Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 4/1 uku. 23
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Habari Zinazolingana
  • Musa—Jinsi Maisha Yake Yanavyokuhusu
    Amkeni!—2004
  • Yesu Kristo Alikuwaje Nabii Kama Musa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Kuzijua Njia za Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Tafuta Upole Umpendeze Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 4/1 uku. 23

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

◼ Mtu akiisha kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova, je! anahesabiwa sikuzote kuwa hivyo?

Hapana, Mashahidi wa Yehova si kama dini zinazoshikilia kwamba, ‘Mtu akiisha kuwa mshiriki, ni mshiriki sikuzote.’ Asilimia ndogo ya watu mmoja mmoja wanachagua kujitenga wenyewe na kundi la Kikristo au wanaondoshwa nje kwa sababu wao ni wakosaji wasiotubu.

Wakati mmoja wanafunzi wengi waligeuka wakamwacha Yesu “wasiandamane naye tena.” (Yohana 6:66) Biblia inaeleza pia kwamba Mkristo akizoea dhambi nzito bila kutubu, kundi linapaswa ‘kumwondoa yule mbaya miongoni mwao’ na ‘kutokuchangamana naye.’—1 Wakorintho 5:9-13.

Hivyo, leo, Mkristo akitumbukia katika mwendo wa dhambi, halmashauri ya wazee wanaostahili kiroho inakutana naye. Wanataka kuona kama anatubu na anaweza kurekebishwa upya. (Wagalatia 6:1) Kama sivyo, wazee wanatii mwelekezo wa Biblia kutenga na ushirika yule mtenda dhambi ili kundi ‘lisitiwe chachu.’—1 Wakorintho 5:7.

Au, kama ilivyotajwa katika Yohana 6:66, mara kwa mara huenda Shahidi akajitakia yeye mwenyewe kuiacha njia ya ukweli. Huenda hata akajulisha kwamba ana uamuzi huo baada ya halmashauri kuanza kuchunguza kosa lake. Huenda akawapasha habari kwa kuandika barua, au akasema mbele ya washuhudiaji, kwamba anataka kujitenga na kundi asiwe akijulikana kuwa Shahidi. Hapo hakutakuwa tena na uhitaji wa wazee kuendeleza uchunguzi wao. Lakini, ikiwa hivyo wazee wangetoa tangazo fupi la kwamba amejitenga na ushirika ili kundi lijue kwamba ‘alitoka kwetu.’ (1 Yohana 2:19) Halafu watashika sana amri iliyoongozwa na Mungu inayosema ‘wasimkaribishe nyumbani mwao, wala wa simpe salamu ili wasishiriki kazi zake mbovu.’—2 Yohana 10,11.

Hivyo, watu hawalazimishwi kuendelea kuwa sehemu ya kundi. Lakini hesabu iliyo kubwa zaidi ya Mashahidi wa Yehova wana nia ya mitume walioshikamana na Yesu kwa kupenda kwao wenyewe, wakapokea msaada wake wa kiroho na kufurahia ushirika wenye uchangamfu wa kundi la Mungu,—Luka 22:28.

◼ Kama kweli Musa alikuwa mpole na mwenye kiasi, angewezaje kuandika katika Hesabu 12:3 kwamba ‘Musa alikuwa mpole sana zaidi ya wanadamu wote’?

Ingawa huenda ikawa haikuwa vyepesi kufanya hivyo, Musa aliweza kuandika maelezo hayo sahihi chini ya uongozi wa Mungu.

Alama moja inayoonyesha Biblia iliongozwa na Mungu ni kwamba waandikaji wake walisema mambo waziwazi. Musa na watu wengine waliotumiwa na Mungu kuandika visehemu vya Maandiko waliandika mambo kwa kuyasema wazi isivyo kawaida.

Kwa mfano, Musa aliandika visa vya hali za kupungukiwa na dhambi zilizotendwa na watu wake, kutia ndani zile za ndugu na dada yake mwenyewe. (Kutoka 16:2, 3; 17:2, 3; 32:1-6; Mambo ya Walawi 10:1, 2) Wala Musa hakujiondoa asijitaje kati ya waliokosa; alisimulia waziwazi makosa yake mwenyewe, hata yale yaliyofanya akaripiwe na Mungu. (Hesabu 20:9-12; Kumbukumbu la Torati 1:37) Kwa hiyo lilikuwa jambo lenye kupatana na hali hizo nyingine Musa kuandika wazi habari ya uhakika ambayo inaonekana Yehova alitaka itiwe ndani—kwamba Musa mwenyewe alikuwa mpole isivyo kawaida. Hali inayohusika katika kisa cha kuandikwa kwa maneno hayo inaonyesha vizuri jambo hilo. Badala ya Musa kuchukizwa sana wakati Miriamu na Haruni walipotokeza mwito wa ushindani juu ya mamlaka yake, yeye aliruhusu Yehova asahihishe hali hiyo.

Musa alitangulia kufananisha Masihi. (Kumbukumbu la Torati 18:15-19) Kwa hiyo Yehova Mungu alipoelekeza fikira kwenye upole wa Musa, Yeye alikuwa akitoa uhakikisho wa kwamba sifa hiyo ya kutamanika ingepatikana katika Masihi. Wakati tunaposoma yale masimulizi mbalimbali ya Injili, je! hatuoni upole wa Yesu ukituvuta, ukitufanya tutake kumkaribia na kutupa sababu ya kumtegemea?—2 Wakorintho 10:1; Waebrania 4:15, 16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki