Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 11/15 uku. 3
  • Imani Imekwenda Wapi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Imani Imekwenda Wapi?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • NI NINI IMANI HIYO?
  • Onyesha Imani Yako Katika Ahadi za Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Ubora Uliojaribiwa wa Imani Waleta Uvumilivu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Zoea Imani Yenye Msingi Wa Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Imani—Sifa Inayotuimarisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 11/15 uku. 3

Imani Imekwenda Wapi?

MWANDIKAJI wa habari za magazeti Mwingereza anayejulikana sana, na ambaye ni mhariri, Malcolm Muggeridge alisema hivi wakati mfupi uliopita:

“Inakuwa wazi zaidi na zaidi kwangu kwamba tatizo ambalo ustaarabu wa nchi za uzunguni unapata kwa msingi linaletwa na upungufu wa imani. . . . Kuna ongezeko la kukubali wazo la kibinadamu kwamba hakuna Mungu, kwamba watu ndio wanaoamua yatakayowapata.”

Wakati wa miaka iliyopita, watu wengi wangekubali wanamwamini Mungu na kwamba wanapendezwa na mapenzi yake. Lakini jambo hilo limebadilika sana. Watu wengi wanaona kwamba maendeleo ya sayansi katika kizazi chetu yamefanya imani kwa Mungu kuwa ya kizamani au isiyo halisi. Wengine wameona kufanikiwa kwa uovu nao wameamua kwamba ama Mungu hajali au yeye hayupo. Kama Muggeridge alivyosema, wanaamini kwamba wanapaswa kujitegemea, wakiongoza njia yao ya maisha bila kumwamini Mungu wala njia zake.

Walakini huenda watu hao wakawa wanakosa jambo jingine zaidi ya imani. Namna gani hivyo? Ikiwa imethibitishwa kwamba imani inafaa leo, wao pia wanakosa faida zinazofaa zinazoletwa na imani.

NI NINI IMANI HIYO?

Neno “imani” linatumiwa katika njia mbalimbali leo. Kwa mfano, huenda ukasikia mtu akisema hivi, ‘Ninaamini kwamba motokaa yangu itawaka lijapokuwapo joto hili jingi.’ Hata hivyo, tunapochunguza ulizo ‘Imani inafaa leo?’ tunamaanisha kumwamini Mungu na kuamini thamani ya uongozi wake.

Watu wengine wanaodai kuwa wana imani hiyo wanakosea kwa kudhani ni mawazo ya utulivu, namna fulani ya kuamini imani ya kidini. Wanaona kwamba ni vema kuamini kitu fulani, na kwa hiyo kwa maono yao wanaona kidogo kwamba lazima Mungu awepo. Imani hiyo ya uvuguvugu haibadili sana maisha zao, nayo inatokomea mara tu jaribu la kweli linapotokea. Kwa hiyo tunaweza kuona sababu gani imani hiyo haifai.

Hata hivyo, kumwamini Mungu ambako Biblia inatia moyo ni tofauti kabisa. Ni “taraja lililohakikishwa la mambo yanayotumainiwa, wonyesho dhahiri wa mambo ya hakika ijapokuwa hayaonwi.”​—Ebr. 11:1, NW.

Neno la Kigiriki ambalo mahali hapo linatafsiriwa “taraja lililohakikishwa” linatoa wazo la kitu kilicho msingi au kinachotoa uhakika wa yanayotazamiwa. Kwa hiyo imani hiyo ya ki-Biblia si maono yasiyofahamika vizuri tu au tumaini lisilotegemeka; uhakika wa kweli unahusika. Neno la Kigiriki ambalo tafsiri yake ni “wonyesho dhahiri” linatoa wazo la kutokeza ushuhuda, sana-sana ushuhuda unaoonyesha kitu kingine tofauti na kile kinachoonekana kuwa kama kilivyo. Hivyo, hata ikiwa watu wengi wanasema kwamba hakuna Mungu, kumwamini ambako tunazungumza juu yake kunahusiana moja kwa moja na ushuhuda thabiti.

Wewe unasimama wapi kuhusiana na hilo? Je! una uhakika, unaotegemezwa na ushuhuda wenye kusadikisha, kwamba Mungu yupo? Tukiendelea zaidi na jambo hilo, Je! kweli kweli inafaa kuwa na imani hiyo na kuongoza maisha yako kulingana nayo? Kwa hiyo, je! imani inafaa siku hizi?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki