Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w82 5/1 kur. 19-24
  • Wenye Bidii kwa “Kazi ya Bwana”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wenye Bidii kwa “Kazi ya Bwana”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • TUNATIWA NGUVU NA TUMAINI LA UFUFUO
  • “MWE IMARA”
  • ‘MWE . . . WASIOONDOLEKA’
  • “SIKUZOTE MWE NA MENGI YA KUFANYA KATIKA KAZI YA BWANA”
  • Zishikeni Sana “Habari Njema”!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Tumaini la Ufufuo Lina Nguvu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • “Wafu Watafufuliwa”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Fundisho la Ufufuo Linakuhusu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
w82 5/1 kur. 19-24

Wenye Bidii kwa “Kazi ya Bwana”

“Mwe imara, bila kuondoleka, sikuzote mwe na mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana.”​—1 Kor. 15:58, NW.

1. Kwa sababu gani tumaini la ufufuo linapasa kuwa na maana halisi kwetu wote?

TUMAINI la ufufuo lapasa kuwa kichocheo kikubwa, sikuzote, kwa kila mmoja wetu. Kwa maana adui kifo kinahusu maisha ya kila mmoja wetu kwa njia ya moja kwa moja au kwa njia isiyo ya moja kwa moja, wakati fulani. Wakati wapendwa wanapokufa, tunaweza kufikiria makusudi bora ya Yehova ili ‘tusije tukahuzunika kama na wengine wasio na matumaini.’ Huenda tukawa na imani kwamba wafu watainuka tena kama Yesu alivyofufuliwa kutoka kwa wafu. (1 The. 4:13, 14) Vilevile, tuna taraja lililohakikishwa kwamba sisi wenyewe tukifa, Yehova atatukumbuka katika ufufuo, mradi tumeendelea kuwa waaminifu katika kuutimiza wakf wetu kwake.​—Yohana 5:28, 29; 6:40.

2. Kwa sababu ya Mhubiri 9:11, nia yetu kuelekea maisha yapasa kuwa nini?

2 Hizi “siku za mwisho” zinaposonga mbele haraka kufikia mwisho wazo, wengi wetu tuna tumaini la kuiokoka ile “dhiki kubwa” pasipo kupata kufa. (Mt. 24:21; 2 Tim. 3:1) Hata hivyo, hata wenye mbio, wenye nguvu, wenye hekima na ufahamu​—“wakati na tukio lisilotazamiwa huwapata wote.” Maradhi yasiyotazamiwa, msiba au maafa yaweza kutupata. Inapokuwa hivyo, ni jambo la kutamanika kama nini kwamba tulikuwa tukijitumikisha sana katika utumishi wa Mungu kwa moyo wetu wote, nafsi, akili na nguvu! Kwa maana ikiwa hivyo kibali yake na kufufuliwa kwetu ni mambo ya hakika. Zaidi ya hayo, kuendelea kuwa wakamilifu kungekuwa kumekuwa kitia-moyo na baraka kwa wengine waliotuona na kutusikiliza, ili wao vilevile waokolewe katika tumaini la ufufuo.​—Mhu. 9:11, NW; Marko 12:30; 1 Tim. 4:15, 16.

TUNATIWA NGUVU NA TUMAINI LA UFUFUO

3. (a) Macho yetu yanapasa kukazwa kwenye mradi gani, na kwa sababu gani? (b) Tumaini la ufufuo linapasa kuwategemeza Wakristo katika njia gani, wawe ni watiwa mafuta au wa ule “mkutano mkubwa”?

3 Mtume Paulo alisema hivi: “Ikiwa tunamtumaini Kristo katika maisha haya peke yake sisi ni wa kusikitikiwa kati ya watu wote.” Imani yetu ingekuwa bure, kuhubiri kwetu kungekuwa bure. Walakini macho yetu yamekazwa kwa uthabiti kwenye mradi huo uliohakikishwa wa uzima katika taratibu mpya ya Yehova​—tuwe tutaupata kwa kuokoka Har–Magedoni, au, kama ilivyo kwa habari ya wengine, kwa kufufuliwa mapema kutoka kwa wafu. Katika siku zake, Paulo alikuwa akizungumza na Wakristo waliokuwa wametiwa mafuta kwa roho ya Mungu, na waliotakiwa wapitie ubatizo katika mauti, kama vile Yesu wakati wa ile miaka mitatu na nusu mpaka kuuawa kwake huko Kalvari. Kwa hiyo Paulo anauliza hivi: “Ikiwa wafu hawatafufuliwa kamwe, kwa nini wao pia wanabatizwa iwe hivyo?” Ndiyo, tumaini la ufufuo liliwategemeza Wakristo hao likawawezesha wavumilie majaribu mengi, nalo laweza kuwategemeza Wakristo leo, tumaini lao liwe ni la uzima wa milele katika ufalme wa kimbinguni au​—kwa hesabu kubwa zaidi​—uzima katika makao ya kidunia ya ufalme huo.​—1 Kor. 15:13-19, 29, NW.

4. Ni kwa sababu gani tunapaswa kuepuka kuchafuliwa na falsafa ya Waipikureo?

4 Akiandika juu ya hali iliyokuwapo katika siku zake, Paulo anaendelea kusema hivi: “Kwa nini sisi pia tumo hatarini kila saa? Kila siku nakabili kifo. Nathibitisha hilo kwa mshangilio juu yenu, ndugu, ambao ninao katika Kristo Yesu Bwana wetu. Ikiwa, kama wanaume, nimepigana na wanyama-mwitu katika Efeso, hayo yana faida gani kwangu? Ikiwa wafu hawatafufuliwa, ‘na tule na tunywe, kwa maana kesho tutakufa.’ “Katika kutangaza “habari njema” zilizokaza fikira juu ya Kristo aliyefufuliwa, Paulo alipatwa na hatari na mateso mengi, na katika mambo hayo yote alipata ulinzi na baraka ya Mungu. Ikiwa ufufuo ulikuwa mzaha tu, yote hayo yangekuwa ni bure. Kama ingekuwa hivyo, basi kama wanafalsafa (wanafilosofia) Waipikureo na wafuasi wao, Paulo na ndugu zake Wakorintho wangalijiingiza sana katika anasa.​—1 Kor. 15:30-32, NW.

5. (a) Tumaini la ufufuo linapasa kuwa halisi kwetu namna gani? (b) Tunapoufanya Ufalme kuwa mradi wetu, tuna mifano gani mizuri ya kisasa?

5 Hata hivyo, tumaini la ufufuo na ufalme wa Kimasihi ni mambo halisi. Yamefungamanishwa pamoja na kusudi la milele la Mungu. Kama vile Wakristo katika nyakati za kimtume walivyotegemezwa na tumaini hilo, ndivyo wanavyotegemezwa leo. Historia ya kisasa ya Mashahidi wa Yehova imepambwa na mfano mzuri wa maelfu ya Wakristo ambao wamekabili kifo bila kusitasita, wakijua kwamba ukamilifu wao umewahakikishia ufufuo wa mapema ama katika “mbingu mpya” au katika “dunia mpya.” Kuna wale mamia ya Mashahidi waliochinjwa, wakapigwa risasi, wakauawa kwa njaa au wakapigwa mpaka kufa katika kambi za mateso za Kikatoliki za Hitler. Hivi karibuni, wengi wamevumilia hatari na mateso katika nchi fulani zenye kufuata siasa za kijamaa na nchi ambazo zimeanza kusitawi karibuni. Walakini sikuzote uhakika wao umetegemea ufalme unaokuja wa Mungu. Huo ndio umekuwa lengo lao, liwe litafikiwa kwa kuokoka na kuipita ile “dhiki kubwa’ au kwa kufufuliwa. Linapasa kuwa lengo la kila mmoja wetu sasa!—Ufu. 21:1-4 NW.

6. Ni mfano gani kutoka Afrika ulio kitia-moyo kwa waangalizi wajitumikishe pasipo woga?

6 Angalia kwa mfano nchi ya Kiafrika ya Zimbabwe, ambayo kwa miaka mingi ilikuwa imegawanywa na magomvi ya nchini. Mashahidi wa Yehova walitokeza sana katika kutokuwamo kwao, na katika kuendelea kuhubiri Ufalme huo wakati wa kipindi hicho cha wakati wa jeuri. (Yohana 17:16) Sana-sana ilikuwa hatari sana kwa waangalizi wasafirio kuendelea kufanya ziara zao zenye kujenga kwa makundi. Walakini waliendelea. Walihatirisha sana maisha zao. Nyakati nyingine ndugu hao waaminifu walikamatwa walipokuwa wakisafiri kutoka kwa kundi moja kwenda kwa jingine. Walishtakiwa kwamba walikuwa wageni na wapelelezi katika eneo hilo, na maisha zao zilitiwa hatarini. Mwangalizi mmoja wa mzunguko aliuawa na mwili wake ukaachwa umelala kando ya baisikeli yake iwe onyo kwa watu wenye kupita. Hata hivyo, waangalizi wa mzunguko wengine waliendelea bila woga katika utumishi wao, mpaka nyakati zenye amani zaidi zilipoleta faraja kutokana na namna hiyo ya hatari. Ikiwa wakati wo wote tutakabiliwa na hali kama hizo, na tuwe wasioogopa jinsi iyo hiyo katika kuendelea na “utumishi mtakatifu” wetu kwa Mungu!—Luka 12:4-7; Rum. 12:1, 2, NW.

7. Ndugu zetu katika El Salvador wamebarikiwaje kwa kushika kwa uimara tumaini lao?

7 Leo, kuna mzozo kama huo huo katika El Salvador, ambapo magomvi ya nchini yamewaka kote kote katika nchi hiyo. Kwa mara nyingine, Mashahidi wa Yehova wameendelea kutokuwamo kabisa kuhusiana na jeuri. Hata hivyo, wengine wao wameuawa wakipitia mahali penye mtupiano wa risasi. Walakini wazee waaminifu wameendelea kutumikia makundi na vikundi vilivyo peke yake, wakivitia nguvu na kuvitia moyo. (Linganisha Isa. 32:1, 2.) Wengine wao wameponea kifo chupu-chupu, walakini wameazimia kuendelea na kazi yao ya kufundisha na kuchunga, hata zijapokuwa hatari zenye kuendelea kukabili maisha zao. (1 Pet. 5:1-4) Makundi yanafanya mikutano yao kabla ya saa wasizoruhusiwa watu kutembea nje, na Yehova amewabariki sana kwa kuwa na ongezeko la asilimia 22 katika wahubiri katika mwaka 1981. Wahubiri hao wa Ufalme 8,242 walikuwa wakiongoza mafunzo ya Biblia ya nyumbani 13,948 pamoja na watu wapya wenye kupendezwa wakati mwaka huo wa utumishi ulipokuwa ukikaribia mwisho wake. Mungu wetu anawabariki sana kama nini wale wote wanaoendelea kusonga mbele bila woga, wajapokuwa ‘hatarini kila saa’!

8, 9. (a)  Wengine katika nchi zenye utajiri wamepotoshwaje? (b) Tunapaswa kutendaje, na kwa sababu gani?

8 Hata hivyo, wengine katika nchi zenye utajiri zaidi na nchi zenye kuelekea kuwa “salama” wamepotoshwa wakaingia katika njia ya kiroho yenye hatari ya maisha. Wanafikiri kwamba wanaweza kuwa na uhusiano wa kirafiki na ulimwengu na kujifurahisha anasa kama Waipikureo, na wakati ule ule waweke mguu mmoja, kama ilivyo, katika tengenezo la Mungu. Huenda wakawa walivutiwa na mashirika yasiyo na hekima ya watu waasi, hivyo kuthamini kwao pendeleo lao la utumishi wa ufalme wa bidii kukapunguzwa. Ni ujinga kama nini! Paulo anawaambia hao moja kwa moja: “Msipotoshwe. Mashirika mabaya yanaharibu mazoea mema.” Mazoea yanayofaa ya kitheokrasi ya kuhudhuria mikutano na utumishi kwa Mungu mahali payo panachukuliwa kwa urahisi na kujiingiza sana katika anasa za ulimwengu uliopotoka. Njozi ya kuiona taratibu mpya ya Mungu inafifia, na pamoja nayo tumaini la ufufuo. Mambo kama hayo yalimpata Himenayo, Aleksanda na Fileto katika siku za Paulo. Na, inasikitisha kusema kwamba mambo hayo yanawapata wengine leo.​—1 Kor. 15:33, NW, 1 Tim. 1:18-20; 2 Tim. 2:15-19.

9 Ni aibu kwa ye yote katika wakati huu ulioendelea sana, kujiondosha mwenyewe kwa kutokuunga mkono kwa moyo wote tengenezo la Yehova na utumishi walo! Taratibu ya ulimwengu iliyopo inasukasuka kuelekea mwisho wayo. Ni kwa kusimama tu katika “habari njema,” kwa ‘kuzishika sana,’ ndipo ‘tunapookolewa pia.’ Ni jambo la lazima kwamba tuendelee na kuongeza maarifa juu ya Mungu. Kwa kufaa, Paulo anawaandikia wale walioshindwa kufanya hivyo, akisema hivi: “Amkeni mwe timamu katika njia yenye haki na msizoee dhambi, kwa maana wengine hawana maarifa juu ya Mungu. Ninasema ili niwasukume mwone aibu.”​—1 Kor. 15:1, 2, 34, NW.

“MWE IMARA”

10. (a) Paulo na jamii ya “mtumwa” wa kisasa wana maoni gani juu ya ‘ndugu wapendwa’? (b) Andiko la Mwaka letu la 1982 linafungamanaje na jambo hilo?

10 Paulo anamalizia hoja yake katika kuunga mkono tumaini la ufufuo lililo zuri sana kwa njia ya uchangamfu na ya kuvutia. “Kwa hiyo, ndugu zangu wapendwa,” ndivyo anavyosema. Yeye anataka ndugu zake wa kiroho wafikie mradi wao. Vivyo hivyo, leo, “mtumwa mwaminifu mwenye akili” anahangaishwa sana na hali ya kiroho ya wale mamilioni ulimwenguni pote wanaopendezwa na ufalme unaokuja wa Yehova. “Mtumwa” huyo anataka kuuona “mkutano mkubwa” wote ukistahili uzima katika makao ya kidunia ya ufalme huo. Wanafanya hivyo kwa ‘kuyasafisha mavazi yao’ na kumtumikia Mungu, ili ‘waipite ile dhiki iliyo kuu’ bila kukwaruzwa. (Mt. 24:45-47; Ufu. 7:9, 14) Mradi huo unaweza kufikiwaje? Ni kwa kushiriki kwa bidii katika kazi ya Bwana Yesu Kristo. Paulo anaonyesha hivyo, katika maneno haya, ambayo ndiyo yanakuwa Andiko la Mwaka la Mashahidi wa Yehova kwa mwaka 1982:

“Mwe imara, bila kuondoleka, sikuzote mwe na mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana.”​—1 Kor. 15:58, NW.

11. Ni nini maana ya ‘kuwa Imara’?

11 Sifa ya uthabiti ni ya lazima kwa wale wanaotaka kuingia katika taratibu mpya ya Yehova. Kuwa imara kunamaanisha kuwa wenye kudumu, imara, wasioyumba-yumba. Hiyo ndiyo namna ya imani tunayopaswa kuwa nayo, tazamio lililohakikishwa la mambo yasiyoonekana yaliyo mbele, lakini ambayo, kupitia, kwa kujifunza kwetu Maandiko, yamekuwa halisi kwetu, kama kwamba yapo kabisa​—Ebr. 11:1, NW.

12. Tuna sababu gani za kutoyumba-yumba katika utumishi wetu?

12 Tunajua kwamba ufalme wa Kimasihi umekaribia, ukiwa umekwisha kusimamishwa mbinguni katika mwaka 1914. Tumekwisha kuiona “ishara” ya “kuwapo” kwa Kristo katika utukufu wa Ufalme katika matukio yenye mchafuko duniani katika hizi “siku za mwisho.” Tumeuona uongozi wa kimalaika kwa watu wa Mungu wakati wanapohubiri kwa bidii ya kimisionari “katika dunia yote inayokaliwa na watu,” na kwa halisi mamilioni ya watu wakisikiliza “habari njema.” Mikazo kutoka ulimwengu wa Shetani itaongezeka bila shaka, walakini hiyo ni sababu ya kutufanya tuyumbe-yumbe katika “utumishi mtakatifu” wetu, utumishi wetu wenye thamani kwa Bwana Mwenye Enzi Kuu wa maisha zetu, Yehova Mungu? Bila shaka sivyo!—Mt. 24:3-14, NW; 25:31- 34, NW; Ufu. 7:15, NW; 14:6,7.

‘MWE . . . WASIOONDOLEKA’

13. Tunawezaje kujionyesha kuwa ‘wasioondoleka,’ kama Ayubu?

13 Paulo anatusihi sisi, pia, tuwe ‘wasioondoleka.’ Jambo hilo linapatana na kuwa thabiti. Linamaanisha kwamba, katika kuzishika amri za Mungu, hatupaswi kamwe kuondolewa katika ukamilifu wetu. Hiyo ndiyo iliyokuwa nia ya Ayubu aliyekuwa mfano mzuri wa kuendeleza ukamilifu ambaye alisema hivi juu ya Mungu wake na Hakimu: “Njia yake nimeishika, wala sikukengeuka. Sikurudi nyuma kuiacha amri ya midomo yake; nimeyatunza maneno ya kinywa chake zaidi ya riziki yangu.” (Ayubu 23:10-12) Ikiwa sisi, kama Ayubu, tutapita hata yale mambo yaliyopangiwa mikutano yetu ya kawaida, tuchimbe sana katika vitabu vya Sosaiti ili tupate maarifa zaidi juu ya matumizi ya kisasa ya Neno la Mungu, tutasaidiwa, hakika, katika kuendelea kuwa thabiti, wasioondoleka.

14. (a) Mnara wa Mlinzi umetoaje maarifa kwa watu wanyofu hatua kwa hatua, na matokeo yakawa nini? (b) Umevumisha onyo gani, na wengi wameitikiaje?

14 Kwa miaka zaidi ya 100 sasa, Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova umekuwa ukijenga, hatua kwa hatua, jumla ya kweli inayohusu ukombozi wa Yesu, tumaini la ufufuo na ufalme unaokuja wa Mungu wetu. Katika kurasa zake zote, umefanya Biblia iwe hai katika akili na mioyo ya mabilioni ya watu wanyofu. Umewasaidia hawa wafahamu makosa ambayo yamefundishwa na dini za Jumuiya ya Wakristo na kwa hakika milki yote ya ulimwenguni pote ya dini ya uongo​—“Babeli Mkuu.” Umekaza fikira kwenye anguko kuu la kiroho la “Babeli Mkuu” na umevumisha amri ya kiunabii ya malaika yule: “Tokeni kwake, enyi watu wangu, msishiriki dhambi zake, wala msipokee mapigo yake.” (Ufu. 17:1, 5, 15, 18; 18:2, 4) Wengi wamesaidiwa wafanye hivyo, na wamekuwa waungaji mkono washikamanifu wa ufalme wa Yehova wa Kimasihi.

15, 16. (a) Wengine wameshindwa kuthamini nini? (b) Ni nani yule “mtumwa” wa Mathayo 24:46? (c) Kuhusu “mtumwa” huyo, ni wakati gani na ni namna gani ilikuwa wazi kwamba Mungu alikuwa akitumia njia moja tu ya kugawanya kweli?

15 Hata hivyo, sikuzote kumekuwa wengine ambao, mahali pa kuendelea kuwa wasioondoleka katika kuunga mkono kwao kwa ushikamanifu Ufalme huo, wanataka kubebwa na mkondo warudi kwenye imani na njia za dini ya uongo. Wao hawathamini kwamba Bwana yao, Kristo Yesu, anatumia baraza ya watiwa mafuta ya wafuasi wake duniani wakiwa “mtumwa mwaminifu mwenye akili” katika kugawa chakula cha kiroho.​—Mt. 24:45-47.

16 Ilikuwa kwanza katika 1895 kwamba rafiki fulani wa Mnara wa Mlinzi wa Sayuni (Kiingereza) wakapendekeza kwamba gazeti hilo lihusianishwe na “mtumwa” huyo​—“mtumishi huyo.”(Mt. 24:46, Authorized Version) Adui walitokeza upinzani wenye jeuri kwa maoni hayo ya rafiki hao, hata kwamba Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) wa Oktoba 1, 1909, ukasema hivi:

“Rafiki zetu wanasisitiza kwamba Andiko hili linaonyesha kwamba katika mwisho wa kipindi cha wakati cha Injili Bwana angetumia si njia nyingi za kutawanya Kweli, bali njia moja. . . Wanashikilia kwamba wote walipokea maarifa yao ya Kweli ya Sasa moja kwa moja kutoka kwa vitabu vya Sosaiti, au kwa njia isiyo ya moja kwa moja kupitia kwa wale ambao wamepokea maarifa yao kupitia njia hiyo. Vivyo hivyo wao wana furaha kushirikiana wakiwa ‘watumishi wenzi’ pamoja na kazi ya Sosaiti, wakiamini kwamba kwa njia hiyo wanafuata maongozo ya Usimamizi wa kimungu, pamoja na maagizo ya Neno la Mungu.”

17. (a) Hapo kwanza, na sasa pia, ni kwa njia gani wengine wamejaribu kuivunjia kweli heshima? (b) Kwa sababu gani tunapaswa kufurahi kubaki tukiwa ‘wasioondoleka’ katika kushirikiana na “mtumwa” huyo?

17 Kisha, ukitaja juu ya adui hao wa ile kweli, Mnara wa Mlinzi ulisema hivi:

“Wanataka kugeuza akili za waliopewa maarifa kuelekea upande mwingine kwa kuwaambia kwamba ‘kila mmoja anapaswa kujilimia’ vito vya thamani vya Kweli ya Mungu; kwamba vitabu vya Sosaiti viliwapa tu mwanzo ambao sasa wanapaswa kuufanyia maendeleo, ili mwishowe mafundisho yayo yawe ya mbali kule-e-e nyuma. ‘Watumishi wenzi’ hao wasio washikamanifu wanaendelea kupendekeza kwamba kuna hatari ya kuiabudu Sosaiti na kwamba ili kuiepuka kwa lazima inafaa kuipiga teke au kuipa kisogo. Wao wanasema, Na tuwe na funzo la Biblia, bali tuviondolee mbali vitabu vya Sosaiti!”

Maneno hayo yaliandikwa miaka 73 iliyopita, na mpaka siku hii kuna wachache wanaojaribu kuvunjia heshima jumla ya kweli ambazo Yehova amejenga hatua kwa hatua, akitumia njia yake moja tu. Kwa kadiri mwanga wa kweli unavyozidi kuwa mwangavu zaidi, tunapaswa kuwa wenye furaha kama nini kuendelea kuwa ‘wasioondoleka’ katika kushirikiana na “mtumwa mwaminifu”!—Kol. 1:21-23.

“SIKUZOTE MWE NA MENGI YA KUFANYA KATIKA KAZI YA BWANA”

18. (a) Ni nini ufunguo wa kuendelea kuwa wenye afya ya kiroho, na Mithali inaonyeshaje jambo hilo? (b) Ni nini baadhi ya sehemu za kuwa “na mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana”?

18 Ndiyo, kuwa na “mengi ya kufanya,” si kwa mtu kufanya jambo lake mwenyewe, bali katika kazi ya Bwana Yesu Kristo. Hapo ndipo ufunguo wa kuendelea kuwa na afya ya kiroho ulipo. Uvivu wa kiroho unaweza kutokeza mashaka. Unaweza kuwa hatari, kama inavyoonyeshwa na Mithali 19:15: “Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito; na nafsi yake mvivu itaona njaa.” Kwa habari ya uvivu wa kiroho wenye kuendelea, kufa njaa kiroho na mauti ndiyo matokeo. Basi, na tujishughulishe sana kuhubiri kwa ukawaida nyumba kwa nyumba (hata katika maeneo yasiyo na itikio), tukitoa ushuhuda wa vivi hivi katika kila nafasi, tukifanya ziara za kurudia kwa watu wenye mfano wa kondoo na kuongoza mafunzo ya Biblia ya nyumbani kwa ukawaida pamoja nao kwa kutumia kimoja-wapo cha vichapo vya Sosaiti. Wengine wetu huenda tukaweza kutumikia tukiwa “mapainia,” au watangazaji wa Ufalme wa wakati wote, katika hii kazi ya Bwana Yesu, ambaye, kwa hakika, ni “painia” wa imani yetu.​—Ebr. 12:2, Moffatt; Isa. 6:8-10.

19. Sisi sote twaweza kuonyesha roho gani, walakini wengine wanawezaje kuwa na sehemu kubwa zaidi ya kushiriki katika kazi hiyo?

19 Tuwe tumejiandikisha kama mapainia au la, wote tunaweza kufanya “utumishi mtakatifu” kwa furaha, kwa roho ya painia ya kweli. Jambo hilo huenda likaelekeza wengine wetu tufanye “upainia msaidizi” wakati kwa wakati, na ikiwa furaha inayoletwa na jambo hilo inaweza kutia wengine wetu moyo wawe mapainia wa kawaida, sehemu yetu ya kushiriki itakuwa kubwa zaidi namna gani katika “kazi ya Bwana”!—Rum. 12:1, 2, NW.

20. (a) Tumependelewa kuwa wafanya kazi wenzi pamoja na nani? (b) Twapaswa kujikaza kufikia mradi huo tukiwa na uhakikisho gani? (c) Mwisho, ni maneno gani ya Paulo tunayopaswa kutaka kufanya yatuhusu, na kwa sababu gani?

20 Kazi hii ya Bwana Yesu, kufuata hatua zake, vilevile ndiyo “kazi ya Yehova.” (1 Kor. 16:10, NW; Yohana 5:17) Sisi tu wenye pendeleo kama nini kuwa wafanya kazi wenzi pamoja na Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, Bwana Yesu Kristo na malaika wa kimbinguni kwenye “umalizio wa taratibu ya mambo”! (1 Kor. 3:9; Mt. 25:31-33; 28:19, 20, NW) Kwa maana tunajua kwamba kazi yetu “si ya bure kuhusiana na Bwana.” Tuwe tutaingia katika Taratibu Mpya kwa kufuliwa au kwa kuokoka kuipita “ile dhiki iliyo kuu,” na tuweze kusema, kwa maneno ya mtume Paulo mwaminifu katika 1 Wakorintho 15:57: “Shukrani zimwendee Mungu, kwa maana anatupa ushindi kupitia Bwana yetu Yesu Kristo!” Ndiyo kushinda kifo, na kuelekea baraka nzuri sana za uzima wa milele!​—Kutoka The Watchtower, December 15, 1981.

Je! unathamini mambo haya makuu?

◼ Kwa sababu gani wakati wote inafaa kuwa na tumaini la ufufuo likiwa hai kabisa

◼ Kitia-moyo ambacho tumaini la ufufuo linawapa ndugu zetu wanaolazimika kukabili kifo kila siku

◼ Kwa sababu gani wale wanaoshirikiana na wenye mashaka au wenye kufikiria ukafiri wanapaswa ‘kuaibika’

◼ Kwa sababu gani sifa ya uimara ni ya lazima ili kuingia katika taratibu mpya ya Yehova

◼ Usemi uliotolewa juu ya “njia moja” katika “Mnara wa Mlinzi’’ miaka zaidi ya 70 iliyopita ni wa maana namna gani?

◼ Namna kupainia au kuwa “na mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana” kunavyoweza kuwa ulinzi kwetu

[Picha katika ukurasa wa 20]

Waangalizi wengine wasioogopa wanatumikia “hatarini kila saa”

[Picha katika ukurasa wa 21]

Mazoea mazuri ya kuhudhuria mkutano na utumishi wa shambani yanatusaidia tuendelee kuwa wenye bidii kwa ajili ya ufalme wa Mungu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki