Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w80 8/1 kur. 5-7
  • Ni Nini Yaliyo Maoni Yako Juu ya Jina la Mungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Nini Yaliyo Maoni Yako Juu ya Jina la Mungu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “NAWEZAJE KWELI KUMJUA MUNGU?”
  • “ENDELEA KUTAFUTA”
  • MAONI JUU YA JINA LA MUNGU
  • WAJIVUNIA KULICHUKUA JINA LAKE
  • OMBI
  • Kwa Nini Ni Lazima Tujue Jina la Mungu
    Jina la Mungu Litakaloendelea Milele
  • Liheshimu Jina Kuu La Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Ujumbe Ambao Ni Lazima Tuutangaze
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Je! Wewe Unatembea katika Jina la Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
w80 8/1 kur. 5-7

Ni Nini Yaliyo Maoni Yako Juu ya Jina la Mungu?

BILA SHAKA, ndani sana moyoni mwako, tayari wewe unasadikishwa kwamba Mungu yuko na ya kwamba alitoa au akaumba vitu vingi vilivyo vizuri ajabu vinavyotuzunguka. Pengine wewe unamheshimu Mungu kweli kweli—na hata hivyo hujisikii ukiwa karibu sana naye. Huenda kwako Mungu akaonekana kuwa hajishughulishi nasi na kwamba hafahamiki.

Walakini, kuja kumjua na kumpenda Mungu kweli kweli, na kumkubali kuwa Baba ya jamaa ya ulimwenguni pote na wewe upate kuwa mshiriki wa jamaa hiyo kubwa ni mambo ya maana sana na yenye uharaka mwingi. Kwa maoni ya kibinafsi, sisi kuja kumjua Mungu, kumheshimu na kumtii kama Baba atupendaye ni jambo linalohusu uzima na mauti. Na kulingana na maoni ya ulimwengu wote, kufanyizwa kwa jamaa hii ya ulimwenguni pote ndilo suluhisho peke yake la taabu kubwa waliyo nayo wanadamu. Unabii wa Kimungu unaonyesha waziwazi kwamba taratibu hii ya mambo ya kale inaelekea msiba wa ulimwenguni pote ambao watakaouokoka peke yake ni wale tu wanaompenda Mungu na jirani zao. (Zab. 37:10, 11, 28, 29) Lakini waweza kuuliza . . .

“NAWEZAJE KWELI KUMJUA MUNGU?”

Tuseme unajifunza jambo fulani kuhusiana na elimu fulani, nawe wamheshimu sana mwalimu fulani wa elimu hiyo anayejulikana sana. Vilevile, tuseme watamani sana kumjua vyema zaidi na kujifunza zaidi kutoka kwake, lakini anaishi katika nchi ya mbali sana. Ufanyeje? Je! hungejitahidi sana kusoma vitabu vyake vyote na kitabu cho chote kilichochapwa juu yake? Je! hungezungumza na wanafunzi wengine ambao tayari wanajua mengi zaidi juu yake na mafundisho yake? Tena, tuseme ulimwandikia upate habari kuhusu maulizo ya kipekee magumu sana, au matatizo nawe ukapokea majibu yenye kuridhisha sana. Ungezidi kumheshimu sana mwalimu huyo mzuri sana nao msaada wake kwako ungekufanya umpende sana.

Je! jambo hilo lawezekana vilevile kwa Yehova, Mwalimu Aliye Mkuu Zaidi? Bila shaka ndiyo. (Isa. 30:20, 21) Lakini namna gani?

Je! wewe umepata kusoma hata kidogo ‘Maandishi Yake’​—Biblia? Pengine umejaribu kufanya hivyo lakini ukaona sehemu nyingine zikiwa ngumu kufahamu. Basi, sababu gani usifuate mfano wa mkuu mmoja wa Kiafrika ambaye vilevile alikuwa akisoma Maandiko akawa na maulizo? Yeye alifanya nini? Alimwuliza Filipo, shahidi wa Yehova, amsaidie. Sababu gani usisome juu ya jambo hili lenye kupendeza katika kitabu cha Matendo, sura ya 8, mstari 26 mpaka 39?

Nawe vilevile waweza kufanya vivyo hivyo leo. Ukisoma Biblia uwe na maulizo, sababu gani usiwaendee Mashahidi wa Yehova? Sikuzote wao wako tayari kusaidia wale wanaotafuta kumjua Baba wa Kimbinguni, Yehova. Nao wana vitabu vyenye msingi wa Biblia (licha ya gazeti hili) vya kuelimisha wanafunzi wenye mioyo minyofu.

Kwa kweli, kuzungumza juu ya Biblia pamoja na mwanafunzi mwenye ujuzi wa Maandiko kwaweza kukuongezea sana maarifa ya kumjua Yehova na kumheshimu pamoja na kumpenda. Kwa mfano, utajifunza kwamba Yehova ni “Mungu mwenye rehema na neema, asiye mwepesi wa hasira na mwingi wa fadhili za upendo na kweli.”‏ (Kut. 34:6, NW) Utaona mifano mingi sana ya rehema na subira ya Yehova, kama vile katika habari ya Daudi, ambaye alitenda dhambi katika njia mbaya sana walakini akatubu akasamehewa.​—2 Sam. 12:13, 14; Zab. 51.

Vilevile utafahamu sababu gani Yehova ameruhusu uovu uendelee, sababu gani hajafutilia mbali uovu na upotovu—jambo ambalo atalifanya hakika kama vile ilivyo hakika kwamba jua litachomoza kesho asubuhi. (Mit. 2:21, 22; 2 Pet. 3:7) Utapata kuthamini ustahimilivu wa Yehova ulio mkubwa sana, hekima yake isiyo na kikomo na ufahamu wake, pamoja na kusudi lake zuri sana la kuisafisha dunia na kurudisha amani na paradiso.​—Linganisha Isaya 65:17, 21-25.

“ENDELEA KUTAFUTA”

Lakini huenda ukapatwa na magumu na upinzani. Huenda watu fulani, hata kati ya rafiki na washiriki wa jamaa yako wakadhihaki jitihada zako za kujifunza Neno la Yehova, na hata wakajaribu kuharibu sifa ya wale wanaojaribu kukusaidia. Yesu aliwaonya wanafunzi wake watazamie mambo kama hayo.​—Mt. 5:11.

Hata hivyo, ikiwa wewe wasadiki kwamba yuko Mtu aliye mtukufu sana ajuaye habari za wakati ujao wa wanadamu, basi shikamana na azimio lako la kutaka kumjua yeye na Mwanawe, Yesu Kristo. Mwana uyu huyu ndiye aliyesema hivi: “Hii ndiyo maana ya uzima wa milele, wapate maarifa ya kukujua wewe, Mungu wa kweli peke yako, na ya yeye uliyemtuma Yesu Kristo.” Yesu vilevile alisema hivi: “Endeleeni kutafuta, nanyi mtapata; endeleeni kupiga hodi nanyi mtafunguliwa.”​—Yohana 17:3, NW; Mt. 7:7, NW.

Ikiwa utafanya hivyo, bila shaka utashangaa kujua namna Yehova alivyo karibu, na namna anavyoambilika kweli kweli. Mtume Paulo alisema hivi katika hotuba aliyoitoa hadharani mbele ya kikundi cha Waathene: ”‏[Mungu] hawi mbali na kila mmoja wetu.” (Matendo 17:27) Naye nabii aliyeongozwa na Mungu aliandika hivi: “Mtafuteni [Yehova], maadamu anapatikana, mwiteni, maadamu yu karibu.” —Isa. 55:6.

Ndiyo, ‘mwite.’ ‘Mkaribie Mungu, naye atakukaribia.’ (Yak. 4:8) Ikiwa unaitafuta kweli, ikiwa una matatizo yenye kuhuzunisha au dhambi zinazokulemea, mwite Yehova, “Baba wa rehema, Mungu wa faraja yote.” (2 Kor. 1:3) Fanya hivyo kwa jina la Mwanawe, Yesu Kristo, aliyesema hivi: “Njoni kwangu ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.”​—Mt. 11:28.

Utafurahia kujua namna jitihada zako za kumkaribia Yehova zinavyoleta tofauti kubwa na yenye kuridhisha maishani mwako. Akili yako itaondolewa maoni pamoja na imani za uongo za kidini zenye kuvuruga akili na zenye kusumbua. Vilevile kwa kujifunza juu ya unabii wa Mungu na makusudi yake utapata kujua sababu gani ulimwengu umejaa sana matatizo, upotovu na woga. Ndiyo, na kujifunza Biblia hivyo kutakufunulia wakati ujao mzuri sana uliowekwa akiba kwa ajili ya dunia na wale watakaopendelewa kuishi ndani yake chini ya ufalme wa Mungu.​—Mt. 6:9, 10.

Je! wewe hukubali kwamba katika wakati huu wenye giza katika historia ya wanadamu, tunahitaji sana ufahamu, maono pamoja na nuru ya kiroho? Kwa kufaa sana Zaburi 119:105 yasema hivi kwa habari ya Mungu: “Neno lako ni taa ya miguu yangu, na mwanga wa njia yangu.” Ndiyo, Neno la Mungu laweza kufunua njia mpya nzuri sana ya maisha sasa na maono mazuri sana ya wakati ujao. Laweza kukuongoza uyapate maarifa sahihi ya kumjua na kumpenda sana Mungu wa kweli, Yehova.

MAONI JUU YA JINA LA MUNGU

Hata mtu awe ana rangi gani ya ngozi au awe wa taifa gani, kichwa cha jamaa mwenye fadhili na upendo na aliye imara anathaminiwa sana. Baba mzuri si mpaji-uzima tu, bali vile-vile ni mshauri, mlinzi, na rafiki katika wakati wa uhitaji. Baba kama huyo anaheshimiwa na kupendwa na watoto wake.

Je! sikuzote wewe

​—hungesema juu yake kwa kumsifu?

​—hungemtetea anapolaumiwa?

​—hungeepuka kumkasirisha?

​—hungejivunia kuchukua jina lake?

Wale wanaopata kuwa washiriki wa jamaa ya Yehova ya ulimwenguni pote sikuzote wanasema juu yake kwa kumsifu. Wao hawajiungi na shughuli yo yote ya kulificha jina la Mungu bali wao wana bidii katika kulijulisha jina lake kuu kati ya mataifa. (Zab. 105:1-3) Sikuzote wao wako tayari ‘kumtolea Mungu dhabihu ya sifa, yaani, tunda la midomo ambalo hulitangaza waziwazi jina lake.’​—Ebr. 13:15, NW.

Watu hao mmoja mmoja wako tayari sikuzote kulitetea jina la Baba yao anapolaumiwa. Kwa kuwa wamekwisha jifunza Neno lake kwa uangalifu, wanaweza kukanusha mafundisho ya kidini yenye kumvunjia Mungu heshima kama vile ya ‘moto wa hell na mateso.’ Wanaweza kuonyesha kwamba “Mungu ni upendo.”‏ (1 Yohana 4:8) Tena, wanaweza kuonyesha kwamba yeye ‘si mfu’ bali yuko hai sana naye anahangaikia sana hali ya dunia naye anakamilisha makusudi yake kwa wanadamu kwa uzuri sana.

Vilevile washiriki wa jamaa hii ya ulimwenguni pote wanajitahidi sikuzote kuepuka kufanya lo lote linaloweza kumkasirisha Baba yao. Wanathamini sana kwa moyo ile amri ya kale: “Haikupasi kulichukua jina la Yehova Mungu wako ovyo-ovyo.” (Kut. 20:7, NW) Wajapokuwa si wakamilifu, na kama vile alivyokuwa Mfalme Daudi, wana maelekeo ya kufanya makosa, wale wanaompenda Yehova wanajaribu kuendeleza kanuni za juu za mwenendo—unyofu, usafi wa mwilini na wa adili na kuepuka ibada ya sanamu, pupa na kutamani. (Luka 12:15; 1 Kor. 6:9, 10; Ebr. 13:18; 1 Yohana 5:21; Ufu. 19:8; 21:8) Wao wanajiepusha na vita vya kisiasa na jeuri yake, ambavyo vyasemekana kwamba vinapiganwa katika jina la Mungu walakini kwa kweli vimeliletea jina lake suto kubwa. (Isa. 2:4; Yohana 15:19) Lakini watumishi wa Mungu wanaheshimu serikali na mamlaka za mitaani nao ni raia wenye kutii sheria, wanaolipa kodi zao na wanaofanyia matajiri wao kazi ifaavyo ili “jina la Mungu lisitukanwe.”​—1 Tim. 6:1; Rum. 13:1-7.

WAJIVUNIA KULICHUKUA JINA LAKE

Iwapo wewe umetoka katika jamaa nzuri, Pengine wewe unajivunia kulichukua jina la baba yako. Na ndivyo ilivyo kwa wale wanaolichukua jina la Yehova leo. Jamaa kubwa katika mataifa yote ulimwenguni pote wanajivunia kulichukua jina la Baba wa kimbinguni wakiwa Mashahidi wa Yehova. (Isa. 43:10, 12; Ufu. 7:4-10) Wajapothamini maarifa yenye kuongezeka pamoja na vifaa ambavyo vimetolewa na wanadamu wenye ujuzi, wao wanamkubali na kumheshimu “Mungu aliye hai aliyeumba mbingu na nchi na bahari na vitu vyote vilivyomo.” Yeye ndiye anayetoa “mvua kutoka mbinguni, na nyakati za mavuno, akiwashibisha mioyo yenu chakula na furaha.” (Matendo 14:15-17) Naye alitoa zawadi iliyo kuu zaidi ya Mwanawe, ambaye kupitia kwake twaweza ‘kupata uzima wa milele.’ (Yohana 3:16) Wasifaji wa Yehova wanamshukuru sana kwa sababu ya zawadi zake zote.​—Yak. 1:17.

Ili kuonyesha shukrani zao kuu kwa Muumba wao, jamaa hii iliyo wakf, ya ulimwenguni pote, inashiriki sana katika kulitukuza jina tukufu na la pekee la Mungu kwa kukubali pahali pake pafaapo katika kitabu kitakatifu chake mwenyewe—katika Maandiko yote mawili ya Kiebrania na ya Kigiriki ya Kikristo. Nao, wakifuata nyayo za Bwana, Yesu Kristo, na za wafuasi wake wa karne ya kwanza, wanaeneza kwa bidii ujumbe wenye maana kubwa sana kwa siku ya leo: kwamba ufalme wa Mungu umekaribia nao ndio tumaini pekee la wanadamu.​—Mt. 4:23; 24:14; 28:19, 20.

OMBI

Twakutolea ombi la haraka sana utafute habari zaidi kuhusu Mungu wa kweli, Yehova, Mwanawe Yesu Kristo, pamoja na jamaa hii yenye furaha na umoja ‘inayolitangaza jina la Mungu katika dunia yote.’ (Kut. 9:16; Rum. 9:17) Si kwamba tu kufanya hivyo kwaweza kubadili maisha yako yote sasa, bali vilevile kwaweza kukufanya uokoke ile “dhiki kubwa” inayokuja na kuishi milele katika taratibu mpya ya mambo iliyoahidiwa na Mungu.​—Mt. 24:21, 22; 2 Pet. 3:13.

Ni jambo la hakika kwamba uhai wako unategemea mwendo utakaofuata. Maandiko yanatoa uhakikisho kwamba “kila [mtu] atakayeliitia Jina la [Yehova] ataokoka.”​—Rum. 10:13; Yoeli 2:32.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki