Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 9/1 kur. 15-20
  • Twashukuru kwa Ajili ya ‘Tumaini Letu la Furaha’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Twashukuru kwa Ajili ya ‘Tumaini Letu la Furaha’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “SHUKURUNI”
  • KUMSHUKURU MUNGU
  • TUMAINI LA FURAHA AMBALO KWALO TWAPASWA KUSHUKURU
  • WENYE SHUKRANI KWA AJILI YA YALE YALIYO MBELE
  • “Toeni Shukrani Kuhusu Kila Jambo”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • Shukrani
    Amkeni!—2016
  • Sitawisha Roho ya Shukrani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Kwa Nini Uwe Mwenye Shukrani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 9/1 kur. 15-20

Twashukuru kwa Ajili ya ‘Tumaini Letu la Furaha’

“Twalingojea tumaini la furaha na kufunuliwa kwenye utukufu kwa Mungu mkuu na kwa Mwokozi wetu, Kristo Yesu.”​—Tito 2:13, NW.

1, 2. Ni katika njia gani mbili kuonyesha shukrani kwaweza kuleta furaha?

WAFANYA kazi wenzake walimjua kuwa karani stadi, mwenye kutimiza mambo na mwenye furaha. Huenda wakawa walimsifu kwa ajili ya mazoezi aliyopewa na uwezo wake wa kutimiza mambo. Walakini wakati alipoulizwa juu ya jambo hilo, mwanamke huyu mwenye ufahamu alivuta fikira kwenye shukrani za tajiri wake. Kwa sababu gani?

2 Yeye alieleza kwamba hata kazi yake iwe ndogo au ya kawaida namna gani, tajiri wake alionyesha shukrani kwa unyofu. Hivyo yeye alijiona kuwa wa maana na kuwa anahitajiwa; naye alikuwa mfanya kazi mwenye furaha vile-vile. Jambo hilo linaonyesha vizuri sana faida moja ya matokeo ya kuonyesha shukrani. Hata hivyo, shukrani hufaidi si mpokeaji tu; bali pia ni njema kwa mtu yule anayezionyesha, ambaye amesitawisha roho ya kuwa mwenye shukrani.

3. Sababu gani yatupasa kusitawisha roho ya kushukuru?

3 Leo inaonekana kwamba watu wengi wanahangaikia sana-sana nafsi yao wenyewe. Hiyo iko tofauti sana na roho ya kushukuru, ambayo katika kuionyesha mtu anawafikiria wengine naye anaonyesha utayari wa kushukuru yale yanayofanywa na wengine. Jambo linaloelekea kuwa ukweli ulio kinyume ni kwamba, ukijitahidi kusitawisha kupendezwa na wengine kwa unyofu na kuwa tayari kuonyesha shukrani kwa ajili ya utumishi wao, matendo na jitihada zao, utakuwa mwenye furaha zaidi. Na zaidi ya hayo, kusitawisha roho ya kushukuru kwaweza kuwa na matokeo katika uhusiano wako na Yehova Mungu. Kunaweza kuwa na matokeo juu ya hali yako yote ya kufurahia maisha sasa na kwa kadiri ambayo katika hiyo unashiriki katika “tumaini la furaha” ambalo Biblia yawatolea Wakristo.​—Tito 2:13, NW.

“SHUKURUNI”

4. Ni nini maoni ya Biblia juu ya kushukuru?

4 Biblia hutusihi tusitawishe roho ya kuwa wenye kushukuru. Kwa mfano, mtume Paulo aliandika hivi: “Shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.” Naye aliwashauri Wakolosai hivi: “Na amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu; ndiyo mliyoitiwa katika mwili mmoja; tena iweni watu wa shukrani.” (1 The. 5:18; Kol. 3:15) Ijapokuwa shauri hilo sana-sana linahusu shukrani zetu kwa Mungu, lapaswa lituonyeshe thamani ya kusitawisha roho ya kushukuru katika mambo ya maisha ya kila siku.

5. Paulo alionyeshaje roho ya kushukuru?

5 Paulo mwenyewe hakusita kuwapongeza wale waliokuwa wametenda mema, au kuwashukuru moja kwa moja. Yasome maneno yake katika Warumi 16:1-4 NW. Katika fungu hilo la maneno peke yake alimpongeza Fibi kwa shukrani ‘akiwa mtu aliyewatetea wengi,’ pengine kwa kutumia uvutano wake katika ujamii huo ili awatetee Wakristo walioshtakiwa kwa makosa au kwa kuonyesha ukaribishaji wageni kwa Wakristo wasafirio. Kisha Paulo aliwashukuru waziwazi watu wawili waliooana Priska na Akila kwa kuwa ‘walikuwa tayari hata kukatwa vichwa ‘vyao’ kwa ajili yake na ya wengine. Waweza kuwazia furaha waliokuwa nayo Fibi, Priska na Akila kwa ajili ya shukrani zilizoonyeshwa waziwazi sana jinsi hiyo. Lakini ilimfaa Paulo pia kwa kuonyesha shukrani katika njia hiyo. Kwa kufanya hivyo aliweza kupata furaha inayotokana na kutoa—kutoa ukubali, heshima, kitia-moyo. Sisi, pia, twaweza kupata furaha kama hiyo tunapoonyesha shukrani.​—Matendo 20:35, NW; 2 Tim. 1:16-18.

6, 7. Wewe waweza kuonyeshaje shukrani?

6 Kila siku tunazo nafasi za kuonyesha kwamba tunashukuru. Laweza kuwa jambo dogo kama vile kuonyeshwa fadhili —pengine mtu fulani anatufungulia mlango au anatuchukulia kitu ambacho tumeangusha. Hata hivyo, kusema “asante” lapaswa liwe jambo zaidi ya kufuata tu kawaida. Ikiwa tunaona kushukuru kweli kweli moyoni mwetu, wengine watajua hivyo na kama matokeo wao watakuwa wenye furaha zaidi—na ndivyo nasi.

7 Hatua nzuri ingekuwa kujaribu kuwa na roho iliyopanuliwa ya kushukuru, pengine kuwashukuru watu tusiowashukuru kwa kawaida. Hao ni watu kama vile karani wa duka, mtumishi wa hoteli au karani wa posta. Tabasamu yako pamoja na kusema “asante” kwa unyofu kutafanya kazi yao kuwa rahisi zaidi, yenye kuthawabisha zaidi. Hata hivyo wale wanaostahili shukrani zetu zaidi ni wale walio karibu yetu ambao tunaelekea kusahau jitihada zao. Unamshukuru mkeo mara nyingi kadiri gani kwa ajili ya chakula kizuri anachopika, kwa ajili ya jitihada zake za kuweka nyumba ikiwa safi au kwa kuwatunza watoto kwa subira? Ni waume wangapi wanaofanya kazi siku baada ya nyingine pasipo kusikia neno la kuonyesha kuthamini kutoka kwa wake zao, pasipo kutaja watoto wao. Enyi vijana, je! mwaweza kufikiria zaidi yale yote mnayofanyiwa na wazazi wenu, kisha mwashukuru kweli kweli kwa moyo? Kadiri utakavyozoea kushukuru, maisha yako yatatajirishwa zaidi. Wengine watakupenda zaidi nacho kifungo cha upendo kitasitawi. Ndiyo, utakuwa mwenye furaha zaidi.

KUMSHUKURU MUNGU

8-10. (a) Kulingana na Zaburi 100, sababu gani inatupasa kumshukuru Mungu? (b) Watu wengi wakoje kuhusiana na jambo hilo?

8 Ikiwa tunakuwa na sababu ya kuwashukuru wanadamu wenzetu kwa ajili ya yale wanayofanya, tuna sababu kubwa hata zaidi za kushukuru Muumba wetu. Zaburi ya 100 ni wimbo wa kushukuru, ukionyesha sababu gani inafaa kumshukuru Mungu. Hapo twasoma hivi: “Ni yeye aliyetuumba, wala si sisi wenyewe.” (Zab. 100:3, NW) Hilo ni jambo linalopatana sana na akili. Tungewezaje kuwa na nafasi yo yote ya kupata furaha ikiwa Mungu hakutuumba sisi wanadamu na kuturuhusu tuishi? (Matendo 17:26-28) Ndiyo, uhakika wenyewe wa kwamba tunao uzima ni sababu ya kushukuru.

9 Zaburi 100:5 hutangaza hivi: “Kwa kuwa Yehova ni mwema.” (NW) Hiyo ni kweli katika njia nyingi. Mojayapo ya hizo ni kwamba Yehova ametupa vitu vizuri vya kuendeleza uhai wetu, na wakati ule ule tupate kuvifurahia. Twaishi juu ya dunia ya Mungu nasi twaendeleza uhai wetu kwa kutumia vitu vingi vilivyo ndani yake. (Isa. 45:18; Matendo 14:15-17) Ikiwa rafiki yako angekupa tunda tamu na lenye kuendeleza afya, bila shaka ungemwambia, “Asante.” Hata hivyo, chanzo hasa cha tunda hilo, pamoja na chakula chote kingine cha asili, ni Yehova Mungu. (Mwa. 2:9, 15, 16; Zab. 104:10-15, 24; 145:15, 16) Kwa habari ya mipango kama hiyo, wewe waonaje juu ya Mungu?​—1 Tim. 4:3, 4.

10 Ili sisi tuwe wenye kumshukuru Mungu ingemaanisha kwamba sisi tuko tofauti sana na watu wengi leo. Wao wana maelekeo ya kutomjali Mungu na yale ambayo amefanya. Hata wale ambao jamaa yao ina desturi ya kusema maneno machache ya “shukrani” kabla ya kula chakula, hawaonyeshi kwa maisha yao kwamba wanamshukuru sana Mungu. Wao hawafikirii mapenzi ya Mungu wanapopanga mambo ya maisha yao. Lakini je! sisi tuko tofauti? Twapaswa kuwa?

11, 12. Ni ishara gani tunayopewa katika Wakolosai 3:15 juu ya kuwa wenye shukrani?

11 Kama vile ilivyotangulia kutajwa, mtume Paulo aliandika hivi: “Na amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu; ndiyo mliyoitiwa katika mwili mmoja; tena iweni watu wa shukrani.” (Kol. 3:15) Hivyo, ili sisi tuwe wenye shukrani kweli kweli kwa Mungu tunahitajiwa kuonyesha zaidi ya maneno ya kushukuru tu. Tunahitajiwa tuonyeshe maishani mwetu kwamba sisi tunamshukuru. Hatua kubwa katika kufanya hivyo ni kujifunza Neno lake tupate kujua ni nini yaliyo mapenzi yake kwetu leo, kisha tuyafanye.​—Yohana 13:17.

12 Maneno ya Paulo katika Wakolosai 3:15 yapaswa vilevile kukumbusha kwamba Yehova Mungu amewaita watu mmoja mmoja pamoja wafanyize kundi la Kikristo lenye umoja. Hao ni wanaokubali kwamba wao ni wenye dhambi walakini wanajua kwamba wanaweza kusamehewa na Mungu kwa msingi wa dhabihu ya ukombozi ya Yesu. (Rum. 6:17, 23; 7:22-25) Ebu fikiria hiyo yaweza kumaanisha nini kwako. Unaweza kuwa na hali yenye kukubalika machoni pa Mungu. Hiyo ni sababu moja ya kumshukuru Mungu.​—Ufu. 7:10, 14.

13. Shukrani zetu zinakuwaje zaidi ya uzima wetu sasa tu?

13 Hata hivyo, tunaweza kufikiria kama roho yetu ya shukrani ni jambo linalohusu tu maisha yetu ya kila siku sasa. Je! ni jambo la kuwa wenye uelekevu zaidi katika kuthamini yale tunayofanyiwa na wengine, wanadamu wale wengine na Mungu mwenyewe? Hapana, kwa kuwa shukrani za Mkristo zahusu wakati ujao, tumaini lake. Paulo aliandika hivi: “Twalingojea tumaini la furaha na kufunuliwa kwenye utukufu kwa Mungu mkuu na kwa Mwokozi wetu, Kristo Yesu.”​—Tito 2:13, NW.

TUMAINI LA FURAHA AMBALO KWALO TWAPASWA KUSHUKURU

14, 15. Ni nini lililokuwa “tumaini la furaha Paulo alitaja katika Tito 2:13, NW?

14 Ni nini lililokuwa “tumaini la furaha” alilokuwa nalo Paulo na ambalo kwalo alishukuru? Lilikuwa taraja lenye furaha la kufufuliwa na kwenda mbinguni, akawe huko kiumbe cha kiroho kisichoweza kufa na mtawala-mwenzi wa Yesu Kristo katika “ufalme wake wa mbinguni.” (2 Tim. 4:18) Tumaini ilo hilo ndilo alilolishiriki Tito pamoja na Wakristo waliozaliwa kwa roho katika Kolosai na Thesalonike.

15 Hivyo Paulo aliweza kuwaandikia Wakolosai hivi: “Twamshukuru Mungu, Baba yake Bwana wetu Yesu Kristo, sikuzote tukiwaombea; tangu tuliposikia habari za imani yenu katika Kristo Yesu, na upendo mlio nao kwa watakatifu wote; kwa sababu ya tumaini mlilowekewa akiba mbinguni; ambalo habari zake mlizisikia zamani.” (Kol. 1:3-6) Kwa hiyo, akiwa na sababu nzuri, Paulo aliweza kuwasihi hao waliokuwa wameitiwa uzima wa kimbinguni hivi: “Iweni watu wa shukrani.”​—Kol. 3:15.

16. “Tumaini” hilo lingetimizwa wakati gani?

16 Hilo “tumaini la furaha” la kufufuliwa kwenye uzima wa kimbinguni lingetimizwa wakati gani? Paulo alijua kwamba halingetimizwa mpaka kwanza matukio fulani ya wakati ujao yatukie. Yeye aliandika kwamba “sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa [kuwapo] kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mautini.” Ndipo “waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.” Kwa hiyo halingetimizwa mpaka kuwapo (Kigiriki, pa·rou·siʹa) kwa Kristo kuanze.​—1 The. 4:15-17.

17, 18. Sababu gani hasa wakati huu ni wa maana kuhusiana na hilo “tumaini la furaha”?

17 Jambo hilo lina vionyesho vyenye kusisimua kwetu sisi. Yesu alitabiri kwamba kuwapo kwake kungeonyeshwa na ishara yenye sehemu nyingi kutia na vita, matetemeko ya ardhi, upungufu wa chakula na mambo mengine mengi yasiyo ya kawaida ambayo yameonekana wazi-wazi tangu Vita ya Ulimwengu ya Kwanza ya mwaka 1914. (Mt. 24:3-14, NW) Ni jambo linalostahili kuangaliwa vilevile kwamba kufufuliwa kwa Wakristo waliotiwa mafuta kwenye uzima wa kimbinguni kulitabiriwa kwamba kungetukia kabla ya Mfalme Yesu Kristo kuchukua hatua katika “dhiki kubwa” inayokuja. (Mt. 24:21, Ufu. 2:26, 27) Kwa hiyo, sisi twaishi katika wakati ambao Paulo, Tito na wengine, waliokuwa na umoja na Kristo lakini wakafa, wanapopata kutimiziwa ‘tumaini lao la furaha.’

18 Ufufuo huo vilevile ni sehemu ya “kufunuliwa kwenye utukufu kwa Mungu mkuu na kwa Mwokozi wetu, Kristo Yesu.” (Tito 2:13, NW) Akisaidiwa na Mungu, Yesu anaonekana au kufunuliwa katika maana ya kwamba anahukumu na kuwathawabisha wale waliokuwa katika umoja na Kristo. Kuhusu jambo hilo Maandiko yalisema kwamba “atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa” waungane pamoja naye mbinguni. (1 The. 4:16) Namna gani Wakristo wale waliobaki wakiwa hai duniani? Kila mmoja wao afapo ‘angegeuzwa, kwa nukta moja.’ Angepewa mwili wa roho na kuchukuliwa mbinguni, na kuthawabishwa na “taji ya uzima.”​—1 The. 4:17; 2 Tim. 4:1, 8; 1 Kor. 15:44, 50-57, HNWW; Yak. 1:12.

19. Ni nani wengine walio na tumaini la furaha?

19 Jambo hilo lililotimizwa na Mwokozi wetu, Kristo Yesu, vilevile ni ufunuo wa utukufu wa Mungu. Walakini kufunuliwa kwa utukufu wa Mungu kupitia kwa Kristo kutatimiza jambo jingine zaidi, ambalo ni la maana hasa kwa wale Wakristo wanaojua leo kwamba wao hawakutiwa mafuta kwa roho ya Mungu na kuchaguliwa kwa ajili ya uzima katika mbingu. Hao ni wale Wakristo waaminifu walio na tumaini la furaha la kupata uzima wa milele katika paradiso ya kidunia itakayorudishwa. Ikiwa hilo ndilo taraja lako, fikiria sababu ya pekee uliyo nayo sasa ya kushukuru.

WENYE SHUKRANI KWA AJILI YA YALE YALIYO MBELE

20, 21. Ilitabiriwa kwamba Yesu angetimiza nini wakati wa kuwapo kwake?

20 Kwa karne nyingi waabudu wa kweli wa Yehova wamelazimika kuvumilia na kushindana na taratibu mbovu ya mambo iliyopo, dini ya uongo ikiwa sehemu yake isiyoweza kutenganishwa. Wakristo wa kweli wameweza kupata furaha nyingi katika kumtumikia Yehova, walakini hawataweza kamwe kupata furaha kamili maadamu hii taratibu mbovu pamoja na dini yake ya uongo ipo. Hata hivyo, kuna sababu halisi ya kuwa na furaha na shukrani sasa! Sababu gani hiyo?

21 Alipokuwa akiwaandikia Wathesalonike juu ya kuwapo kwa Kristo, mtume Paulo aliongozwa kwa roho aahidi kwamba kipindi hiki kingeleta mabadiliko mazuri sana. Jambo moja ni kwamba, Kristo angechukua hatua na kuiharibu “kwa kufunuliwa kwa kuwapo kwake” sehemu ile ya dini ya uongo inayoitwa “mtu wa uasi.” Hasa huo ni ukafiri wa kumpinga Kristo unaoendelezwa na viongozi wa kidini, sana-sana viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo.​—2 The. 2:3-8, NW.

22, 23. Ni kwa sababu gani kukomeshwa kwa dini ya uongo kutakuwa jambo ambalo kwalo tutashukuru?

22 Kukomeshwa kwa dini ya uongo kungekuwa sababu ya kumshukuru Mungu. Lakini Kristo atafanya mengi zaidi. Akisaidiwa na Yehova Mungu, Yesu atawaharibu wale wote “wasiomjua Mungu, na wao wasiotii Injili ya Bwana wetu Yesu.” (2 The. 1:6-10) Sisi twaishi katika wakati wa kuwapo kwa Kristo na wa “kufunuliwa kwenye utukufu kwa Mungu mkuu na kwa Mwokozi wetu, Kristo Yesu.” Hiyo yamaanisha kwamba twaishi katika wakati ambapo kukomeshwa huko kwa dini ya uongo na kwa wale wote wanaokataa kumtumikia Muumba kwa kweli kutatukia. Ikiwa Paulo aliweza kuwaandikia Wathesalonike huko nyuma, “shukuruni kwa kila jambo,” ebu fikiria sababu tuliyo nayo ya pekee ya kufanya hivyo!—1 The. 5:18.

23 Kuondolewa kwa dini ya uongo kutakuwa baraka. Hayatakuwapo tena mafundisho yenye kupotoa ambayo yamewaogopesha watu milioni nyingi kwa muda mrefu sana—juu ya nafsi zisizoweza kufa zikiteseka katika moto au juu ya roho za wafu. (Yohana 8:32) Wanadamu wote watiifu ‘watatii habari njema ya Bwana wetu Yesu’ na kumtumikia Yehova. Hiyo italeta umoja na amani. Je! hilo si jambo ambalo kwalo twapaswa kushukuru?

24, 25. Ni baraka gani zaidi zilizoko mbele ya wanadamu watiifu?

24 Wakati wale wasioitii ‘Injili’ watakapokuwa hawapo tena, wanadamu watajifunza na kufuata njia za haki. (Isa. 11:9; 26:9) Hata sasa waweza kuliona kuwa jambo la kuridhisha kuzungumza pamoja na jamaa yako jinsi jambo hilo litakavyoleta tofauti. Lilinganishe na yanayowapata sasa kazini, au katika kushughulika na wakuu wa serikali, au wakati mnapokuwa mkisafiri katika sehemu msizofahamiana nazo.

25 Ile taratibu mpya vilevile itakuwa na baraka ya mambo yanayoonekana kutoka kwa Mungu. Yeye ataondoa magonjwa na kifo. (Ufu. 21:1-4) Atabariki kazi ya mikono yetu ili tuweze kujifurahisha na mambo mengi yaliyo ya lazima maishani. (Zab. 67:6; linganisha Isaya 65:21-25) Hata amani itakuwako kati ya wanadamu na viumbe-wanyama vya Mungu; Yehova atahakikisha jambo hilo, hata kama vile ilivyokuwa katika ile paradiso ya kwanza wakati wanyama walipokuwa wakila majani nao hawakuwaumiza wanadamu.

26. Wewe una sababu gani za kushukuru na kuwa na furaha?

26 Baraka hizo ziko mbele yetu tu. Wewe unaweza kuendelea kuishi upate kuziona. Hivyo, ni wakati wa pekee kama nini ambao katika huo twaishi! Ijapokuwa wanadamu kwa jumla hawana shukrani wala furaha leo, sisi tuna sababu nyingi za kumshukuru Mungu, na sana-sana kwa sababu ya tumaini la furaha tulilo nalo. Acheni tumshukuru kwa ukawaida kwa sababu yalo.

—Kutoka The Watchtower Apr. 1, 1981.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki