Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 8/1 kur. 29-31
  • Kujitiisha Wenyewe kwa Yehova Kupitia Wakfu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kujitiisha Wenyewe kwa Yehova Kupitia Wakfu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “Acha Iwe Hivyo, Wakati Huu”
  • Uamuzi Wenye Kutegemea Maarifa
  • Mavazi Yanayofaa
  • Ubatizo​—Takwa kwa Wakristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • Kwa Nini Ubatizwe?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Maana ya Ubatizo Wako
    Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
  • Ubatizo​—Lengo Muhimu!
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 8/1 kur. 29-31

Kujitiisha Wenyewe kwa Yehova Kupitia Wakfu

“TUNAJUA tunatokana na Mungu, lakini ulimwengu wote uko katika uwezo wa yule mwovu.” Kwa usemi huo mtume Yohana anatokeza ukweli usiokaribishwa na watu wengi, yaani, kwamba ulimwengu wote uko katika uwezo wa “yule mwovu,” Shetani. Lakini, Shetani “haimarishi kushika kwake” wale wanaotokana na Mungu wa kweli, Yehova. Kwa hiyo jamaa yote ya kibinadamu lazima ijikute ama chini ya utawala wa Shetani au chini ya utawala wa Yehova. Ni jambo la mtu binafsi kujiamulia. Wewe utajitiisha kwa nani? Kwa Shetani au kwa Yehova?​—1 Yohana 5:18-20; New International Version; Today’s English Version.

Sasa zaidi ya wakati mwinginewo wote ni wakati wa kila mtu kuchagua. (Luka 21:31, 32) Yesu alionyesha kwamba hakuwezi kuwako msimamo wa katikati, au kusimama mguu mmoja upande huu na mwingine upande huu. Alisema, “Mtu asiye pamoja nami yu kinyume changu; na mtu asiyekusanya pamoja nami hutapanya.” (Mathayo 12:30) Tunaweza kuwaje na uhakika kwamba tunakusanya pamoja na Kristo? Dini nyingine zilizogawanyika na zinazotofautiana zinadai ni za Kikristo, ‘zimeokolewa’ na ‘kuzaliwa tena,’ na kufanya semi hizo zikawa hazina maana. (Mathayo 19:16-26; Yohana 3:3; 10:9) Jambo la kuongozea ni hili: Je! sisi tunasadiki na kutangaza aliyosadiki Yesu na kuyatangaza? Akiwa Myahudi, bila shaka hakujaribu kujitukuza mwenyewe kwa kufundisha fundisho la Utatu ulio fumbo. (Yohana 14:28; 17:1-5) Lakini alitangaza ujumbe ulio wazi, ujumbe wa Ufalme wa Mungu. Akiwa anatambua mgawo wake, Yesu alisema: “Imenipasa kuihubiri habari njema ya ufalme wa Mungu katika miji mingine pia; maana kwa sababu hiyo nalitumwa.”​—Luka 4:43.

“Acha Iwe Hivyo, Wakati Huu”

Kabla Yesu hajaanza huduma yake ya peupe ya kutangaza Ufalme wa Mungu, alichukua hatua ya maana sana ambayo ni mfano kwa wale wote ambao, kama yeye wangependa kujitiisha kwa Babaye. Masimulizi ya Mathayo yanatuambia hivi: “Ndipo Yesu akatoka Galilaya kuja Yordani kwa Yohana, ili abatizwe naye.” Yohana alipopinga kwamba ndiye anapaswa kubatizwa, jibu la Yesu lilikuwa hili: “Acha iwe hivyo, wakati huu, kwa maana kwa njia hiyo inatufaa sisi kutimiza yote ambayo ni uadilifu.”​—Mathayo 3:13-15, NW.

Akiwa amekwisha kuweka mfano katika “yote ambayo ni uadilifu” kwa kuzamishwa katika Yordani, Yesu angeweza baadaye kuwapa wanafunzi wake amri hii: “Kwa hiyo nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, kuwabatiza katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu, kuwafundisha kushika mambo yote ambayo nimewaamuru ninyi.” (Mathayo 28:19, 20, NW) Kati ya mambo mengine, hatua hiyo ya ubatizo ingetambulisha wale ambao wamechagua kujitiisha kwa Mungu wa kweli, Yehova, badala ya kujitiisha kwa Shetani. Wakati wa mwaka wa utumishi uliopita (Septemba 1983-Agosti 1984) karibu watu 180,000 ulimwenguni pote walionyesha uchaguzi wao kwa ubatizo wa maji. Walionyesha kwamba wanapendelea enzi kuu ya Yehova badala ya ile ya Shetani.​—Mithali 27:11.

Uamuzi Wenye Kutegemea Maarifa

Hali moja na hiyo mwaka huu maelfu mengi wanafikiria hatua ya ubatizo wakati wa “Washika Ukamilifu” Kusanyiko litakalofanyiwa sehemu nyingi za ulimwengu. Kabla ya kufikia hatua hiyo ya ubatizo, wote wanaotarajia kubatizwa wanakuwa wamekwisha kurudia kwa uangalifu wakiwa na wazee wa kundi mafundisho makuu ya Biblia na miongozo ya mwenendo wa Kikristo ili kuhakikisha wanastahili ubatizo kweli kweli. Kwa hiyo uamuzi wa kubatizwa si tendo la kusukumwa ghafula tu na mawazo. Badala yake, kila mmoja ‘amejithibitishia mwenyewe mapenzi ya Mungu yaliyo mema na yenye kukubalika na makamilifu’ na anataka kujitiisha chini ya mapenzi hayo.​—Warumi 12:2, NW.

Mwishoni mwa hotuba ya ubatizo ya kusanyiko, watakaobatizwa watakuwa katika hali ya” kujibu kwa ufahamu wa kindani na kuthamini kwa moyo maulizo mawili rahisi yanayothibitisha kwamba wanatambua yanayomaanishwa na kufuata mfano wa Kristo. Swali la kwanza ni hili:

Kwa msingi wa dhabihu ya Yesu Kristo, je, wewe umetubu dhambi zako na kujiweka wakfu kwa Yehova ili ufanye mapenzi yake?

La pili ni hili:

Je! wewe unaelewa kwamba wakfu na ubatizo wako unakutambulisha wewe kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova kwa kushirikiana na tengenezo la Mungu lenye kuelekezwa na roho yake?

Wakiisha kujibu ndiyo maswali hayo, wanaotarajia kubatizwa wako katika hali inayofaa kupata ubatizo wa Kikristo.

Mavazi Yanayofaa

Nyakati nyingine maswali yanatokezwa juu ya mavazi yanayowafaa wanaobatizwa. Bila shaka kiasi chapasa kuonyeshwa na namna ya vazi la majini linalotumiwa. Hilo ni jambo la maana leo wakati ambao wabuni wa mitindo yaelekea wanataka kuonyeshana mambo ya ngono na kutokeza karibu hali ya uchi kabisa. Jambo jingine la kufikiria ni kwamba mavazi mengine yanayoonekana kuwa yenye kiasi yanapokuwa makavu hayawi hivyo yanapolowa na maji. Hakuna ye yote anayebatizwa angependa kuondosha fikira kando au kuwa kikwazo wakati wa tukio zito kama ubatizo.​—Wafilipi 1:10.

Katika wakati uliopita, wengine wamepita mipaka kwa kutoa zawadi za bei kubwa na kufanya karamu kubwa kwa ajili ya watu waliotoka kubatizwa. Ubatizo ni pindi ya furaha kubwa inayoweza kushirikiwa na wengine, lakini labda inafaa hapa kutoa maneno ya kutahadharisha. Biblia inasema: “Heri mwisho wa neno kuliko mwanzo wake.” (Mhubiri 7:8) Ubatizo ni mwanzo​—mwanzo wa mbio za Kikristo za kuokolewa mpaka kwenye uzima. Bila shaka, wakati huo kunakuwa hakuna kumbukumbu ndefu ya utumishi wa uaminifu iliyokwisha kuwekwa. Kwa hiyo sababu gani kuwafanya waliotoka kugeuzwa wajione ni wa maana isivyofaa?​—Linganisha 1 Timotheo 3:6.

Maandishi ya Biblia yanasema ni nini yaliyotukia baada ya watu elfu tatu kubatizwa katika Pentekoste mwaka wa 33 W. K.? “Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali.” Walikaza fikira juu ya mambo ya kiroho na kukaribishana. (Matendo 2:41, 42) Ubatizo ni wakati wa kutafakari na kufikiria kwa utimamu. Tunafurahi kuona wanafunzi wa Biblia wetu wakichukua hatua hiyo ya maana sana. Na mavazi yetu kwenye mahali pa ubatizo yanapasa kuonyesha kwamba uamuzi wa maana sana umefanywa​—kujitiisha kwa Mungu akiwa Bwana Mwenye Enzi Kuu na, kama shahidi wa Yehova, kutokuwa sehemu ya ulimwengu ulio “katika uwezo wa yule mwovu.”​—1 Yohana 5:19, NW; Mathayo 4:10.

[Blabu katika ukurasa wa 30]

Tangu Juni 1984, jumla ya makusanyiko 808 ya “Ongezeko la Ufalme” ya Mashahidi wa Yehova yamefanywa duniani pote. Hudhurio la jumla lililoripotiwa lilikuwa ni 5,002,684. Kati ya hao 63,556 walibatizwa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki