“Mimi Nilijawa na Uchangamfu”
Burt anaishi Uingereza. Alitumia majuma sita katika Australia akitembelea Eric ndugu yake na mke wake, ambao ni Mashahidi wa Yehova, katika Australia. Ndugu yake alipomkaribisha ahudhurie kwenye Jumba la Ufalme, Burt alisita-sita kwa sababu dini yake ni tofauti. Lakini alishangaa sana aliposalimiwa kwa roho ya uchangamfu na urafiki hata kwamba, baada ya kurudi Uingereza, akaandikia kundi hilo barua ya kuthamini:
“Nalazimika kukiri kwamba mimi si Shahidi, kwa kuwa mimi ni mshiriki mwenye bidii wa Kanisa la Uingereza. Kwa hiyo nilifanya wasiwasi kwa kadiri fulani nilipoambatana na Eric na Joan kwenye ibada yao ya Jumapili.
“Nisingalihitaji kuwa na woga wo wote. Ukaribishaji niliopewa karibu na kundi lote ulikuwa wa kidugu kweli kweli na wa moyo mweupe. Lakini zaidi ya hilo mimi nilijawa na uchangamfu wa kwamba, ingawa nilikuwa mtu asiyejulikana nao hata kidogo, nilikubaliwa, si kama mgeni hasa bali kama mshiriki wa kundi anayekaribishwa.
“Ingawa sikuelewa mambo yote katika ibada na ushuhuda wenu, hata hivyo mkutano ulipoisha niliondoka nikijisikia nimefaidika sana kutokana na tukio hilo na kujiuliza ni kwa nini upendo na weupe wa moyo ulioonekana wazi wakati wa ibada yote usienee katika pande zote za ulimwengu wetu huu wenye misukosuko mingi
Wenu kwa moyo mweupe,
Burt B.”