Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w82 6/15 uku. 23
  • Maswali kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Elisha Aliona Magari ya Vita Yenye Moto​—Je, Unayaona?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Kielelezo cha Kujidhabihu na cha Uaminifu-Mshikamanifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Jeshi la Yehova Lenye Farasi na Magari ya Vita ya Moto
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
w82 6/15 uku. 23

Maswali kutoka kwa Wasomaji

● Unapopatwa na majaribu magumu au madaraka magumu ya kutimiza, je! inafaa uombe “sehemu maradufu” ya roho ya Mungu, kama Elisha alivyofanya?

Badala ya kujisikia kwamba unahitaji kuomba “sehemu maradufu” ya roho ya Mungu wakati wa tukio fulani, ni afadhali zaidi kuomba Mungu akupe roho takatifu kulingana na mahitaji yako.

Nabii Eliya alipokwisha kuvuka Mto Yordani, muda mfupi tu kabla hajainuliwa juu upande wa mbinguni akiwa katika gari-farasi lenye kuwaka moto, nabii Elisha aliyekuwa mshirika na mrithi wake alimwomba kitu cha pekee. Kulingana na Union Version, Elisha alimwambia hivi Eliya mwenye kwenda zake: “Nakuomba, sehemu maradufu ya roho yako na iwe juu yangu.” (2 Wafalme 2:9) Wakristo wengine wametumia usemi huo kwa kufikiria wanahitaji “sehemu maradufu ya roho,” hata wakafikia kumwomba Mungu awape hiyo sehemu maradufu.

Walakini, New World Translation inatusaidia tufahamu kilichofanya Elisha aombe hivyo. Inasema hivi: “Tafadhali, na iwe kwamba sehemu mbili katika roho yako zinijie mimi.” (2 Wafalme 2:9) Elisha alikuwa akiomba sehemu ya mzaliwa wa kwanza ya roho ya Eliya. Namna gani?

Maneno ya Elisha yanahusu mazoea katika Israeli wa kale ya kugawanya mali za mtu wakati alipokufa. Ijapokuwa wana wale wengine walipokea sehemu fulani ya urithi huo, mzaliwa wa kwanza, au mwana mkubwa zaidi aliyekuwa hai, ndiye aliyepokea sehemu maradufu, na vilevile akapokea daraka la kuwa kichwa katika jamaa hiyo.​—Kumbukumbu la Torati 21:17.

Wakati ambao mapenzi ya Mungu yangehitaji amwondoe Eliya mahali hapo alipotumikia akiwa nabii aliye mkuu wa Israeli, Elisha angemrithi. Elisha asingebaki akiwa ndiye nabii wa pekee wakati huo. Wanaume mbalimbali walishirikiana naye, nao waliitwa “wana wa manabii.” (2 Wafalme 2:3, 5) Lakini Elisha ndiye angekuwa wa kwanza kati yao, akiwa ndiye mrithi mkuu wa Eliya. (2 Wafalme 4:38; 6:1-3) Kwa hiyo ingawa inaelekea wao walikuwa na kiasi fulani cha roho ya Mungu na walitimiza kazi fulani-fulani za kiunabii, Elisha alikuwa kama mwana mzaliwa wa kwanza wa Eliya na basi kwa kufaa angeweza kuomba sehemu mbili za roho ya Eliya.

Yehova Mungu hutolea waabudu wake waaminifu roho takatifu kulingana na mahitaji na hali zao. Wakati Musa alipohitaji usaidizi kwa sababu ya hesabu kubwa sana ya watu waliokuwako, Mungu aliagiza kwamba wanaume wazee 70 wenye kustahili wachaguliwe kusaidia. Yehova alimwambia Musa hivi: “Nitatwaa sehemu ya roho iliyo juu yako na kuiweka juu yao; nao watachukua mzigo wa watu hawa pamoja nawe.” (Hesabu 11:16, 17) Hilo halimaanishi kwamba baada ya hapo sasa Musa angebaki na roho takatifu isiyomtosha, roho yenye upungufu. Bali, Mungu angempa Musa na wale wasaidizi 70 roho ya kuwatosha ili watimize madaraka yaliyokuwa mbele yao. Vivyo hivyo, Elisha na “wana wa manabii” pia wangepata roho takatifu ya kutosha kutimiza wajibu wao mbalimbali na kuyakabili majaribu yaliyokuwa mbele yao.

Wakristo, pia, wanaweza kupokea kiasi cha kutosha cha nguvu ya utendaji ya Mungu, au roho yake. Ni jambo lenye kufahamika wazi kwamba wanapaswa waishi kwa njia isiyozuia mmiminiko na utendaji wa roho takatifu. (Linganisha Waefeso 4:30.) Tena inawapasa waombe wapate roho, wakiyaamini aliyoyasema Yesu: “Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa [roho takatifu] hao wamwombao?” (Luka 11:13) Tunaweza kuwa na uhakika kwamba Mungu “haitoi roho kwa kipimo,” au ‘kwa unyimivu.’ (Yohana 3:34, NW, chapa ya 1950; Centenary Translation of the New Testament) Badala ya kutupa “sehemu maradufu,” yeye atatupa kiasi cha roho takatifu tunachohitaji ili tushindane na matatizo ya maisha, tushiriki katika kazi ya maana ya kuzihubiri “habari njema za ufalme” na kulielewa Neno lake kisha kulifuata.​—Mt. 24:14, NW.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki