Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 3/1 kur. 8-13
  • “Endeleeni Kama Wanaume”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Endeleeni Kama Wanaume”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Yule Mwanamume Ambaye Tunapaswa Kuendelea Kama Yeye
  • Wakati Watu Waliokufa Watakapoishi Tena!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Yesu Kristo—Alitumwa na Mungu?
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Kwa Nini Tumpende Yesu?
    Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu
  • Kuifungua Njia ya Kurudi ya Kwenye Paradiso
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 3/1 kur. 8-13

“Endeleeni Kama Wanaume”

“Mwendelee kukesha, msimame imara katika imani, endeleeni kama wanaume, iweni wenye nguvu.”​—1 Wakorintho 16:13, NW.

1. Kwa kutumia maneno “Tazama, mtu huyu!” Pilato alikuwa akimmaanisha Yesu kuwa nini?

“TAZAMA, MTU HUYU!” Kwa maneno hayo yanayojulikana sana katika historia, gavana Mrumi Pontio Pilato alimleta mbele ya kundi kubwa la Wayahudi wakatili waliokusanyika mbele ya jumba lake la utawala katika Yerusalemu yule mtu mwenye sifa kubwa zaidi katika historia ya kibinadamu. Huyo alikuwa yule Myahudi mwenye kuitwa Yesu Kristo, ambaye wakati huo alivikwa vazi la rangi ya zambarau yenye kuonyesha hali ya kifalme, na taji ya miiba juu ya kichwa chake. Alivikwa namna hiyo ili kumfanyia dhihaka kwa sababu alidai ndiye Mfalme wa Kimasihi aliyeahidiwa. (Yohana 19:5-15) Walakini, kwa kutumia maneno “Tazama, mtu huyu!” Pilato alikuwa akimtaja Yesu kuwa mtu aliye mashuhuri zaidi kati ya wanadamu wote, mtu asiyestahili kukataliwa.

2. Ni kupitia mtu gani wanadamu waliokufa watafufuliwa kwa wafu, na juu ya msingi wa toleo gani?

2 Mtume Paulo alimtaja mwanamume huyu, aliyekuwa mlinganifu wa mwanamume Adamu mwenye ukamilifu wakati wa siku ya kuumbwa kwake, alipoandika maneno yanayofuata katika 1 Wakorintho 15:21, NW: “Kwa kuwa kifo ni kupitia mtu mmoja [yule anʹthro·pos Adamu], ufufuo wa wafu pia ni kupitia mtu mmoja [yule anʹthro·pos Yesu Kristo].” Mtume Paulo alikuwa akimaanisha mwanamume uyo huyo aliponena na washiriki wa mahakama ya Athene juu ya Areopago, au Kilima Marsi, na kusema: “Kweli, Mungu amejifanya hakutazama zile nyakati za ujinga wa namna hiyo, lakini sasa yeye anaambia watu [kwa halisi, walio wanaume] kwamba wao wanapaswa wote kila mahali kutubu. Kwa sababu yeye ameweka siku moja ambayo katika hiyo yeye anakusudia kuhukumu dunia inayokaliwa na watu katika uadilifu kwa mwanamume ambaye yeye ameweka, na yeye ametoa uhakikisho kamili kwa watu wote kwa sababu yeye amefufua huyo kutoka kwa wafu.” (Matendo 17:30, 31, NW) Kwa kutoa uhai wake mkamilifu wa kibinadamu uwe dhabihu kwa ajili ya wanadamu wote, huyu Yesu aliyefufuliwa angeweza kutolea wanadamu wote ukombozi hata wanadamu wafu waweze kufufuliwa na kupata nafasi ya kuwa na uzima wa milele juu ya dunia ya paradiso chini ya ufalme wake wa mileani (miaka elfu).

3. Ni toleo la nani la ukombozi unaolingana lililopasa kutolewa ushuhuda katika wakati barabara, na kwa sababu gani sasa ndio wakati unaofaa zaidi wa kutoa ushuhuda huo?

3 Kwa kupatana na uhakika huo wenye kufurahisha, mtume Paulo alimwandikia Timotheo mfanya kazi mwenzake akasema: “Kwa maana kuna Mungu mmoja, na mpatanishi mmoja kati ya Mungu na watu, mtu Kristo Yesu, ambaye alijitoa mwenyewe kuwa ukombozi unaolingana kwa ajili ya wote​—hili ndilo linalopaswa kushuhudiwa kwa nyakati zake zenyewe.” (1 Timotheo 2:5, 6, NW) Na sasa, leo, wakati wa kuwapo kwake akiwa Mfalme mwenye kutawala aliyekalia kiti chake cha kimbingu kwenye mkono wa kuume wa Mungu, ni wakati unaofaa zaidi jamii yote ya kibinadamu ipewe ushuhuda huo.

4. Wakati Pilato alipomtokeza Yesu mbele ya lile kundi la watu, ni kwa njia gani sura yake ilitofautiana na ile ya siku aliyopanda punda kuingia Yerusalemu, na wa sababu gani Pilato alishangaa sana?

4 Walakini, sasa tukiirudia ile Siku ya Kupitwa yenye kustahili kukumbukwa ya mwaka wa 33 WK, wakati gavana Mrumi wa Yudea, Pontio Pilato, alipomtokeza Yesu baada ya kupigwa mijeledi na kuaibishwa sana, akawa mbele ya kundi hilo lenye makusudi maovu, mbele ya jumba lake la utawala na kupaza sauti akisema: “Tazama, mtu huyu!” hakika hapo Yesu alikuwa tamasha kubwa! Sasa alikuwa katika sura tofauti sana na namna alivyokuwa mapema katika juma iyo hiyo. Huo ni wakati alipojiendesha kwa ushindi akiwa amepanda punda kuingia Yerusalemu akiwa mfalme-mchaguliwa. Alikuwa akienda akasherehekewe kuwa mfalme katika mji mkuu. Huo ulikuwa utimizo mdogo wa unabii wa Zekaria 9:9, tunaposoma hivi: “Furahi sana, Ee binti Sayuni; piga kelele, Ee binti Yerusalemu; tazama, mfalme wako anakuja kwako; ni mwenye haki, naye ana wokovu. Ni mnyenyekevu, amepanda punda, naam, mwana-punda, mtoto wa punda.” (Mathayo 21:1-9; Yohana 12:12-16) Baadaye, siku ya Kupitwa, Yesu alilazimika kuonyesha kistadi sana sifa za kiume, kuvumilia dhuluma yote na matendo mabaya aliyotendwa bila kulalamika, kwa kunyenyekea kabisa mapenzi ya Mungu Aliye Juu Zaidi, Baba yake wa kimbingu! Hiyo ndiyo sababu Gavana Pilato alishindwa na jambo jingine la kufanya isipokuwa kushangazwa sana na hali ya kiume iliyo imara kabisa ya Myahudi huyu ambaye macho ya ulimwengu mzima yalimwelekea.

5, 6. (a) Kwa sababu gani wanaopenda wakapate uzima katika paradiso wanastahili kuiga mfano mkamilifu wa Yesu Kristo katika mwendo wao? (b) Kulingana na maelezo ya Paulo, miendo ya Adamu na Yesu Kristo ilikuwaje na matokeo tofauti-tofauti juu ya wanadamu?

5 Mtu huyo mwenye hali ya kiume ni mfano unaostahili kuigwa, unaostahili kukaziwa macho na watu wote wapendao kupata uzima katika ukamilifu wa kibinadamu juu ya dunia ya paradiso hivi karibuni. Yesu akiwa mtu mzima alikuwa mwanadamu mkamilifu kama yule mtu wa kwanza, Adamu, wakati Muumba wake alipomweka katika bustani ya Edeni. Lakini Yesu hakuuharibu mfano wa Mungu ambao akiwa katika huo aliwekwa duniani; yeye hakuumbua sura ya Mungu ya kibinadamu ambayo kulingana nayo alikuwa amelelewa akiwa mwanadamu. (Mwanzo 1:26, 27) Kwa hiyo, mwendo wa Adamu wa kutokutii na mwendo wa Yesu Kristo wa ushikamanifu na utii ni miendo miwili ambayo imeleta matokeo yenye kutofautiana sana juu ya wanadamu wote!

6 Mtume Paulo alilitaja jambo hilo kifupi, kwa kuliandikia kundi la Kikristo maneno haya katika ule mji wa Korintho wa watu wenye akili nyingi sana, huko Ugiriki: “Kwa maana sawa na vile katika Adamu wote wanakufa, hivyo pia katika yule Kristo wote watafanywa hai. Lakini kila mtu katika daraja lake mwenyewe: Kristo yule malimbuko, baada ya hapo wale walio wa Kristo wakati wa kuwapo kwake.” (1 Wakorintho 15:22, 23, NW) Kwa sababu hiyo Mungu hakumwacha Mwanaye mwaminifu katika hali ya kufa. Kulingana na ahadi yake mwenyewe isiyoweza kuvunjika, Mungu alimfufua kutoka kwa wafu siku ya tatu, akawa ndiye wa kwanza kuinuliwa kutoka kwa wafu na kupewa uzima wa milele. Kupitia ufufuo Mungu alirudisha Mwanaye mtiifu mahali alipokuwa pamoja naye hapo kwanza, katika mbingu zisizoweza kuonekana. Jambo hilo lilifanya iwe inawezekana kurudisha wafu wa kibinadamu kwenye uzima duniani, wakiwa na nafasi ya kuinuliwa pole kwa pole wafikie uzima mkamilifu wa kibinadamu juu ya dunia ya paradiso wakati wa utawala wa Yesu Kristo usioweza kuonekana utakaoisimamia milki yake ya kidunia kwa miaka elfu.

7. Kwa sababu gani Yesu Kristo si tena mwanadamu mkamilifu, lakini ataweza kuwarudishia nini wazao wa Adamu na Hawa?

7 “Kuwapo” kwake kusikoonekana, lakini kunakoweza kufahamika, akiwa Mfalme juu ya wanadamu waliokombolewa kutatimiza maajabu yatakayofanya watu wajue kunafanya kazi. Sasa Yesu Kristo amekuwa tena kiumbe cha kiroho, lakini sasa kifo hakiwezi kumgusa, amekuwa asiyeweza kufa. Mtume Paulo anaonyesha wazi jambo hili anapoendelea kuliambia hivi kundi la Korintho: “Ikiwa uko mwili wa asili, na wa roho pia uko. Ndivyo ilivyoandikwa, Mtu wa kwanza, Adamu, akawa nafsi iliyo hai; Adamu wa mwisho ni roho yenye kuhuisha.” (1 Wakorintho 15:44, 45; Mwanzo 1:26, 27; 2:7) Kwa kuwa yeye si tena kiumbe wa kibinadamu mwenye nyama na damu, bali sasa amekuwa roho hodari kwa nguvu mbinguni, Yesu Kristo ataweza kurudishia wazao wa Adamu na Hawa uzima, kwa sababu yeye aliutoa uhai wake mkamilifu wa kibinadamu akiwa mwanamume kwa ajili ya jamaa ya kibinadamu.

Yule Mwanamume Ambaye Tunapaswa Kuendelea Kama Yeye

8. Yesu Kristo ni mfano unaostahili kuigwa na watafutaji wa kitu gani, na ni juu ya msingi gani Paulo angeweza kuambia washiriki wa kundi katika Korintho wawe waigaji (wafuataji) wake?

8 Kwa kuwa Yesu Kristo alikuwa mfano mkamilifu alipokuwa akikaa duniani, anastahili kuigwa na wote leo wanaojaribu kupata uzima wa milele, wawe watakuwa washirika wenzake wa kimbingu katika ufalme au watakuwa wana na binti zake wakamilifu wa kibinadamu juu ya dunia ya paradiso. Kwa hiyo, kwa kufaa kabisa kabisa, mtume Paulo aliweza kuandikia wafuasi wa Kristo katika Korintho wa kale na kusema: “Msiwakoseshe Wayahudi wala Wayunani wala [kundi] la Mungu; vile vile kama mimi niwapendezavyo watu wote katika mambo yote, nisitake faida yangu mwenyewe, ila faida yao walio wengi, wapate kuokolewa. Mnifuate mimi kama mimi ninavyomfuata Kristo.”​—1 Wakorintho 10:32–11:1.

9. Katika 1 Wakorintho 16:13 (NW) neno la Kigiriki la kitendo lililotafsiriwa “endeleeni kama wanaume” limetolewa katika jina (noun) gani, na jina hilo linafanyiza tofauti gani?

9 Maneno hayo yanatusaidia tuwe na maoni yanayofaa juu ya kitia-moyo zaidi cha Paulo kinachopatikana katika maneno yake ya kumalizia aliyoliandikia kundi katika Korintho, Ugiriki: “Mwendelee kukesha, msimame imara katika imani, endeleeni kama wanaume, iweni wenye nguvu.” (1 Wakorintho 16:13, NW) Hapa neno moja la Kigiriki lililotafsiriwa “endeleeni kama wanaume” ni neno la kitendo lililotolewa katika jina an·erʹ lenye kuonyesha hali aliyo nayo mtu, yaani, kutokana na neno an·drosʹ. Jina (noun) hilo la Kigiriki linamaanisha mwanamume, mwanamume katika mwili, tofauti na mwanamke, mtu wa kike. Kwa mfano, Mathayo 14:21 (NW) inasema: “Hata hivyo wale wenye kula waliokuwa karibu wanaume elfu tano, bila kuhesabu wanawake na watoto wachanga.” (Angalia pia Mathayo 15:38; Marko 6:44; Yohana 6:10, NW.) Malalamiko yalifanywa katika Yerusalemu juu ya mtume Petro kwamba “alikuwa ameenda ndani ya nyumba ya watu ambao hawakuwa wametahiriwa na akawa amekula pamoja nao.” (Matendo 11:3, NW) Kwenye 1 Wakorintho 11:3 (NW) tunasoma hivi: “Kichwa cha kila mwanamume ni yule Kristo; halafu tena kichwa cha mwanamke ni yule mwanamume; halafu tena kichwa cha yule Kristo ni Mungu.”

10. Katika Matendo 17:31, ni jina gani la Kigiriki ambalo Paulo alitumia kuonyesha yule ambaye Mungu alikusudia kumtumia ahukumu dunia inayokaliwa na watu?

10 Mtume Paulo alisema maneno yanayofuata kuhusu Yesu Kristo, akiwaambia washiriki wa Mahakama ya Areopago katika Athene wa kale, Ugiriki: “Yeye [Mungu] ameweka siku moja ambayo katika hiyo yeye anakusudia kuhukumu dunia inayokaliwa na watu katika uadilifu kwa mwanamume [an·erʹ] ambaye yeye ameweka, na yeye ametoa uhakikisho kamili kwa watu [kigiriki, pa’sin] wote kwa sababu yeye amefufua huyo wa kiume kutoka kwa wafu.”​—Matendo 17:31, NW.

11. Katika Matendo 14:15, maandishi ya kwanza ya Kigiriki yanaonyeshaje tofauti kati ya mtu wa kiume na mwanadamu wa kawaida tu?

11 Katika Matendo 14:15 (NW) tunasoma kwamba Paulo na Barnaba walipiga kelele hivi: “Enyi wanaume [Kigiriki: an’dres], kwa nini ninyi mnafanya mambo haya? Sisi pia ni watu [Kigiriki: anʹthro·poi ] wenye udhaifu ule ule kama ninyi.” Hivyo tunaweza kuona namna maandishi ya Kigiriki yanavyoonyesha tofauti kati ya mtu wa kiume na mwingine aliye binadamu wa kawaida tu.

12. (a) Ni kwa njia gani akina dada katika kundi la Korintho walipaswa kuendelea “kama wanaume,” na hapo tafsiri nyingine za Kiingereza zinasema nini? (b) Ni mara ngapi neno la Kigiriki la kitendo, an·driʹzo, linatokea katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, lakini linatokea mara ngapi katika Septuagint Version ya Kigiriki?

12 Maneno ya Paulo kwenye 1 Wakorintho 16:13, NW, “endeleeni kama wanaume” (an·driʹzo), waliandikiwa washiriki wote wa kundi, akina dada na vilevile akina ndugu. Kwa hiyo hata akina dada walipaswa kutenda kwa njia ya kiume, yaani, kwa ushujaa wa Kikristo, kwa kumwiga Yesu Kristo, yule Kichwa cha kundi la Kikristo. Katika maandishi ya kwanza ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo neno la kitendo, an·driʹzo linatokea mara moja tu, yaani katika 1 Wakorintho 16:13, ambapo New World Translation inalitafsiri kuwa “endeleeni kama wanaume.” Authorized Version ya Mfalme James inasema hivi: “Mwenende kama wanaume.” The Living Bible inasema: “Tendeni kama wanaume.” New Testament in Modern English ya Phillip nayo inasema: “Ishini kama wanaume.” Walakini, katika maandishi ya kwanza ya Kigiriki ya Septuagint Version ya Kigiriki, neno la kitendo an·driʹzo linatokea mara 21.

13. Neno la Kigiriki la kitendo linatafsiriwa namna gani katika Kumbukumbu la Torati 31:6, 7, 23 kulingana na tafsiri ya Septuagint iliyofanywa na Charles Thomson?

13 Kwa mfano, katika Kumbukumbu la Torati 31:6, 7, 23 tunasoma maneno haya kama yalivyotafsiriwa na Charles Thomson: “Tendeni kiume kabisa, na mwe na nguvu; . . . Halafu Musa akaita Yoshua, akamwambia mbele ya Israeli wote, Uwe mwenye ushujaa, na mwenye nguvu; . . . Na Bwana akampa Yoshua agizo, akasema, Uwe mwenye ushujaa, na mwenye nguvu, kwa maana wewe utawaongoza watoto wa Israeli waje ndani ya ile nchi ambayo Bwana aliwaahidi kwa uzito, na yeye atakuwa pamoja na wewe.” (Angalia maneno yanayofanana na hayo katika chapa iliyochapishwa na S. Bagster na Wanaye wa London, Uingereza.)

14. Tafsiri ya Charles Thomson inafasirije neno la Kigiriki la kitendo katika Nahumu 2:1?

14 Katika ile mara ya mwisho ya zile mara 21 ambazo neno hilo la Kigiriki la kitendo linatokea katika Septuagint Version ya Kigiriki kwenye Nahumu 2:1, tunasoma hivi: “Ndani ya kuwapo kwako alikuja juu akihema mmoja ambaye anakombolewa kutoka kwenye kutaabishwa. Iangalie njia kwa tahadhari; tia nguvu viuno vyako; tenda kiume kabisa kwa nguvu zako zote.” (Angalia pia chapa ya Bagster ya Septuagint.)a

15. Kwa hiyo, kulingana na habari zilizotangulia, tafsiri nyingine za kisasa zinafasirije neno la Kigiriki la kitendo katika 1 Wakorntho 16:13 kwa njia ambayo ni wazi inaweza kutumiwa kwa wanawake hata wanaume?

15 Kulingana na tafsiri za “Septuagint za neno la Kigiriki la kitendo, an·driʹzo inaeleweka sababu iliyofanya tafsiri nyingine za kisasa za Biblia Takatifu zilifasiri neno hilo la Kigiriki la kitendo katika 1 Wakorintho 16:13 sawasawa na tafsiri za Septuagint Version (LXX) ya Kigiriki. Kwa mfano, The Revised Standard Version inasema: “Mwe wenye ushujaa.” Today’s English Version inasema: “Mwe na uthabiti wa moyo.” New International Version nayo inasema: “Mwe wanaume wa ushujaa.” Kisha The New English Bible inasema: “Mwe hodari kwa ushujaa.” The Jerusalem Bible inasema: “Mwe na ujasiri.” Katika maana hiyo neno la Kigiriki la kitendo lingetumika kwa wanawake Wakristo waliojiweka wakf na wakabatizwa na vilevile kwa wanaume Wakristo waliojiweka wakf na wakabatizwa na vile vile kwa wanaume Wakristo waliojiweka wakf na wakabatizwa. Kwa hiyo, ilifaa kabisa Paulo akatumia neno hilo la Kigiriki la kitendo katika 1 Wakorintho 16:13. Ndivyo ilivyo hata kama kwa njia ya kimwili kila mmoja wa wanawake ni “chombo dhaifu zaidi, huyo mwanamke.”​—1 Petro 3:7, NW.

16. Baada ya kuambia Wakristo waendelee kama wanaume, Paulo anaongeza maneno gani, na kitia-moyo hicho kinaweza kutimizwaje?

16 Mtume Paulo akiisha kuambia Wakristo waliojiweka wakf na wakabatizwa ‘waendelee kama wanaume’ anaongeza maneno haya: “Iweni wenye nguvu.” Kupatana na hilo, Paulo aliandika hivi, kwenye Waefeso 6:10: “Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake.” Yehova Mungu Mwenye Nguvu Zote anaweza kututia nguvu ‘tuwe na nguvu,’ ndiyo, tutende mambo makuu katika utumishi mtakatifu wake. (Danieli 11:32) Yeye amevika watu wake waliojiweka wakf na wakabatizwa fahari ya kuwa na utumishi bora zaidi unaoweza kufanywa na mtu duniani. Jambo hilo linapasa kuwachochea sana mabaki waliotiwa mafuta na wenzi wao wenye mfano wa kondoo wafanye kama vile Paulo anavyotutia moyo, “Endeleeni kama wanaume.”

17. Ni kwa njia gani mabaki waliotiwa mafuta wa leo wana pendeleo lenye kuheshimika zaidi ya lile la Yohana Mbatizaji?

17 Letu leo ni pendeleo kubwa zaidi na lenye kuheshimika zaidi ya lile la Yohana Mbatizaji wa karne ya kwanza. Yeye alipewa heshima ya pendeleo la kuwa mtangulizi wa Yesu Kristo, yule ambaye angekuwa Mfalme, kwa utimizo wa unabii wa Malaki 3:1 kwa njia ya kufananisha au kwa kiasi kidogo. (Marko 1:1, 2) Alipokuwa akisema habari za huyu “mjumbe wa agano,” Yesu alisema hivi: “Amin, nawaambieni, Hajaondokea mtu katika wazao wa wanawake aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji; walakini aliye mdogo katika ufalme wa mbinguni ni mkuu kuliko yeye.” (Mathayo 11:7-11) Leo, tangu mwisho wa Vita ya Ulimwengu ya Kwanza katika mwaka wa 1918, mabaki ya warithi watiwa mafuta wa ule ufalme wa kimbingu wanatenda kama mabalozi, si wa serikali ya kifalme ya wakati ujao, bali wa ufalme wa juu mbinguni ambao ulisimamishwa ukaanza kazi yalipomalizika Majira ya Mataifa mwaka wa 1914, Yesu Kristo aliyetukuzwa akiwa amekalishwa katika kiti cha ufalme. Maneno aliyoyaandika mtume Paulo yanatumika kwao, lakini katika maana kubwa zaidi: “Kwa hiyo sisi tu mabalozi badala ya Kristo, kana kwamba Mungu alikuwa akisihi kupitia kwa sisi. Kama walio badala ya Kristo tunaomba: ‘Mpatanishwe na Mungu.’”​—2 Wakorintho 5:20, NW.

18. (a) Tangu mwaka wa 1935, ni akina nani wameitikia ombi la kupatanishwa na Mungu ambalo limetangazwa na mabaki ya ‘mabalozi walio badala ya Kristo’? (b) Ni akina nani wamejiunga na wanaume katika kuzihubiri habari za ufalme, na jambo hilo lilionyeshwaje katika Zaburi 68:11?

18 Tangu vita ya ulimwengu ya kwanza ilipomalizika mwaka wa 1918, na zaidi hasa tangu ule mwaka wa 1935 unaostahili kukumbukwa, kundi kubwa la watu wa mataifa yote limeitikia ombi hilo linalotolewa na mabaki waliotiwa mafuta wa warithi wa ufalme. Hawa wenye kuitikia wamezifuata zile hatua zinazoelezwa na Maandiko ili wapatanishwe na Mungu aliye Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo na sasa wao wako katika hali ya amani pamoja naye. Kwa sababu ya kuthamini jambo hilo wanatenda kama wenzi wa mabaki ya “mabalozi badala ya Kristo,” na basi wenzi hao wanaweza kuchukuliwa kuwa wajumbe walio badala ya Kristo’ katika kutolea watu wengine zaidi wenye mfano wa kondoo ombi la kupatanishwa pamoja na Mungu. Wao pia, wanawake kwa wanaume, wanaenda kiume na kishujaa kuzihubiri ‘habari njema hizi za ufalme katika dunia yote inayokaliwa na watu kwa ushuhuda.’ (Mathayo 24:14, NW; Ufunuo 7:9-17) Ni sawa na vile Zaburi 68:11 ilivyotabiri: “[Yehova] analitoa neno lake; wanawake watangazao habari [njema] ni jeshi kubwa.”

[Maelezo ya Chini]

a Ili uone mahali pengine-pengine ambapo neno la Kigiriki la kitendo, an·driʹzo, linapatikana katika LXX ya Kigiriki (maana yake “Septuagint” au “sabini”) angalia: Yoshua 1:6, 7, 9, 18; 10:25:2 Samweli 10:12 13:28; 1 Mambo ya Nyakati 19:13; 22:13; 28:20; 2 Mambo ya Nyakati 32:7; Zaburi 26:1427:14; 30:2531:24; Yeremia 2:25; 18:12; Danieli 10:19; Mika 4:10; linganisha mistari hii na maneno ya tafsiri za maandishi ya kwanza ya Kiebrania ya mistari hiyo, kwa mfano ulinganishe mistari hiyo na tafsiri za kisasa za Kiingereza zilizoonyeshwa juu. Kwenye Yeremia 2:25 tunasoma hivi: “Lakini huyo mwanamke akasema, Mimi nitatenda kama mmoja ambaye amefikia kukomaa [an·driʹzo]. Kwa sababu huyo mwanamke alipenda watu wa kigeni, basi nyuma yao alienda.”​—Charles Thomson.

Je! unaweza kujibu maulizo haya?

□ Kuletwa kwa Yesu na Pilato mbele ya kundi la watu kwa kutajwa kuwa “mtu huyu” kulimaanisha nini juu ya Yesu?

□ Sura ya kuonekana kwa Yesu wakati huu ilikuwaje tofauti na vile ilivyokuwa mapema wakati wa juma iyo hiyo?

□ Yesu aliwekea wafuasi wake wote mfano wa namna gani kwa tabia yake siku hiyo ya mwisho ya maisha yake ya kuwa hapa duniani?

□ Amri ya kimtume ya ‘kuendelea kama wanaume’ ilielekezwa kwa nani?

□ Ni kwa njia gani wanawake Wakristo wanapaswa kuendelea kama watu wa kiume?

[Picha katika ukurasa wa 9]

“Tazama, mtu huyu!”

Maneno hayo ya Pilato ya kumjulisha kwa watazamaji yalikuwa na maana gani?

[Picha katika ukurasa wa 12]

Wanawake wanapaswa ‘kuendelea kama wanaume’ kwa njia gani?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki