Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • tr sura 10 kur. 82-93
  • Ufalme wa Mungu Huanza Kutawala Katikati ya Adui Zake

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ufalme wa Mungu Huanza Kutawala Katikati ya Adui Zake
  • Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • UTIMIZO WA “ISHARA”
  • MWAKA WA 1914 NI MWAKA ULIOTIWA ALAMA
  • Uharibifu wa Ulimwengu Uliotabiriwa Utakuja Lini?
    Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?
  • Ambayo 1914 Ungemaanisha Kwako Wewe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • “Mwisho wa Ulimwengu” Ni Karibu!
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Zile “Siku za Mwisho” na Ule Ufalme
    “Ufalme Wako Uje”
Pata Habari Zaidi
Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
tr sura 10 kur. 82-93

Sura ya 10

Ufalme wa Mungu Huanza Kutawala Katikati ya Adui Zake

1. (a) Watu wenye imani wametazamia nini kwa muda mrefu? (b) Je! Mungu hakuwa Mfalme sikuzote?

KWA maelfu ya miaka watu wenye imani wameishi kwa kutazamia sana siku wakati ufalme wa Mungu ungeanza utawala wake. Wao wameona sana haja kwa Mungu kuongoza mambo ya dunia. Je! hii ina maana kwamba Mungu amekuwa siye Mfalme wakati wa karne zilizopita? La, kwa maana sikuzote Yehova amekuwa ni Mtawala Mkuu kupita wote wa ulimwengu wote. (Yeremia 10:10) Lakini hapa duniani pametokezwa mwito wa kuthibitisha haki ya utawala wake. Na, kama tulivyokwisha kuona, kwa sababu nzuri na kwa sababu ya kusudi la upendo, Mungu ameziruhusu serikali za kibinadamu chini ya uongozi wa Shetani kutawala kwa kipindi cha wakati uliowekwa.

2. Ufalme wa Mungu ni nini, na ni kwa nani yeye hutoa mamlaka ya kutawala?

2 Walakini, Yehova aliahidi kwamba mwishoni mwa wakati huo yeye angechukua kitendo juu ya waasi wote na wapinzani wa utawala wake. Angeileta kabisa dunia na wakaaji wake chini ya utawala wake tena. Jinsi gani? Kwa njia ya Ufalme, serikali mpya ya kimbinguni chini ya Mwanawe Kristo Yesu. Kwa hiyo kutawala kwa ufalme huo humaanisha kwamba mabadiliko makubwa yako karibu. Humaanisha kwamba Yehova Mungu amempa Mwanawe “mamlaka, na utukufu, na ufalme, ili watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, wamtumikie.”—Danieli 7:13, 14.

3. Kwa nini huenda watu wengine kwanza wakaona kuwa jambo geni kufikiri kwamba ufalme wa Mungu umekwisha kuanza kutawala?

3 Tukio hilo limekwisha kutukia mbinguni. Mamlaka ya Ufalme imekwisha kupewa kwa Mwana wa Yehova. Je! hilo linaonekana jambo geni kwako! Huenda ikawa, hasa kwa sababu ya hali za kutisha zinazowatesa wanadamu. Lakini, kweli, ni kwa sababu ya hali hizi hizi kwamba twaweza kujua hakika kwamha hii ni kweli. Kwa nini iko hivi?

4. (a) Kwa nini viumbe vyote havishangilii ufalme wa Mungu? (b) Hivyo ni kitu gani kilichotabiriwa kwamba Mungu angesema kwa Mwanawe wakati wa kumpa mamlaka kutenda kama Mfalme?

4 Iko hivyo kwa sababu kuanza kutawala kwa ufalme wa Yehova hakushangiliwi na viumbe vyote. Si kila mtu anataka kuishi chini ya serikali ambayo husema kwa nguvu juu ya haki. (Luka 19:11-14) Kwa sababu hii, zamani Yehova aliandika katika Neno lake kwamba wakati yeye ‘anaanza kumiliki’ kama mfalme kuelekea dunia ‘mataifa wangekasirika.’ (Ufunuo 11:17, 18) Yeye alitabiri kwamba, wakati wa kumwezesha Mwanawe kutenda, ingekuwa lazima kwake kusema: “Nenda ukishinda katikati ya adui zako.”—Zaburi 110:2, NW.

5. Ni tendo gani lililopaswa kutukia mbinguni wakati huo, na pamoja na matokeo gani kwa dunia?

5 Ndipo Kristo Yesu angemfukuza Shetani kutoka mbinguni, kiti cha serikali, akimtupa chini karibu na dunia, katika kutayarisha kumzuia kufanya kazi. Wakati huo tangazo la maana lingefanywa katika mbingu: “Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake.” Lakini kwa dunia, nini? “Ole . . . ! kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu.” (Ufunuo 12:5, 7-10, 12) Utawala kamili wa dunia kwa ufalme wa Mungu lazima ufuate upesi! Walakini, mwanzo wa utawala kwa ufalme wa Mungu hauna maana ya amani na haki ya mara hiyo duniani. Kwa kinyume, huleta muda wa taabu isiyo na kifani kwa wakaaji wa dunia.

6. (a) Ni swali gani ambalo wafuasi wa Yesu walimwuliza juu ya kuwapo kwake mara ya pili? (b) Kwa nini “ishara” ionekanayo ingekuwa ya lazima? (c) Ushuhuda huu uonekanao ungekuwa uthibitisho wa nini kuhusu taratibu hii ya mambo?

6 Kwa kujua hili, tunaweza kuelewa maana ya jambo ambalo Yesu aliwaambia wafuasi wake juu ya kuwapo kwake mara ya pili. Walikuwa wamemwuliza hivi: “Tuambie, ni lini mambo haya yatakapokuwa, na ni nini itakayokuwa ishara ya kuwapo kwako na ya mwisho wa taratibu ya mambo?” (Mathayo 24:3, NW) Ndipo Yesu aliposimulia, kwa faida yao na kwa faida yetu, mambo ambayo yangetukia duniani wakati yeye angeanza kutawala mbinguni. Katika njia hii, ijapokuwa matukio mbinguni yangekuwa yasiyoonekana kwa macho ya kibinadamu, ungekuwapo uthibitisho uonekanao wa kwamba Kristo hatimaye aliketi penye kiti cha enzi, akitenda kama mfalme. Ungekuwa uthibitisho wa kwamba taratibu mbovu ya mambo ambayo imewadhulumu wanadamu kwa karne nyingi ilikuwa imeingia katika “siku za mwisho” zake. (2 Timotheo 3:1) Ijapokuwa ilitabiriwa kwamba wangekuwapo wenye dhihaka ambao wangejaribu kudharau mambo ya hakika, lakini ushuhuda ungekuwa wazi.—2 Petro 3:3, 4.

7. (a) Je! kuna tukio fulani moja tu, ambalo lingekuwa uthibitisho wa kwamba “mwisho” u karibu? (b) Jinsi gani tunajua wakati kiangazi ki karibu? Hivyo jinsi gani tuwezavyo kujua wakati Ufalme umeanza utawala wake?

7 Wakati tuangaliapo ushuhuda pamoja, ni muhimu kujua kwamba Yesu hakusema kwamba tukio moja tu, kama vile tisho la vita au tetemeko la dunia la kutisha, ndilo lingekuwa uthibitisho wa kwamba “mwisho” ulikuwa karibu. (Mathayo 24:6) Bali, yeye alisema hivi: “Uangalieni mtini na miti mingine yote: Wakati inapokwisha kuchipuka, kwa kuitazama mnajua ninyi wenyewe kwamba sasa kiangazi kiko karibu. Katika njia hii ninyi pia, wakati mnapoyaona haya yote yakitukia, mjue kwamba ufalme wa Mungu u karibu.” (Luka 21:29-31, NW) Tukiuona mti mmoja unatoa majani yake katikati ya kipupwe kwa sababu hali ya hewa ni yenye joto kwa siku chache, hatufikiri kwamba kiangazi kimekuja, sivyo? Lakini tuonapo miti yote inachanua na siku zinazidi kuwa ndefu zaidi tunajua kwamba kiangazi kitakuwa karibu. Hali kadhalika, wakati mambo yote ambayo Yesu alisimulia yanapotukia, twaweza kujua kwa hakika kwamba Kristo yupo penye kiti chake cha enzi cha kimbinguni na ya kwamba ufalme wake, kweli, umeanza kutawala kwa utendaji. Jambo hilo litukiapo, ukombozi u karibu!

UTIMIZO WA “ISHARA”

8. (a) Kama ilivyoandikwa katika Mathayo 24:7, ni nini Yesu alisema ingeonyesha kuwapo kwake mara ya pili? (b) Kwa nini vita iliyoanza katika mwaka wa 1914 hupatana na maelezo yake?

8 Hasa ni kitu gani Yesu alionyesha kama kikionyesha kuwapo kwake mara ya pili na “mwisho wa taratibu ya mambo”? Yeye alisema: “Taifa litainuka juu ya taifa na ufalme juu ya ufalme, na kutakuwapo upungufu wa chakula na matetemeko ya dunia hapa na hapa.” (Mathayo 24:7, NW) Hapa Yesu hutuambia kutazamia aina mpya ya vita—vita ya jumla! (Vita ya ulimwengu ambayo katika hiyo silaha zote zipatikanazo, vifaa na watu hutumiwa) Vita iliyoanza katika mwaka wa 1914 hupatana na maelezo yake. Majeshi hayakupigana katika viwanja vya mapigano tu; idadi za raia ambao si askari zilitengenezwa pia kutoa msaada kamili kwa vita. Kama Yesu alivyotabiri, mataifa mazima na falme nzima zilikuwa zikipigana juu ya mmoja na mwenzake. Kwa mara ya kwanza katika historia ulimwengu mzima ukawa katika vita. Kwa hiyo inaitwa “Vita ya Ulimwengu ya Kwanza.” Kwa habari yake kitabu World War I kilisema:

“Katika eneo lake, jeuri yake, na zaidi, katika ujumla wake, ilisimamisha kifani. Vita ya Kwanza ya Ulimwengu iliingiza karne ya Vita ya Jumla—katika maana kamili ya neno—ya vita ya dunia yote.

“Vita ya mwaka wa 1914-1918 ilitumia zaidi ya vifaa vipatikanavyo vya wapiganaji zaidi sana na ilienea sehemu kubwa zaidi ya dunia, kuliko vita nyingine yo yote katika historia. Kulikuwako mataifa zaidi yaliyo-tiwa ndani yake. Uuaji ulikuwa mkubwa zaidi na bila kupambanua.”a

Kitabu The World Book Encyclopedia kiliandika kwamba hesabu ya askari jeshi waliouawa na kujeruhiwa ilikuwa zaidi ya 37,000,000, na kikaongeza:

Hesabu ya vifo vya raia ambao si askari katika maeneo yenye vita halisi ilikuwa jumla yapata 5,000,000. Sababu za karibu 80 kwa kila 100 ya vifo hivi vya raia ambao si askari zilikuwa njaa kali, maradhi, na kuachwa nje kwenye hatari. Tauni, ambayo watu wengine walilaumu kuwa imetokana na vita, ilileta makumi ya mamilioni ya vifo vingine.”b

Hii ilikuwa tu kama Yesu alivyotabiri. Yakiwekwa pamoja, mambo haya ya hakika huonyesha mwaka wa 1914 kama mwanzo wa “siku za mwisho” na mwaka ambao ufalme wa mbinguni wa Mungu ulianza utawala wake wa utendaji.—Tazama pia Luka 21:10, 11.

9. Ni matukio gani mengine yenye kuonyesha “siku za mwisho” yametukia kwa mfululizo usio wa kawaida tangu mwaka wa 1914?

9 Pia, baada ya mwaka wa 1914 mifululizo ya matetemeko ya dunia yalitikisa dunia, yakileta hasara kubwa. Katika mwaka wa 1915, katika Italia, karibu watu 30,000 waliuawa. Katika mwaka wa 1920, katika China, watu 180,000 walikufa. Katika mwaka wa 1923, watu 143,000 walikufa katika Japan. Na matetemeko ya dunia makubwa sana yameendelea kutukia kwa mfululizo usio wa kawaida tangu wakati huo. Kama Yesu alivyotabiri, hayo ni ishara nyingine ya “siku za mwisho.”

10. Nini huonyesha kwamba matukio yaliyoonyesha mwaka wa 1914 yalikuwa “mwanzo wa maumivu makali ya ghafula ya taabu” tu?

10 Walakini, Yesu alisema kwamba matukio ambayo yalionyesha mwanzo wa “siku za mwisho” katika mwaka wa 1914 yalikuwa tu “mwanzo wa maumivu makali ya ghafula ya taabu.” (Mathayo 24:8, NW) Taabu iliyo kubwa zaidi ilikuwa inakuja. Kupatana na unabii wake, ilikuja. Kitabu The World Book Encyclopedia husema: “Vita ya Kwanza ya Ulimwe-ngu na mambo yaliyotokea baada yake iliongoza kwenye upungufu mkubwa zaidi wa uchumi kuliko wote katika historia wakati wa mwaka wa 1930 na miaka michache iliyofuata. Matokeo ya vita na matatizo ya upatanisho kwa amani yakaongoza kwenye wasiwasi katika karibu kila taifa.” Hii ilitengeneza njia kwa Vita ya Ulimwengu ya Pili. Na kwa habari ya vita hiyo chanzo kile kile huandika:

“Vita ya Ulimwengu ye Pili iliua watu zaidi, iligharimu fedha zaidi, iliharibu mali zaidi, iliwapata watu zaidi . . . kuliko vita nyingine yo yote katika historia . . . Imekadiriwa kwamba hesabu ya waliokufa kwa vita, raia ambao si askari na raia ambao ni askari wa vita, ilijumlika zaidi kuliko 22,000,000. Hesabu ya waliojeruhiwa imekadiriwa kuwa zaidi kuliko 34,000,000.”c

Kweli, “maumivu makali ya ghafula ya taabu” amba-yo Yesu alitabiri yamekuwa makubwa zaidi kadiri “siku za mwisho” zinavyosonga kuelekea ukomo wazo.

11. (a) Ni kwa kiasi gani upungufu wa chakula umeongeza kwa taabu, kama Yesu alivyotabiri? (b) Ni nini kitabu kiitwacho “Famine-1975!” husema juu ya wakati ujao?

11 Wakati na baada ya Vita ya Ulimwengu ya Pili upungufu wa chakula wa kuenea mahali pote uliongeza kwa taabu. Upesi baada ya vita gazeti Look likasema:

“Sehemu ya nne ya ulimwengu inakufa njaa leo. Kesho itakuwa hata baya zaidi. Njaa kuu juu ya karibu ulimwengu wote sasa ni yenye kutisha zaidi kuliko zaidi ya sisi tuwezavyo kuwaza. . . . Sasa kuna watu zaidi wenye kutafuta sana chakula kuliko katika wakati mwingine wo wote katika historia.”d

Karibuni sana, kitabu kiitwacho “Famine-1975!” kilisema kuhusu upungufu wa chakula wa leo:e

“Njaa inaenea katika nchi baada ya nchi, kontinenti baada ya kontinenti kuzunguka sehemu isiyo na maendeleo ya nchi za joto jingi na nchi za joto kidogo zaidi. Hatari ya leo yaweza kuongoza tu katika njia moja —kuelekea msiba mkubwa sana. Leo ni mataifa yenye njaa; kesho ni mataifa yenye kufa njaa.

“Karibu na mwaka wa 1975 mchafuko wa raia, mchafuko wa utawala, uonezi wa kijeshi la vita, upandishaji wa fedha, kuharibika kwa usafirishaji na wasiwasi wa mchafuko yatakuwa ndiyo mambo ya kila siku katika mengi ya mataifa yenye njaa.”*

12. (a) Ni hali gani nyingine, zilizotabiriwa katika, Biblia, zimetokea kwa kiasi cha mpasuko tangu mwaka wa 1914? (b) Hivyo ni aina gani ya ripoti zinazokuja kutoka kwa taifa baada ya taifa?

12 Tena Yesu alitabiri “kuongezeka kwa uasi wa sheria” kama ishara ya “siku za mwisho.” (Mathayo 24:12, NW) Na Mungu alimwongoza mtume Paulo kuongeza: “Siku za mwisho watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, . . . wasiotii wazazi wao, . . . wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema, . . . wapendao anasa kuliko kumpenda . . . watu watu wabaya na wadanganyaji wataendelea, na kuzidi kuwa waovu.” (2 Timotheo 3:1-5, 13) Hizi ndizo hali ambayo zimetokea kwa kiasi cha mpasuko tangu mwaka wa 1914! Wewe umeziona na macho yako mwenyewe, je! hujaziona? Katika ulimwengu mzima, uasi wa sheria unaongezeka. Akasema mwanasheria mmoja: “Karibu kila mahali, kutia na Soviet Russia, kunaonekana kuwa na ongezeko katika uvunjaji wa sheria, na hasa, ole, katika uvunjaji wa sheria wa watoto.”f Kutoka taifa baada ya taifa huja ripoti kama ifuatayo:

“Wimbi la uvunjaji wa sheria na ghasia linapita kwa kasi kuvuka United States . . . Katika miji mingi, wanawake huogopa kutoka nje baada ya kuwa giza. Na wanayo sababu nzuri. Kulalwa kwa wanawake kwa nguvu bila idhini yao, mashambulio, mipasuko ya gha-fula ya kikatili ya jeuri ya upuzi inaongezeka. Mara nyingi uvunjaji wa sheria huonekana kufanywa kwa ukatili mtupu . . . Heshima kwa sheria na taratibu inapungua.”g

13. (a) Katika Luka 21:25, 26, ni sehemu gani nyingine ya “siku za mwisho” ambayo Yesu alitabiri? (b) Jinsi gani utimizo wa unabii huu huonekana katika habari za wakati wetu?

13 Kama sehemu nyingine ya “siku za mwisho,” Yesu alisema juu ya mchafuko mkubwa na hofu kubwa miongoni mwa mataifa na viongozi wao. Alitabiri: “Duniani huzuni kuu ya mataifa, wasijue njia ya kutokea . . . wanadamu wakizimia moyo kwa sababu ya hofu na kwa kutazamia kwa mambo yanayokuja juu ya dunia inayokaliwa na watu.” (Luka 21:25, 26, NW) Utimizo wa unabii huu u wazi katika habari za wakati wetu. U.S. News & World Report likasema:

“Je! ulimwengu uko katika msukosuko mkubwa zaidi kuliko kabla ya Vita ya Ulimwengu ya Pili? Bila shaka.

“Taabu za kupiga bunduki, kwa wastani, hutokea mara moja kila mwezi. Bila kuhesabu vita halisi kama vile vya Korea na Vietnam, maandishi yangali yakionyesha zaidi ya mapinduzi makuu 300, mapinduzi ya ghafula ya serikali, maasi juu ya serikali na maasi ulimwenguni pote tangu mwisho wa Vita ya Ulimwengu ya Pili.”h

Kuongeza kwa mambo haya yote ni hofu ya kuharibiwa na akiba kubwa mno ya silaha za atomiki ambazo mataifa mengine yanazo. Mtengenezaji mmoja wa gazeti alieleza: “Jambo la hakika ni kwamba leo ono la moyoni lililo kubwa zaidi kuliko yote linalotawala maisha zetu ni hofu.”i Ni kama Yesu alivyotabiri: wanadamu ni wenye hofu na mataifa yamo katika huzuni kuu.

14. Ushuhuda wote huonyesha nini kwa habari ya mwaka wa 1914?

14 Ishara zote za “siku za mwisho” zilizotabiriwa zipo hapa. Zinathibitisha pasipo shaka kwamba sisi tumekuwamo katika “siku za mwisho” tangu mwaka wa 1914. Kwa hiyo ilikuwa ni katika mwaka huo kwamba ufalme wa mbinguni wa Mungu ulianza kutawala!—Ufunuo 11:17, 18.

15. Kwa nini kizazi chetu hakifanani na vingine vyote?

15 Ni kweli kwamba katika vizazi vilivyopita vilikuwako vipindi vilivyoonyeshwa kwa jeuri na mwenendo mwingi wa ufisadi. Kuharibika kwa Milki ya Kirumi ni mfano. Lakini hapajawapo kamwe wakati katika historia ya kibinadamu ambao watu wameona hali zote zilizoainishwa na Yesu katika kizazi kimoja. Na hapajakuwapo kamwe wakati ambao hali hizi zi-likuwapo kwa wakati mmoja katika kila taifa la dunia. Leo tunaishi, si katika siku za mwisho tu wa milki moja ya kisiasa, bali katika “siku za mwisho” wa taratibu nzima mbovu inayotawalwa na Shetani.

MWAKA WA 1914 NI MWAKA ULIOTIWA ALAMA

16. Je! wanafunzi wa Biblia walijua miaka iliyotangulia kwamba yangekuwapo mabadiliko makubwa katika mwaka wa 1914?

16 Miaka iliyotangulia wanafunzi wa Biblia walijua kwamba mwaka wa 1914 ulipaswa kuwa mwaka wenye maana kuu. Elimu ya tarehe ya Biblia huelekeza dhahiri kwenye mwaka huo,j na wanafunzi wenye uangalifu wa Neno la Mungu walijua hilo. Walitazamia mabadiliko makubwa kutukia, na mambo ya hakika huthibitisha kwamba mwaka wa 1914 ulikuwa kweli, ni mwaka uliotiwa alama.

17. Waandikaji wa historia husema nini juu ya mwaka wa 1914?

17 Wengine wenye maarifa ya mambo ya ulimwengu hukubali kabisa kwamba mwaka wa 1914 ulikuwa ni mwaka uliotiwa alama. Gazeti la London Evening Star lilieleza kwamba Vita ya Ulimwengu ya Kwanza “ilitenga mbali taratibu nzima ya siasa ya ulimwengu. Hapana kitu ambacho kingeweza kuwa namna ile ile sikuzote. . . . mwandikaji fulani wa historia katika karne itakayofuata angekuwa na sababu nzuri ya kusema kwamba siku ambayo ulimwengu ulipata wazimu ilikuwa Agosti 4, 1914,”k Kwa habari ya badiliko kubwa lililofanywa na mwaka wa 1914, mwandikaji wa historia H. R. Trevor-Roper alisema:

“Ni jambo la kufundisha kulinganisha Vita ya Uliwengu ya kwanza na ya pili . . . vita ya kwanza ilitia alama ya badiliko kubwa zaidi katika historia. Ilifunga wakati mrefu, wa amani ya watu wote na ikaanza kizazi kipya chenye jeuri ambacho katika hicho vita ya pili ni jambo mojawapo katika mfululizo wa mambo tu. Tangu mwaka wa 1914 ulimwengu umekuwa na tabia mpya: tabia ya machafuko ya mambo ya utawala ya mataifa yote. Hivyo Vita ya Ulimwengu ya kwanza ilitia alama mahali pa kugeukia katika historia ya kisasa.”l

18. Wengine wamesema nini juu ya, maana ya mwaka wa 1914?

18 Viongozi wa ulimwengu pia wameeleza juu ya maana ya mwaka wa 1914. Mkuu wa serikali wa zamani wa Ujeremani ya Magharibi Konrad Adenauer alisema juu ya wakati “kabla ya mwaka wa 1914 wakati kulipokuwa amani halisi, utulivu na usalama juu ya dunia hii—wakati tulipokuwa hatujui hofu.” Ndipo akaongeza: “Usalama na utulivu vimetoweka katika maisha za wanadamu tangu mwaka wa 1914. Na amani? Tangu mwaka wa 1914, Wajeremani hawakujua amani halisi wala mengi ya wanadamu.”a Angalia, pia, maelezo katika kitabu kiitwacho “1914.” Mtungaji husema: “Katika mwaka wa 1914 ulimwengu, kama ulivyojulikana na kukubaliwa wakati huo, ukaja kwenye kikomo. Zaidi sana kuliko mwaka wo wote kabla au tangu wakati huo hapajakuwapo mwaka wa kutia alama ya badiliko la karne ya ishirini kama mwaka wa 1914 . . . tangu wakati huo na kuendelea hapana kitu ambacho kingeweza sikuzote kuwa namna ile ile.”b

19. Kwa nini taratibu hii mbovu ya mambo imetenda kiwazimu sana tangu mwaka wa 1914?

19 Shetani Ibilisi na malaika zake wanajua wana “wakati mchache tu” ubakio kabla ya uharibifu wao. (Ufunuo 12:12) Hata wakati Yesu alipokuwa duniani, mashetani walijua kwamba wakati fulani wao wangeharibiwa. Walionyesha nia ya ukali nyuma wakati huo, na sasa kwamba wanajua wakati wao u mfupi ni wakali zaidi kuliko sikuzote. (Luka 8:2733) Wanaazimu kuchochea taabu yote wawezayo, ili kuvuta nia ya wanadamu kuwa mbali na ufalme wa Mungu. Hii ndiyo sababu taratibu hii mbovu ya mambo imekuwa ikitenda kiwazimu tangu mwaka wa 1914. Inatenda kama pia, kibaramwezi cha mtoto, ambacho huyumbayumba sana kabla hakijaanguka kwa kutulia kabisa.

20 (a) Kwa nini haitupasi kuvunjwa moyo na hali za ulimwengu? (b) Ni nini Yesu alitabiri kwamba wafuasi wake wangekuwa wakihubiri wakati huu? Je! inafanyika?

20 Je! tunavunjwa moyo na hali hii? Yesu alisema kwamba wanafunzi wake wangekuwa na sababu kwa kuinua vichwa vyao. Kwa nini? Kwa sababu wao wanajua maana yake yote. Wao huona katika matukio haya uthibitisho wa kwamba ukombozi u karibu! (Luka 21:28) Na hawaweki habari hizi zenye furaha kwao wenyewe, bali katika dunia yote wanahubiri habari zenye furaha kwamba ufalme wa Mungu sasa unatawala. (Mathayo 24:14) Hii, pia, ni sehemu ya “ishara.” Katika Amerika ya Kaskazini na Amerika ya Kusini, Ulaya, Afrika, Asia na visiwa vya bahari mashahidi wa Yehova kwa bidii huendelea kuutangaza ujumbe huu wa haraka. Mwote katika miji mikubwa na vitongojini utawaona wao, katika sehemu zote za dunia. Naam, sehemu hii ya “ishara” inatimizwa pia.

21. (a) Ebu eleza jambo lililotukia katika mwaka wa 1914. (b) Jibu kwa sala kwa ufalme wa Mungu “uje” litamaanisha nini?

21 Kupita shaka yote, ushuhuda huelekeza kwenye mwaka wa 1914 kama mwaka wakati ufalme wa Mungu ulipoanza kutawala, na tukio hilo linafanya mambo kutukia hapa duniani. Katika mwaka uo huo “taratibu mbovu ya mambo iliyopo” iliingia katika “siku za mwisho” wake. (Wagalatia 1:4, NW) Karibuni, sasa, sala kwa ufalme wa Mungu “uje” itajibiwa, wakati utakapoonyesha nguvu zake kuu kwa kuiharibu taratibu mbovu yote ya Shetani. Ndipo ufalme wa Mungu peke yake utakapotenda kazi kama serikali peke yake kutawala dunia katika umilele wote. (Danieli 2:44) Ukichukua utawala kamili wa mambo yote ya dunia, utaleta kwa wingi juu ya wanadamu watiifu baraka za amani, furaha na uzima. Sala kwa ‘mapenzi ya Mungu yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni,’ itakuwa imepata utimizo wa utukufu, kwa maana ufalme wa Mungu utakuwa umekuja kutawala milele na milele. Na ebu fikiri juu yake! Wewe unaweza ukajifurahisha uzima wa milele chini ya utawala wenye upendo wa ufalme huo.—Mathayo 6:9, 10.

[Maelezo ya Chini]

a World War I, cha H. W. Baldwin, mwaka wa 1962, kur. 1, 2.

b The World Book Encyclopedia, cha mwaka wa 1966, Vol. 20, ukur. 377.

c The World Book Encyclopedia, cha mwaka wa 1966, Vol. 20, kur. 379, 380, 410.

d Look, la Juni 11, 1946.

e Famine-1975, cha W. & P. Paddock, cha mwaka wa 1967, kur. 52, 55, 61.

f U.S. News & World Report, Ia Nov. 1, 1965, ukur. 80.

g Ibid., Ago. 1, 1966, kur. 46, 47.

h U.S. News & World Report, la Nov. 27, 1967, ukur. 62.

i Ibid., Okt. 11, 1965, ukur. 144.

j Kwa habari zaidi kuhusu hili, tazama kitabu “Babylon the Great Has Fallen!” Gods Kingdom Rules!, kurasa za 174-181; pia Kutoka Paradiso Iliyopotea mpaka Paradiso Iliyopatikana, ukurasa wa 173.

k London Evening Star, lililotajwa katika New Orleans Times-Picayune, Ago. 5, 1960.

l The New York Times Magazine, Ago. 1, 1954, ukur. 9.

a Cleveland West Parker, Jan. 20, 1966, ukur. 1

b 1914, cha J. Cameron, cha mwaka wa 1959, kur. za v, vi.

(c) Basi ni mwaka gani ulioonyesha mwanzo wa “siku za mwisho” na wakati ufalme wa Mungu ulipoanza utawala wake wa utendaji?

[Picha ktika ukurasa wa 85]

Yesu akawaambia wanafunzi wake jambo ambalo lingekuwa uthibitsho uonekanao wa kuwapo kwake bila kuonekana katika mamlaka ya kifalme

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki