Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 12/15 kur. 21-26
  • Urafiki Ulio Bora Zaidi Unadumu Katika Ulimwengu Usio na Urafiki

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Urafiki Ulio Bora Zaidi Unadumu Katika Ulimwengu Usio na Urafiki
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kukubaliwa Katika Urafiki Ulio Bora Zaidi
  • “Jina Jipya” Kutoka kwa Rafiki Aliye Bora Zaidi
  • Kusitawisha Urafiki Ulio Bora Zaidi Katika Ulimwengu Wote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • “Nimewaita Rafiki”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • “Ninyi Ni Rafiki Zangu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Tutakuwa Upande wa Nani Taabu ya Ulimwengu Ifikiapo Upeo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 12/15 kur. 21-26

Urafiki Ulio Bora Zaidi Unadumu Katika Ulimwengu Usio na Urafiki

“Jifanyieni rafiki kwa mali ya udhalimu, ili itakapokosekana wawakaribishe katika makao ya milele.”​—LUKA 16:9.

1. Ni kwa sababu gani andiko la Mithali 14:20 halikumhusu Yesu Kristo akiwa duniani?

“MASKINI huchukiwa hata na jirani yake; bali tajiri ana rafiki wengi.” (Mithali 14:20) Mithali hiyo ya Mfalme Sulemani wa Israeli haikumhusu mwanamume mkuu zaidi aliyepata kuwapo duniani, Yesu Kristo, aliye mkuu zaidi ya Sulemani. Yesu hakuwavuta Waisraeli kwenye ushirikiano wa karibu pamoja naye kwa kutumia utajiri wa kimwili; wala yeye hakutambua utajiri wa kidunia kuwa msingi wa urafiki wa kweli wenye kudumu.

2. Yesu aliwaambia wanafunzi wake wafanye urafiki pamoja na nani, na kwa sababu gani?

2 Ni kweli kwamba katika pindi moja Yesu alisema: “Jifanyieni rafiki kwa mali ya udhalimu, ili itakapokosekana wawakaribishe katika makao ya milele.” (Luka 16:9) Lakini “rafiki” ambao Yesu alikuwa akifikiria ni Yehova Mungu, Chanzo cha mali zote zinazofaa, na pia yeye mwenyewe akiwa Mwana wa Babaye mwenye utajiri tele. Sisi leo tukifuata shauri lilo hilo, tunaingizwa katika urafiki bora zaidi uwezao kufurahiwa duniani, urafiki pamoja na Yehova Mungu kupitia Mwanaye mwenye kujinyima, Yesu Kristo.

3. Marafiki hao wa kimbingu wanaweza kutuingiza katika “makao” gani?

3 Kwa sababu ya uhai wao usioweza kufa, Watu hao wa kimbingu wanaweza kubaki wakiwa Marafiki wetu imara na wanaweza kutuingiza katika “makao ya milele.” Ndivyo ilivyo hata iwe hayo “makao ya milele” yatakuwa juu mbinguni pamoja na malaika watakatifu wote au hapa chini duniani katika Paradiso itakayorudishwa.​—Luka 23:43, ZSB.

Kukubaliwa Katika Urafiki Ulio Bora Zaidi

4. (a) Ni mfano gani wa Biblia unaoonyesha kama urafiki na Mungu unaweza kununuliwa? (b) Ni katika njia gani inayofaa tunaweza kutumia mali zetu?

4 Urafiki wa Mungu Aliye Juu Zaidi na wa Mwanaye mzaliwa wa pekee, Yesu Kristo, hauwezi kununuliwa kwa pesa. Jambo hilo lilikaziwa katika kisa cha Anania na Safira katika kundi la Kikristo la karne ya kwanza. Bila kutafuta kujulikana na kuwa na sifa kama walivyofanya, tunaweza kutumia mali zetu za kidunia katika njia inayokubaliwa na Yehova Mungu na Yesu Kristo. (Matendo 5:1-11) Hayo ndiyo yaliyomaanishwa na Yesu Kristo aliposema: “Tumieni utajiri wa kilimwengu kujipatia marafiki, ili huo ukiisha kushindwa, mkaribishwe katika makao ya milele.”​—Luka 16:9, New International Version.

5. Zakayo alifuata mwendo gani, na matokeo yakawa nini?

5 Yesu aliposema maneno hayo, hakuwa akitafuta kibali ya watoza ushuru wa Milki ya Roma na wafanya dhambi wengine. Yeye hakuwa na tamaa ya kujipatia utajiri wo wote wa kimwili hapa duniani, kwa maana alikuwa amekwisha kuwaambia wanafunzi wake wajiwekee wenyewe hazina katika mbingu zilizo juu. Zakayo, mtoza ushuru Myahudi kwa niaba ya serikali ya Roma, aliamua kutenda kulingana na shauri hilo la Masihi Yesu na akatangaza waziwazi kusudi lake la kufanya hivyo. Kwa sababu ya tendo hilo la kuunga mkono faida za Ufalme, mgeni aliye mashuhuri zaidi wa Zakayo alisema: “Leo wokovu umefika nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Ibrahimu. Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea.” (Luka 19:1-10) “Kilichopotea” kilitia ndani Zakayo mwenyewe.

6. Zakayo alikubaliwa aingie ndani ya nini, lakini ni mwendo wa nani wenye kosa unaotuonya?

6 Zakayo alikubaliwa aingie katika urafiki bora zaidi katika ulimwengu wote, ule wa Mungu aliye Baba ya huyo mgeni maalum aliyekuwa akimkaribisha wakati huo. Maandishi ya Biblia hayasemi kama Zakayo alimwona Yesu baada ya kufufuliwa Kwake kutoka kwa wafu na kama alikuwa mmoja wa wale wanafunzi 120 hivi waliokusanyika katika chumba cha orofani Yerusalemu wakati wa siku hiyo yenye kutokeza ya Pentekoste ya 33 W.K. Hata hivyo, bila shaka, Zakayo alikuwa kati ya wale wanafunzi 5,000 wapakwa mafuta waliozaliwa kwa roho ambao waliripotiwa muda mfupi baada ya hapo. (Matendo, sura za 2 na 4; 1 Wakorintho 15:1-6) Lakini ni tofauti kubwa na Hanania na Safira, waliotangulia kutajwa! Watu hao wawili waliokuwa wakishirikiana na kundi la Yerusalemu walijaribu kuongeza sifa yao kati ya wanafunzi kwa kutaja kiasi cha uwongo cha mchango waliokuwa wametoa. Adhabu iliyowapata kwa sababu ya udanganyifu wao iliwapotezea urafiki wao ulio bora zaidi na ni kionyo kwa Wakristo wote leo.​—Matendo 4:34–5:11.

7. Ijapokuwa hali isiyo ya urafiki ya ulimwengu huu, Mashahidi wa Yehova wanafurahia kitu gani kilicho haba?

7 Ijapokuwapo hali ya kukosa urafiki ya ulimwengu wa karne ya 20, Mashahidi wa Yehova wanaendelea kufurahia urafiki ulio bora zaidi. Lakini kwa sababu gani wafurahie kitu hiki kilicho haba wakati mifumo tofauti tofauti ya dini zaidi ya elfu moja haikifurahii? Ushuhuda unaonyesha kwamba ni kwa sababu Mashahidi wa Yehova wamefanya jambo ambalo ni la lazima, jambo ambalo wanadini wa Jumuiya ya Wakristo hawajafanya. Kwanza, Mashahidi wametoka katika mifumo ya dini za uwongo, kwa maana wanatambua kwamba dini hizo ndizo zinafanyiza milki ya ulimwengu ya dini ya uwongo, inayotajwa katika Biblia kuwa Babuloni Mkuu. Bila shaka, tendo lenyewe tu la kutoka katika dini fulani ya uwongo halimweki mtu katika tengenezo la Yehova, kwa maana mtu anaweza kujiunga na mfumo mwingine wa kidini wa milki ya ulimwengu ya dini ya uwongo.

8. Amri ya kutoka katika Babuloni Mkuu imeelekezwa moja kwa moja kwa nani leo?

8 Tunapaswa kuangalia kwamba amri ya kimungu ya kutoka Babuloni Mkuu imeelekezwa kwa “watu wangu.” (Ufunuo 18:4) Kulingana na Maandiko ya Kiebrania, mwito huo wa kimungu unafanana na amri iliyotolewa na Mungu kwa wahamishwa wa Israeli katika nchi ya Babuloni. (Isaya 52:11) Kwa hiyo, mtajo “watu wangu” unahusu moja kwa moja mabaki ya wanafunzi wapakwa mafuta wa Kristo Yesu, waliozaliwa kwa roho ambao wangali duniani. Wakati wa Vita ya Ulimwengu ya Kwanza ya 1914-18, Babuloni Mkuu ilikuwa imewateka wapakwa mafuta hao kupitia sehemu za kisiasa, kijeshi, na za mahakama za ulimwengu huu ili kukomesha utendaji wa mabaki hao wa kiroho. Kwa kusema kwa njia ya mfano, mabaki waliingia katika hali ya utumwa, wakapoteza uhuru wa kutenda katika utumishi wa Yehova.

9. Mashahidi wa Yehova walipaswa kufikia hatua gani ili watoke katika Babuloni Mkuu?

9 Katika Ufunuo sura ya 17, Babuloni Mkuu unafananishwa na malaya aliyepanda juu ya mnyama mwenye vichwa saba na pembe kumi. Mnyama huyo wa mfano anayeingia katika shimo refu na kutoka tena anafananisha tengenezo la kisasa la amani ya ulimwengu, yaani, Umoja wa Mataifa, ambao ulikuwa mrithi wa Ushirika wa Mataifa ulioingia katika shimo refu wakati Vita ya Ulimwengu ya Pili ilipoanza. Kwa hiyo watu wa Yehova, ambao anawaita “watu wangu,” walipotii mwito wake wa kutoka Babuloni Mkuu, walifanya nini? Walitoka si katika utawala na nguvu za milki hiyo ya ulimwengu ya dini ya uwongo tu bali pia walitoka chini ya utawala wa washiriki wake wa kisiasa, sehemu za kisiasa ambazo sasa zimetiwa ndani ya Umoja wa Mataifa.

10. Mashahidi wa Yehova hawajihusishi na tengenezo gani la mataifa yote leo, na kwa sababu gani hawajihusishi?

10 Mabaki wapakwa mafuta wamefuata na kudumisha kutokuwamo kabisa kwa habari ya mambo ya kisiasa na kijeshi ya huu mfumo wa mambo. (Yohana 15:19) Kwa umoja wanaunga mkono Ufalme wa Mungu ulio mikononi mwa Yesu Kristo, ambao ulisimamishwa mbinguni mwishoni mwa Nyakati za Mataifa mwaka wa 1914. Kwa kukaidi Ufalme huo, Ushirika wa Mataifa ulisimamishwa na kuidhinishwa na Babuloni Mkuu baada ya mwisho wa Vita ya Ulimwengu ya Kwanza mwaka wa 1918. Kwa hiyo, tengenezo hilo la mataifa yote lililoundwa na wanadamu linamchukiza Yehova Mungu na pia mabaki waaminifu wa Waisraeli wa kiroho duniani. Wanautumaini Ufalme wa Yehova wenyewe wala si kibandiko cho chote cha kidunia chenye kuchukua mahali pa huo. (Mathayo 24:15, 16) Ni hali moja na “mkutano mkubwa” wa kisasa, uliofananishwa na Wanethini na ‘wana wa watumwa wa Sulemani.’​—Ufunuo 7:9-17; Ezra 2:43-58.

11. (a) Kwa sababu gani ni kosa kwa wanafunzi wa Yesu kuwa marafiki wa ulimwengu huu? (b) Ulimwengu huu una nia gani kuelekea Mashahidi wa Yehova, lakini wao wanaendelea kufurahia nini?

11 Yesu alipokuwa akihukumiwa uhai wake mbele ya gavana Mroma Pontio Pilato, alisema: “Ufalme wangu si sehemu ya ulimwengu huu. Kama ufalme wangu ungalikuwa sehemu ya ulimwengu huu, wahudumu wangu wangalikuwa wamepiga vita kwamba nisitolewe nipewe kwa Wayahudi. Lakini, kama ilivyo, ufalme wangu si wa kutoka chanzo hiki.” (Yohana 18:36, NW) Kwa hiyo lingekuwa kosa kabisa kwa “wahudumu” wa Yesu, au wanafunzi, kuwa marafiki wa ulimwengu huu. Mapema, Yesu alikuwa amewaambia wa kwanza wa “wahudumu” wake, wale mitume 11 waaminifu, kwamba ‘hawakuwa sehemu ya ulimwengu’ ambao Shetani Ibilisi ndiye “mtawala.” (Yohana 14:30, NW; 15:19, NW; linganisha 2 Wakorintho 4:4.) Hiyo ndiyo sababu ulimwengu uliwachukia au ukawa usiowaonyesha urafiki. Ni hali moja na wanafunzi wa Yesu wa hii karne ya 20 wanaojikuta katika ulimwengu usio na urafiki. Ijapokuwa hivyo, wanaendelea kufurahia urafiki ulio bora zaidi katika ulimwengu wote, urafiki na Mungu mwenye ulimwengu wa uadilifu utakaokuja, na pia mwenye “mbingu mpya na dunia mpya” za ulimwengu huo.​—2 Petro 3:13, NW.

12. Mtu anapotoka katika Babuloni Mkuu na kutoka kati ya wenzi wake wa kilimwengu, anapaswa kuchukua msimamo wake upande gani peke yake, na hiyo inatia nini ndani?

12 Mtu anapotoka katika Babuloni Mkuu na wenzi wayo wa kilimwengu, Biashara Kubwa-Kubwa na Siasa na Mambo ya Kijeshi, panaweza kuwapo mahali pengine pamoja tu pa kwenda. Yaani, upande wa tengenezo la ulimwenguni pote la Mungu mmoja aliye hai na wa kweli, Yehova. Hakuna mahali pa katikati. Hiyo inataka mtu avumilie hali isiyo ya urafiki ya ulimwengu huu, na jambo hilo linafanya iwe vigumu sana kwa mtu kuamua kuacha Babuloni Mkuu na ulimwengu ambao Babuloni ni sehemu yake maarufu.

“Jina Jipya” Kutoka kwa Rafiki Aliye Bora Zaidi

13. Katika karne ya kwanza W.K., wanafunzi wa Yesu waliitwa nini kwa uongozi wa Mungu?

13 Urafiki wetu wenye thamani pamoja na Mungu unatufanya sisi wenye furaha tuitwe Mashahidi wa Yehova. Ni kweli kwamba wanafunzi wa Kristo wa karne ya kwanza hawakuwa wamelichukua jina “Mashahidi wa Yehova.” Lakini tafadhali fikiria uhusiano wao pamoja na Rafiki bora zaidi ya wote. Andiko la Matendo 11:26 (NW) linaarifu hivi: “Ilikuwa kwanza katika Antiokia [Siria] kwamba kwa uongozi wa kimungu wanafunzi waliitwa Wakristo.” Unaona kwamba Biblia ya New World Translation of the Holy Scriptures inasema kwamba ‘waliitwa Wakristo kwa uongozi wa kimungu.’ Neno la Kigiriki hapa linalotafsiriwa ‘kuitwa kwa uongozi wa kimungu’ linadokeza kitu kinachopewa jina lisilo la kushtukiwa tu. Rafiki bora zaidi katika ulimwengu alilikubali jina hilo “Wakristo.”

14. Ni mambo gani yanayoweza kusemwa juu ya jina “Jumuiya ya Wakristo,” na ni maulizo gani yanayotaka kuzungumzwa?

14 Kutokana na neno “Wakristo” kumetokea jina Jumuiya ya Wakristo, ambalo linatumiwa kuhusu milki yote ya wanaodai kuwa Wakristo pamoja na madhehebu zayo nyingi. Kwa hiyo jina “Jumuiya ya Wakristo” halikutolewa “kwa uongozi wa kimungu,” ama kupitia mitume ama ‘kwa majaliwa’ kulingana na mapenzi ya Mungu. Kwa hiyo hali leo ni tofauti sana na ile ya karne ya kwanza. Ni Wakristo wa kweli peke yao wanaoweza kufurahia urafiki ulio bora zaidi katika ulimwengu huu usio na urafiki. Kwa hiyo ulizo kubwa zaidi leo ni hili, Ni nani Wakristo halisi, wa kweli, wanaojipatanisha na Maandiko yaliyoongozwa na Mungu? Ulizo jingine la maana ni hili, Je! Mashahidi wa Yehova ni Wakristo wa kweli ambao Yehova Mungu na Yesu Kristo ni Rafiki zao? Kuhusiana na hayo, jina alilojichagulia Mungu, Yehova, linahusika.

15. Ni kwa sababu ya hali gani wakati umefika kwa Yehova kujifanyia jina, na “watu kwa ajili ya jina lake” wana sehemu gani katika jambo hilo?

15 Inawezekanaje Jumuiya ya Wakristo, pamoja na dini zayo nyingi, ifurahie urafiki pamoja na Yehova? Jumuiya ya Wakristo imelitanguliza jina la Yesu Kristo, karibu kuliondoa kabisa jina la Babaye wa kimbingu, Yehova. Lakini, kwa kupatana na unabii wa Biblia, wakati umekuja Yehova ajifanyie jina. Kwa hiyo, jina lake lazima litangulizwe. Kwa ajili ya hilo, angetumia mashahidi wake wa kweli, watu wake waliochaguliwa, wale wanaofurahia urafiki wake. Kwenye mkutano wa pekee wa karne ya kwanza uliofanywa na mitume na wafuasi wengine wa kwanza kabisa wa Yesu Kristo, mwanafunzi Yakobo alisema: “Simeoni amesimulia kikamilifu jinsi Mungu kwa mara ya kwanza alivyogeuza fikira zake kwa mataifa ili achukue katika hao watu kwa ajili ya jina lake.”​—Matendo 15:14, NW.

16, 17. Ni jambo gani limefanywa kuhusu jina la Mungu katika tafsiri za Biblia za Jumuiya ya Wakristo, lakini Biblia ya New World Translation ikoje katika habari hiyo?

16 Ingetazamiwa kwamba ‘watu kwa ajili ya jina la Mungu’ wangekuwa rafiki zake nao wangetegemeza jina lake la kimungu. Lakini imekuwaje katika Jumuiya ya Wakristo? Katika tafsiri zake za Biblia zinazopendwa na wengi, jina la Yehova limefichwa kwa kubadilishwa na mtajo wa cheo. Jina lake linapatikana mara kumi na mbili tu katika tafsiri ipendwayo sana ya Kiswahili leo! (Kutoka 6:2, 3, 6-8; Zaburi 68:20; 83:18; Isaya 12:2; 26:4; 49:14; Yeremia 16:21 na Habakuki 3:19, Union Version) Zaidi ya hayo, hata katika tafsiri za Kiyahudi za Maandiko ya Kiebrania, jina la Mungu limetafsiriwa “BWANA.” Jaribio hilo la kuficha jina la Yehova si kazi ya watu walio rafiki zake.

17 Hata hivyo, katika mwaka 1950, Biblia ya New World Translation of the Holy Scriptures ilianza kujitokeza katika uwanja wa kidini, nayo imeliweka jina la kimungu kila mahali linapoonekana katika maandishi ya awali ya Biblia ya Kiebrania. Pia Biblia ya New World Translation imerudisha jina la kimungu kwenye mahali pake panapofaa katika maandishi makuu-makuu ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, linaloitwa Agano Jipya​—ndiyo, mara 237. Hiyo ndiyo kazi ya rafiki za Yehova.

18. Katika maana ya andiko la Isaya 62:2, ni hatua gani ambayo watu wa Mungu walichukua mwaka wa 1931, nao wamekuwa wakitimiza daraka gani?

18 Yenye kupendeza rafiki za Yehova ni maneno ya Isaya 62:2. Mstari huo, unaoelekezwa kwa tengenezo lionekanalo la wanafunzi wa Masihi walio wakfu, wakabatizwa na kuzaliwa kwa roho, unasema hivi: “Na mataifa wataiona haki yako, na wafalme wote watauona utukufu wako; nawe utaitwa jina jipya, litakalotajwa na kinywa cha [Yehova].” “Jina” hilo linamaanisha hali ya kubarikiwa ambayo katika hiyo wanafunzi hao wa kisasa waliopakwa mafuta wamekwisha kukusanywa. Kuongezea hayo, ili wawe ‘watu kwa ajili ya jina la Mungu,’ mabaki ya washiriki wa tengenezo lake linaloonekana kwa kufaa wanapaswa kuitwa kwa jina lake, wanapaswa kulichukua jina lake. Uhakika huo ulitambuliwa kwa wakati wake. Kwa hiyo, kwa maana ya Isaya 62:2, tengenezo la Mungu lililozaliwa kwa roho, kwenye kusanyiko katika Columbus, Ohio, mwaka 1931, lilikubali kwa furaha jina “mashahidi wa Yehova.” Kwa kufuata mfano huo, makundi yote ya watu wa Yehova walio wakfu yalikubali jina hilo. Na jina hilo limedumu kujapokuwa matabiri ya kilimwengu kwamba halingedumu. Kwenye Ufunuo 3:14 Yesu Kristo aliyetukuzwa alijiita “Shahidi aliye mwaminifu na wa kweli.” Kwa kufaa, basi, tangu mwaka huo wa kukumbukwa wa 1931 na kuendelea, makundi ya wanafunzi wake duniani wamelishika jina hilo kwa uongozi wa Mungu. Tangu wakati huo, wamejitahidi kutimiza daraka lao la kuishi kupatana na jina hilo na kujulisha watu juu yalo. Kwa sababu hiyo, jina la Yehova​—jina la Rafiki yao aliye bora zaidi lisiloweza kulinganishwa na jingine​—limetangulizwa duniani pote. Na Yehova ametoa ushuhuda wenye kutokeza sana kwamba urafiki wake kuelekea mashahidi wake umekuwa ukivumilia mpaka tarehe hii iliyosonga sana.

19. (a) Ni kwa sababu gani mashahidi walio wakfu wa Yehova hawaogopi hali ya kukosa urafiki ya ulimwengu huu, nao wenye kushika ukamilifu watathawabishwa kwa kupewa pendeleo gani kwenye Har–Magedoni? (b) Shukrani na sifa zetu zote zapasa kumwendea Yehova kwa sababu ya nini?

19 Kwa kuwa Yehova Mungu anatuunga mkono sisi mashahidi wake tulio wakfu, kweli kweli ni nani anayeweza kutupinga akafaulu? (Warumi 8:31-34) Kwa hiyo sisi hatuogopi hali ya kukosa urafiki ya ulimwengu huu wenye uadui. Kwa hiyo, tunaendelea tukiwa mabalozi au wajumbe wa Ufalme wa Kimasihi, tukiwaita watu wenye mfano wa kondoo wajipatanishe na Yehova Mungu kupitia Kuhani Mkuu wake wa kifalme, Yesu Kristo. (2 Wakorintho 5:20) Ingawa kwa sababu hiyo uhasama wa ulimwengu huu unaendelea kuongezeka dhidi ya mabaki wapakwa mafuta na wenzi wao, “mkutano mkubwa,” urafiki bora zaidi katika ulimwengu wote, ule wa Yehova Mungu, umeendelea kudumu kwa ushikamanifu. (Ufunuo 7:9) Hautavunjwa kamwe usituelekee sisi tukiwa washika-ukamilifu kwake. Kwa kweli, karibuni, kama isivyokuwa katika wakati mwingine uliotangulia, urafiki huo utaonyeshwa wakati wa vita ile inayoshinda zote, “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi,” kwenye Har–Magedoni. (Ufunuo 16:14, 16) Hapo, Yehova atatetea enzi kuu Yake ya ulimwengu wote kwa kuelekeana uso kwa uso na Shetani Ibilisi na majeshi yake ya mashetani na tengenezo lake lote lionekanalo la kidunia, ajipatie ushindi Wake ulio mkubwa zaidi ya mwinginewo wote katika vizazi vyote. Sisi, ambao tumeendelea kuonyeshwa urafiki wa Yehova mpaka sasa, tutapendelewa wakati huo kwa kuhifadhiwa na kupewa heshima ya kushuhudia ushindi wake mkubwa ajabu kupitia Mfalme wake mwenye kushinda, Yesu Kristo. (Zaburi 110:1, 2; Isaya 66:23, 24) Shukrani na sifa zetu zote za kutoka moyoni zamwendea Yehova Mungu kwa sababu ya urafiki wake wenye kudumu!—Zaburi 136:1-26.

[Picha katika ukurasa wa 23]

Zakayo aliingizwa katika urafiki bora zaidi uwezao kupatikana katika ulimwengu wote. Je! imekuwa hivyo kwako?

[Picha katika ukurasa wa 25]

Wakifurahi kuwa na Mungu kama Rafiki bora zaidi wao, mwaka 1931 Mashahidi wa Yehova waliazimia kujulikana kwa jina lake lisilolinganika na jingine

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki