Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 4/15 kur. 18-23
  • “Inabaki Wakati Kidogo”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Inabaki Wakati Kidogo”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Umebaki Wakati Mrefu Kadiri Gani?
  • Tumesonga Sana Katika “Wakati wa Mwisho”
  • Ishi kwa Kupatana na Mashauri ya Biblia
  • Fanya Kazi ya Bwana kwa Juhudi
  • Huu Ndio Wakati wa Kutenda!
  • Siku za Mwisho za Taratibu Hii Mbovu ya Mambo
    Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
  • Iweke Karibu Akilini Siku ya Yehova
    Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
  • Karibuni Kusudi la Mungu Kutimizwa
    Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?
  • Uharibifu wa Ulimwengu Uliotabiriwa Utakuja Lini?
    Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 4/15 kur. 18-23

“Inabaki Wakati Kidogo”

1. Ni kwa sababu gani wengine wanafikiri kwamba wakati wa wanadamu unakaribia kumalizika?

WAKATI wa mfumo wa mambo huu kukoma unakwisha. Sababu moja ambayo wengi wamekata maneno hivyo ni kwamba kuwapo kwenyewe kwa wanadamu kunahatirishwa. Maangamizi makubwa ya nyukilia yanaonekana yamekaribia sana leo hata kwamba inasemwa ni “dakika tatu kabla ya usiku wa manane” (yaani, maangamizi yamekaribia sana)!

2. Mwandikaji mmoja wa safu za magazeti alisema nini juu ya tisho la silaha za nyukilia?

2 Akiandika juu ya habari ya “Uvuli wa Kombora,” mwandikaji wa safu za magazeti wa Australia, Nick Brash alisema: “Kijiti cha baruti ya kupasulia miamba chenye uzito wa nusu kilo kinatosha kumlipua mtu. Na hali rundo la silaha za nyukilia leo linalingana na tani nne za baruti ya aina hiyo kwa kila mwanamume, mwanamke na mtoto duniani. Dola zaidi ya bilioni 500 zimetumiwa kwa ajili ya silaha za nyukilia na zaidi ya dola bilioni 40 zitatumiwa kwenye silaha ulimwenguni pote mwaka huu [1983]. Ni kiasi kikubwa mno cha wingi wa silaha ambazo zimerundikwa. Ni sawa na kunyunyizia mbu mikebe 10 ya [dawa ya kuua wadudu].”​—The Sun Weekend Magazine (Melbourne, Australia), Aprili 23, 1983

3. Ni nini yanayoweza kusemwa juu ya inavyoweza kuwa kukiwa vita vya nyukilia?

3 Ni vigumu kuwazia matokeo yanayoweza kuwa ya vita ya kutumia silaha za nyukilia. Licha ya kifo cha mamia ya mamilioni, utando wa miale ya nyukilia duniani pote, kuharibika kwa mazingira na viumbe na kadhalika, kungekuwako mvurugo mkubwa sana wa mambo ya kijamii, kisiasa na kiuchumi duniani pote. Kwa kweli, Dakt. Brian Martin, mtaalamu wa fizikia na uchunguzi kwenye Chuo Kikuu cha Taifa cha Australia, anakubali hivi: “Kwa maneno machache yanayojulikana si ya kutosha kuweza kutabiri kwa uhakika matokeo yote ya vita ya nyukilia duniani pote.”

4. (a) Ni kwa sababu gani tunaweza kuwa na uhakika kwamba wanadamu hawatajiangamiza katika maangamizi makubwa ya nyukilia? (b) Tunajuaje kwamba wakati wa mfumo wa mambo uliopo uko karibu kumalizika?

4 Wakati ujao unaonekana kuwa wenye kuhuzunisha sana. Lakini wanaompenda Mungu wanachangamka! Ingawa wakati wa mfumo wa mambo uliopo unakwisha, wanadamu hawatajiangamiza katika maangamizi makubwa yaliyovurugika ya silaha za nyukilia. Tunaweza kuwa na uhakika juu ya hilo, kwa maana Yehova, “Muumba na Mtengenezaji” wa dunia, “hakuiumba kuwa mvurugo, aliiumba ikaliwe na watu.” (Isaya 45:18, Byington) Bila shaka, ikiwa wanadamu wataokolewa wasijiangamize, ni lazima hatua ya mara moja ya mtu mwenye nguvu zaidi ya zile za kibinadamu ichukuliwe ili kukomesha mfumo huu, na pia wazimu wake wa silaha za nyukilia. Kwa furaha, Muumba wa Dunia-sayari na wanadamu karibuni ataharibu mfumo huu mbovu wenye kufa. Wakati wa mfumo huu ni mfupi kwa sababu ‘siku iliyo kuu ya Yehova’ imekaribia! (Sefania 1:14-18) Hata hivyo, inafariji kama nini kujua kwamba wakati wa siku hiyo ya kutozwa hesabu inayokaribia haraka sana, ‘Yehova atawahifadhi wote wampendao, na wote wasio haki atawaangamiza’!​—Zaburi 145:20.

Umebaki Wakati Mrefu Kadiri Gani?

5. Kulingana na Ufunuo 6:9, 10, wafuasi wapakwa mafuta wa Yesu walipendezwa kujua nini?

5 Bila shaka Mungu atachukua hatua juu ya maadui wake. Lakini itakuwa muda mrefu kadiri gani kabla hajakomesha mfumo mbovu wa mambo uliopo na kuleta Utaratibu Mpya wa amani na uadilifu? Huenda wewe ni shahidi wa Yehova ambaye angependa kujua jibu la ulizo hilo. Kwa habari hiyo, unahisi kama wale Wakristo wapakwa mafuta waliochinjwa wanaowakilishwa katika Ufunuo kama kwamba wakilia hivi: “Ee Mola, Mtakatifu, Mwenye kweli, hata lini kutokuhukumu, wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi?” (Ufunuo 6:9, 10) Ndiyo, kwa usemi wa mfano wapakwa mafuta hao walitaka kujua ni wakati gani Mungu angelipiza kisasi damu yao. Haishangazi kwamba Mashahidi wa Yehova wote leo wanatarajia kwa shauku sana “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi” kwenye Har–Magedoni!—Ufunuo 16:14-16.

6, 7. (a) Kuhusu wakati, Paulo alisema nini kwenye 1 Wakorintho 7:29? (b) Ni usemi gani wa Petro unaokazia uhakika wa kwamba mfumo huu utapatwa na mwisho wenye msiba?

6 Mashahidi hao wapakwa mafuta ambao damu yao ilikuwa imemwagwa kwa sababu ya uaminifu wao kwa Yehova wangepewa thawabu, kwa maana masimulizi ya Biblia yanasema: “Wakapewa kila mmoja nguo ndefu, nyeupe, wakaambiwa wastarehe bado muda mchache, hata itakapotimia hesabu ya wajoli wao na ndugu zao, watakaouawa vile vile kama wao.” (Ufunuo 6:11) Tunaweza kuwa na uhakika kwamba Mungu atachukua hatua katika wakati wake uliowekwa. Kwa kweli, maneno ya mtume Paulo katika 1 Wakorintho 7:29 yanafaa sana. Yeye aliwaambia waamini wenzake waziwazi hivi: “Inabaki wakati kidogo.”​—ZSB.

7 Si kwamba tu maneno ya Paulo yanawapa kitia-moyo watumishi wa kisasa wa Yehova bali pia yanaonyesha kwamba maisha ya Wakristo yanapaswa kukazwa juu ya kazi inayotaka hatua ya haraka ichukuliwe ambayo Mungu amewagawia kufanya. Kwa maneno hayo, mtume Petro aliandika hivi: “Mwisho wa mambo yote umekaribia.” (1 Petro 4:7) Petro alijua kwamba mfumo huu umehukumiwa mwisho wenye msiba. Unaelekea huko!

8. Uhakika wa kwamba mwisho wa mfumo huu umekaribia wapasa kuwa na matokeo gani juu ya watu wa Yehova?

8 Paulo na Petro walikazia uhakika wa kwamba huu mfumo wa mambo umehukumiwa maangamizi. Hilo ni jambo ambalo Wakristo wa kweli hawapaswi kusahau kamwe. Mwisho utakuja katika siku zetu, na ushuhuda wote unaonyesha kwamba umekaribia sana sana. Kwa hiyo, siku baada ya siku kielelezo chetu cha maisha chapasa kuonyesha usadiki huo. Zaidi ya hayo, uhakika wa kwamba tumesonga sana katika siku za mwisho-mwisho za huu mfumo wapasa kutujaza azimio la kufanya yote tuwezayo katika kazi njema na ya uharaka sana ya kutangaza habari njema tukiwa mashahidi wa Yehova waliosafishwa na wenye bidii.​—Tito 2:13, 14.

Tumesonga Sana Katika “Wakati wa Mwisho”

9. Kwa ujumla leo watu wanashughulikia nini, na je, hilo limepata kutokea hapo mbele?

9 Yesu Kristo alitabiri kwamba wakati wa kuwapo kwake kusikoonekana watu wangejishughulisha mno na mambo ya maisha. Fikira zao zingekuwa kwingine, sawa na walivyokuwa watu katika siku za Noa na za Loti. “Hivyo ndivyo itakavyokuwa siku ile atakayofunuliwa Mwana wa Adamu,” Yesu alisema, akizungumza juu ya wakati wa kuwapo kwake kusikoonekana, wakati ambapo uharibifu ungefikilizwa juu ya mfumo huu mbovu.​—Luka 17:26-30.

10, 11. Ni ushuhuda gani unaotolewa hapa kuonyesha kwamba mwisho wa mfumo huu umekaribia?

10 Fikiria pia unabii mbalimbali ulioandikwa katika Mathayo 24, Marko 13 na Luka 21. Yesu alitabiri mambo ambayo mwanadamu hawezi kuyaongoza hata kidogo​—mambo kama magonjwa ya kuambukia na matetemeko makubwa ya ardhi. Zaidi ya hayo, kumekuwako ongezeko la “kutokutii sheria” tangu 1914. Habari za leo, sana sana katika miji mikubwa, mara nyingi ni orodha ya uhalifu na ukosefu wa adili. Hayo yana maana kubwa zaidi ya takwimu za uhalifu zenye kuongezeka, kwa maana roho ya kutoheshimu vizuizi vya kisheria sasa imeenea sana, na upendo wa walio wengi hakika umepoa.​—Mathayo 24:12, NW.

11 Zaidi ya hilo, “huzuni kuu ya mataifa” sasa inaonekana wazi kwa sababu watu hawajui njia ya kusuluhisha matatizo yao yenye kuongezeka. (Luka 21:25, 26, NW) Halafu, pia, kumekuwako kupungua kwa wale wa “kizazi hiki” cha 1914, ambacho hakitapita kabla ya utimizo wa yote ambayo Yesu alitabiri yangekuwako wakati wetu. (Mathayo 24:34) Hicho ni kionyesho kingine kilicho wazi kwamba mfumo huu umekaribia mwisho wake.

12. Bila shaka ni nini ambacho ni uthibitisho mkubwa zaidi kwamba tumeingia sana katika “wakati wa mwisho”?

12 Ushuhuda mwingi zaidi ungeweza kutolewa kuthibitisha kwamba tumeingia sana katika “wakati wa mwisho.” (Danieli 12:4) Lakini bila shaka uthibitisho mkubwa zaidi kwamba tumekaribia mwisho wa mfumo huu ni kazi ya kuhubiri Ufalme ulimwenguni pote inayofanywa na Mashahidi wa Yehova. Jambo kama hilo halijapata kutokea hapo mbele. Kweli kweli, katika nchi 205 kuzunguka dunia yote mashahidi wa Yehova zaidi ya 2,840,000 wanafanya kwa bidii kazi njema ya kueneza ujumbe wenye kutia moyo kwamba Kristo amekuwa akitawala katika uwezo wa Ufalme tangu 1914. Na Yesu alitangaza kwamba habari njema hizi za Ufalme zikiisha kuhubiriwa katika dunia yote inayokaliwa na watu, ndipo “mwisho utakapokuja.”​—Mathayo 24:14.

Ishi kwa Kupatana na Mashauri ya Biblia

13. Tunapaswa kuwa na maoni gani juu ya usemi wa Paulo kwamba “wale walio na wake na wawe kama hawana”?

13 Kwa wazi ikiwa wakati uliobaki ni mchache na mwisho umekaribia, watu wa Yehova wanahitaji kuishi kwa kupatana na mashauri ya Biblia, kama vile maneno ya mtume Paulo katika 1 Wakorintho 7:29-31. Baada tu ya kusema kwamba “inabaki wakati kidogo” (ZSB), yeye aliandika hivi (UV): “Tokea sasa wale walio na wake na wawe kama hawana.” Hapa mtume huyo hakuwa akimaanisha kwamba mume Mkristo anapaswa kumtupa mkeye. Hapana, bali kwamba mwanamume ajapoangalia kwa uaminifu madaraka yake ya ndoa, anapaswa kuweka kwanza katika moyo na akili uhusiano wake na Mungu, ahakikishe kwamba ndoa yake inaelekeza kwenye jambo hilo.

14. Kulingana na 1 Wakorintho 7:30, watangazaji wa Ufalme wanapaswa kuonaje matatizo ya kibinafsi, na kadhalika?

14 Katika mstari wa 30, Paulo aliendelea kusema (UV): “Wale waliao [wawe] kama hawalii; na wale wafurahio [wawe] kama hawafurahi; na wale wanunuao, [wawe] kama hawana kitu.” Hiyo ina maana gani? Maneno hayo yaliyoongozwa na roho ya Mungu yanakazia uhakika wa kwamba mambo ya kibinafsi, yawe yanahusu mali, huzuni au furaha, siyo mambo yaliyo makubwa kwa wahudumu wa Ufalme. “Wakati na tukio lisilotazamiwa” linatupata sisi sote na mambo hayo yanaweza kubadili hali zetu ghafula. (Mhubiri 9:11, NW; Yakobo 4:14) Kwa hiyo halingekuwa jambo la hekima kujishughulisha mno na huzuni, magumu na matatizo mbalimbali ya kibinafsi hata kwamba mahangaiko hayo yazuie sana huduma yetu, pendeleo letu la utendaji wa kuhubiri habari njema za Ufalme.

15. Kwa sababu gani ungekuwa ujinga mkubwa mno kwa Mkristo kushughulikia mno mambo ya kibinafsi yanayohusu mali, na kadhalika?

15 Katika 1 Wakorintho 7:31 (NW), mtume Paulo anasema: “Wale wanaotumia ulimwengu [wawe] kama wale wasioutumia sana.” Kwa sababu watu wa ulimwengu hawana tumaini lenye msingi wa Biblia, fikira zao zote ziko juu ya mahitaji yao ya kila siku na tamaa zao. Mara nyingi wanatafuta kuvutia wengine kwa mali zao. Lakini, kama mtume Yohana alivyoonyesha wazi, “kujionyesha kwa mtu mali yake” ni wonyesho mmoja wa “kila kitu kilichomo katika ulimwengu” ambacho “hakitokani na Baba, bali chatokana na ulimwengu.” Na Yohana anatuhakikishia kwamba “ulimwengu unapita na ndivyo na tamaa yake, lakini yeye anayefanya mapenzi ya Mungu anadumu milele.” (1 Yohana 2:16, 17, NW) Kwa hiyo, ungekuwa ni ujinga mkubwa kwa Mkristo ye yote, mwenye taraja la wakati ujao wa milele mbele yake, kushughulikia mno mambo ya kibinafsi hata akose wakati kwa ajili ya faida za Ufalme. (Mathayo 6:25-32; linganisha Wafilipi 2:19-22; 2 Timotheo 4:10.) Ingawa si vibaya kufurahia mali zenye faida na hata kufurahia anasa fulani zenye kujenga, tusiruhusu kamwe mambo hayo yawe jambo kuu maishani mwetu.​—Luka 12:15.

16. Mara nyingi watu wa ulimwengu wanakuwa na nia na miradi gani, lakini kwa watumishi wa Yehova ni nini kinachopaswa kuwa chenye umaana mkubwa zaidi?

16 Ni kawaida ya watu wa kilimwengu, au wale wenye kukosa hali ya kiroho, kulalamika juu ya hali yao ya maisha. (Linganisha Yuda 16.) Ikiwa ni wagonjwa-wagonjwa, huenda sikuzote wakawa wanalalamika wanaumwa. Hali moja na hiyo, maskini huenda wakalalamika kwa sababu wao si matajiri. Mambo hayo kama afya njema na utajiri mwingi huenda yakawa miradi yenye kuwavuta kabisa maishani mwao! Wanang’ang’ana kuifikia, na wakishindwa huenda wakashuka moyo sana. Lakini kwa watu wa Yehova walio wakfu “utumishi mtakatifu” ndio wa maana kubwa zaidi. (Warumi 12:1, 2, NW) Ni kweli ingawa sisi ni watumishi wa Yehova, tuna matatizo ya kukabili. Hata hivyo matatizo hayo hayatufanyi tuwe wanung’unikaji, walalamikaji juu ya fungu letu maishani. Tuna kazi ya kufanywa tuliyopewa na Mungu, na utendaji huo uliobarikiwa ndio tunaokazia fikira kwanza. Hakika, tunafurahi kwa sababu tunaweka faida za Ufalme kwanza maishani.​—Mathayo 6:33.

17. Kwa habari ya vinavyoweza kuwa vikengeuo, watu wa Yehova hawapaswi kuruhusu nini kamwe?

17 Basi, ni nini mwendo wa hekima kwa watumishi wa Yehova Tunaweza kutumia mambo fulani na utumishi fulani mbalimbali ambao ulimwengu unatoa, lakini tusiruhusu kamwe vikengeuo viondoshe fikira zetu kwa utumishi wa Mungu. (Luka 21:34-36) Kumbuka kwamba hakuna cho chote katika mfumo wa sasa kilicho cha kudumu. Kubadilika-badilika kwao kwenyewe kwaweza kuwa chanzo cha kuvuta fikira kando. Ndiyo, ni kama Paulo alivyosema, “Tamasha ya ulimwengu huu inabadilika.” (1 Wakorintho 7:31, NW) Lakini hatupaswi kamwe kuruhusu hilo liondoe fikira zetu kutoka kwa utumishi wa Yehova.

Fanya Kazi ya Bwana kwa Juhudi

18. (a) Kwa kuwa tumekuwa katika “wakati wa mwisho” tangu 1914, tunapaswa kujaza maisha zetu kazi gani? (b) Tukijishughulisha sana katika kazi ya Bwana, inaelekea itakuwaje kwa matatizo ya maisha?

18 Tukiwa na ufahamu wa kiroho, tunautambua ushuhuda wenye nguvu kwamba tumekuwa katika “wakati wa mwisho” tangu 1914. Basi, kwa hakika, hatutaki kuutumia ulimwengu sana kama kwamba tungekuwa tunakosa jambo tusipofanya hivyo. Badala yake, na tujaze maisha zetu “kazi ya Bwana.” Tunapaswa ‘kuwa na mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana, tukijua kwamba kazi yetu yenye bidii kuhusiana na Bwana si ya bure.’ (1 Wakorintho 15:58, NW) Kwa hiyo shughulika mno na kuhubiri na kufundisha kweli za Ufalme. Halafu inaelekea itakuwaje kwa matatizo ya maisha? Yataelekea kurudi nyuma na kuwa yasiyo na maana sana, yasiyotaabisha sana!

19. Maana yake nini ‘kusubiri mpaka mwisho’?

19 Alipokuwa akitoa unabii wake mkuu kuhusu siku za mwisho za mfumo huu, Yesu alisema kwamba wafuasi wake wangekuwa ‘wakichukiwa’ kwa ajili ya jina lake. “Lakini,” akaongeza, “mwenye kusaburi hata mwisho, ndiye atakayeokoka.” (Marko 13:10-13) Kwa sisi tukiwa watu mmoja mmoja waliojiweka wakfu kwa Yehova, “mwisho” waweza kuwa ama “umalizio wa mfumo wa mambo” ama kifo chetu wenyewe, pengine baada ya kuteseka mikononi mwa watesi. (Mathayo 24:3) Kwa vyo vyote, tuna wakati wenye kipimo wa kufanya kazi ya Bwana. Basi, je, hatupaswi kuwa wenye juhudi na bidii katika kutangaza ujumbe wa Ufalme? Bila shaka ndiyo!

Huu Ndio Wakati wa Kutenda!

20. Waisraeli waliofunguliwa kutoka utumwa wa Babuloni waliwezaje kuonyesha kuhangaika kwao ibada ya Yehova?

20 Wahamishwa Wayahudi walipofunguliwa kutoka utumwa wa Babuloni katika karne ya sita K.W.K., walilazimika kufanya uamuzi. Je! wangerudi katika nchi ya kwao na kurudisha ibada ya Yehova huko, au je, wangebaki katika Babuloni? Kwa lasima Waisraeli waliokaa katika mji huo hawakuwa waovu, kwa maana Danieli mzee alikuwa mmoja wao. Wangeweza kuwapa mabaki wenye kurudi utegemezo wa kimwili na kuwatia moyo na pia wangeweza kupeleka “vitu vitolewavyo kwa hiari” kwa ajili ya nyumba ya Yehova katika Yerusalemu. (Ezra 1:2-4) Kwa njia hiyo wangeweza kusaidia kusogeza mbele ibada ya kweli. Waabudu wote wa Yehova wangeweza kuwa wenye furaha kama nini wakati mabaki hao walipofunga safari ya kwenda kwenye nchi ya kwao, wakiwa wamebeba vyombo vitakatifu kwa ajili ya matumizi kwenye hekalu la Yehova! Na wachukuaji wa vyombo vya patakatifu walipaswa kuhakikisha kwamba walikuwa wamejisafisha wenyewe na uchafu wo wote wa kidini na kiadili wa Babuloni.​—Isaya 52:11.

21. (a) Ni maswali gani yanayotokezwa ili uyafikirie? (b) Kwa kuwa “inabaki wakati kidogo,” ikoje kuhusu nafasi za kueneza habari njema?

21 Je! wewe unahangaikia ibada ya kweli kama Waisraeli hao waliofunguliwa karne 25 hivi zilizopita? Je! wewe unaliona kuwa pendeleo lenye furaha kutoa utumishi mtakatifu kwa Yehova ukiwa sehemu ya tengenezo lililosafishwa na lenye bidii ambalo linaheshimu jina lake takatifu? Je! wewe unatambua ushuhuda mwingi mbalimbali kwamba tunaishi ndani sana katika “wakati wa mwisho”? Ukijibu maswali hayo ndiyo, basi hakikisha kwamba unachukua hatua inayofaa sasa hivi. Kaza fikira juu ya kuweka faida za Ufalme kwanza maishani mwako. Kwa kuwa “inabaki wakati kidogo,” nafasi zetu za wakati huu za kueneza habari njema zinakuwa zenye umaana ulio mkubwa zaidi na zaidi. Wabarikiwa ni wote wanaotegemeza maisha zao juu ya Ufalme wakiwa mashahidi wa Yehova walio washikamanifu wenye mengi ya kufanya katika kuhubiri habari njema maadamu kungali wakati!—Kutoka w11/15/84.

Wewe Ungetoa Majibu Gani?

◻ Ni kwa sababu gani wakati wa huu mfumo wa mambo unamalizika?

◻ Tunajuaje kwamba tumeingia ndani kabisa katika “wakati wa mwisho”?

◻ Tukiendelea kuwa wenye shughuli sana katika kazi ya Bwana, inaelekea itakuwaje kwa matatizo yetu?

◻ Kwa kuwa mwisho uko karibu, tunapaswa kutegemeza maisha zetu juu ya nini?

[Picha katika ukurasa wa 21]

Matatizo ya maisha na yasiondoshe fikira zetu kutoka kazi ya kuuhubiri Ufalme

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki