Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • pr seh. ya 7 kur. 25-29
  • Karibuni Kusudi la Mungu Kutimizwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Karibuni Kusudi la Mungu Kutimizwa
  • Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Hukumu za Mungu
  • Utawala wa Mungu Kutoka Mbinguni
  • Tuko Karibu Kadiri Gani?
  • Kuhubiri Habari Njema
  • Jinsi Sisi Tujuavyo Kwamba Tumo Katika “Siku za Mwisho”
    Je, Kweli Mungu Anatujali?
  • Uharibifu wa Ulimwengu Uliotabiriwa Utakuja Lini?
    Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?
  • Je, Tunaishi Katika “Siku za Mwisho”?
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Ufalme wa Mungu Huanza Kutawala Katikati ya Adui Zake
    Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
Pata Habari Zaidi
Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?
pr seh. ya 7 kur. 25-29

Sehemu ya 7

Karibuni Kusudi la Mungu Kutimizwa

1 Ingawa kwa maoni ya kibinadamu, ni kwa muda mrefu kwamba Mungu ameruhusu kutokamilika na kuteseka kuendelee, yeye hataruhusu hali mbaya ziendelee kwa muda usio dhahiri. Biblia hutuambia kwamba Mungu ana kipindi cha wakati hususa cha kuruhusu mambo hayo yatukie.

2 “Kwa kila jambo kuna majira yake.” (Mhubiri 3:1) Wakati uliowekwa na Mungu wa kuruhusu uovu na kuteseka umalizikapo, ndipo atakapoingilia mambo ya kibinadamu. Yeye atakomesha uovu na kuteseka na atatimiza kusudi lake la awali la kuwa na dunia iliyojaa familia kamilifu ya kibinadamu yenye furaha inayoonea shangwe amani na usalama kamili wa kiuchumi katika mazingira ya Paradiso.

Hukumu za Mungu

3 Angalia unabii mchache kati ya unabii mwingi wa Biblia unaosema juu ya yale yatakayomaanishwa kwa familia ya kibinadamu wakati Mungu atakapoingilia mambo, yaani, matokeo ya hukumu zake:

4 “Maana wanyofu watakaa katika nchi, na wakamilifu watadumu ndani yake. Bali waovu watatengwa na nchi, nao wafanyao hila watang’olewa.”—Mithali 2:21, 22.

5 “Maana watenda mabaya wataharibiwa, bali wamngojao BWANA [Yehova, NW] ndio watakaoirithi nchi. Maana bado kitambo kidogo asiye haki hatakuwapo . . . Bali wenye upole watairithi nchi, watajifurahisha kwa wingi wa amani.”—Zaburi 37:9-11.

6 “Wewe umngoje BWANA [Tumaini katika Yehova, NW], uishike njia yake, naye atakutukuza uirithi nchi, wasio haki watakapoharibiwa utawaona. Umwangalie sana mtu mkamilifu, umtazame mtu mnyofu, maana mwisho wake mtu huyo ni amani. Wakosaji wataangamizwa pamoja, wasio haki mwisho wao wataharibiwa.”—Zaburi 37:34, 37, 38.

7 Kwa hiyo, kwa kufikiria wakati ujao mzuri ajabu ambao utawajia wale wanaotambua haki ya Muumba ya kututawala, sisi tunahimizwa hivi: “Moyo wako uzishike amri zangu. Maana zitakuongezea wingi wa siku, na miaka ya uzima, na amani.” Kwa kweli, uzima wa milele utaongezwa kwa wale wanaochagua kufanya mapenzi ya Mungu! Hivyo, Neno la Mungu latushauri hivi: “Mtumaini BWANA [Yehova, NW] kwa moyo wako wote, wala usizitegemee akili zako mwenyewe; katika njia zako zote mkiri yeye, naye atayanyosha mapito yako.”—Mithali 3:1, 2, 5, 6.

Utawala wa Mungu Kutoka Mbinguni

8 Mungu atatimiza usafishaji huu wa dunia kupitia serikali bora zaidi ambayo ainabinadamu ingeweza kuwa nayo. Hiyo ni serikali yenye hekima ya kimbingu kwa sababu inatawala kutoka mbinguni chini ya mwelekezo wa Mungu. Na Ufalme huo wa kimbingu utaondoa aina zote za utawala wa kibinadamu kutoka duniani. Wanadamu hawatakuwa tena kamwe na chaguo la kujaribu kujitawala bila kumtegemea Mungu.

9 Kuhusiana na hilo, unabii kwenye Danieli 2:44 husema: “Na katika siku za wafalme hao [serikali za kisasa] Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme [mbinguni] ambao hautaangamizwa milele, wala watu wengine hawataachiwa enzi yake [wanadamu hawataruhusiwa tena kamwe kutawala bila kumtegemea Mungu]; bali utavunja falme hizi zote [zilizoko sasa] vipande vipande na kuziharibu, nao utasimama milele na milele.”—Ona pia Ufunuo 19:11-21; 20:4-6.

10 Hivyo, ainabinadamu haitakuwa tena kamwe na namna za utawala zenye ufisadi, kwa kuwa baada ya Mungu kuleta mfumo huu kwenye mwisho wao, utawala wa wanadamu usiomtegemea hautakuwako tena kamwe. Na Ufalme unaotawala kutoka mbinguni hautafisidiwa, kwa kuwa Mungu ndiye Mwanzilishi na Mhifadhi wao. Badala ya hivyo, huo utatenda kazi kwa manufaa bora za raia zao za kibinadamu. Hapo ndipo mapenzi ya Mungu yatakapofanywa kotekote duniani kama vile yalivyo mbinguni. Hiyo ndiyo sababu Yesu angeweza kuwafunza wanafunzi wake kusali kwa Mungu hivi: “Ufalme wako uje, Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.”—Mathayo 6:9, 10.

Tuko Karibu Kadiri Gani?

11 Tuko karibu kadiri gani kwenye mwisho wa mfumo huu wa mambo usioridhisha na mwanzo wa ulimwengu mpya wa Mungu? Unabii wa Biblia hutupa sisi jibu waziwazi. Mathalani, Yesu mwenyewe alitabiri mambo ambayo tungetafuta ili tuweze kujua tumefikia wapi kuhusiana na “mwisho wa mfumo wa mambo” (NW), kama vile Biblia isemavyo. Hayo yamerekodiwa katika Mathayo sura 24 na 25, Marko 13, na Luka 21. Pia, kama ilivyorekodiwa katika 2 Timotheo sura ya 3, mtume Paulo alitabiri kwamba kungekuwa na kipindi cha wakati kiitwacho “siku za mwisho” wakati matukio mbalimbali yangethibitisha zaidi mahali tulipo katika mkondo wa wakati.

12 Yesu alisema kwamba kipindi hiki cha wakati kingeanza kwa matukio haya: “Taifa litaondoka kupigana na taifa, na ufalme kupigana na ufalme; kutakuwa na njaa, na matetemeko ya nchi mahali mahali.” (Mathayo 24:7) Luka 21:11 huonyesha kwamba yeye pia alitaja kungekuwa na “tauni mahali mahali.” Na alionya, pia, juu ya “kuongezeka maasi.”—Mathayo 24:12.

13 Mtume Paulo alitabiri hivi: “Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi, wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema, wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu; wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake . . . Watu wabaya na wadanganyaji wataendelea, na kuzidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika.”—2 Timotheo 3:1-5, 13.

14 Je! mambo hayo ambayo Yesu na Paulo walitabiri yametukia katika wakati wetu? Ndiyo, hakika yametukia. Vita ya Ulimwengu 1 ndiyo iliyokuwa vita mbaya zaidi kufikia wakati huo. Hiyo ndiyo iliyokuwa vita ya ulimwengu ya kwanza na ilitia alama wakati wa badiliko kubwa katika historia ya kisasa. Pamoja na vita hiyo ukaja upungufu mwingi wa chakula, magonjwa ya kuambukiza, na majanga mengineyo. Matukio hayo kuanzia 1914 na kuendelea yalikuwa, kama vile Yesu alivyosema, “mwanzo wa utungu.” (Mathayo 24:8) Yalianzisha kipindi cha wakati kilichotabiriwa kiitwacho “siku za mwisho,” mwanzo wa kizazi cha mwisho wakati ambapo Mungu angeruhusu uovu na kuteseka.

15 Inaelekea kwamba unayajua sana matukio ya karne ya 20. Unajua juu ya matata ambayo yametokea. Watu milioni 100 hivi wameuawa katika vita. Mamia ya mamilioni wengine wamekufa kwa njaa na magonjwa. Matetemeko ya ardhi yameua watu wasiohesabika. Kutojali uhai na mali kwaendelea kuongezeka. Hofu ya uhalifu imekuja kuwa sehemu ya maisha ya kila siku. Viwango vya kiadili vimepuuzwa. Ongezeko la ghafula la watu limeleta matatizo ambayo hayatatuliwi. Uchafuzi unaharibu ubora wa uhai na hata unauhatarisha. Kwa kweli, tumekuwa katika siku za mwisho tangu 1914 na tunakaribia upeo wa unabii mwingi wa Biblia unaotia ndani wakati wetu.

16 Siku hizo za mwisho zingekuwa na urefu gani? Yesu alisema hivi kuhusu kizazi ambacho kingepatwa na “mwanzo wa utungu” kuanzia 1914 na kuendelea: “Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia.” (Mathayo 24:8, 34-36) Hivyo, sehemu zote za siku za mwisho lazima zitukie katika wakati wa kizazi kimoja, kizazi cha 1914. Kwa hiyo watu fulani waliokuwa hai katika 1914 bado watakuwa hai wakati mfumo huu ufikiapo mwisho wao. Kizazi hicho cha watu sasa ni kizee sana, ikionyesha kwamba hakuna wakati mwingi unaobaki kabla Mungu hajakomesha mfumo huu wa mambo wa sasa.

17 Unabii mwingine unaoonyesha kwamba mwisho wa mfumo huu ni karibu sana ulitolewa na mtume Paulo, aliyetabiri hivi: “Siku ya Bwana [Yehova, NW] yaja kama vile mwivi ajavyo usiku. Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula . . . , wala hakika hawataokolewa.”—1 Wathesalonike 5:2, 3; ona pia Luka 21:34, 35.

18 Leo Vita Baridi imekwisha, na huenda vita ya kimataifa isiwe tena tisho kubwa. Kwa hiyo huenda mataifa yakahisi kwamba yanakaribia sana kupata utaratibu wa ulimwengu mpya. Lakini wakati watakapohisi kwamba jitihada zao zinafanikiwa, itamaanisha kinyume cha yale wanayofikiri, kwa kuwa hicho kitakuwa ndicho kionyo cha mwisho kabisa kwamba kuharibiwa kwa mfumo huu na Mungu ni karibu sana. Kumbuka, mashauriano na mapatano ya kisiasa hayafanyizi mabadiliko halisi yoyote katika watu. Hayo hayafanyi watu wapendane. Na viongozi wa ulimwengu hawakomeshi uhalifu, wala hawakomeshi magonjwa na kifo. Kwa hiyo usiweke tumaini lako katika maendeleo yoyote ya amani na usalama wa kibinadamu na kufikiri kwamba ulimwengu huu unaelekea kusuluhisha matatizo yao. (Zaburi 146:3) Kilio hicho kwa kweli kitamaanisha kwamba ulimwengu huu u karibu sana kutoweka kabisa.

Kuhubiri Habari Njema

19 Unabii mwingine unaoonyesha kwamba tumekuwa katika siku za mwisho tangu 1914 ni ule ambao Yesu alitoa: “Sharti Habari Njema ihubiriwe kwanza katika mataifa yote.” (Marko 13:10, Zaire Swahili Bible) Au, kama vile Mathayo 24:14 husema: “Habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote [dunia yote inayokaliwa, NW], kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja.”

20 Leo kuliko wakati mwingine wowote wa historia, habari njema kuhusu mwisho wa ulimwengu huu na za kuja kwa ulimwengu mpya wa Paradiso chini ya Ufalme wa Mungu zinahubiriwa duniani kote. Zinahubiriwa na nani? Na mamilioni ya Mashahidi wa Yehova. Wao wanahubiri katika kila nchi duniani.

21 Kuongezea kuhubiri kwao juu ya Ufalme wa Mungu, Mashahidi wa Yehova wanatenda katika njia inayowatambulisha kuwa wafuasi wa kweli wa Kristo, kwa kuwa yeye alijulisha hivi: “Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi.” Hivyo, Mashahidi wa Yehova wameunganishwa katika udugu wa tufeni pote kwa kifungo cha upendo kisichoweza kuvunjwa.—Yohana 13:35; ona pia Isaya 2:2-4; Wakolosai 3:14; Yohana 15:12-14; 1 Yohana 3:10-12; 4:20, 21; Ufunuo 7:9, 10.

22 Mashahidi wa Yehova huamini yale ambayo Biblia husema: “Mungu hana upendeleo; bali katika kila taifa mtu amchaye na kutenda haki hukubaliwa na yeye.” (Matendo 10:34, 35) Wao huwaona Mashahidi wenzao katika nchi zote kuwa ndugu na dada za kiroho, bila kujali kabila au rangi. (Mathayo 23:8) Na uhakika wa kwamba udugu huo wa tufeni pote upo katika ulimwengu leo waongeza uthibitisho kwamba kusudi la Mungu litatimizwa karibuni.

[Maswali ya Funzo]

1, 2. Kwa nini tunaweza kuwa na uhakika kwamba Mungu atachukua hatua ya kukomesha uovu na kuteseka?

3, 4. Kitabu cha Mithali kinaelezaje matokeo ya Mungu kuingilia mambo?

5, 6. Zaburi 37 inaonyeshaje kile kitakachotukia wakati Mungu atakapoingilia mambo?

7. Ni shauri gani lifaalo ambalo Neno la Mungu latupatia?

8, 9. Mungu ataisafisha dunia hii kwa njia gani?

10. Kwa nini tunaweza kuwa na uhakika kwamba chini ya Ufalme wa kimbingu wa Mungu, hakutakuwa tena kamwe na ufisadi katika utawala?

11. Ni wapi katika Biblia tunapopata unabii mwingi ambao utatusaidia tujue ni kadiri gani tuko karibu na mwisho wa mfumo huu?

12, 13. Yesu na Paulo walisema nini kuhusu wakati wa mwisho?

14, 15. Matukio ya karne ya 20 yanathibitishaje kwamba kwa kweli tumekuwa katika siku za mwisho?

16. Siku za mwisho zinatia ndani kipindi cha wakati chenye urefu gani?

17, 18. Ni unabii gani unaoonyesha tuko karibu sana na mwisho wa ulimwengu huu?

19, 20. Ni unabii gani unaohusu kuhubiri katika siku za mwisho tunaoona ukitimizwa?

21, 22. Ni nini, hasa, hutambulisha Mashahidi wa Yehova kuwa Wakristo wa kweli?

[Picha katika ukurasa wa 26]

Ufalme mkamilifu wa kimbinguwa Mungu ndio utakaokuwa utawala pekee wa ainabinadamu katika ulimwengu mpya

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki