Moyo Wao Umo Ndani
Kila mwaka makumi ya maelfu wasioweza kuwa mapainia wa kawaida wanajiandikisha kuwa mapainia wasaidizi kwa mwezi mmoja au zaidi ili wawe na sehemu kubwa zaidi katika kushiriki na jirani zao habari njema za Ufalme. Wengi wanapanga kuufanya mwaka huu. Namna gani wewe?
Wote wanaoufanya wanakubali kwamba, ‘Inahitaji mpango wa uangalifu na orodha inayofaa.’ Wengi wao wangali wanahudhuria shule, lakini orodha yao ya shule iko hivi, wakiamka mapema na kutumia wakati wao vizuri, vilevile wanaweza kutumia saa mbili kila siku kwenye utumishi wa shambani. Maelfu ya Mashahidi wachanga Wanapata furaha nyingi katika kutumia vipindi vya likizo kwa ajili ya utumishi huo.
Alipoulizwa ni kwa sababu gani alitia jitihada hiyo ya ziada ili afanye upainia msaidizi, Shahidi mmoja alisema hivi: “Hiyo ndiyo njia yangu ya kusema, ‘Asante, Yehova, kwa ajili ya mambo yote ambayo umenifanyia.’”