Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w82 1/15 kur. 4-8
  • Kushindania Mamlaka Kutakuwa na Matokeo Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kushindania Mamlaka Kutakuwa na Matokeo Gani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “WAFALME” WAWILI WENYE KUSHINDANA
  • “MUNGU WA NGOME”
  • ‘KUSHINDANA’ KWA “MFALME WA KUSINI”
  • NAMNA “MFALME WA KASKAZINI” Anavyotenda
  • “WAFALME” WOTE WAWILI WAFIKIA MWISHO WAO
  • Wafalme Washindani Wakaribia Mwisho Wao
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
  • “Mfalme wa Kaskazini” Katika Wakati wa Mwisho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Ushindi wa Mwisho wa Mikaeli, Yule Mwana-Mfalme Mkuu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Sikiliza Neno la Kiunabii la Mungu kwa Siku Zetu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
w82 1/15 kur. 4-8

Kushindania Mamlaka Kutakuwa na Matokeo Gani?

“MASHARIKI NI MASHARIKI, na Magharibi ni Magharibi, na hizo mbili hazitakutana kamwe, Mpaka Dunia na Anga zisimame kwenye Kiti cha Hukumu kikuu cha Mungu.” Matukio ya hivi karibuni ya kushindania mamlaka kati ya mwungano wa mataifa ya Mashariki na mwungano wa mataifa ya Magharibi yanafanya maneno hayo ya kimashairi ya Rudyard Kipling yasikike kwa kushangaza kuwa ya kisasa.

Hata hivyo, tunapofikiria, mtu anaposema juu ya mashindano ya Mashariki na Magharibi, usemi “Mashariki” haumaanishi kwa halisi mashariki kama vile tu ‘Magharibi” isivyomaanisha mataifa yote yaliyoko upande wa magharibi wa sehemu fulani ya dunia.’ Leo mataifa ya Kikomunisti yanatia ndani si Urusi tu na mataifa ya Ulaya ya upande wa mashariki bali pia mataifa mengine ya Kiafrika pamoja na Cuba. Kati ya hayo hakuna lo lote linaloweza kusemwa kuwa liko upande wa mashariki. Vivyo hivyo, mataifa ya “Magharibi” yanatia ndani nchi kama Canada, Denmark (kutia na Greenland), Iceland, Norway, Australia, New Zealand na Japan. Baadhi ya nchi hizo haziko upande wa magharibi. Kwa hiyo kwa nini watu huzungumza juu ya “mashindano kati ya Mashariki na Magharibi”? Kwa sababu hapo kwanza “Vita vya Maneno” vilikuwa hasa kati ya mataifa mawili yenye nguvu nyingi sana​—Urusi na Amerika​—moja wa sehemu kubwa likiwa upande wa mashariki mwa Ulaya, na lile jingine magharibi. Hivyo, kwa kadiri ambavyo mambo yameendelea kutokea, “Mashariki” la “Magharibi” zimekuwa na maana za mfano.

“WAFALME” WAWILI WENYE KUSHINDANA

Vivyo hivyo, katika sura ya 11 ya Danieli, kwa kufaa Biblia inatumia semi mfalme wa kaskazini” na “mfalme wa kusini” kuonyesha mfuatano wa mamlaka za kisiasa zenye kushindana. Hapo kwanza wafalme” hao wawili walikuwa upande wa kaskazini na kusini wa nchi ya watu wa Danieli​—kwa kweli yakiwa pande hizo pia za nchi ya watu wa kale wa Yehova Mungu​—katika Mashariki ya Kati.

Unabii huo ulianza kutimizwa baada ya kifo cha Aleksanda Mkuu na kugawanywa kwa Mamlaka yake ya Makedonia kati ya warithi wake wanne. Wawili kati yao, Seleuko I akawa “mfalme wa kaskazini” wa kwanza na Ptolemy I akawa “mfalme wa kusini” wa kwanza. Mmoja wa watu hao alianzisha Mamlaka ya Seleuko ya kaskazini na yule mwingine akawa wa kwanza wa Mafarao wa Ptolemy wa Misri, upande wa kusini. Kwa karne nyingi, nchi ya wale ambao kufikia wakati huo walikuwa watu wa Yehova ilikuwa kitu cha kushindaniwa kati ya mamlaka hizo mbili, zilipokuwa zikipigania utawala.

Kama ilivyo, kadiri wakati ulivyopita, mamlaka zenye kufananishwa na “mfalme wa kaskazini” na “mfalme wa kusini” ziliendelea kubadilika. Walakini pambano la utawala liliendelea, wakati wa karne zote zilizopita. Vilevile unabii huo ulitabiri kwamba mashindano kati ya hao ‘wafalme wawili’ yangeendelea mpaka “wakati wa mwisho.” (Dan. 11:27, 35, 40)a Leo tunaona mashindano ya kutaka mamlaka ya ulimwengu mzima yakiendelea kuliko wakati mwingine wo wote uliopita kati ya wenye kufuata Ukomunisti na wasiofuata Ukomunisti. Je! inawezekana kuonyesha vikundi hivyo viwili vya mataifa kuwa ndio hao ‘wafalme wawili’? Na tuone.

“MUNGU WA NGOME”

Mara tu ukiisha kusema juu ya “wakati wa mwisho,” unabii wa Danieli unaendelea kusema hivi:

“Naye mfalme [wa kaskazini] atafanya kama apendavyo; naye atajitukuza na kujiadhimisha juu ya kila mungu, naye atanena maneno ya ajabu juu ya Mungu wa miungu. . . . Wala hataijali miungu ya babu zake; . . . Lakini katika mahali pake atamheshimu mungu wa ngome; na mungu ambaye baba zake hawakumjua atamheshimu, kwa dhahabu, na fedha.”​—Dan. 11:36-38.

Kati ya mataifa hayo mawili yenye nguvu nyingi sana ni lipi ambalo bila aibu limenena maneno ya kumpinga “Mungu wa miungu,” Yehova, na kuiita dini kuwa ndiyo “kasumba ya watu”? Ni lipi kati yao ambalo kwa miaka mingi limepanga uchumi walo wote ili kuweka kwanza utokezaji wa bunduki mahali pa siagi; vifaru na ndege za kivita mahali pa chakula, mavazi na bidhaa zinazohitajiwa na watu wa kawaida, na kwa njia hiyo kutukuza “mungu wa ngome”? Ni “mfalme” yupi ambaye ameabudu “mungu ambaye baba zake hawakumjua,” yaani sayansi yenye kutokeza silaha za kijeshi, akimheshimu, “kwa dhahabu, na fedha,” asiyesita kutumia asilimia kubwa ya mali za nchi kwa ajili ya ufundi wa kijeshi na vikosi vya vita? Hakuwezi kuwa shaka kwamba “mfalme wa kaskazini” wa kisasa ni kile kikundi cha mataifa ya Kikomunisti, ambacho kinaongozwa na Urusi.

Huko nyuma katika mwaka 1977, Shirika la Upelelezi la Ulinzi wa Amerika lilikubali kwamba jeshi la Urusi “ndilo lenye nguvu zaidi ulimwenguni, lenye silaha nyingi zaidi zenye baruti na lenye kuweza kusonga hapa na hapa kwa urahisi zaidi.” Utayari huo unaungwa mkono na mafundisho ya kijeshi shuleni. Wanaume wote wenye miaka 18 wanatakiwa na sheria wafanye utumishi wa kijeshi, na kutumia miaka miwili katika jeshi la nchi kavu au jeshi la wanahewa, au miaka mitatu katika jeshi la majini. Na wakiisha kutoka wanaweza kuitwa wakati wo wote watumikie jeshi mpaka wanapofika umri wa miaka 50, na hiyo ni kusema kwamba wakati huu makumi ya mamilioni ya raia wa Urusi wamepata mazoezi ya kijeshi nao wanaweza kukusanywa haraka kwa kusudi la kijeshi.

‘KUSHINDANA’ KWA “MFALME WA KUSINI”

Kwa kuwa “mfalme wa kaskazini” wa kisasa ni kikundi cha mataifa ya Ukomunisti, yakiongozwa na Urusi, “mfalme wa kusini” hawezi kuwa mwingine ila kikundi cha mataifa yasiyo ya Kikomunisti yanayoshindana nao, yakiwa chini ya uongozi wa Amerika. Kuhusu “wafalme” hao, unabii wa Danieli unaendelea kusema hivi “Na wakati wa mwisho mfalme wa kusini atashindana naye [mfalme wa kaskazini].”​—Dan. 11:40.

‘Kushindana’ kwa “mfalme wa kusini” kulikofuata baada ya ile vita kuu kulikuwa na mwanzo hafifu tu, katika mwaka 1947, wakati wa “Fundisho la Truman” la ‘kutopanua mipaka.’ Kufuata hilo, katika mwaka 1949, shirika NATO likatokezwa na, baadaye, matengenezo mengine ya ulinzi ya kusaidiana yakaanzishwa sehemu-sehemu. ‘Kushindana’ huko kukawa kukali zaidi wakati wa vita ya pili ya Vietnam. Walakini pambano hilo na matokeo yake mabaya kwa upande wa Magharibi yakaonekana kama kwamba yanaunga mkono hoja ya kina “njiwa”​—wale walioko Amerika na walioko kati ya mataifa yenye kuiunga mkono wanaopendelea maoni ya kufanya mapatano na mataifa yenye kuunga mkono Urusi.

Hata hivyo, matukio ya hivi karibuni yaonekana yanaonyesha kwamba kina “njiwa” kwa sasa wanapitwa na kina “mwewe”​—wale wanaopendelea maoni makali kuelekea kikundi cha mataifa ya Ukomunisti. ‘Kushindana’ kwa “mfalme wa kusini” juu ya “mfalme wa kaskazini” yaelekea kunaongezeka kuwa kukali. Kwa kupendeza, umoja wa Uingereza na Amerika katika ‘kushindana’ huko ulithibitishwa na habari ifuatayo: “Waziri Mkuu wa Uingereza Margaret Thatcher, ambaye kama Bw. Reagan hasadiki Kremlin (Urusi), ndiye aliyekuwa kiongozi pekee wa ushirika wa NATO kukazia msimamo wa Reagan waziwazi. Alisema Alhamisi usiku [Januari 29, 1981] kwamba hakukuwako ishara yo yote ya Urusi kupendezwa kwa kweli na mazungumzo ya kuondoa wasiwasi.” (International Herald Tribune, Januari 31, 1981) Itapendeza kutazama katika siku zijazo huyo, “mfalme wa kusini” ‘atashindana’ kadiri gani.

Kama ilivyo, “mfalme wa kaskazini,” ambaye sasa anafananishwa na kikundi cha mataifa ya Ukomunisti, anachukua hatua kwa sababu ya ‘kushindana’ huko. Jambo hilo pia lilitabiriwa katika unabii wa Danieli, sura ya 11. Na tuendelee kusoma:

“Na mfalme wa kaskazini atamshambulia [mfalme wa kusini] kama upepo wa kisulisuli, pamoja na magari ya vita, na wapanda farasi, na merikebu nyingi; naye ataingia katika nchi hizo, na kufurika na kupita katikati. . . . Naye ataunyosha mkono wake juu ya nchi hizo, . . . Atakuwa na nguvu juu ya hazina za dhahabu na fedha.”​—Dan. 11:40-43.

NAMNA “MFALME WA KASKAZINI” Anavyotenda

Maitikio ya Urusi juu ya msimamo mkali ambao hivi karibuni umechukuliwa na “mfalme wa kusini” yanaonyesha kwamba “mfalme wa kaskazini” hana nia ya kushindwa nguvu za utawala. Tangu vita ya Ulimwengu ya Pili, Urusi imekuwa ‘ikinyosha mkono wake’ ili kutwaa uongozi juu ya “nchi” mbalimbali na “hazina” (“hazina zilizofichwa,” NW), kutia ndani mafuta.

Utatizi kwa Magharibi vilevile umekuwa kuhusu maongozi ya kisiasa, kwa kuwa serikali nyingi zilizofuata baada ya ukoloni za Mataifa Machanga zimefuata maongozi ya Marx (Ukomunisti). Matukio hayo yamewezesha uongozi wa Urusi uingie katika Asia, Mashariki ya Kati, Afrika na hata kwenye bara za Amerika. Pamoja na hayo, “mfalme wa kaskazini” amefaulu sana katika kuunga mkono maasi yenye kuongozwa na Ukomunisti, na hiyo ikamwezesha kuingia kwenye “nchi” ambazo zinafuata maongozi yake ya kisiasa na ya kijeshi na kutegemea msaada wake wa mambo ya ufundi.

Watu zaidi ya milioni nne wakiwa na silaha katika Urusi na Ulaya ya upande wa mashariki, pamoja na vifaru 50,000, ndege za kivita 5,775, manowari kubwa zinazopita juu ya maji 289 na manowari zinazopita chini ya maji zisizopungua 257, hakika “mfalme wa kaskazini” ana uwezo wa kushambulia “kama upepo wa kisuli-suli, pamoja na magari ya vita, na wapanda farasi, na merikebu nyingi . . . na; kufurika na kupita katikati.”

Kulingana na ripoti mbalimbali, tayari askari wa Urusi wako katika Afghanistan, Cuba, Ethiopia, Iraq, Libya, Mali, Mauritania, Vietnam, Syria na Yemen ya Kusini, licha ya washauri wa kijeshi katika nchi nyingine nyingi. Manowari (merikebu za kivita) za Urusi zinapita wakati wote kwenye bahari zote zinazofaa kivita, kutia ndani Bahari ya Mediterania. Kadiri ambayo “mfalme wa kaskazini” wa Ukomunisti atasukuma mbele vikosi hivyo na ‘kuingia nchi’ nyingine ni wakati ujao tu utakaoonyesha.

“WAFALME” WOTE WAWILI WAFIKIA MWISHO WAO

Hata kadiri ya ‘kujisukumiza’ ya “mfalme wa kusini” iwe nini, na kama “mfalme wa kaskazini” ‘atafurika’ kwa halisi kwa kuingilia nchi nyingine au sivyo, jambo moja ni hakika: Kulingana na unabii wa Danieli, hakuna “mfalme” ye yote kati ya hao wawili atakayepata ushindi kamili juu ya mwingine. Kumhusu “mfalme wa kaskazini,” unabii unasema hivi: “Atafikia mwisho wake, wala hakuna atakayemusaidia.” (Dan. 11:45, ZSB) Zaidi ya hayo, unabii unaolingana na huo unasema kwamba Mamlaka ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika, ambayo pia inafananishwa na “mfalme wa kusini,” “atavunjika, bila kazi ya mikono.”​—Dan. 8:25.

“Wafalme” hao watafikiaje mwisho wao “bila kazi ya mikono” na ‘bila wa kuwasaidia’? Mwisho wao hautaletwa na wanadamu. Unabii wa Danieli unaendelea kusema hivi: “Wakati huo Mikaeli atasimama, jemadari mkuu, asimamaye upande wa wana wa watu wako [wa Danieli na kwa hiyo wa Yehova]; na kutakuwa na wakati wa taabu, mfano wake haukuwapo tangu lilipoanza kuwapo taifa hata wakati uo huo.” (Dan. 12:1) Mikaeli si mwingine ila Mfalme Yesu Kristo aliyewekwa na Yehova. (Linganisha Ufunuo 12:7-10.) Huo “wakati wa taabu” ni “dhiki kubwa” inayotajwa katika unabii wa Yesu juu ya “mwisho wa taratibu ya mambo” na “kuwapo” kwake katika ufalme wake.​—Mt. 24:3, 21, NW; Luka sura 21.

Utimizo wa kisasa wa unabii huo unaonyesha kwamba tunaishi katika huo “wakati wa mwisho.” Karibuni Kristo atakomesha “mfalme wa kaskazini” wa Ukomunisti na “mfalme wa kusini” ambaye si wa Ukomunisti. Hakika, Mfalme Yesu Kristo aliyetawazwa ‘atawapiga’ wao pamoja na mataifa yale mengine yote ya kisiasa kwa “upanga mrefu mkali,” naye “atawachunga kwa ufito wa chuma.” (Ufu. 19:11-21, NW) Na unabii mwingine wenye kutokeza sana katika kitabu cha Danieli kwa njia hiyo utafikia utimizo wake kikamilifu, maana tunasoma hivi: “Na katika siku za wafalme hao [mamlaka za kisiasa] Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaangamizwa milele, wala watu wengine hawataachiwa enzi yake; bali utavunja falme hizi zote vipande vipande na kuziharibu, nao utasimama milele na milele.”​—Dan. 2:34, 35, 44.

Ufalme huo utaleta amani yenye kudumu duniani katika taratibu mpya yenye haki. (2 Pet. 3:13; Ufu. 21:1-5) Katika hiyo hakutakuwako tena “wafalme” wa kisiasa wenye kuonea. Huo ndio “ufalme” wenyewe ambao wewe umeuomba iwapo umekuwa ukisema “Sala ya Bwana.” (Mt. 6:9, 10) Huo ndio tumaini pekee la wanadamu. Mashahidi wa Yehova watakuwa na furaha kukusaidia upate tumaini hilo.

[Maelezo ya Chini]

a Kwa maelezo kamili ya Danieli, sura ya 11, tazama kitabu “Your Will Be Done on Earth,” kilichochapishwa mwaka 1958.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki