Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 2/15 kur. 4-7
  • Unaweza Kuwa na Wakati Ujao Wenye Furaha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Unaweza Kuwa na Wakati Ujao Wenye Furaha
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Tunaweza Kupata Wapi Maarifa Kama Hayo?
  • Habari za Lazima
  • Usiogope Hekima
  • “Hazina Zote za Hekima”
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
  • ‘Lo! Kina cha Hekima ya Mungu!’
    Mkaribie Yehova
  • Je, “Hekima ya Kutoka Juu” Inakuongoza Maishani?
    Mkaribie Yehova
  • Wewe Unapangiaje Wakati Ujao?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 2/15 kur. 4-7

Unaweza Kuwa na Wakati Ujao Wenye Furaha

TUKIO la kutokeza wakati wa karne ya kwanza ya Wakati wa Kawaida wetu lilionyesha namna jambo fulani linalozidi hekima iliyo ya kawaida linavyohitajiwa ndipo tuweze kupangia wakati ujao wenye mafanikio. Katika siku hizo sehemu kubwa ya ulimwengu ilikuwa chini ya utawala wa kikoloni wa Roma. Nchi alimozaliwa Yesu Kristo, Palestina, ilikuwa sehemu ndogo tu ya Milki ya Roma iliyokuwa kubwa sana. Lakini Wayahudi walijitakia makuu. Hawakutaka kufuata utawala wa Kiroma na waliasi mara nyingi. Kati yao, hekima iliyo ya kawaida ilionyesha kwamba Mungu alikuwa upande wao.

Katika mwongo wa saba wa karne ya kwanza, Wayahudi walifanya jitihada kubwa ya kutaka kujiondoa katika kongwa la Waroma. Jeshi fulani la Kiroma liliwajilia likakaribia kuuteka mji wa Yerusalemu lakini likaondoka tena. Waasi wale waliwaza walikuwa wameshinda kwa msaada wa Mungu. Lakini, Yesu alikuwa amekwisha kutoa unabii kwamba mji huo ungeharibiwa. Kwa hiyo, Wakristo waaminifu walitumia kurudi kwa Waroma kuwa nafasi ya kuukimbia mji. (Mathayo 23:33-39; Luka 21:20-24) Muda mfupi baada ya wao kuondoka, Waroma walirudi tena. Mwaka wa 70 W.K. mji wa Yerusalemu uliharibiwa kisha wakaaji wake wakachinjwa au kuuzwa utumwani. Ni wale tu waliokuwa wamefanya hekima kutii onyo la Yesu waliookoka tukio hilo la kuogofya sana.

Huo ulikuwa wonyesho wa kutazamisha juu ya ukweli wa usemi huu wa Biblia: “Hekima ni ulinzi, kama vile fedha ilivyo ulinzi; na ubora wa maarifa ni ya kwamba hekima humhifadhi yeye aliye nayo.” (Mhubiri 7:12) Kupitia Kristo, Mungu alikuwa amewapa wafuasi wa Yesu maarifa ya kujua mambo ambayo yangetukia. Wao walikuwa wametenda kwa hekima kulingana na maarifa hayo, na “hekima ya Mungu” hiyo ilikuwa imewaokoa katika hali ambamo fedha, elimu ya kilimwengu wala mambo ya namna hiyo yangalikuwa ya bure tu.​—1 Wakorintho 1:21.

Katika ulimwengu wa sasa usiowapa watu uhakika wa mambo, wengi wanaogopa kwamba wangeweza kupatwa na matokeo kama ya hao Wayahudi waliokuwa Yerusalemu. Mipango yao yote kwa ajili ya wakati ujao ingeweza kuvurugwa na mabadiliko makubwa ya ghafula wasiyoweza kuzuia. Kwa hiyo, tunachohitaji ni namna ile ile ya maarifa ambayo Wakristo wa karne ya kwanza walikuwa nayo​—ufahamu wa mambo yaliyoko kweli kweli wakati ujao na mwendo ulio wa hekima zaidi kufuatwa.

Tunaweza Kupata Wapi Maarifa Kama Hayo?

Kila mwaka maelfu ya vitabu vinachapishwa, vikizungumza kila habari inayoweza kuwaziwa. Lakini, kujapokuwa na habari zote hizo, wakati ujao unaonekana wa kutisha. Hata hivyo, leo tuna kitabu kilicho tofauti na vichapo vingine vyote. Kuandikwa kwacho kulikuwa kumeanza kabla ya siku za Sulemani, na ndani yacho yameandikwa ‘maneno mengi ya wenye hekima’ yaliyo mfano wa “michokoo”​—yakichokoa mtu mwenye kuitikia atende kwa hekima. (Mhubiri 12:11) Kufikia wakati ambao Yesu alikuja duniani, sehemu iliyo kubwa zaidi ya kitabu hicho ilikuwa imeandikwa, naye alitumia mashauri yacho kwa wingi kusaidia wafuasi wake watende kwa hekima. Yesu alielekeza kwenye semi hizo za hekima aliposema hivi: “Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.”​—Mathayo 4:4.

Bila shaka, kitabu hicho ni Biblia. Lakini Biblia inatofautianaje na mfuatano mrefu wa vitabu vinavyochapishwa leo? Kwanza, inatoa maarifa ya namna tofauti. Ni wapi penginepo unapoweza kujifunza ukweli juu ya namna mwanadamu alivyoumbwa na kwa sababu gani anakufa? Ni kitabu gani kingine kinachojibu maulizo kama haya: Kwa sababu gani Mungu anaruhusu uovu? Ulimwengu huu unaelekea wapi? Je! kuna kusudi katika maisha? Biblia inatoa majibu ya ukweli kwa maulizo hayo na mengine mengi ya namna hiyo.

Pia Biblia inatupa mashauri ya hekima na yenye mafaa juu ya maisha ya kila siku. Inaonya juu ya matokeo mabaya ya ulevi, uasherati na uchafu wa kimwili. Inakazia faida zinazotokana na upendo, kujiweza na kutokuwa na choyo. Inaweka kiwango cha ndoa kinachofanya kazi kweli kweli na kutoa msaada wenye thamani kuelekea kupata maisha yenye furaha ya jamaa. Kufuata mashauri ya Biblia kutatuwezesha tupange wakati ujao unaothawabisha.​—1 Wakorintho 6:9-11; 13:4-8; Wagalatia 5:22-24; Waefeso 5:21–6:4.

Habari za Lazima

Lakini, Biblia ina thamani kubwa hasa kwa sababu inatuambia juu ya Yehova Mungu, Muumba. Kujua juu ya Yehova kunahitajiwa kabisa kwa sababu ndiye Chanzo cha maarifa yote. Kwani, hata mambo ambayo wanadamu wanajifunza juu ya uumbaji na ulimwengu mzima yanaweza kuwafunza jambo fulani juu ya Mungu! Biblia inasema: “Mbingu zauhubiri utukufu wa Mungu, na anga laitangaza kazi ya mikono yake.” Kweli ‘sifa za Mungu zisizoonekana zinafahamiwa kwa vitu alivyofanya.’ (Zaburi 19:1, UV; Warumi 1:20, NW) Inaelekea sana kuwa wachunguzi na wanasayansi wanaomweka Mungu kando wanapopanga mambo yao watakata maneno kwa njia mbaya au isiyo kamili.

Kujifunza juu ya Yehova kunahitajiwa kabisa pia kwa sababu kunaonyesha kwamba Mungu ana makusudi yake mwenyewe kwa ajili ya dunia na wanadamu. “Ni mingi mipango iliyo katika moyo wa mwanadamu, lakini shauri la Yehova ndilo litakalosimama.” (Mithali 19:21, NW) Hata watu wajaribu kutimiza nini, ikiwa mipango yao haipatani na makusudi ya Mungu, mwishowe itabomoka.​—Zaburi 127:1.

“Kumcha [Yehova] ni chanzo cha maarifa,” akasema Mfalme Sulemani. (Mithali 1:7) Hekima inayotegemea maarifa ya namna hiyo ina thamani halisi wakati mwanadamu anapopangia wakati ujao. Lakini Biblia inatambulisha Yesu Kristo pia kuwa “Mshauri wa ajabu.” (Isaya 9:6) Kwa hiyo tunawezaje kufanikiwa katika kupangia wakati ujao tukimpuuza? Lazima tutii ‘maneno yake ya uzima wa milele’ yaliyohifadhiwa katika Biblia. (Yohana 6:68) Zaidi ya hilo, lazima tumtambue yeye kuwa Mfalme mkuu aliyewekwa na Mungu, Yule atakayehukumu wanadamu wote. (Yohana 5:22) Na inatupasa tuitikie upendo mkuu alioonyesha kwa kutoa uhai wake uwe dhabihu kwa ajili ya dhambi za wanadamu.​—Yohana 3:16; 1 Yohana 2:1, 2.

Ndiyo, Yesu ni mtu wa maana zaidi ya wote katika historia ya kibinadamu, na mipango yo yote isiyomfikiria yeye itatikisika tu. Ndivyo hasa ilivyo tunapofikiria vile nabii Danieli alivyosema juu yake. Akisema juu ya Ufalme wa Mungu ulio chini ya Yesu Kristo, yeye alisema: “Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaangamizwa milele, wala watu wengine hawataachiwa enzi yake; bali utavunja falme hizi zote vipande vipande na kuziharibu, nao utasimama milele na milele.” (Danieli 2:44; Zaburi 2:1, 9) Basi, karibuni Ufalme wa Mungu chini ya Mfalme Yesu Kristo utachukua mahali pa falme zote za dunia hii. Kwa sababu hiyo, mambo yanayosumbua sasa wanadamu​—tatizo la uchafuzi, tisho la vita ya nyukilia, wasiwasi unaoletwa na ukosefu wa imara katika uchumi na siasa​—karibuni yatakuwa mambo ya zamani. (Ufunuo 11:18) Ndiyo, wakati ujao wako unaweza kuwa wenye furaha kweli kweli katika Paradiso ya kidunia inayokuja chini ya utawala wa Ufalme.​—Luka 23:43, ZSB.

Maarifa ya kujua hivyo yanatupa usawaziko wa akili tunapofikiria kwamba watawala wa ulimwengu hawawezi kutatua mambo yanayotatiza sana. Lakini kuna tatizo tunalopaswa kushinda.

Usiogope Hekima

Katika karne ya kwanza, Yesu alifundisha kwa njia isiyopata kufanywa na mwingine. Mamlaka yake ilionyeshwa alipoponya wagonjwa, vipofu na viwete, na hata akafufua wafu. (Mathayo 11:5, 6) Miujiza hiyo ya kutokeza ilifuatana na namna ya Yesu mwenyewe ya maisha yasiyo na kosa. (Waebrania 7:26) Kwa uhakika, mambo kama hayo yalithibitisha kwamba Yesu ndiye aliyekuwa Masihi aliyeahidiwa tangu zamani. Hata hivyo yeye hakuwa akihubiri kulingana na hekima iliyo ya kawaida, na Wayahudi walio wengi walimkataa.

Miaka kadha baadaye Paulo mtume Mkristo alimhubiria Mfalme Agripa. Akiitikia maneno yenye kusihi ya Paulo, Agripa alisema: “Baada ya muda mfupi ungenivuta kwa usadikisho niwe Mkristo.” (Matendo 26:28, NW) Kwa wazi, yeye aliweza kuona nguvu za ujumbe wenyewe. Lakini ilionekana kwamba haikuwa kawaida ya watu wengi kuufuata na kwamba ungalimhitaji afanye mabadiliko makubwa katika namna ya maisha yake. Kwa hiyo Agripa hakuwa kamwe Mkristo.

Kama Mfalme Agripa au Wayahudi walioshindwa kuitikia semi za Yesu, watu wengi leo wanaona ni jambo jepesi zaidi kufuata hekima iliyo kawaida ya wengine wote badala ya kukubali hekima ya Mungu. Lakini kumbuka kwamba ni Wayahudi wale tu walioitikia ujumbe wa Yesu waliokoka uharibifu wa Yerusalemu.

Vivyo hivyo leo, ni kwa kuitikia tu hekima ya Mungu wanadamu wataweza kutenda kwa hekima kupanga wakati ujao wetu. Ni kweli kwamba maadamu mfumo huu upo tutapaswa pia kutumia akili zetu tunapopanga maisha zetu. Lakini ikiwa mipango yetu yote ya wakati ujao imetia nanga katika mfumo huu wa mambo, mwishowe itakuwa bure kabisa, kwa maana mwisho wake ni karibu. Ni mwendo wa hekima ya kweli kusoma Biblia kwa uangalifu ili kujifunza juu ya makusudi ya Mungu. Inatupasa tujifunze hiyo kikamili ili tujue mapenzi yake ni nini kwetu sasa. Nasi tutakuwa tukitenda kwa hekima tukitimiza mapenzi hayo kwa kuyadhamiria.

“Hekima ya Mungu” inazaa matunda mema. Yakobo ndugu wa mzazi mmoja na Yesu alisema: “N’nani aliye na hekima na ufahamu kwenu? Na aonyeshe kazi zake kwa mwenendo wake mzuri, katika upole wa hekima. . . . Hekima itokayo juu, kwanza ni safi, tena ni ya amani, ya upole, tayari kusikiliza maneno ya watu, imejaa rehema na matunda mema, haina fitina, haina unafiki.” (Yakobo 3:13-17) Hakika hekima ya namna hiyo ‘itawahifadhi wao walio nayo’! (Mhubiri 7:12) Itakuwezesha wewe ufanikiwe katika kupanga wakati ujao wenye furaha.

[Blabu katika ukurasa wa 5]

“Hekima ya Mungu” iliokoa Wakristo wa kwanza katika hali ambamo fedha zilikosa ubora

[Blabu katika ukurasa wa 7]

Hekima inayotegemea maarifa kutoka kwa Mungu ina ubora kweli kweli wakati mwanadamu anapopangia wakati ujao

[Picha katika ukurasa wa 6]

Kujifunza Biblia kwa uangalifu kunafunua kwamba Mfalme Yesu Kristo ‘atayaponda mataifa kwa fimbo ya chuma’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki