Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 9/1 kur. 10-15
  • Kupata Furaha ya Kweli kunategemea Wewe

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kupata Furaha ya Kweli kunategemea Wewe
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • FURAHA NA UHITAJI WAKO WA KIROHO
  • FURAHA​—KUTOKANA NA KUSIKIA NA KUTENDA
  • FURAHA​—MRADI AU MATOKEO?
  • Jinsi ya Kupata Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Furaha ya Kweli Yaweza Kupatikana Wapi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Wenye Furaha Ni Watu Wanaomtumikia “Mungu Mwenye Furaha”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • Furaha ya Kweli Katika Kumtumikia Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 9/1 kur. 10-15

Kupata Furaha ya Kweli kunategemea Wewe

“Wenye furaha ni watu ambao Yehova ndiye Mungu wao!”​—Zab. 144:15, NW.

1. Sababu gani inakupasa kufikiri juu ya kile kinachokuletea furaha?

NI NINI kinachoweza kukufanya kuwa mwenye furaha? Ni kwa kadiri gani furaha yako inategemea hali zinazokuzunguka, vitu vya kimwili au watu wengine? Je! Mungu na Biblia huhusika katika kupata furaha yako? Ebu na tuchunguze mambo haya, kwa kuwa sisi sote tunataka furaha.

2, 3. (a) Ni katika njia gani vitu au watu wengine wanaweza kukuongezea furaha? (b) Ni nini maoni ya Mungu juu ya jambo hilo?

2 Kwa wazi mambo ya nje yanaweza kusaidia kutufanya kuwa wenye furaha, kama vile kufurahia chakula kingi kitamu katika mazingira yenye kupendeza. Hasa tunaweza kuthamini hili ikiwa katika wakati uliopita tulipatwa na maumivu makali na ya muda mrefu ya njaa. Si jambo lisilopatana na mapenzi ya Mungu kwetu sisi kupata kadiri fulani ya furaha kutokana na chakula kizuri. Mfalme Sulemani aliandika hivi chini ya uongozi wa kimungu:

“Mimi najua ya kwamba hakuna jema kwao kupita kufurahi, na kufanya mema maadamu wanaishi. Tena ni karama ya Mungu kila mtu apate kula na kunywa, na kujiburudisha kwa mema katika kazi yake yote.”​—Mhu. 3:12, 13; linganisha Zaburi 104:14, 15.

3 Vilevile, watu wengine, waweza kusaidia kutuletea furaha. Lo! namna lilivyo jambo lenye kuridhisha kuwa na wapendwa wanaotujali, wawe washiriki wa jamaa au rafiki!—Zab. 127:3-5; 128:3.

4. Ni kwa sababu gani kuwa na vitu au rafiki hakuhakikishi kuwa utakuwa na furaha? (Mit. 23:4, 5; Mhu. 5:11; Luka 12:16-20)

4 Walakini huenda ukawa unajua kwamba kuwa na vitu vya kimwili na washiriki wa karibu hakumhakikishii mtu furaha ya kweli na yenye kudumu. Watu wengine wana chakula kilicho bora zaidi tena kingi na wanazungukwa na mambo mengi ya anasa ya kisasa; hata hivyo hawaioni furaha. Miaka miwili kabla ya kufa kwake, tajiri wa mafuta mwenye mamilioni mengi ya fedha J. P. Getty alisema hivi: “Kwa lazima fedha haileti furaha. Pengine inatokeza kutokuwa na furaha.” (1 Tim. 6:9, 10) Wala fedha haitatusaidia kuwa na furaha ya kweli ikiwa wale wanaodai kutujali ni watu ambao ushirika wao unanunuliwa kwa njia fulani.​—Mit. 19:6.

5. Ni kwa sababu gani furaha inaonekana kuwa “ukweli wenye kinyume?

5 Imepata kuonekana kwamba, katika njia fulani, furaha ni jambo linaloonekana kuwa kinyume cha ukweli. Ijapokuwa neno “furaha” huenda likaleta akilini mwako hali zenye kupendeza, inaweza kusitawi katika hali zo zote, iendelee chini ya hali za kila namna, na kushinda mazingira ya kila namna. Furaha haitegemei sana vitu tulivyo navyo bali jinsi tulivyo sisi. Ndiyo sababu wengi wanaoishi maisha ya anasa si wenye furaha hasa, hali wengine walio na vitu vichache kwa kulinganisha na ambao maisha yao ni mepesi wanapata furaha. Na zaidi, huenda ukawa umepata kuona watu waliolazwa hospitalini au watu waliolemaa walio na maoni maangavu, ya uchangamfu na ya furaha. Ni kweli, hawafurahii kuwa wagonjwa au vilema nao wanaona afadhali mambo yangekuwa vingine. (Matendo 3:1-8) Hata hivyo, wanaona sababu ya kufurahia maisha.

FURAHA NA UHITAJI WAKO WA KIROHO

6, 7. (a) Wengi wamefanya makosa gani katika kujitahidi kupata furaha? (b) Je! wewe unaweza kufikiria mifano halisi ya hili?

6 Watu wengi wanawaonea wivu wale wenye furaha, wakitaka kuwa hivyo pia. Huenda wakajaribu kuondoa hali yao isiyo ya furaha kwa kutumia njia za kutumia dawa za kulevya, vileo, ngono zisizo halali, uzembe—na bado washangae sababu gani hawapati furaha. Msisimko wo wote wanaopata kutokana na kufuatilia mambo hayo huwa ni furaha ya uongo tu, ambayo ikijaribiwa, inaonekana kuwa isiyo na maana kama vile fedha za bandia.

7 Ushuhuda wa historia ya muda mrefu na mambo waliyoyaona watu milioni nyingi wanaoishi hivi sasa huthibitisha kwamba hatuwezi kupuza kanuni za adili za Mungu na bado tuwe na furaha ya kudumu. Wale ambao ‘wamekwisha kupita ufahamu wote wa yaliyo adilifu, wakajitoa kwa mwenendo mpotovu kufanya machafu ya kila namna kwa pupa’ si ndio walio na furaha. (Efe. 4:17-19, NW; Rum. 13:13) Mwendo wa namna hiyo, huleta masikitiko zaidi mara hiyo au baadaye na kuzuia njia ya kupatia furaha. Waweza kufikiria visa halisi vinavyounga mkono jambo hilo? Kwa upande mwingine, kufanya mambo katika njia ya Mungu—kulingana na kanuni zake za adili—kunapunguza magumu ya maisha na hivyo kuondoa vizuizi vya kupata furaha. Hata hivyo kujiepusha tu na magumu kwenyewe hakutuhakikishii kwamba tutakuwa na furaha. Mengi yanahitajiwa. Tunaweza kuwa na hakika ya jambo hilo, kwa kuwa Muumba wetu anatuambia hivyo.

8, 9. (a) Tuna uhitaji gani wa msingi? (b) Yesu alisema nini juu ya hilo?

8 Tunahitaji kusitawisha uhusiano na Muumba, tujifunze mapenzi na makusudi yake na kuyakubali sisi wenyewe. Ndiyo, tunahitaji jambo hilo. Katika kitabu chake Man, God and Magic (Mwanadamu, Mungu na Uchawi), Dakt. Ivar Lissner anataja kwamba “tofauti kubwa kati ya mwanadamu na mnyama” ni kwamba “mwanadamu hatosheki na kulala tu, kula na kujipasha joto.” Sisi wanadamu tuna “tamaa tunayorithi isiyo ya kawaida” inayoweza kuitwa ‘hali ya kiroho.’ Kwa kweli, Dakt. Lissner anaripoti kwamba ‘wanadamu wote wamekuwa wakimtafuta Mungu.’​—Matendo 17:26-28.

9 Yesu alikubaliana na tamaa hiyo ya msingi, akisema: “Wenye furaha ni wale wanaoona uhitaji wao wa kiroho,” au wale wanaotambua na kutosheleza njaa yao ya kiroho. (Mt. 5:3, NW) Walakini, ni rahisi, kupuza uhitaji huo. Hata mtu ambaye amekuwa akishirikiana na Mungu anaweza kupoteza kuthamini kwake juu ya namna uhusiano huu unavyoleta furaha nyingi. Anaweza kuona wengine wakiwa na mambo ya anasa au wengine wanaofuatilia utendaji fulani wa kupisha wakati unaopendwa na wengi na namna fulani za tafrija. Kwa hiyo huenda akaona hivi kwa wivu, ‘Pengine mambo mazuri yananipita.’ Akifuata mwendo wao kwa kutumia wakati na kupendezwa alikokuwa akitumia kwa ajili ya uhusiano wake na Mungu, huenda maisha yake yakaonekana kuwa na mambo mbalimbali kwa maana ya kimwili, yakipatana zaidi na mtindo wa kisasa. Walakini je! atakuwa kweli kweli mwenye furaha zaidi? Mtu mwenye njaa, anaweza kujifurahisha kuendesha gari lake au kutazama sinema badala ya kula chakula. Utendaji wa namna hiyo waweza kumfurahisha. Lakini je! utatosheleza njaa yake?

10. Kupata kwako furaha kunahusianaje na kutambua uhitaji huo?

10 Vermont Royster, mhariri wa zamani wa gazeti The Wall Street Journal, alitaja juu ya maendeleo ya wanadamu katika ufundi. Kisha akaongeza hivi:

“Hapa kuna ajabu moja. Tunapomfikiria mwanadamu mwenyewe, matatizo yake, katika mahali pake katika ulimwengu wote huu ulio mkubwa mno, hatujaendelea sana kuliko tangu wakati ulipoanza. Tungali na maulizo ya sisi ni nani na sababu tupo na ni wapi tunakokwenda.”​—“Science Digest.”

Unaweza kuthamini kwamba wale wasio na uongozi, wasio na majibu, hawawezi kujiona kuridhika au kuwa na furaha kabisa. Walakini, tunapoangalia mahitaji yetu ya kiroho inavyostahili na kutafuta ufahamu kutoka kwa Neno la Mungu, tunaona mahali petu. Maisha yetu yanakuwa na uongozi mzuri zaidi, yana maana zaidi, tunakuwa na uwezekano zaidi wa kupata furaha.

11. Ni kwa sababu gani utakuwa mwenye furaha zaidi kwa kukubali kanuni za Mungu? (Zab. 19:7, 8, 11)

11 Katika njia nyingine, pia, tunaongeza furaha yetu kwa kutambua uhitaji wetu wa kiroho na kwa kuwa na uhusiano na Mungu. Tumekwisha taja kwamba kukubali kanuni za Mungu za adili kunatusaidia kuepuka magumu, walakini kuna zaidi ya hayo. Tunahitaji kanuni zinazopatana na akili na zenye kutegemeka. Neno la Mungu linatosheleza uhitaji huo barabara. Kwa kuwa kanuni za Mungu zinapatana na ufahamu wetu tunaozaliwa nao wa dhamiri. Kwa hiyo kadiri tunavyojipatanisha navyo tunajisikia vizuri zaidi, tunakuwa katika hali nzuri zaidi, tunakuwa na amani zaidi. (Zab. 1:1-4; Rum. 2:14, 15) Hata tunaweza kusaidia watoto wetu wapate furaha kwa kushiriki kanuni za Mungu pamoja nao. Dakt. Robert Coles wa Chuo Kikuu cha Harvard alisema hivi juu ya vijana:

‘Wanahitaji kutiwa adabu si ili tu wajizuie kupita kiasi katika maono yao ya moyoni bali adabu vilevile kuhusiana na kanuni za adili zilizoelezwa waziwazi. Wanahitaji kitu cha kuamini ambacho ni kikubwa kuliko tamaa na misukumo yao ya ndani. . . . Wanahitaji maoni yaliyopanuliwa ya ulimwengu, kwa kweli, maana ya adili—imani inayoonyesha maana ya maisha haya ambayo sisi sote tunaishi.’

12. Unaweza kufikia ukweli gani wa msingi kuhusiana na furaha?

12 Basi, ni haki kusema kwamba, furaha ya kweli inafungamanishwa na kutambua kwetu uhitaji wetu wa kiroho na kuwa na uhusiano pamoja na Mungu, hata vile Biblia ilivyoonyesha kwa usahihi: “Mwenye furaha ni mtu hodari ambaye amemweka Yehova kuwa tumaini lake,” ‘anayemfanya kuwa kimbilio lake,’ ‘anayemwogopa Yehova,’ atembeaye “katika sheria ya Yehova,” na ambaye ‘humtafuta Mungu kwa moyo wake wote.’ (Zab. 40:4, 34:8, NW; 112:1, NW; 119:1, 2, NW) Kwa unyofu Mungu anataka kututolea upendo wake na kuja katika uhusiano pamoja nasi. Je! sisi nasi kwa kupatana tunaonyesha kwamba tunathamini kuwa katika uhusiano pamoja naye?​—Rum. 8:38, 39.

FURAHA​—KUTOKANA NA KUSIKIA NA KUTENDA

13. Yesu alitutoleaje ufahamu juu ya kuwa na furaha?

13 Wakati mmoja, mwanamke mmoja aliyesikia Yesu akifundisha alipaza sauti hivi: “Ni lenye furaha lile tumbo lililokubeba wewe na matiti uliyonyonya wewe!” (Luka 11:27, NW) Inaelekea, mwanamke huyo alifahamu kwamba Biblia huitukuza hali ya kuwa mama, na kwa wazi yeye alifikiri kwamba Mariamu alikuwa mwenye kubarikiwa au angeweza kuwa na furaha hasa kwa kuwa mwana wake Yesu alikuwa mwalimu mwema na mwenye haki jinsi hiyo. Walakini Yesu alijua kwamba kulikuwako furaha kubwa zaidi kuliko ile ya kuwa baba au mama, hata kuwa mama ya Masihi. Yeye alijibu hivi: “Hasha, badala yake, Wenye furaha ni wale wanaolisikia neno la Mungu na kulishika!”​—Luka 11:28, NW.

14, 15. “Kusikia neno la Mungu” kunahusu nini katika upande wako?

14 Angalia namna Yesu alivyokazia kujishughulisha na—kusikia au kusoma—​“neno la Mungu.” Tumehakikishiwa mara nyingi katika Biblia kwamba kuna faida za kujishughulisha na Neno la Mungu. Zaburi ya Kwanza inasema hivi juu ya ‘mtu mwenye furaha’: “Kupendezwa kwake ku katika sheria ya Yehova, na katika sheria yake husoma kwa sauti ndogo mchana na usiku.” (Zab. 1:1, 2, NW) Kwa hiyo tunaweza kuuliza, ‘Je! mimi ninapata furaha kutokana na chanzo hicho?’

15 Maandiko ni kama ghala ya furaha, kwa kuwa yanatajirisha akili na moyo. Yanaipa roho uhai. Yanatoa tumaini. Yanaionyesha njia ya kupatia maisha yenye kupendeza na yenye matokeo. Yana mawazo ya Mungu ambayo tunaweza kufikiria wakati wo wote. Ndiyo msingi wa hekima ya kweli.​—Linganisha Mithali 3:13-18.

16. Hivyo, basi, kwa kufanya marekebisho fulani unawezaje kuzidisha furaha yako?

16 Kuna vitu vingi vilivyochapwa tunavyoweza kusoma—magazeti, vitabu vya hadithi, vitabu vya historia, jarida za habari juu ya mambo ya nyumbani au ufundi fulani. Ijapokuwa baadhi yavyo huenda vikawa vyenye kupendeza navyo vina mahali pavyo, tunaweza kujiuliza hivi: ‘Kwa faida ya furaha yangu, je! naweza kufanya marekebisho fulani katika orodha yangu au mazoea yangu ya kusoma ili nipate kusoma na kufurahia Neno la Mungu zaidi?’ Ndiyo, bila shaka, lisome kwa furaha yenyewe tu ya kusoma. Soma sehemu yake kila siku, kulingana na orodha ukitaka. Isome Biblia kulingana na utaratibu wa vitabu vyake. Yasome Maandiko kwa kutumia misaada yenye thamani ya kuifahamu Biblia. Mara kwa mara soma tafsiri nyingine za Biblia, au katika lugha nyingine ikiwa unajua lugha nyingine. Naam, kusoma Neno la Mungu zaidi kutakuwa hatua ya kukuelekeza katika kupata furaha.​—Ufu. 1:3.

17, 18. Ni sehemu gani moja ya ‘kulishika Neno la Mungu’ inayoweza kukuongezea furaha?

17 ‘Kulishika Neno la Mungu akasema Yesu, kunahusika pia katika kuwa na furaha. Tulitangulia kuona kwamba inakuwa hivyo kwa kuwa kufanya hivyo kunatusaidia kuepuka matatizo. Lakini inakuwa hivyo vilevile tunapofikiria mambo mengine.

18 Watu wengi leo wanahangaikia sana-sana “MIMI.” Wanajifikiria sana katika jitihada na mahangaiko yao. Walakini, je! wao ni wenye furaha kweli kweli? Tofauti na hilo, Neno la Mungu huonyesha roho ya kupendezwa na wengine, ya kutoa, ya kusaidia watu wengine. Tunaweza kuona mfano wa hilo katika Yehova mwenyewe, kwa kuwa Yeye “aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye . . . awe na uzima wa milele.” Yehova anaitwa “Mungu wa furaha.” (Yohana 3:16; 1 Tim. 1:11, NW) “Kristo naye hakujipendeza mwenyewe,” bali alikufa kwa ajili yetu.​—Rum. 15:3; Gal. 1:3-5.

19-21. (a) Unawezaje kufanya jambo hilo kwa ukamili zaidi? (b) Unafikiri hiyo itakuleteaje furaha zaidi?

19 Kutoa kwetu kwaweza kuwa, nako kunapaswa kuwe kwa namna nyingi. Lakini si lazima liwe jambo lenye mapambo mengi nalo halipaswi liwe jambo linalokusudiwa kuwavutia wengine. Yesu alishauri hivi:

“Ufanyapo chakula cha mchana au cha jioni, usiwaite rafiki zako, wala ndugu zako, wala jamaa zako, wala jirani zako wenye mali; wao wasije wakakualika wewe ukapata malipo. Bali ufanyapo karamu waite maskini, vilema, viwete, vipofu, nawe utakuwa heri [“mwenye furaha,” NW], kwa kuwa wao hawana cha kukulipa [nacho]; kwa maana utalipwa katika ufufuo wa wenye haki.”​—Luka 14:12-14.

20 Hiyo inakazia ukweli wa kwamba furaha inatokana na kutoa. (Matendo 20:35, NW) Kwa habari ya chakula au kitu kingine cho chote, je! unaweza kufikiria namna unavyoweza kutumia shauri hilo la Yesu? Ikiwa wewe ni mume, mke au mshiriki mwingine wa jamaa, sababu gani usiazimie leo kuzungumza namna ya kutenda kwa kutumia pendekezo hilo la Yesu? Ndipo utakapoona jinsi utakavyokuwa mwenye furaha.

21 Njia moja ya kupata furaha ya namna hiyo ni kushiriki na wengine kweli za Biblia zinazoweza kuongeza furaha yao. Ebu wazia jinsi utakavyoona ikiwa utapata mtu anayeona njaa ya kiroho kweli kweli nawe umsaidie kutosheleza uhitaji huo. (Matendo 13:48, 52) Ni kweli, huenda ikahitaji utumie jitihada yenye kuendelea ili kupata mtu wa namna hiyo na kutumia uangalifu wenye subira ili umsaidie atwae chakula cha kiroho kutoka kwa Neno la Mungu. Hata hivyo yeye atapata kuona utimizo wa maneno ya Yesu: “Wenye furaha ni wale wanaolisikia neno la Mungu na kulishika!” (Luka 11:28, NW; Yohana 13:17) Nawe pia, utakuwa mwenye furaha zaidi kwa kujitoa mwenyewe umfurahishe mwingine.

FURAHA​—MRADI AU MATOKEO?

22-24. (a) Furaha Inapaswa kuwa mradi wako kwa kadiri gani? (b) Basi, wawezaje kupata furaha ya kweli? (Mit. 8:32-35)

22 Tumekwisha kuona kwamba furaha sana-sana si maisha ya kuwa na vitu, bali ya jinsi tulivyo na kufurahia. Mara nyingi tunahitajiwa kurekebisha maoni yetu ili tutosheke na vile tulivyo navyo, tukijua kwamba “utauwa pamoja na kuridhika” ni faida kubwa. (1 Tim. 6:6) Lakini ni kwa kadiri gani twapaswa kufanya kupata furaha kuwe mradi wetu, upeo wa kufikiliwa?

23 Kwa kweli, yale ambayo tumezungumza kuhusu kupata uhusiano pamoja na Mungu na juu ya kutoa kwapaswa kutusaidie kuona hili: Furaha haipaswi kuwa ndilo jambo tunalofuatilia sana-sana. Haipatikani kwa kuifanya iwe mradi, bali ni matokeo ya kuishi maisha yetu mbele za Mungu, tukionyesha sifa zake na kutenda kama anavyotutaka tutende. Ni tunda la upendo na utumishi. Furaha imepata kufananishwa na kipepeo. Tukiikimbilia kwa shauku, tukijaribu kuipata inatuponyoka nyakati zote. Tunapoiondoa akilini mwetu na kuendelea kwa amani kulingana na mapenzi ya Mungu, “kipepeo” huyo atakuja na kutua begani mwetu.​—Rum. 12:9-21.

24 Kwa hiyo, ni kweli kwamba kwa kadiri iliyo kubwa furaha inakutegemea wewe. Usiifuatilie kwa shauku na kuifanya kuwa mradi wako mkubwa maishani. Badala yake, tambua uhitaji wako wa kiroho, uhitaji wako wa kujifunza juu ya Muumba wako na kumwabudu. Kufuata kanuni zake za adili kutakulinda na magumu mengi na kuyapa maisha yako uimara unaohitajiwa. Jitahidi kuwa na uhusiano wa karibu na Yehova Mungu, kwa kuwa utapata uradhi na furaha katika kuwa kama huyo “Mungu wa furaha.” Jipatie wakati zaidi maishani mwako wa ‘kusikia neno la Mungu.’ Kisha upate thawabu inayotokana na kutoa, ukisaidia wengine wamjue Yehova na makusudi yake. Bila shaka utapata kuona, kama vile wengine milioni nyingi wamepata kuona leo kwamba, utakuwa umepata baraka ya kuwa na furaha nyingi.​—Zab. 146:5.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki