Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 3/1 uku. 23
  • Maswali kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Habari Zinazolingana
  • Kitabu Cha Biblia Namba 32—Yona
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Yona Ajifunza Juu ya Rehema ya Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Alijifunza Kutokana na Makosa Yake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Alijifunza Kutokana na Makosa Yake
    Igeni Imani Yao
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 3/1 uku. 23

Maswali kutoka kwa Wasomaji

◼ kwa sababu gani nyakati nyingine wasikilizaji wanakaribishwa wasimame kwa ajili ya wimbo na sala kwenye mikutano na makusanyiko ya Kikristo?

Wimbo na sala ni mambo ambayo kwa muda mrefu yamekuwa sehemu ya ibada ya kweli. (1 Mambo ya Nyakati 16:7-9; Mathayo 26:26-30; Yakobo 5:13, 14) Hivyo, ni mambo ya kawaida na ni sehemu ya maana ya ibada kwenye mikutano ya kundi au kwenye makusanyiko ya Mashahidi wa Yehova.

Nyimbo nyingi ziko katika namna ya sala au sifa zenye kuelekezwa kwa Mungu. Wakati watu wengi wanaposimama kwa umoja kwa ajili ya wimbo na sala, jambo hilo linaweza kuchukuliwa kwamba ni kuonyesha heshima kwa kuja mbele za Mungu wakiwa na shukrani.​—1 Wafalme 8:14, 22, 23.

Hata hivyo, inapasa kufahamiwa kwamba Biblia inaonyesha kusali au kuimbia Mungu sifa kunaweza kufanywa mtu akiwa katika hali ya kikao cho chote. (Linganisha Luka 22:39-41; Matendo 16:24, 25.) Kwa hiyo hakuna sheria katika habari hii. Ikiwa afya au hali za mtu zinafanya iwe vizuri zaidi awe ameketi wakati kundi linapoimba au sala inapotolewa, si kosa kufanya hivyo. Mara nyingi Wakristo wanakuwa wameketi wakati wa kusali kwenye Mafunzo ya Kitabu ya Kundi yaliyo madogo kuliko mikutano ile mingine. Wanafanya hivyo pia kwenye mafunzo ya nyumbani ya Biblia na nyakati za vyakula.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki