Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 9/15 kur. 4-6
  • Kufumbua Fumbo la Lile Jina Linalokosekana

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kufumbua Fumbo la Lile Jina Linalokosekana
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Jina Lenyewe Lilitumiwa Katika Nyakati za Kale?
  • Je! Mapokeo ya Kiyahudi Yameleta Badiliko Katika Biblia Yako?
  • Kusudi Limekuwa Ni Nini?
  • Jina la Mungu Katika Nyakati za Baadaye
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Jina la Mungu na Watafsiri wa Biblia
    Jina la Mungu Litakaloendelea Milele
  • Yehova
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Magumu ya Kujua Maana ya Jina la Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 9/15 kur. 4-6

Kufumbua Fumbo la Lile Jina Linalokosekana

WAKATI Musa kiongozi wa Waisraeli alipoanza kuandika historia ya wanadamu karibu miaka 3,500 iliyopita, lilikuwa jambo la kawaida akatumia lugha yake ya kienyeji ya Kiebrania. Historia hiyo imo katika vile vitabu 5 vya kwanza kati ya vile 39 vinavyofanyiza Maandiko ya Kiebrania, ambavyo pia vinajulikana sana kuwa Agano Jipya. Maandiko hayo yanatia ndani jina la Mungu lenye kumtofautisha karibu mara 7,000. Hilo ni jina gani? Jina lenyewe ni takatifu sana kiasi cha kwamba Muumba aliwapa Israeli amri inayohusu matumizi yalo, akisema: “Wewe hutatamka jina la Yahweh [Kiebrania: יְהוָה] Mungu wako kwa matumizi mabaya.” (Kutoka 20:7, The Jerusalem Bible) “Wewe hutalitumia jina la Yehova Mungu wako bila heshima ya kumcha.” (The Living Bible) Je! wewe unalitambua jina hilo “Yahweh” au “Yehova”? Au linasikika kwako kuwa geni?

Tafadhali angalia linalosemwa na amri hiyo. Je! Mungu alikataza matumizi au kutamkwa kwa jina lake? Hapana. Ni wazi kwamba alikataza matumizi mabaya ya jina hilo.

Liangalie andiko hilo​—Kutoka 20:7—katika nakala yako mwenyewe ya Biblia. Huenda ukashangaa ukifanya hivyo. Katika tafsiri zilizo nyingi andiko hilo linasema jambo kama hili: “Usilitaje bure jina la Bwana, Mungu wako.” (Union Version) “Wewe hutalichukua jina la Bwana Mungu wako kwa ubatili.”​—Revised Standard Version, ya mwaka wa 1952; Chapa ya Kikatoliki, ya mwaka wa 1957.

Je! wewe unaona jambo lo lote la kushangaza? Ndiyo, katika tafsiri nyingi za Biblia Jina la Kimungu limeondolewa! Jina lililo la maana kupita majina yote katika ulimwengu mzima wote limefutwa katika mamilioni ya nakala za tafsiri nyingi sana zilizo mashuhuri, za Jumuiya ya Wakristo na za dini ya Kiyahudi. Ajabu gani hiyo-o!

Je! sababu ingeweza kuwa ni kutokufahamu vizuri? Au ni jaribio lililofanywa mkusudi kumshushia; heshima Bwana Yehova Mwenye Enzi Kuu? Ikiwa sababu ni hii ya pili, huo ni udanganyifu mbaya kabisa, udanganyifu unaoharibu uhusiano wa mtu na Muumba wake.

Je! Jina Lenyewe Lilitumiwa Katika Nyakati za Kale?

Jina la Mungu limekuwa likitumiwa tangu mwanzo wenyewe wa historia ya mwanadamu. Tunaweza kuwaje na uhakika wa jambo hilo? Ni kwa sababu kumbukumbu la historia ya Biblia linatuamba hivi: “Ikawa Adamu alifanya ngono pamoja na Hawa mke wake na mwanamke akawa mwenye mimba. Baada ya muda mwanamke akazaa Kaini na kusema: ‘Mimi nimetokeza mwanamume kwa msaada wa Yehova.’” Katika Biblia ya The NIV Interlinear Hebrew-English Old Testament maneno hayo yanaonekana yakiwa hivi:

אֶת־ קַיִן וַתֹּאמֶר קָנִיתִי

I-brought-forth and-she-said Cain ***

אִישׁ אֶת־ יְהוָה ‏׃ וַתֹּסֶף

and-she-continued (2) Yahweh with man

Hapa jina la Mungu lenye kumtofautisha na wengine linaonekana wazi kuwa ni “Yahweh.”​—Mwanzo 4:1.

Hiyo inaonyesha nini? Kwamba wakaaji wale wa kibinadamu wa kwanza kabisa duniani walilijua jina la kibinafsi la Muumba wao. Jina hilo liliendelea kushirikishwa na yule Mungu mmoja tu wa kweli wakati wa kuandikwa kwa Maandiko ya Kiebrania yote​—kipindi cha miaka zaidi ya elfu moja. Basi, ulizo ni hili: Ni namna gani na wakati gani mazoea ya kuficha jina “Yehova,” au “Yahweh,” yalianza?

Je! Mapokeo ya Kiyahudi Yameleta Badiliko Katika Biblia Yako?

Ni vigumu kutaja kabisa tarehe fulani ambayo jina la Mungu liliacha kutumiwa. Lakini, kuna ushuhuda wa kwamba kabla ya mwaka wa 70 W.K. ushirikina fulani ulikuwa umesitawi kati ya Wayahudi wenye kufuata sana mapokeo ukawafanya waepuke kutamka jina la kibinafsi la Mungu. Baada ya Jina la Kimungu kuwa limetumiwa kwa karne nyingi, inaonekana kwamba wakuu wa dini ya Kiyahudi waliamua kwamba lilikuwa takatifu mno hata lisistahili kutamkwa na kwamba njia ya pekee ya kuepuka kulitumia vibaya ilikuwa ni kulipiga marufuku kabisa lisitamkwe. Jamani, hiyo ni sawa na kusema ndoa ipigwe marufuku kwa kusudi la kuzuia uzinzi!

Je! hayo mapokeo ya Kiyahudi yamewavuta watafsiri wa Biblia wa Jumuiya ya Wakristo? Je! wao wamelitukuza jina la Mungu, au wameendeleza kwa muda mrefu kosa hilo la Kiyahudi wakaligandamiza jina la Mungu? Je! Biblia yako ina kasoro (ukosefu) katika jambo hilo? Ukitazama kwa ufupi tafsiri kadha za kisasa utaweza kujibu maulizo hayo.

Mhariri wa Biblia ya An American Translation (ya mwaka wa 1923, iliyofanywa na Smith na Goodspeed) aliandika hivi: “Katika tafsiri hii tumefuata mapokeo ya Kiyahudi yanayokubaliwa sana tukaweka maneno ‘Bwana’ badala ya jina ‘Yahweh.’ “(Sisi ndisi tumelaza maneno yale ya kutia mkazo) Dibaji ya Biblia The New International Version (1978) inasema hivi: “Kwa habari ya jina la kimungu YHWH . . . watafsiri walifuata njia inayotumiwa katika tafsiri zilizo nyingi za Kiingereza za kufasiri jina hilo kuwa ‘BWANA’.”

Biblia ya Revised Standard Version (1952), inakataa kufuata mfano mwema wa tafsiri iliyoitangulia, yaani American Standard Version (1901), iliyotumia Yehova bila ugeugeu, na inaeleza hivi: “Usahihishaji wa sasa unarudia mtindo wa Tafsiri ya King James [1611], ambayo inafuata kanuni ya watafsiri wa kale wa Kigiriki na Kilatini na yale mazoea yaliyoimarika kwa muda mrefu yaliyotumika katika usomaji wa maandiko ya Kiebrania katika sinagogi.”​—Sisi ndisi tumelaza maneno ya kutia mkazo.

Pasipo shaka hata moja mapokeo ya Kiyahudi yameshiriki kufanya watu ulimwenguni pote wasilijue lile jina lililo la maana kupita majina yote katika ulimwengu mzima wote. Na wengi wa watafsiri wa Jumuiya ya Wakristo wamefurahia hali hiyo ya watu kukosa kulijua. Lakini kwa sababu gani? Kwa sababu gani wasitake wewe ulione jina Yehova, au Yahweh, katika Biblia yako?

Kusudi Limekuwa Ni Nini?

David Clines, mhatibu katika idara ya Uchunguzi wa Kibiblia kwenye Chuo Kikuu cha Sheffield huko Uingereza, anatudokezea makusudi ya kufanya hivyo bila ya yeye kujua amedokeza. Katika gazeti Theology anaandika hivi: “Tokeo moja la kutojulikana kwa Yahweh na Wakristo limekuwa ni maelekeo ya kukaza fikira juu ya Kristo kuwa ndiye udhihirisho wa pekee wa uungu . . . Katika nyimbo za kidini kama . . . ‘Yesu ni rafiki kweli kweli’ . . . tunaona yametumiwa maneno ambayo kwa mdomo yangefanyiwa ubishi sana kwamba hayatumiki, yaani kutajwa kuwa mtu mmoja kwa yule anayeitwa nafsi ya pili ya Utatu.” Profesa Clines anaendelea kumalizia hivi: “Jambo ambalo limeelekea kutukia kwa matendo ni kwamba mafundisho ya kidini ya utatu yameinua zaidi cheo cha utu na kazi ya Kristo. Vyeo vya Baba [Yehova] na Roho, viwe ni katika mafundisho ya kidini au ni katika ibada ya kanisani, vimekuwa vikishushwa kwa kuwekwa chini ya kile cha Mwana.”

Matokeo ya kufanya hivyo ni nini? Kwa Wayahudi Bwana Yehova Mwenye Enzi Kuu amefanywa isivyofaa awe bila jina bila kujulikana alivyo hasa​—akaitwa “Mwenye Uungu.” Kwa Waprotestanti wengi yeye ameingizwa ndani ya Kristo wakawa mtu mmoja lakini akashushiwa cheo awe wa pili katika mwungano wa Mungu mmoja katika watatu. Katika mazoea ya kidini ya Kikatoliki Yehova ameondoshwa mahali pake na nafasi hiyo ikachukuliwa si na Yesu Kristo tu, bali pia na Mariamu mama ya Yesu. Kwa sababu gani? Kwa sababu Mariamu, kulingana na lile wazo la Utatu, anaonwa pia kuwa ndiye “Mama ya Mungu.” Jambo hilo limemwondoa Yehova katika mapendo ya moyoni ya Mkatoliki wa kawaida.

Kwa hiyo je! wewe unamchukua Yehova kuwa mwenye umaana gani? Je! wewe utapata kumjua kwa undani? Uamuzi wako wa kibinafsi utahusu sana wakati ujao wako kwa sababu Yehova amesema: “‘Mimi kwa uhakika nitatakasa jina kuu langu, ambalo lilikuwa likifanyiwa madharau kati ya mataifa, . . . na hayo mataifa yatalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova,’ ndilo tamko la Bwana Yehova Mwenye Enzi Kuu, ‘wakati mimi nitakaswapo kati yenu mbele za macho yao.’”​—Ezekieli 36:23, NW.

Jambo la kufurahisha kwa wanadamu ni kwamba, Yehova ameinua mashahidi wake ambao, katika karne hii ya 20, wanatangaza bila woga jina na kusudi lake. Ikiwa wewe ungetaka kumjua Mungu wa kweli aliye hai, Yehova, waendee Mashahidi wa Yehova katika ujirani wenu au upashane habari na wachapishaji wa gazeti hili. Wao watakusaidia kwa furaha bila malipo wala masharti umjue yule Baba ya kimbingu, Yehova.​—Isaya 43:10; Mathayo 6:9.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki