Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 2/15 kur. 3-4
  • Wewe Unapangiaje Wakati Ujao?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wewe Unapangiaje Wakati Ujao?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Wakati Ujao Una Uhakika Gani?
  • Jambo Fulani Limekosekana
  • Unaweza Kuwa na Wakati Ujao Wenye Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Jinsi ya Kuwa na Maisha Bora ya Wakati Ujao
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2021
  • ‘Lo! Kina cha Hekima ya Mungu!’
    Mkaribie Yehova
  • “Heri Mtu Yule Aonaye Hekima”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 2/15 kur. 3-4

Wewe Unapangiaje Wakati Ujao?

“AFADHALI tuufikirie wakati ujao kwa uzito kwa sababu tutatumia maisha yetu yote katika wakati huo!” Labda wewe unakubaliana na maneno hayo. Wengi wetu tunaona hekima ya kufanya matayarisho fulani kwa ajili ya wakati ujao.

Katika jamii fulani za watu, watu waliooana wanajaribu kuwa na watoto wengi ili wawe na mtu wa kuwatunza watakapokuwa wazee. Huenda vijana wakaenda kwenye vyuo vya masomo ya juu kujitayarishia kazi nzuri. Huenda watu wazima wakaweka akiba ya fedha zao wakijitahidi kujihakikishia watakuwa na usalama wakiwa wazee. Na wengi wanaoziona fedha kuwa ndizo uhakikisho bora zaidi wa wakati ujao wanatumia mwingi wa wakati na nishati zao, hata afya, wakijitahidi kuwa matajiri.

Wakati Ujao Una Uhakika Gani?

Njia hizo za kujitayarishia wakati ujao zinaweza kuitwa hekima iliyo ya kawaida, nazo zina mafaa fulani bila shaka. Tatizo ni kwamba si sikuzote zinapokuwa na matokeo mazuri. Huenda wazazi maskini wakawa na watoto wengi lakini waje kuwaona wakifa kutokana na ugonjwa au ukosefu wa chakula kinachofaa. Au watoto wengi waliokua wanakataa kutunza wazazi wao. Nyakati nyingine wanaohitimu vyuo vya masomo ya juu wanajikuta bila kazi au wakiwa wenye huzuni. Hata wanaume na wanawake walio matajiri sana wanakuja kuona namna yalivyo kweli maneno haya ya Yesu Kristo: “Uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu vyake alivyo navyo.”​—Luka 12:15.

Zaidi ya hilo, wengi wanahangaishwa na uchafuzi unaoongezeka, ongezeko la mabohari ya kuwekea makombora ya nyukilia, kuzidi kwa ukosefu wa imara katika uhusiano wa mataifa na hali ya uchumi iliyoharibika sana, na pia maadili yanayoshuka vibaya sana. Wana wasiwasi mwingi kwamba wakati ujao wanaojitayarishia kwa uangalifu sana utavurugwa na matukio wasiyoweza kuzuia. Daktari wa akili Karl Menninger alieleza maoni ya wengi aliposema hivi:

“Ulimwengu umo katika hali ya wasiwasi na ukosefu wa utulivu ambao katika huo mambo mabaya sana yanaweza kutukia.”

Tena, mara nyingi watu wanachafua mipango yao wenyewe ya wakati ujao. Ijapokuwa ushuhuda unakuwa mwingi juu ya hatari za matumizi mabaya ya dawa za kulevya, watu wengi zaidi na zaidi wanatumia dawa za kulevya. Uchunguzi umethibitisha kwamba kuvuta sigara kunaweza kuleta kansa na magonjwa mengine yanayoelekea kuua. Hata hivyo watu wengi wanaendelea tu kuvuta sigara. Wengine wanakufa katika misiba ya magari inayotokea kwa sababu wao au mtu mwingine aliendesha gari akiwa mlevi. Lakini bado watu wanakunywa na kuendesha magari. Mara nyingi uasherati unaleta magonjwa yanayopitishwa kutoka mtu mmoja mpaka mwingine kwa njia ya ngono, lakini bado watu wengi hawaachi kuwa waasherati.

Jambo Fulani Limekosekana

Uhakika ni kwamba jambo fulani limekosekana katika njia ambayo watu wengi wanapangia wakati ujao. Hekima iliyo ya kawaida haifikirii mambo yote ya uhakika wala haitoshelezi mahitaji yote ya mwanadamu. Kwa sababu hiyo, huenda ukapendezwa kujua kwamba Biblia inataja namna mbili za hekima​—“hekima ya ulimwengu” na “hekima ya Mungu.” (1 Wakorintho 1:20, 21, NW) Ingawa kujitayarishia wakati ujao kwa njia zile za kawaida kuna ubora fulani kwa sasa, kufuata hekima iliyo ya kawaida ni kama bure tu katika kujitayarishia wakati ujao utakaodumu.

Yesu alisema: “Hekima inathibitishwa kuwa adilifu na kazi zake.” (Mathayo 11:19, NW) Basi, sababu gani usitumie dakika kadha ukifikiria “hekima ya Mungu” na kuona namna inavyoweza kuhusu maoni yako unapopangia wakati ujao?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki