atafufuliwa kwenye uzima hapa duniani. Daudi, Ayubu, Yohana Mbatizaji na wanaume na wanawake wengine wote waaminifu waliokufa kabla ya Kristo watafufuliwa kwenye uzima hapa duniani. Watakuwa raia za kidunia za ufalme wa Mungu.

Yesu Kristo atatawala akiwa mfalme huko mbinguni. Mitume wake pamoja na Wakristo wengine waliozaliwa kwa roho watakwenda mbinguni wakatawale pamoja naye, kama vile inavyosema Biblia: “Watatawala kama wafalme juu ya dunia.” (Ufu. 5:10, NW) Biblia inaonyesha kwamba ni hesabu iliyo na kikomo tu ya watu, “kundi dogo,” itakwenda mbinguni ikawe wafalme hao. Biblia inatoa jumla ya hesabu yao kuwa 144,000. Wanadamu wengine wote waaminifu wataishi duniani chini ya watawala hao.​—Luka 12:32; Ufu. 14:1, 3.

Hali zitakuwaje duniani wakati ufalme wa Mungu utakapokuwa ukitawala? Dunia itakuwa paradiso duniani pote, hata kama vile ilivyokuwa kusudi la Mungu mwanzoni wakati alipowaweka Adamu na Hawa katika paradiso ya Edeni. Wakati huo ahadi hii ya Biblia itatimizwa: “Wenye haki watairithi [dunia], nao watakaa humo milele.”​—Zab. 37:29.

[Picha katika ukurasa wa 8]

Mfalme Daudi yuko mbinguni ama wapi?

Je! Tumaini la Ayubu lilikuwa kwenda Mbinguni?

Yohana Mbatizaji alikwenda mbinguni?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki