Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w80 8/1 kur. 3-4
  • Jina la Mungu Katika Nyakati za Baadaye

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jina la Mungu Katika Nyakati za Baadaye
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • JINA “YEHOVA” LAJULIKANA POTE
  • JIBU LA WAFASIRI
  • CHUKI YA KIDINI?
  • KANUNI MBIU
  • TAFSIRI NYINGINE
  • JINA HILI LA PEKEE LINAMAANISHA NINI?
  • Jina la Mungu na Watafsiri wa Biblia
    Jina la Mungu Litakaloendelea Milele
  • Yehova
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Kufumbua Fumbo la Lile Jina Linalokosekana
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • A4 Jina la Mungu Katika Maandiko ya Kiebrania
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
w80 8/1 kur. 3-4

Jina la Mungu Katika Nyakati za Baadaye

HAKUNA shaka yo yote kwamba jina la Mungu lilikuwa likitumiwa katika wakati wa mapema wa historia. Lakini namna gani juu ya nyakati za baadaye? Sababu gani tafsiri nyingine za Biblia zikaacha kutumia jina hilo? Nalo lina maana na ubora gani kwetu sisi?

JINA “YEHOVA” LAJULIKANA POTE

Linalopendeza ni kwamba, mtawa mmoja Mspania, Raymundus Martini, ndiye aliyekuwa wa kwanza kuandika jina hilo la kimungu katika namna ya “Yehova.” Namna hiyo ilitokea katika kitabu chake Pugeo Fidei, kilichochapwa katika mwaka 1270 W.K.​—zaidi ya miaka 700 iliyopita.

Wakati ulivyoendelea, navyo vyama vya watu wenye kutaka mabadiliko ya kidini vikatokea ndani na nje ya Kanisa Katoliki, iliwezekana watu wote wajipatie Biblia, nalo jina “Yehova” likajulikana zaidi mahali pote. Katika mwaka 1611 W.K., ikachapwa tafsiri ya Biblia ya Kiingereza iitwayo King James au Authorized Version (Tafsiri Iliyoruhusiwa). Inatumia jina Yehova mara nne. (Kut. 6:3; Zab. 83:18; Isa. 12:2; 26:4) Tangu wakati huo, Biblia imetafsiriwa mara nyingi sana. Tafsiri fulani zinafuata mfano wa Authorized Version na kulitia jina la Mungu mara chache tu (kwa mfano tafsiri ya Kiswahili ya Union Versiori).

Mojawapo ya hizi ni An American Translation (ya Smith na Goodspeed) ikiwa na tofauti kidogo kwa vile inatumia “Yahweh” badala ya “Yehova.” Hata hivyo, waweza kuuliza: “Ni kwa sababu gani wafasiri wamefanya hivyo? Ikiwa kutumia ‘Yehova’ au ‘Yahweh’ ni kosa, sababu gani walitie ndani hata kidogo? Na ikiwa inafaa, sababu gani wasilitumie kila mahali linapopatikana katika maandishi ya awali ya Biblia?”

Tukiwa na msingi huo wa kihistoria na wa kweli, ebu sasa na tuchunguze wanayosema wafasiri katika kujibu.

JIBU LA WAFASIRI

Maneno ya utangulizi ya An American Translation yasema hivi: “Katika tafsiri hii tumefuata desturi ya Wayahudi tukatumia ‘Bwana’ mahali pa jina ‘Yahweh.’ “Walakini kwa kufuata “desturi ya Wayahudi,” je! wafasiri hao walifahamu namna linavyoweza kuwa jambo lenye kuharibu, kudharau kusudi la Mungu kwamba ‘jina lake litangazwe duniani pote’? Tena, Yesu alilaumu desturi au mapokeo ya wanadamu ambayo yalifanya neno la Mungu lionekane kuwa la bure.​—Kut. 9:16; Marko 7:5-9.

Maneno ya utangulizi ya Revised Standard Version yasema hivi: “[Tafsiri] ya sasa iliyofanywa upya inafuata kawaida ya King James Version, inayofuata . . . desturi iliyoanzishwa muda mrefu uliopita katika kusoma maandiko ya Kiebrania katika sinagogi, . . . . Kwa sababu mbili Halmashauri imerudia matumizi yanayofahamika zaidi ya King James Version: (1) Neno ‘Yehova’ haliwakilishi kwa usahihi namna yo yote ya Jina lililotumiwa katika wakati wo wote katika Kiebrania; na (2) matumizi ya jina lo lote la kibinafsi kwa ajili ya Mungu aliye mmoja na wa pekee, kana kwamba kulikuwako miungu wengine ambao lazima atofautishwe nao, yaliachwa kufuatwa katika dini ya Kiyahudi kabla ya wakati wa Kikristo nalo ni jambo lisiloifaa imani ya ulimwenguni pote ya Kanisa la Kikristo.” (Ni sisi tumelaza maneno.)

Wafasiri hao walifanya kosa kubwa kwa kufuata mfano wa King James Version na desturi ya Kiyahudi. Je! kweli wao walifikiri kwamba yalikuwa mapenzi ya Yehova kwamba jina lake lifichwe? Je! jina la Mungu ni jambo la kuonea aibu hivi kwamba lapaswa kuachwa kutumiwa katika Biblia?

CHUKI YA KIDINI?

Linalopendeza ni kwamba tafsiri ya American Standard Version, iliyochapwa katika mwaka 1901, inatumia jina la Yehova katika Maandiko ya Kiebrania yote. Tofauti na hiyo, Revised Standard Version, chapa ya 1952, inataja kifupi tu zile herufi nne (Tetragrammaton) katika maelezo yake ya chini (katika Kutoka 3:15). Katika kipindi hicho cha wakati, Mashahidi wa Yehova walikuwa wakilitangaza jina la Mungu ulimwenguni pote. Je! yawezekana kwamba tafsiri fulani ziliacha kutumia jina la Mungu kwa sababu ya kuchukia utendaji wa kutoa ushuhuda wa Mashahidi wa Yehova?

Kwamba inaweza kuwa hivyo katika visa fulani inaonyeshwa na usemi unaofuata uliotokea katika Katholische Bildespost (gazeti la Kikatoliki la Ujeremani): “Walakini, jina la Mungu, ambalo wao [Mashahidi wa Yehova] wamegeuza liwe ‘Yehova’ ni ubuni tu wa madhehebu hiyo.” (Agosti 24, 1969) Usemi huo unaonyesha chuki ya kidini. Vilevile unaonyesha namna wasivyofanya uchunguzi vizuri, kwa kuwa, kama vile ilivyotangulia kutajwa, mwandikaji wa kwanza kutumia namna ya “Yehova” alikuwa mtawa Mkatoliki—kwa wazi hakuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova!

KANUNI MBIU

“Neno ‘Yehova’ haliwakilishi kwa usahihi namna yo yote ya Jina lililotumiwa katika wakati wo wote katika Kiebrania,” yasema maneno ya utangulizi ya Revised Standard Version. Lakini ni neno gani ‘linalowakilisha kwa usahihi’ jina la Mungu katika Kiebrania? Watu fulani wanapendelea “Yahweh,” wengine “Yehwah,” wengine “Yave,” na vivyo hivyo. Tatizo ni kwamba wakati wa kuandika Kiebrania cha kale konsonanti (herufi bubu) peke yake ndizo zilizotumiwa na hata wataalam wanakubali kwamba inakisiwa tu ni vokali zipi zilizokamilisha jina la Mungu.

Vilevile wale wanaopinga matumizi ya namna ya “Yehova” waweza kuulizwa sababu gani hawapingi matumizi ya majina mengine kama vile “Yesu” au “Petro.” Sababu gani wachambuzi hawa hawasisitizi kwamba namna za Kigiriki cha asili za majina hayo zitumiwe (Iesoús and Petros)’! Je! watu hao mmoja mmoja hawana hatia ya kutumia kanuni mbili katika kulikataa jina “Yehova”?

TAFSIRI NYINGINE

Kwa kweli, tafsiri nyingi hutumia “Yehova” au “Yahweh” au namna nyingine inayowakilisha zile herufi nne. Tena, kunazo tafsiri kama 40 hivi za lugha za kienyeji za Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo (“Agano Jipya”) zinazotumia namna ya kienyeji ya zile herufi nne kama vile Iehova (Kihawaii) na uJehova (Kizulu).

Tafsiri The Bible in Living English (ya Stephen T. Byington) vilevile inatumia “Yehova” katika maandishi yote ya Kiebrania. Katika maneno yake ya utangulizi, Byington asema hivi kwa habari ya jina “Yehova”: “Uendelezaji na matamshi si ndiyo mambo ya maana zaidi. Jambo lililo la maana zaidi ni kuonyesha wazi kwamba hili ni jina la kibinafsi.” Ndiyo, jina la Mtu aliyetukuka zaidi katika ulimwengu wote ni la pekee, halilinganiki, ni tukufu mno.

JINA HILI LA PEKEE LINAMAANISHA NINI?

Ili kujibu swali hili, tukio lililotukia kweli kweli huko nyuma linafaa sana. Alipoagizwa na Aliye Juu Zaidi awaongoze Waisraeli kutoka Misri, “Musa alimwambia Mungu wa kweli: ‘Tuseme sasa mimi nimekuja kwa wana wa Israeli nami niwaambie, “Mungu wa baba zenu amenituma kwenu,” nao waniambie, “Jina lake ni jipi?” Nitawaambia nini?’ Basi Mungu akamwambia Musa: “NITAJITHIBITISHA KUWA NITAKAVYOJITHIBITISHA KUWA.” Naye akaongeza hivi: ‘Hivi ndivyo utakavyowaambia wana wa Israeli, “NITAKAVYOJITHIBITISHA KUWA amenituma kwenu.” ‘ “(Kut. 3:13, 14, NW) Hiyo inamaanisha kwamba Yehova angetimiza kusudi lake kuu la kulitetea jina lake na enzi yake kuu, nalo jambo hilo latusaidia kufahamu maana ya jina hilo la kumbukumbu “Yehova,” linaloonyeshwa katika mstari wa 15. Kulingana na asili ya Kiebrania ya jina hilo linaonekana likimaanisha “Yeye Hufanya Iwe” (au, “Anajithibitisha Kuwa”) kwa habari yake yeye mwenyewe. Hivyo jina la Mungu lina maana halisi kwa watu wenye kufikiri. Jina hilo lamfunua kuwa Yeye ambaye hutimiza anayoahidi bila kushindwa naye ana mamlaka kamili kuweza hali yo yote itokeayo.

Lo! jinsi jina hilo la Mungu lilivyo na maana takatifu, maana yenye kina! Ndilo jina zuri sana katika ulimwengu wote, jina lililo tukufu sana. Neno “Bwana” linafifia na halileti maana likilinganishwa nalo. Yesu alilipenda na kuliheshimu jina la Baba yake naye pindi moja alimwambia hivi: “Baba, litukuze jina lako.” Nayo masimulizi yaendelea kusema hivi: “Basi ikaja sauti kutoka mbinguni, Nimelitukuza, nami nitalitukuza tena.”​—Yohana 12:28.

Ikiwa Yesu angekuwa mfasiri wa Biblia leo, je! yeye angeacha kutumia jina la Baba yake katika tafsiri mpya? Hata kidogo! Pasipo shaka yo yote, Yesu, zaidi ya mtu mwingine ye yote, alikuwa na maoni yaliyofaa kumwelekea Mungu Mwenye Nguvu Zote pamoja na jina Lake. Kwa hiyo maoni yetu kumwelekea Mungu na jina lake yapaswa kuwa maoni gani?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki