Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 2/15 uku. 23
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Mungu Anaweza Kuhuzunika—Jinsi Tunavyoweza Kumfurahisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Kwa Nini Shetani Alitumia Nyoka Kuzungumza na Hawa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 2/15 uku. 23

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

◼ Katika bustani ya Edeni nyoka alimpashaje Hawa habari juu ya kile kishawishi?

Andiko la Mwanzo 3:1 linasema: “Basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa mwitu aliowafanya [Yehova] Mungu. Akamwambia mwanamke, Ati! hivi ndivyo alivyosema Mungu, Msile matunda ya miti yote ya bustani?”

Njia mbalimbali zimedokezwa kuwa ndivyo nyoka alivyompasha habari Hawa, kutia ndani ile ya kwamba alifanya hivyo kwa usemi wa kutumia mwili au ishara. Kwa mfano, Joseph Benson kiongozi wa kidini Mwingereza alisema hivi: “Hatujulishwi alisema naye kwa njia gani: lakini inaelekea sana kuwa ni kwa ishara za namna fulani. Watu wengine wamedhania kwamba uwezo wa kufikiri na usemi ndiyo mambo yaliyokuwa katika nyoka siku hizo, na basi Hawa hakushangaa wakati nyoka alipotumia uwezo wa kufikiri na kusema, na watu hao wanafikiri angalishangaa bila shaka kama haingekuwa kwamba nyoka walikuwa na uwezo huo: lakini hakuna jambo la kuthibitisha hivyo.”a

Imefikiriwa kwamba kuwapo kwenyewe kwa nyoka na matendo yake kungeweza kupitisha ujumbe. Bila shaka, haikuwa kwa wanyama, bali kwa mtu (Adamu) kwamba Mungu akasema hivi: “Walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula . . . utakufa hakika.” (Mwanzo 2:17) Hata hivyo, ikiwa nyoka​—aliyejulikana kuwa “mwerevu” sana​—alikuwa juu ya mti huo, Hawa angaliweza kuwa alikata shauri kwamba mti huo usingeweza kuwa hatari sana. Nyoka hata angaliweza kuwa alijisogeza-sogeza kwa njia ya hila kisha miendo yake hiyo ikaelekea kuonyesha kwamba alikuwa amepata faida fulani-fulani kwa kujihusisha na mti huo.

Lakini ni vigumu kusema kwamba miendo ya kimwili ndiyo iliyohusika katika yote tunayosoma katika Mwanzo 3:1-5, kama lile jambo la kwamba nyoka alionyesha Hawa angekuwa kama Mungu na aweze kuamua jema na baya. Zaidi ya hilo, historia iliyoongozwa na Mungu inasema kwamba nyoka “akamwambia mwanamke.” Hawa alimpa jibu, na inaweza kusemwa kwa akili nzuri kwamba alijibu kwa usemi. Halafu, “nyoka akamwambia mwanamke” jambo fulani zaidi. Kushikilia maoni kama ya Joseph Benson kwamba nyoka alimpasha habari kwa ishara au kwa kujisogeza-sogeza kungeongoza kwenye maoni ya kwamba Hawa naye alijibu kwa kutumia ishara pia.

Hata hivyo, mtume Paulo alitaja kisa hicho na akawaonya Wakristo Wakorintho, “Nachelea; kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa kwa hila yake, asije akawaharibu fikira zenu.”‏ Hatari hiyo ilitokana na “mitume wa uongo, watendao kazi kwa hila.” Kwa hakika tisho lililotokezwa na “mitume walio wakuu” halikuwa kupitia ishara tu na sura; lilitia ndani usemi wao, maneno yao ya ujanja yaliyosemwa ili kudanganya wengine.​—2 Wakorintho 11:3, 5, 13.

Lakini, nyoka halisi hakuwa na misuli ya kooni ya kumwezesha kutamka usemi. Hakuna jambo linadokeza hivyo. Wala hakuihitaji. Wakati Yehova aliposema na Balaamu kupitia mnyama wa kubeba mizigo, hiyo haikumaanisha kwamba punda-jike yule alikuwa na koromeo yenye visehemu vingi vya kutokeza sauti kama ile iliyokuwa katika koo la kibinadamu la Balaamu. Tunasoma hivi “[Yehova] akakifunua kinywa cha yule punda, naye akamwambia Balaamu . . . ” Balaamu alijibu ulizo la mnyama huyo, akafanya elezo jingine litokezwe na mnyama huyo ambaye akiwa peke yake hangeweza kutamka usemi wa kibinadamu. (Hesabu 22:26-31) Katika kisa hicho, Yehova alifungua macho ya Balaamu aone kwamba malaika alikuwapo, roho mwenye nguvu zipitazo za kibinadamu. Kwa hiyo wakati ‘mnyama wa kubeba mizigo asiyeweza kusema aliponena kwa sauti ya kibinadamu,’ kisababishi na uwezo wa tendo hilo vilitoka kwenye makao ya roho.​—2 Petro 2:16.

Basi je, Yehova alitumia namna fulani ya mwujiza wa kufanya sauti itoke katika mnyama huyo lakini ionekane kama maneno yalitoka kwa mtu mwingine? Labda, lakini hatuwezi kusisitiza mno juu ya njia ya kabisa iliyotumiwa. Maandiko ya Yohana 8:44 na Ufunuo 12:9 yanaonyesha kwamba yule aliyekuwa nyuma ya nyoka halisi katika Edeni ni yule aliyekuja ‘kuitwa Ibilisi na Shetani.’ Yeye, pia, ni roho mwenye nguvu zipitazo za kibinadamu, lakini roho mwovu.​—Linganisha 1 Samweli 28:7, 8, 15-19.

Kwa hiyo, hata ikiwa miendo ya nyoka halisi huenda ikawa ilielekea kuthibitishia Hawa ujumbe wake, kwa wazi usemi halisi​—maneno yenye kusikika ambayo Hawa angeweza kusikia na kuyajibu​—ulihusika. Na jambo hilo lilifanyika kwa kuchochewa na yule mdanganyaji mkuu, Shetani, ambaye “hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru.”​—2 Wakorintho 11:14.

[Maelezo ya Chini]

a Mwaka wa 1907, C. T. Russell aliandika hivi: “Kama alisema kwa sauti yenye kusikika au kwa vitendo vyake tu hatuwezi kujua​—inawezekana sana kuwa ni kwa njia ile ya pili, kwa maana nyakati nyingine tunasema, ‘Vitendo vinasema kwa sauti kubwa kuliko maneno.’”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki