Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w82 12/15 uku. 19
  • Maoni ya Hekima Juu ya Elimu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maoni ya Hekima Juu ya Elimu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Mtoto Wako Aende Shule ya Bweni?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Elimu—Gharama Yake? Faida Yake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Wazazi, Mnataka Watoto Wenu Wawe na Maisha ya Aina Gani Wakati Ujao?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Mapainia Hutoa na Kupokea Baraka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
w82 12/15 uku. 19

Maoni ya Hekima Juu ya Elimu

BIBLIA huwashauri wazazi kuwalea watoto wao katika “nidhamu na rekebisho la akilini la Yehova.” (Waefeso 6:4, NW) Mazoezi hayo ni ya maana zaidi ya elimu ya kidunia.

Baba mmoja wa Nigeria anakubaliana na hilo. Yeye anasema: “Kwa ukawaida nilizungumza mambo ya kiroho, kutia andiko la siku, pamoja na watoto wangu. Nilitaka kuwasaidia wampende Yehova na kutii mashauri yake. Vilevile nilitaka kuwapa imani yenye nguvu.

“Nilikuwa najua uvutano usio wa Kikristo waliokabili shuleni. Kwa hiyo sikuwaingiza katika shule za bweni (za kulala). Nilitaka warudi nyumbani kila siku ili niendelee kuwazoeza kulingana na Maandiko. Nakumbuka kwamba, baada ya shule siku moja, binti yangu aliniambia mwanamume mmoja tajiri alikuwa amemwalika amtembelee. Nilienda kumtembelea mwanamume huyo nikakuta kwamba alikuwa na kusudi la kufanya uasherati pamoja naye. Nilifurahi binti yangu hakuwa katika shule ya bweni, ambako singeweza kumpa uongozi wangu.

“Vilevile niliwawekea watoto upainia [kuhubiri kwa wakati wote] uwe mradi wao, na watatu kati yao walijiandikisha wawe mapainia mara tu walipoondoka shuleni. Mikaeli alipokuwa shuleni, alionyesha tamaa ya kuwa mtaalamu wa dawa kama mimi. Nilimwambia alikuwa anafikiria kazi nzuri, lakini kwamba ikiwa angekwenda kwa masomo ya chuo kikuu, kungekuwa na hatari ya kumezwa na taratibu ya kilimwengu. Mjue, nilikuwa nimeona kwamba wengi waliofuzu (waliohitimu) walikuwa wamesitawisha tabia nyingi mbaya. Baadhi yao walikuwa wenye kiburi wakaacha kumthamini Mungu na utumishi wake.

“Kwa wazi Mikaeli aliyafikiria mambo hayo kwa uzito kwa sababu, miaka michache baadaye, yeye alikataa nafasi za kuhudhuria chuo kikuu na, mahali pake, akajiandikisha awe painia. Yeye na mkewe, Eunike, ambaye pia alianza kupainia mara tu alipomaliza shule, sasa wanatumikia katika Betheli [afisi ya tawi ya Sosaiti] katika Lagos.”

Kijana aitwaye Christian, pia, alifunzwa kweli na wazazi wake na uvutano wa wazazi wa mamaye waliokuwa mapainia ulikuwa wenye nguvu sana juu yake. Alipomaliza masomo ya shule ya juu, yeye mwenyewe alipainia kwa miezi kadha na akaonyesha tamaa ya kufanya upainia uwe kazi yake ya maisha.

Hata hivyo, babaye alidhani kwamba lilikuwa jambo la maana kwake apate elimu ya chuo kikuu ili kuhakikisha angekuwa na wakati ujao salama. Kwa hiyo akasisitiza kwamba huyo kijana Christian ajiandikishe katika mtaala wa chuo kikuu wa miaka mitano.

Christian angefanya nini? Dhamiri yake ilimwongoza amtii babaye, kama Biblia inavyoamuru. (Waefeso 6:1) Lakini yeye alichukua hatua za kulinda hali yake ya kiroho wakati ambapo angekuwa kwenye chuo kikuu. Kwa kweli, alipopata kwamba mtaala wake haukuwa ukichukua wakati mwingi sana, yeye alijiandikisha awe painia.

Hapo kwanza baba yake alipinga hilo, lakini hatimaye akaacha. Kijana Christian aliyajumulisha maono yake kwa maneno haya aliyomwambia babake: “Ninathamini sana yote ambayo umenifanyia nami nataka kukutii. Ndiyo sababu nilikubali kwenda chuo kikuu, nami nakusudia kutimiza mwafaka huo. Hata hivyo, mimi nimejiweka wakf kwa Yehova, ndiyo kusema lazima niweke faida zake kwanza. Nasadiki kwamba upainia ni njia moja bora ya kufanya hivyo.”—Mathayo 6:33; Mhubiri 12:1.

Katika visa vyote viwili vilivyotangulia kutajwa, vijana hao walibarikiwa. Lakini Wakristo kwa ujumla wanapaswa kuionaje elimu? Soma makala yetu ifuatayo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki