Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 5/1 kur. 19-23
  • Gospeli (Injili) ya Yohana Inapasa Kuwa na Matokeo Gani Kwako?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Gospeli (Injili) ya Yohana Inapasa Kuwa na Matokeo Gani Kwako?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Utangulizi Wenye Kufanyiwa Ubishani
  • Nuru Inakuwa na Matokeo Gani Juu Yetu?
  • Ni Uzima Wenye Ubora Gani Unaotolewa Tuupokee?
  • Ni Tumaini Gani kwa Watu?
  • Upendo wa Kristo Unakuwa na Matokeo Gani Juu Yako?
  • Kitabu Cha Biblia Namba 43—Yohana
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Fuata Nuru ya Ulimwengu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • “Nuru Imekuja Ulimwenguni”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Onyesha Upendo na Imani Sikuzote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 5/1 kur. 19-23

Gospeli (Injili) ya Yohana Inapasa Kuwa na Matokeo Gani Kwako?

KWA sababu gani zile Gospeli (Injili) nne za Kikristo ziliandikwa? Je! ziliandikwa ili tu ziwe kumbukumbu la kihistoria juu ya maisha ya Masihi? Au kulikuwa na kusudi kubwa zaidi? Amri ya mwisho ya Kristo ambayo aliwapa wanafunzi wake inatoa mwangaza juu ya maulizo hayo: “Kwa hiyo nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, . . . kuwafundisha kushika mambo yote ambayo nimewaamuru ninyi.”​—Mathayo 28:19, 20, NW.

Ni wazi kwamba ujumbe wa Kikristo ungepasa kusukuma watu ulimwenguni pote waige mfano wa Yesu. Kwa kweli ingewalazimu waamini kwamba Kristo ndiye Mwokozi. Hivyo mtume Yohana anasema aliandika hadithi ya maisha ya Yesu “ili mpate kuamini ya kwamba Yesu ndiye Kristo, Mwana wa Mungu; na kwa kuamini mwe na uzima kwa jina lake.”​—Yohana 20:31.

Utangulizi Wenye Kufanyiwa Ubishani

Ni mahali gani katika wakati ambapo Yohana anatujulisha sisi kwa Yesu? Je! ni kwenye wakati wa kuzaliwa kwake, kama vile wanavyofanya waandika-Gospeli Mathayo na Luka? Hapana. Kabla hajaandika jambo hilo anaeleza habari zilizotokea vizazi vingi mno mapema. Anatupeleka huko nyuma kwenye mwanzo wa uumbaji akitumia utangulizi wenye kueleweka vyepesi lakini wa kindani: “Katika mwanzo yule Neno alikuwako, na yule Neno alikuwa pamoja na Mungu, na yule Neno alikuwa mungu [alikuwa wa kimungu, Schonfield]. Huyu alikuwako katika mwanzo pamoja na Mungu. Vitu vyote vilikuja kuwako kupitia kwake, na bila kupitia kwake hata kitu kimoja hakikuja kuwako.”​—Yohana 1:1-3, NW.

Utangulizi huo unaweza kuwa mgumu kufahamiwa na mtu asipokuwa kwanza na maarifa ya sehemu ile nyingine yote ya Biblia. Kwa mfano, kwenye Mithali 8:22-31 Neno (Kristo kabla hajaja kuwa mwanadamu) anatajwa kwa kufananishwa na hekima akiwa “stadi wa kazi” mwenye kushirikiana na Mungu katika kazi Yake ya kuumba. (Angalia pia 1 Wakorintho 1:24.) Mtume Paulo anathibitisha wazo hilo katika barua yake kwa Wakolosai, ambapo Kristo anatajwa kuwa “mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote. Kwa kuwa katika yeye vitu [vingine] vyote viliumbwa.” Kutokana na maneno hayo tunaweza kuona kwamba yule Neno ambaye “alifanyika mwili, akakaa kwetu” alikuwa ndiye uumbaji wa kwanza wa Mungu halafu akatumiwa na Baba yake kutimiza kazi nyingine yote ya kuumba.​—Wakolosai 1:15, 16; Yohana 1:14.

Maarifa ya kujua hivyo yanapasa yawe na matokeo gani juu yetu? Je! haitupasi kuwa wenye shukrani kwa Yehova, Muumba, kwa sababu ya uhai wenyewe unaotuwezesha kuwako? Na je! hatulithamini lile daraka ambalo yule Neno ametimiza katika jambo hilo? Mungu alimpa mwanamume na mwanamke nguvu za uzazi ambazo zimetokeza jamaa ya sasa ya kibinadamu ya watu zaidi ya bilioni nne. Walakini, kuna sababu nyingine nyingi za kumpa Mungu na Mwanaye shukrani nazo zinahusiana na vile vichwa vikuu vya Gospeli ya Yohana​—nuru, uzima, upendo na ushikamanifu.

Nuru Inakuwa na Matokeo Gani Juu Yetu?

Katika mstari wa tatu na wa nne wa sura ya kwanza ya Gospeli yake, Yohana anatuingiza katika viwili vya vichwa vile vikuu vinavyounganishwa-unganishwa pamoja na kujumlika kuwa masimulizi yake yaliyoongozwa na Mungu, kwa kusema: “Kile ambacho kimekuja kuwako kupitia yeye [Neno] kilikuwa uzima, na ule uzima ulikuwa nuru ya wanadamu.” (NW) Yohana anatupasha habari gani kwa kusema hivyo? Aneleza kwamba Neno, au Kristo, alikuwa ndiye Wakili Mkuu wa Mungu wa kuwapokeza wanadamu uzima na nuru pia. (Matendo 3:15) Yohana anaendelea kutuambia kwamba Yohana Mbatizaji aliinuka atoe ushuhuda juu ya “nuru ya kweli ipayo nuru kwa kila namna ya mwanadamu.” (Yohana 1:9, NW) Ndiyo, kwa kila namna ya mwanadamu, kwa sababu Kristo hakuingia ulimwenguni awe Masihi kwa ajili ya Wayahudi peke yao. Alikuja kufaidi wanadamu wote, kama vile yeye mwenyewe alivyoeleza: “Mungu aliupenda ulimwengu [wa wanadamu tangu Habili], hata akamtoa Mwanawe pekee [Kristo, yule Neno] ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.”​—Yohana 3:16.

Basi, andiko hilo ambalo hutajwa mara nyingine linapasa kuwa na matokeo gani juu yetu? Ikiwa Mungu alituma Mwanaye duniani atende kama nuru katika giza la kiroho la ulimwengu, je! haitupasi angalau kuangazia wengine nuru hiyo? Mwendo wa Mungu usio na uchoyo unapasa uguse mioyo yetu itake kusaidia watu. Ni nani kati yetu angekuwa na nia ya kumtoa kipenzi wetu tumpendaye zaidi, awe dhabihu katika kifo cha aibu kwa ajili ya watu wasiojali hasa? Basi upendo wa Mungu unapasa utusukume kufanya nini? Kuonyesha imani yenye bidii katika Yesu Kristo na katika ubora wenye kukomboa uhai wa dhabihu yake. Matokeo yatakuwa kupata uzima, kwa maana Yesu alisema: “Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.”​—Yohana 8:12.

Ni Uzima Wenye Ubora Gani Unaotolewa Tuupokee?

Bila kujifanya ati ana maarifa ya kindani ya kanuni za kisayansi, Yohana anataja kanuni moja, yaani, kwamba uzima wa kidunia unategemea nuru. Na katika maana ya mfano ndivyo ilivyo kabisa. Kristo ndiye nuru inayoongoza watu kwenye uzima. Lakini ni uzima wa namna gani? Jibu la Yesu kwa mwanamke Msamaria aliyekuwa kwenye kisima cha Yakobo linatudokezea: “Ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.” (Yohana 4:7-15) Kristo aliutoa “uzima ulio kweli kweli,” uzima wa milele pamoja na baraka ya Mungu.​—1 Timotheo 6:19.

Uzima wa milele huo ungefurahiwa wapi? Kwa ile hesabu iliyo ndogo kwa kulinganishwa, ambayo inakuwa “kundi dogo,” Yesu anajibu hivi: “Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali.” Ni wazi kwamba alikuwa akimaanisha makao ya kimbingu.​—Luka 12:32; Yohana 14:2.

Lakini Kristo alisema hivi pia: “Na kondoo wengine ninao, ambao si wa zizi hili; na hao nao imenipasa kuwaleta; na sauti yangu wataisikia; kisha kutakuwako kundi moja na mchungaji mmoja.” Yohana alijua kutokana na kitabu chake cha Ufunuo alichokuwa ametangulia kukiandika kwamba “kundi dogo” lingekuwa na washiriki 144,000, hali “kondoo wengine” wangekuwa ndani ya hesabu yao na “mkutano mkubwa” na raia wengine wa kidunia chini ya utawala wa Ufalme wa Kristo.​—Yohana 10:16; Ufunuo 7:4, 9, 10.

Sasa, taraja hilo la uzima wa milele, ama mbinguni ama duniani, linapasa kuwa na matokeo gani juu yetu? Ni jambo jepesi sana kusema “uzima wa milele,” lakini kwa muda mfupi fikiria maana yenyewe hasa ya maneno hayo. Ni kuishi milele! Kufurahia uzima kwa ukamili wake wote ukiwa na baraka ya milele ya Mungu. Ni kuwa huru pasipo wasiwasi wa uzee au afya yako. Lile ulizo la “Wewe una umri gani?” halitakuwa la kuhangaikiwa tena.

Kwa wale walio na mwito wa kimbingu, uzima wa milele utafurahiwa wakiwa sehemu ya serikali ya Kristo isiyoonekana, yenye kuelekeza mambo ya dunia na kutumia ubora wa dhabihu yake ili wanadamu watiifu wapate faida za kimwili na kiroho. Ni pendeleo kubwa kama nini! Bila shaka hata moja Gospeli ya Yohana inapasa itusukume tuthamini fadhili zisizostahilika za Yehova.​—Ufunuo 20:4-6.

Ni Tumaini Gani kwa Watu?

Sasa ulizo jingine linatokea kuhusu karama ya uzima wa milele. Wafu watapokeaje uzima huo ulioahidiwa? Yesu alijibu ulizo hilo kwa njia yenye kusadikisha kwa kufufua kihalisi watu mbalimbali, kutia na Lazaro rafiki yake mkubwa, aliyekuwa amekuwa mfu kwa siku nne. Masimulizi ya Yohana yasiyo na kifani yanatufahamisha kwamba Yesu alisema hivi wakati huo: “Mimi ndimi ule ufufuo na ule uzima. Yeye azoezaye imani katika mimi, hata ingawa afa, atakuja kwenye uzima.” Kichwa hicho kimekuzwa pia katika sura ya tano, ambapo Yesu anatangaza hivi: “Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake [Mwana wa Mungu]. Nao watatoka.”​—Yohana 11:1-44, NW; 5:25-29.

Ahadi hiyo ya ufufuo inakuwa na matokeo gani juu yako? Ebu fikiria wale ambao wamekuwa vipenzi vyako lakini sasa hawako hai. Je! usingesisimuka kuwaona tena na kuzungumza pamoja nao? Yehova Mungu ameahidi kutakuwa na mwujiza huo. Ndiyo sababu Martha, dada ya Lazaro mfu, alikuwa amelisadiki tumaini hilo hata kabla Yesu hajafufua ndugu yake kwenye uzima, kwa maana Martha alisema hivi: “Najua ya kuwa atafufuka katika ufufuo siku ya mwisho.” Je! sisi Wakristo tuna usadiki huo wenye nguvu?​—Yohana 11:24.

Upendo wa Kristo Unakuwa na Matokeo Gani Juu Yako?

Kama ingetupasa kuitaja Gospeli ya Yohana kwa neno moja tu, tungetumia neno jipi? Ni nuru, uzima au ni ufufuo? Hapana, tungetumia UPENDO. Kwa sababu gani? Kwa sababu baraka nyingine hizo zote zinatokana na upendo wa Mungu. Yesu aliutangaza upendo huo na akauonyesha. Hivyo alisema: “Kama vile Baba alivyonipenda mimi, nami nilivyowapenda ninyi, kaeni katika pendo langu. Mkizishika amri zangu, mtakaa katika pendo langu.” Amri ya Yesu yenye kutokeza zaidi ilikuwa nini? “Amri yangu ndiye hii, Mpendane, kama nilivyowapenda nyinyi. Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.”​—Yohana 15:9-14,

Je! Kristo mwenyewe aliyatimiza maneno hayo? Je! alidhihirisha upendo bora kupita upendo mwingineo wote kwa ajili ya rafiki zake? Maandishi ya Yohana yenye maelezo marefu yanajibu kwa mkazo Ndiyo! Masimulizi ya sura ya 18 na 19 yanaeleza namna Yesu alivyokamatwa kisha akawekwa katika wajibu wa kutoa majibu kwa mfululizo wa maulizo na vilevile akateswa sana mwilini na wakuu wa Kiyahudi na Kirumi. Muda wote wa kutendwa vibaya hivyo Yesu alitoa ushuhuda kuhusu ufalme wa Mungu. Alishuhudia hivi. “Ufalme wangu si sehemu ya ulimwengu huu . . . ufalme wangu si wa kutoka chanzo hiki.” Upendo wake kwa Baba yake na wanadamu ulikuwa wenye nguvu sana hata ukamzuia asitafute njia rahisi ya kuondoka katika magumu hayo au kujaribu kupunguza uzito wa ujumbe wake ili asipatwe na mateso. “Kwa ajili ya hili mimi nimezaliwa, . . . kwamba nitoe ushuhuda kwa ile kweli.” Akiwa ameduwaa, jambo la pekee ambalo Pilato aliweza kufanya ni kujibu: “Kweli ni nini?”​—Yohana 18:36-38, NW.

Baada ya kukaliwa na kundi kubwa la Wayahudi wenye kuongozwa na viongozi wa dini, Yesu alilaaniwa afe kisha akatundikwa juu ya mti wa mateso. Alipatwa na tendo la aibu zaidi ambalo Myahudi angeweza kutendwa, yaani, kufa akiwa mlaaniwa juu ya mti. (Kumbukumbu la Torati 21:22, 23; Wagalatia 3:10-13) Hata hivyo ushindi ukawa wake. Imani yake mwenyewe katika ufufuo iliondolewa lawama kwa kuonyeshwa kuwa ni ya kweli. Siku ya tatu alifufuliwa kwa wafu. Mariamu Magdalene, ambaye alikuwa mwanafunzi, alimwona na akasema naye. Ebu wazia mwanamke huyo alisisimuka namna gani alipoletea wanafunzi habari za kwamba: “Nimemwona Bwana”!—Yohana 20:18.

Basi, dhabihu ya Kristo na ufufuo ni mambo yanayopasa kuwa na matokeo gani juu yetu? Je! hayapasi kutujaza sisi pia usadiki, tumaini na shauku? Tunaijua kweli juu ya Kristo, inayotegemea maandishi ya kihistoria ya zile Gospeli (Injili). Ni maandishi yenye kuonyesha upendo wa vitendo. Je! yatatuvuta moyo tuonyeshe upendo huo wa Kikristo unaopita mambo mengine na kutolea wengine ujumbe wa Ufalme?​—Yohana 20:31; Mathayo 24:14.

Mwisho, katika kurudia kuchunguza masimulizi ya Yohana, ni somo gani zaidi tunaloweza kupata? Ni somo la ushikamanifu​—ushikamanifu wa Kristo kwa kusudi la Baba yake; ushikamanifu wake kwa wafuasi wake wajapokuwa walimwacha wakatoroka. (Marko 14:50; Yohana 18:15-27) Hapo kwanza, wale mitume 12 pia walikuwa wameonyesha ushikamanifu. Baadaye wakati wanafunzi wengi walipomwacha Yesu, jibu la Petro kwa ulizo la Yesu lenye kugonga mioyo lilikuwa la kuvuta namna gani: “Je! ninyi nanyi mwataka kuondoka?” Simoni Petro alimjibu hivi: “Bwana! Twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele. Nasi tumesadiki, tena tumejua, ya kuwa wewe ndiwe Mtakatifu wa Mungu.”​—Yohana 6:66-69,

Je! wewe unaamini kwamba Yesu ndiye “Mtakatifu wa Mungu,” “Mwana wa Mungu”? Ikiwa ndivyo, basi wewe pia unaweza kutembea katika nuru inayoongoza kwenye uzima. Wewe, pia, unaweza kudhihirisha upendo na ushikamanifu kwa Yehova Mungu na ufalme wake ulio mikononi mwa Kristo. Wewe, pia, unaweza kufaidiwa na Gospeli ya Yohana yenye kusisimua nafsi.​—Yohana 20:31.

[Picha katika ukurasa wa 20]

Yesu anatoa maji yapayo uzima wa milele

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki